Pre GE2025 Ushauri kwa Mkurugenzi Mkuu wa TISS Kuhusu Kero Sugu ya Uhalifu wa Kiuchaguzi Unaofanywa na Wanasiasa Matapeli Wakati wa Chaguzi tangu 2010 hadi 2024

Pre GE2025 Ushauri kwa Mkurugenzi Mkuu wa TISS Kuhusu Kero Sugu ya Uhalifu wa Kiuchaguzi Unaofanywa na Wanasiasa Matapeli Wakati wa Chaguzi tangu 2010 hadi 2024

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hakuna ushahidi wa CCM kuiba uchaguzi? We una akili kweli?

Nilidhani nazungumza na mtu mwenye akili kumbe naongea na mjinga na chawa.

Haya kakojoe ukalale.
Akili unazo wewe mwenye ushahidi wa kupika na kutengeneza ukihusisha wataalam wasio na nia njema na taifa hili na wanaotumika kutokea nje ya nchi.....
 
Akili unazo wewe mwenye ushahidi wa kupika na kutengeneza ukihusisha wataalam wasio na nia njema na taifa hili na wanaotumika kutokea nje ya nchi.....
Endeleza ujinga wako. Najuta kutumia muda wangu kumjibu mtu kumbe ni mjinga, chawa asiyejielewa.

Tafuta clip ya Nape akiwa jimboni kwa Byabato akielezea kuwa sio kura za wananchi zinazoamua mshindi wa uchaguzi ila mtangaza matokeo waliyemweka alafu ukimaliza tafuta clip ya aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Longido akielezea namna gani CCM wanafanya kwenye chaguzi.

Ingawa najua umeziona ila fanya hivyo tu alafu kakojoe ukalale.
 
Kwani utawala wa majimbo upo Ethiopia tu? Mbona Afrika Kusini upo, Mbona Kenya upo? Mbona Marekani upo?

Kama CCM wanaiba uchaguzi kwa kupindua matokeo halali wana tofauti gani na Mobutu?
Yanayoendelea Kenya na SA si ya kujifunza....

Kenya bado ina siasa za KIKABILA....Tanzania haina hayo!

Afrika Kusini wanaendelea kupambana na athari za "apartheid"....wewe huoni misimamo ya akina Elon Musk na boss wake mh.Trump juu ya yale maeneo ya "ardhi"?!!

Bado hoja yangu haijapata kuota kutu ; watanzania hatutaki katiba yenye vipengele vya MAJIMBO ya kiutawala kwani hakuna faida ya kuiga kutoka kwa Kenya ,SA na US.....
 
Endeleza ujinga wako. Najuta kutumia muda wangu kumjibu mtu kumbe ni mjinga, chawa asiyejielewa.

Tafuta clip ya Nape akiwa jimboni kwa Byabato akielezea kuwa sio kura za wananchi zinazoamua mshindi wa uchaguzi ila mtangaza matokeo waliyemweka alafu ukimaliza tafuta clip ya aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Longido akielezea namna gani CCM wanafanya kwenye chaguzi.

Ingawa najua umeziona ila fanya hivyo tu alafu kakojoe ukalale.
Huyo DC wa Longido ni mropokaji tu....ni aina ya viongozi wasiojitambua na kutambua nafasi zao kwa kufurutu ada ya kujiamini juu ya vyeo vyao na ufurahishaji genge kwa maslahi binafsi anayoyajua mwenyewe.....

Mh.Nape Nnauye ni mpenda sifa na mropokaji tu....simshangai kwa maneno hayo aliyotamka.....

Bado huo si ushahidi kwani haikutamka tume ya uchaguzi.....
 
Itakayoamua nani ashinde Dola na apewe ni dola yenyewe!

Kama Dola itaona mambo yalivyo ndivyo yanavyopaswa kuwa basi yataendelea kuwa yalivyo!

Kama ikiona hayana tija kwa taifa bas watarekebisha wenyewe hali!
 
Huyo DC wa Longido ni mropokaji tu....ni aina ya viongozi wasiojitambua na kutambua nafasi zao kwa kufurutu ada ya kujiamini juu ya vyeo vyao na ufurahishaji genge kwa maslahi binafsi anayoyajua mwenyewe.....

Mh.Nape Nnauye ni mpenda sifa na mropokaji tu....simshangai kwa maneno hayo aliyotamka.....

Bado huo si ushahidi kwani haikutamka tume ya uchaguzi.....
Uchaguzi ni nini?

Viongozi wa dini mfano Mufti na Askofu hata Pope wanachaguliwaje?

Nimekaa pale 🐼
 
Hoja nzuri, utafiti mzuri, ila sio realistic!.

Uchaguzi is a process, kuna siku Uchaguzi mkuu uliwahi kusogezwa mbele kwassbabu ya kurekebisha jambo lolote?.

TAL anayo the capacity & capability yoyote kusema no reforms no election?.

Hana!.

There will be no reforms, na uchaguzi utafanyika!. TAL na Chadema has no capacity wala capability kuzuia uchaguzi usifanyike!.

Nashauri watu wenye uwezo wa kusaidia, tumsaidie TAL, tuisadie Chadema iachane na Utopian politics and come to face with the real polititcs, TAL wala Chadema hawawezi kuzuia uchaguzi mkuu.
P
Mkuu wakati mwingine vaa viatu vya wananchi wa Tanzania, unaona busara kwa wananchi kumchagua kiongozi wao wanaemwoka anafaa then kiongozi huyo asitangazwe kisa mwenyekiti anamtaka kiongozi mwingine asiyewafaawananchi?
Tunapompata mtu mwenye uwezo wa kusema tusitishe uchaguzi wa namna hiyo ili kurekebisha kasoro hizo tunatakiwa kumuunga mkono siyo kutoa kejeli.
 
Mkuu wakati mwingine vaa viatu vya wananchi wa Tanzania, unaona busara kwa wananchi kumchagua kiongozi wao wanaemwoka anafaa then kiongozi huyo asitangazwe kisa mwenyekiti anamtaka kiongozi mwingine asiyewafaawananchi?
Tunapompata mtu mwenye uwezo wa kusema tusitishe uchaguzi wa namna hiyo ili kurekebisha kasoro hizo tunatakiwa kumuunga mkono siyo kutoa kejeli.
Hakuna mtu mwenye uwezo wa kusitisha UCHAGUZI MKUU...nchi haiko katika "taharuki na machafuko....".
 
(b) Kimaadili, sheria ya maadili asilia inatupa jukumu la kutekeleza matendo mema na kuzuia matendo maovu, kwa kuhakikisha kwamba, kisiasa, inasimikwa serikali iliyotokana na wapiga kura halali, inayofanya kazi kwa niaba ya watu wote, na yenye kutekeleza majukumu yake kwa faida ya watu wote.
Mwisho wa Kunukuu
 
View attachment 3242826
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akimwapisha Suleiman Abubakar Mombo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Ikulu ya Dar es Salaam , 11 Julai 2024.

I. USULI

Naandika dokezo la kisera, lenye kubeba taarifa za intelijensia ya kisiasa na kijasiriadola, kwa ajili ya kutetea rai ifuatayo:

Kwamba, kwa kuwa uhalifu wa kiuchaguzi unaowafanywa na wanasiasa matapeli wakati wa chaguzi zetu umekithiri kwa miaka 15 sasa kutokana na matobo ya kikatiba na kisheria, basi, tunapaswa kurekebisha ratiba ya uchaguzi mkuu wa 2025, kisha tufanye mageuzi ya kikatiba na kisheria, na hatimaye tufanye uchaguzi mkuu baadaye, na sio kinyume chake.

II. UTANGULIZI


Napendekeza kuanza dokezo hili kwa nukuu muhimu kuhusiana na mtazamo wa Chadema kuhusu Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika 2025.

"Mtu yeyote mwenye akili na macho ya kuona anajua kuwa chaguzi za nchi hii zimekuwa za hovyo sana na kwamba ni za hovyo kwa sababu mfumo mzima wa kiutawala wa nchi hii ni mfumo wa hovyo" -- Tundu lissu, Mwenyekiti CHADEMA.

“Hivyo, hatuzungumzii kususuia uchaguzi, hatutasusia bali tutaenda kuwaambia Watanzania, jumuiya ya kimataifa na walimwengu kwamba kama CCM na Serikali hawako tayari kufanya mabadiliko kwenye mfumo wa uchaguzi ili kuwepo chaguzi huru na haki, uchaguzi wa mwaka huu usifanyike kabisa” -- Tundu lissu, Mwenyekiti CHADEMA.


Huu ndio msimamo ulioibuliwa na Chadema kuhusu kile ambacho baadhi ya vyombo vya Habari, kama vile gazeti la Mwananchi la leo, vinakiita “Njiapanda ya Chadema Kuhusu Uchaguzi Mkuu wa 2025.”

Lakini, napendekeza kwamba, kutokana na uzito wa hoja yenyewe, hasa tunapaswa kuwa tunaongelea “Njiapanda ya Watanzania Kuhusu Uchaguzi Mkuu wa 2025.”

Kwa njia ya swali, “njiapanda” inayoongelewa kwenye vyombo vya habari, ndani na nje ya Chadema pia, inaweza kusomeka hivi:

Je, kwa kuzingatia uhalifu wa kiuchaguzi ambao umekuwa ukifanyika nchini Tanzania tangu 2010 kutokana na uwepo wa milima, mabonde na makorongo yaliyopo kwenye uwanja wa uchaguzi wa vyama vingi nchini Tanzania, tufumbe macho na kuendelea na utekelezaji wa ratiba ya uchaguz mkuu wa Oktoba 2025 au tusogeze ratiba hii mbele kidogo ili uchaguzi huu ufanyike baada ya mageuzi ya kikatiba na kisheria kufanyika ili kusawazisha milima, mabonde na makorongo yaliyopo?

Kutokana na utafiti nilioufanya, dokezo hili linapendekeza kwamba, tunapaswa kusogeza ratiba ya uchaguzi mkuu mbele kidogo ili uchaguzi huu ufanyike baada ya mageuzi ya kikatiba na kisheria kufanyika ili kusawazisha milima, mabonde na makorongo yaliyopo.

III. UTARATIBU WA UTAFITI (METHODOLOJIA)

Katika utafiti wangu nilikusudia kujibu maswali yafuatayo:
  1. Hoja ya Chadema kuhusu changamoto ya uhalifu wa kiuchaguzi nchini Tanzania inasema kitu gani kuhusu uwanja wa siasa za uchaguzi wa vyama vingi?
  2. Je, ni kweli kwamba kuna milima, mabonde na makorongo kwenye uwanja wa siasa za uchaguzi wa vyama vingi nchini Tanzania?
  3. Kama jawabu kwa swali la kwanza ni “ndiyo,” milima, mabonde na makorongo haya yamekuwa na madhara gani katika matokeo ya uchaguzi?
  4. Kutokana na majibu ya maswali haya mawili hapo juu, nah atua gani zichukuliwe tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu wa 2025.

IV. MATOKEO YA UTAFITI

Hoja ya Chadema


Maneno ya Tundu Lissu kuhusu msimamo wa kisera wa chama chake juu ya umuhimu na ulazima wa kusogeza mbele ratiba ya Uchaguzi Mkuu ujao yamenukuliwa hapo juu.

Kwa maoni yangu, haya ndio maneno yanayotueleza msimamo rasmi wa Chadema. Maneno haya yanaweza kufafanuliwa katika muundo wa hoja rasmi kama ifuatavyo:

1. Kama tungekuwa na mifumo ya kikatiba na kisheria inayowanyima wanasiasa matapeli fursa ya kufanya uhalifu wa kiuchaguzi kwenye michakaato ya chaguzi zetu basi tungekuwa na sababu nzuri ya kushiriki Uchaguzi Mkuu Ujao kabla ya kufanyika kwa mageuzi ya kimfumo.

2. Lakini, uzoefu wetu kutokana na chaguzi zote za 2010, 2015, 2019, 2020 na 2024 unaonyesha kwamba tunayo mifumo ya kikatiba na kisheria inayowapatia wanasiasa matapeli fursa ya kufanya uhalifu wa kiuchaguzi kwenye chaguzi zetu, kiasi kwamba, kwa kipindi cha miaka 15, tumekuwa tukiongozwa na serikali haramu zilizotokana na mbinu haramu.

3. Hivyo, bila kufanya mageuzi ya kuboresha mifumo ya kikatiba na kisheria inayowapatia wanasiasa matapeli fursa ya kufanya uhalifu wa kiuchaguzi kwenye chaguzi zetu hatuwezi kupata serikali halalai iliyotokana na mbinu halali.

4. Kwa mujibu wa sheria ya makosa ya jinai, kama ilivyotafsiriwa kwenye Kesi ya Abdallah Zombe na wenzake 12, Kesi ya Mahakama Kuu Na. 26/2006, kuna njia tatu za mtu mmojawapo kushiriki katika kitendo cha uhalifu wa kiuchaguzi, kabla, wakati na baada ya mchakato wa uchaguzi:
  • (a) Ama kwa mtu huyo kutekeleza uhalifu wa kiuchaguzi kwa kutumia mikono yake mwenyewe; au
  • (b) kwa mtu huyo kumpa ushirikiano wa aina yoyote mtu baki mwenye nia ya kutenda uhalifu wa kiuchaguzi na hivyo kumsaidia mtu baki kufanikisha utekelezaji wa uhalifu; au
  • (c) kwa mtu huyo kuficha taarifa muhimu zinazohitajika kwa ajili ya ama kuzuia uhalifu wa kiuchaguzi kutendeka au zinazoweza kusaidia kuwatia hatiani watu waliotenda uhalifu wa kiuchaguzi.
5. Hivyo, kama tunao wajibu wa kupigania ujio wa serikali halali iliyotokana na mbinu halali, basi, tunapaswa kupigania ujio wa serikali halali kwa kufanya yafuatayo:
  • (a) Ama kujizuia na kumshawishi kila mtu baki kujizuia kutekeleza uhalifu wa kiuchaguzi kwa kutumia mikono yake mwenyewe; au
  • (b) Kujizuia na kuwashawishi watu baki kujizuia kumpa ushirikiano wa aina yoyote mtu mwenye nia ya kutenda uhalifu wa kiuchaguzi na hivyo kumfanya mtu baki asifanikishe utekelezaji wa uhalifu; au
  • (c) Kufichua taarifa muhimu zinazohitajika kwa ajili ya ama kuzuia uhalifu wa kiuchaguzi kutendeka au zinazoweza kusaidia kuwatia hatiani watu waliotenda uhalifu wa kiuchaguzi.
6. Kwa hakika, tunao wajibu wa kisheria na kimaadili wa kupigania ujio wa serikali halali, jambo linalomaanisha kwamba tunao wajibu wa kisheria na kimaadili wa kuzuia ujio wa serikali haramu, kwa sababu zifuatazo:
  • (a) Kisheria, ibara ya 28(1) ya Katiba ya Tanzania (1977) inampa kila raia “wajibu wa kulinda, kuhifadhi na kudumisha uhuru, mamlaka, ardhi na umoja wa taifa.”
  • (b) Kimaadili, sheria ya maadili asilia inatupa jukumu la kutekeleza matendo mema na kuzuia matendo maovu, kwa kuhakikisha kwamba, kisiasa, inasimikwa serikali iliyotokana na wapiga kura halali, inayofanya kazi kwa niaba ya watu wote, na yenye kutekeleza majukumu yake kwa faida ya watu wote.
7. Kwa hiyo, raia wa Tanzania tunao wajibu wa kupigania uchaguzi utakaofanikisha ujio wa serikali halali na kupinga uchaguzi utakaofanikisha ujio wa serikali haramu. Hii ndio mantiki ya kaulimbiu isemayo kwamba “Bila Kufanya Mageuzi Kwanza Hakuna Kufanya Uchaguzi,” yaani “No Reforms, No Elections.”

Kwa ujumla, ni wazi kwamba hitimisho hili lisemalo linawaweka njiapanda baadhi ya wanachama wa Chadema wanaotaka kugombea Udiwani, Ubunge na Urais kwa tiketi ya Chadema.

Pia, ni wazi kwamba vyama vingine vinaweza kuendelea na maandalizi ya uchaguzi, maana hii sio sera yao. Na wanachadema wanaopinga sera hii wanayo hiari ya kutafuta jukwaa jingine la kisiasa lisilotambua sera hii ili wapewe fursa ya udhamini wanaoutaka.

Milima, mabonde na makorongo ya kisiasa

Tuhuma kwamba chaguzi zote za 2010, 2015, 2019, 2020 na 2024 unaonyesha kuwa tunayo mifumo ya kikatiba na kisheria inayowapatia wanasiasa matapeli fursa ya kufanya uhalifu wa kiuchaguzi kwenye chaguzi zetu, kiasi kwamba, kwa kipindi cha miaka 15, tumekuwa tukiongozwa na serikali haramu zilizotokana na mbinu haramu, nazi zinao ushahidi wa kuziunga mkono kama ifuatavyo:

(a) Uchaguzi unaosimamiwa na ma-WEO, ma-DED, ma-DC, ma-DAS, na ma-RAS unakosa uhuru, uwazi na ushindani wa kweli, kwa sababu wao ni watumishi wa serikali ya chama tawala, na hivyo kufanya uhalifu wa kiuchaguzi kwa faida ya chama tawala.

(b) Sheria za uchaguzi zinawaruhusu Watumishi wa umma kuvaa kofia za Watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakati w auchaguzi na hivyo kufungua milango ya uhalifu wa kiuchaguzi.

(c) Tume ya Taifa ya Uchaguzi imo kwapani mwa Rais wa nchi, ambaye ndiye huteua wajumbe wake, na hivyo kushindwa kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria pekee kwa sababu ya kuyumbishwa na maagizo kutoka Ikulu.

(d) Tume ya Taifa ya Uchaguzi haina uwezo wa kisheria wala kifedha wa kusimika watumishi wake kwenye kila jimbo la uchaguzi kwa mujibu wa sheria.

(e) Katiba inamruhusu Rais wa nchi aliye madarakani na ambaye ni mgombea kuendelea kutekeleza majukumu yake ya Urais wakati wa kampeni za uchaguzi ilihali yeye ni Amiri Jeshi Mkuu, Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, na Msimamizi Mkuu wa Jeshi la Polisi.

Jambo hili linafungua mianya kwa baadhi ya vyombo vya ulinzi na usalama, kama vile Jeshi la Polisi na TISS, kufanya uhalifu wa kiuchaguzi ili kumsaidia “bosi” wao kushinda.

(f) Katiba inaruhusu Rais wa nchi kushika nafasi ya mwenyekiti wa chama cha siasa, kabla na wakati wa uchaguzi, na hivyo, kufungua mlango wa Rais huyu kuvitumia vyombo vya ulinzi na usalama kwa faida ya chama tawala.

(g) Katiba na sheria zetu vinazuia matokeo ya uchaguzi wa Rais yanayobishaniwa kupingwa mahakamani kisheria. Hivyo, uhalifu wa kiuchaguzi kuhusiana na kura za urais hauwezi kukosolewa kimahakama.

(h) Sheria na Katiba havijapiga marufuku tabia ya uhalifu wa kiuchaguzi wa kugeuza mchakato wa uchaguzi kuwa mashindano ya kujaza fomu za wagombea, jambo ambalo linazalisha wagombea wa kupigiwa “kura za ndio au Hapana,” na hivyo kukiuka kanuni ya uchaguzi wenye ushindani.

Madhara ya milima, mabonde na makorongo haya

Makorongo haya kwenye uwanja wa siasa za vyama vingi yamekuwa na madhara ya kisiasa tangu zamani, hata kabla ya hayati Magufuli hajakanyaga Ikulu. Mfano:

(a) Mwaka 2010 na 2015 enzi za Kikwete

Katika zama hizi kulikwa na “vikosi kazi” vya kukomboa majimbo yaliyo hatarini.

Kwa kila jimbo ambalo tayari lilithibitika kuanguka mikononi mwa wapinzani, vikosi hivi vilikuwa vinashirikiana na baadhi ya ma-WEO, ma-DC, ma-DAS, ma-DED, ma-DSO, ma-OCD, ma-RSO, ma-RAS na ma-RC kufanya “ukombozi.”

Mfano mmoja ni ule wa Jimbo la Karagwe mwaka 2010. Mgombea wa CCM, Gosbert Blandes Begumisa, alipoteza jimbo hilo kwa tofauti ya kura zipatazo 500. Mgombea wa Chadema alishinda.

Kikosi kazi kikafika Karagwe haraka. Kiongozi wa kikosi kazi kile alikuwa ni Afisa Usalama aliyeitwa “Haule.” Wakachakachua takwimu Blandes akatangazwa mshindi.

Niliambiwa kuwa, Kila kikosi kilikuwa kinapewa magari, fedha taslimu na wakati mwingine helikopta. Na kwa kila jimbo lililokuwa linakombolewa “malipo ya kazi maalumn” yalikuwa fedha ipatayo TZS 100,000,000 (soma milioni mia moja).

Hivyo, wajumbe wa “vikosi kazi” hivi enzi za Kikwete walifanikiwa kujenga majumba, kununua magari, na kuanzisha biashara kubwa. Kwao, wakati wa msimu wa uchaguzi wajibu wao ulikuwa ni kuiba majimbo na ulikuwa ni msimu wa “mavuno” makubwa.

View attachment 3242827
Gosbert Blandes Begumisa, Mbunge wa zamani wa Karagwe

(b) Mwaka 2019 na 2020 enzi za Magufuli

Wakati wa JPM idadi ya “vikosi kazi” iliongezeka, kiasi kwamba uhalifu wa kiuchaguzi ikawa sera rasmi ya kila jimbo la uchaguzi. Ma-WEO, ma-DC, ma-DAS, ma-DED, ma-DSO, ma-OCD, ma-RSO, ma-RAS na ma-RC wote walipewa maagizo rasmi ya kusimamia ushindi wa wagombea wa CCM.

Uliotegemewa kuwa uchaguzi haali uligubikwa na uhalifu wa kiuchaguzi wenye sura zifuatazo:
  • Kutoandikisha wapiga kura kwenye ngome za wapinzani,
  • Kuwaengua wagombea wao wengi,
  • Kutowaruhusu mawakala wa vyama vya upinzani na
  • Kutowatangaza wapinzani hata pale walipoonekana kushinda.

Hatimaye wapinzani hawakuambulia kitu.

(c) Mwaka 2024 enzi za Samia Suluhu Hasan

Wakati wa SSH utaratbu wa hayati Magufuli ulifufuliwa na kutekelezwa kikamilifu. Ma-WEO, ma-DC, ma-DAS, ma-DED, ma-DSO, ma-OCD, ma-RSO, ma-RAS na ma-RC wote walipewa maagizo rasmi ya kusimamia ushind wa wagombea wa CCM. Wapinzani hawakuambulia kitu pia.

Kwa mara nyingine tena, uliotegemewa kuwa uchaguzi haali uligubikwa na uhalifu wa kiuchaguzi wenye sura zifuatazo:
  • Kutoandikisha wapiga kura kwenye ngome za wapinzani,
  • Kuwaengua wagombea wao wengi,
  • Kutowaruhusu mawakala wa vyama vya upinzani na
  • Kutowatangaza wapinzani hata pale walipoonekana kushinda.
Tena wapinzani hawakuambulia kitu.

View attachment 3242833
Jakaya Mrisho Kikwete

V. MAPENDEKEZO YA HATUA ZINAZOPASWA KUCHUKULIWA

Kutokana na yaliyojadiliwa hapo juu, napenda kutoa wito na mapendekezo yafuatayo kwa Serikali, Bunge, Makanisa, Misikiti, Azaki, Wanazuoni wa Vyuo Vikuu na watu wote wenye mapenzi mema kwa Tanzania:

1. Kwa kuwa Tanzania sio dola ya Kiimla, wala Himaya ya Kifamle wala Taifa la Kijeshi, bali ni Dola ambayo ni Jamhuri ya Kikatiba na Kidemokrasia, inayofuata demokrasia ya vyama vingi vya siasa tangu mwaka 1992;

2. Kwa kuwa, sifa kuu ya dola ambayo ni Jamhuri ya Kikatiba na Kidemokrasia ni uchaguzi unaofanyika kwa uhuru, uchaguzi unaofanyika kwa uwazi, uchaguzi unaofanyika kwa haki na uchaguzi unaofanyika kwa ushindani wa hoja za kisera;

3. Kwa kuwa chaguzi za 2019, 2020 na 2024 zilifanyika kwa njia ya udanganyifu ulioratibiwa na matapeli wa kisiasa waliokuwa wanafuata nyayo za Hayati JMP;

4. Kwa kuwa udanganyifu wa kisiasa katika chaguzi za 2019, 2020 na 2024 ulitekelezwa na ma-WEO, ma-DED, ma-DC, ma-DAS, ma-DAS na Wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya sasa;

5. Kwa kuwa udanganyifu wa kisiasa ulifanikiwa kwa sababu ya uwepo wa mifumo mibovu ya kikatiba na kisheria;

6. Kwa kuwa sheria na Katiba ya sasa vinasabaisha kuwepo kwa uwanja wa uchaguzi usio tambarare bali uwanja wenye milima, mabonde na makorongo yanayowakandamiza wagombea wa vyama vya upinzani;

7. Na kwa kuwa serikali inayoingia madarakani kwa njia za udanganyifu inakuwa haina uhalali ikiwa ni sawa na serikali zilizokuwepo enzi wa ukoloni chini ya wazungu na serikali zilizokuwepo enzi za utumwa chini ya waarabu;

8. Hivyo basi, natoa wito kwamba, Serikali na Bunge vinapaswa kuandaa vikao maalum vya Bunge kwa ajili ya kupitisha Mabadiliko ya 15 ya Katiba ya Tanzania (1977) pamoja na marekebisho stahiki ya sheria za uchaguzi ili mambo yafuatayo yawezekane kabla ya uchaguzi mkuu wa 2025:

(a) Sheria na Katiba vikataze ma-WEO, ma-DED, ma-DC, ma-DAS, ma-RAS kusimamia chaguzi.

(b) Sheria na Katiba vitamke kuwa chaguzi zote nchini zitasimamiwa na Watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi iliyo huru.

(c) Tume ya Taifa ya Uchaguzi iondolewe kwapani mwa Rais wa nchi kusudi iweze kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria pekee bila kuyumbishwa na maagizo kutoka Ikulu.

(d) Tume ya Taifa ya Uchaguzi iweke watumishi wake kwenye kila jimbo la uchaguzi kwa mujibu wa sheria.

(e) Katiba ikataze Rais wa nchi aliye madarakani na ambaye ni mgombea kuendelea kutekeleza majukumu yake ya Urais wakati wa maandalizi na uendeshaji wa kampeni za uchaguzi.

(f) Katiba ikataze Rais wa nchi kushika nafasi ya mwenyekiti wa chama cha siasa.

(g) Katiba na sheria zetu viruhusu matokeo ya uchaguzi wa Rais yanayobishaniwa kupingwa mahakamani kisheria.

(h) Sheria na Katiba vipige marufuku tabia ya udanganyifu wa kugeuza mchakato wa uchaguzi kugeuzwa mashindano ya kujaza fomu za wagombea.

(i) Rais Mstaafu wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, anayejua vizuri sana haya "mambo mambo" alisaidie Taifa kuondokana na hii Kero Sugu ya Uhalifu wa Kiuchaguzi, hata kama chama chake cha CCM kitangoka madarakani kwa sababu hiyo. Tanzania ni kubwa kuliko vyama vya siasa.

(j) Wanasheria wa Tanganyika Law Society watusaidie kuandaa miswada ya sheria zinazopaswa kuwasilishwa Bungeni muda wowote kwa ajili ya kutekeleza mapendekezo hapo juu. Tumechelewa sana, hivyo inabidi tukimbie.

VI. MAPINGAMIZI NA MAJIBU YAKE

Mapendekezo yangu hapo juu yanaweza kupingwa na watu kadhaa kwa njia mbalimbali. Baada ya mapingamizi ninayoyatarajia na ambayo nataka kuyajibu kabla hayajaibuka ni kama ifuatavyo:

Pingamizi: “Hoja ni nzuri, utafiti mzuri, ila sio realistic, kwa maana kuwa hayana uhalisia kama tukiangalia muda uliobaki. Tuachane na utopian politics”

Majibu: Naamini kuwa hoja yangu inatekelezeka kwa kuwa kazi ya kuandaa miswada kwa hati ya dharula inawezekana. Bajeti ya kuitisha Bunge maalum kwa ajili ya kupitisha miswada hiyo iko ndani ya uwezo wa serikali. Wabunge bado wapo maana Bunge halijavunjwa.

Pingamizi: “Uchaguzi is a process inayosimamiwa na serikali. Hakuuna siku serikali iliwahi kuahirisha uchaguzi mkuu kwa kuusogeza mbele kwa sababu ya kurekebisha jambo lolote.”

Majibu: Ukweli kwamba huko nyuma hatujawahi kufanya jambo Fulani hakumaanishi kuwa leo au kesho hatuwezi kufanya jambo hilo. Tukumbuke kuwa uchaguzi upo kwa ajili ya watu na sio watu kuwepo kwa ajili ya uchaguzi. Pia, ratiba ya uchaguzi sio msahafu.

Pingamizi: Tundu Lissu na Chadema yake hawana uwezo wala mamlaka ya kusema “no reforms no election” na kauli yake ikatekelezwa na serikali. Kwa hiyo, hakuna mageuzi yoyote na uchaguzi utafanyika.

Majibu: Mawazo hayo yana-personalise hoja yangu. Lissu ameanzisha hoja. Mie nimejielekeza kwenye hoja na kumweka pembeni. Tujiepushe na tatizo hilo la ARGUMENTUM AD HOMINEM. Yaani tutofautishe hoja na mleta hoja. Tufikirie juu ya uwezekano kwamba hoja ni nzuri, serikali itaweza kuipenda, Bunge litaweza kuichagamkia. Let us think positively. Namna hiyo, tutakuwa na mchango ambao sio biased sana.

Nawasilisha.
A veru nice, brave report
 
Bado tuna imani Dr Samia ni Mwislam safi hatapenda kupata vitu visivyo halali hivyo anaweza kuufanyia kazi Ushauri wako Murua kwa manufaa ya Watanzania wote.

Ni jambo linalowezekana njenya hapo ni visingizio tu
Muislamu safi ila amezungukwa na mashetani kila kona kwa kifupi ni mateka wa mfumo...inabidi awe mpole vinginevyo wanaweza kumfanya kitu kibaya
 
Huyo DC wa Longido ni mropokaji tu....ni aina ya viongozi wasiojitambua na kutambua nafasi zao kwa kufurutu ada ya kujiamini juu ya vyeo vyao na ufurahishaji genge kwa maslahi binafsi anayoyajua mwenyewe.....

Mh.Nape Nnauye ni mpenda sifa na mropokaji tu....simshangai kwa maneno hayo aliyotamka.....

Bado huo si ushahidi kwani haikutamka tume ya uchaguzi.....
Huna akili
 
Hoja nzuri, utafiti mzuri, ila sio realistic!.

Uchaguzi is a process, kuna siku Uchaguzi mkuu uliwahi kusogezwa mbele kwassbabu ya kurekebisha jambo lolote?.

TAL anayo the capacity & capability yoyote kusema no reforms no election?.

Hana!.

There will be no reforms, na uchaguzi utafanyika!. TAL na Chadema has no capacity wala capability kuzuia uchaguzi usifanyike!.

Nashauri watu wenye uwezo wa kusaidia, tumsaidie TAL, tuisadie Chadema iachane na Utopian politics and come to face with the real polititcs, TAL wala Chadema hawawezi kuzuia uchaguzi mkuu.
P
Umeandika vitu vingi ila mimi nauliza swali moja tu , wewe kama wakili na kada wa CCM kwanini hamtaki kuwepo na tume huru ya uchaguzi kama ile IEBC ya majirani?
 
Nilitamani CCM iungane na CHADEMA kudai reforms; maana ni dhahiri marekebisho hayo yanafaida zaidi kwa CCM kuipa uhalalali kuliko kung'ang'ania mazoea ambayo yanao ukomo.

4R's zithibitike kivitendo!
Duuuh
 
View attachment 3242826
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akimwapisha Suleiman Abubakar Mombo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Ikulu ya Dar es Salaam , 11 Julai 2024.

I. USULI

Naandika dokezo la kisera, lenye kubeba taarifa za intelijensia ya kisiasa na kijasiriadola, kwa ajili ya kutetea rai ifuatayo:

Kwamba, kwa kuwa uhalifu wa kiuchaguzi unaofanywa na wanasiasa matapeli wakati wa chaguzi zetu umekithiri kwa miaka 15 sasa kutokana na mapungufu yaliyomo kwenye mifumo yetu ya kikatiba na kisheria, basi, tunapaswa kurekebisha ratiba ya uchaguzi mkuu wa 2025, kisha tufanye mageuzi ya kikatiba na kisheria, na hatimaye tufanye uchaguzi mkuu baadaye, na sio kinyume chake.

II. UTANGULIZI


Napendekeza kuanza dokezo hili kwa nukuu muhimu kuhusiana na mtazamo wa Chadema kuhusu Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika 2025.

"Mtu yeyote mwenye akili na macho ya kuona anajua kuwa chaguzi za nchi hii zimekuwa za hovyo sana na kwamba ni za hovyo kwa sababu mfumo mzima wa kiutawala wa nchi hii ni mfumo wa hovyo" -- Tundu lissu, Mwenyekiti CHADEMA.

“Hivyo, hatuzungumzii kususuia uchaguzi, hatutasusia bali tutaenda kuwaambia Watanzania, jumuiya ya kimataifa na walimwengu kwamba kama CCM na Serikali hawako tayari kufanya mabadiliko kwenye mfumo wa uchaguzi ili kuwepo chaguzi huru na haki, uchaguzi wa mwaka huu usifanyike kabisa” -- Tundu lissu, Mwenyekiti CHADEMA.


View attachment 3243758

Huu ndio msimamo ulioibuliwa na Chadema kuhusu kile ambacho baadhi ya vyombo vya Habari, kama vile gazeti la Mwananchi la leo, vinakiita “Njiapanda ya Chadema Kuhusu Uchaguzi Mkuu wa 2025.”

Lakini, napendekeza kwamba, kutokana na uzito wa hoja yenyewe, hasa tunapaswa kuwa tunaongelea “Njiapanda ya Watanzania Kuhusu Uchaguzi Mkuu wa 2025.”

Kwa njia ya swali, “njiapanda” inayoongelewa kwenye vyombo vya habari, ndani na nje ya Chadema pia, inaweza kusomeka hivi:

Je, kwa kuzingatia uhalifu wa kiuchaguzi ambao umekuwa ukifanyika nchini Tanzania tangu 2010 kutokana na uwepo wa milima, mabonde na makorongo yaliyopo kwenye uwanja wa uchaguzi wa vyama vingi nchini Tanzania, tufumbe macho na kuendelea na utekelezaji wa ratiba ya uchaguz mkuu wa Oktoba 2025 au tusogeze ratiba hii mbele kidogo ili uchaguzi huu ufanyike baada ya mageuzi ya kikatiba na kisheria kufanyika ili kusawazisha milima, mabonde na makorongo yaliyopo?

Kutokana na utafiti nilioufanya, dokezo hili linapendekeza kwamba, tunapaswa kusogeza ratiba ya uchaguzi mkuu mbele kidogo ili uchaguzi huu ufanyike baada ya mageuzi ya kikatiba na kisheria kufanyika ili kusawazisha milima, mabonde na makorongo yaliyopo kwenye uwanja wa kisiasa.

III. UTARATIBU WA UTAFITI (METHODOLOJIA)

Katika utafiti wangu nilikusudia kujibu maswali yafuatayo:
  1. Hoja ya Chadema kuhusu changamoto ya uhalifu wa kiuchaguzi nchini Tanzania inasema kitu gani kimaudhui na inao muundo gani kimantiki?
  2. Je, ni kweli kwamba kuna milima, mabonde na makorongo kwenye uwanja wa siasa za uchaguzi wa vyama vingi nchini Tanzania?
  3. Kama jawabu kwa swali la kwanza ni “ndiyo,” milima, mabonde na makorongo haya yamekuwa na madhara gani katika matokeo ya uchaguzi?
  4. Kutokana na majibu ya maswali haya mawili hapo juu, nah atua gani zichukuliwe tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu wa 2025.
Vyanzo vyangu vya taarifa ni kuona matukio kwa macho, kujadiliana na wadau baki walioona matukio kwa macho, na kusoma nyaraka kama vile sheria za Bunge, Katiba ya nchi, kusikiliza video, na makala nyingine kwa ajili ya kupanua maarifa yangu juu ya suala hili.

IV. MATOKEO YA UTAFITI

Hoja ya Chadema


Maneno ya Tundu Lissu kuhusu msimamo wa kisera wa chama chake juu ya umuhimu na ulazima wa kusogeza mbele ratiba ya Uchaguzi Mkuu ujao yamenukuliwa hapo juu.

Kwa maoni yangu, haya ndio maneno yanayotueleza msimamo rasmi wa Chadema. Maneno haya yanaweza kufafanuliwa katika muundo wa hoja rasmi kama ifuatavyo:

1. Kama tungekuwa na mifumo ya kikatiba na kisheria inayowanyima wanasiasa matapeli fursa ya kufanya uhalifu wa kiuchaguzi kwenye michakaato ya chaguzi zetu basi tungekuwa na sababu nzuri ya kushiriki Uchaguzi Mkuu Ujao kabla ya kufanyika kwa mageuzi ya kimfumo.

2. Lakini, uzoefu wetu kutokana na chaguzi zote za 2010, 2015, 2019, 2020 na 2024 unaonyesha kwamba tunayo mifumo ya kikatiba na kisheria inayowapatia wanasiasa matapeli fursa ya kufanya uhalifu wa kiuchaguzi kwenye chaguzi zetu, kiasi kwamba, kwa kipindi cha miaka 15, tumekuwa tukiongozwa na serikali haramu zilizotokana na mbinu haramu.

3. Hivyo, bila kufanya mageuzi ya kuboresha mifumo ya kikatiba na kisheria inayowapatia wanasiasa matapeli fursa ya kufanya uhalifu wa kiuchaguzi kwenye chaguzi zetu hatuwezi kupata serikali halalai iliyotokana na mbinu halali.

4. Kwa mujibu wa kifungu cha 22 katika Sheria ya Makosa ya Jinai (Sura ya 16, Toleo la 2002), kama ilivyotafsiriwa kwenye Kesi ya Abdallah Zombe na wenzake 12 dhidi ya Ephraim Chigumbi na wenzake wawili, Kesi ya Mahakama Kuu Na. 26/2006, kuna njia nne za mtu mmojawapo kushiriki katika kitendo cha uhalifu wa kiuchaguzi, kabla, wakati na baada ya mchakato wa uchaguzi:

(a) Ama kwa mtu huyo kutekeleza uhalifu wa kiuchaguzi kwa kutumia mikono yake mwenyewe; au

(b) kwa mtu huyo kumpa msaada wa aina yoyote mtu baki mwenye nia ya kutenda uhalifu wa kiuchaguzi na hivyo kumsaidia mtu baki kufanikisha utekelezaji wa uhalifu; au

(c) kwa mtu huyo kumpa ushauri mtu baki ili ajenge nia ya kutenda uhalifu wa kiuchaguzi na hivyo kumshawishi mtu baki kufanikisha utekelezaji wa uhalifu; au

(d) kwa mtu huyo kuficha taarifa muhimu zinazohitajika kwa ajili ya ama kuzuia uhalifu wa kiuchaguzi kutendeka au zinazoweza kusaidia kuwatia hatiani watu waliotenda uhalifu wa kiuchaguzi.

5. Hivyo, kama tunao wajibu wa kupigania ujio wa serikali halali iliyotokana na mbinu halali, basi, tunapaswa kupigania ujio wa serikali halali kwa kufanya mambo yafuatayo:

(a) Ama kujizuia na kumshawishi kila mtu baki kujizuia kutekeleza uhalifu wa kiuchaguzi kwa kutumia mikono yake mwenyewe; au

(b) Kujizuia na kuwashawishi watu baki kujizuia kutoa msaada wa aina yoyote kwa mtu mwenye nia ya kutenda uhalifu wa kiuchaguzi na hivyo kumfanya mtu baki asifanikishe utekelezaji wa uhalifu; au

(c) Kujizuia na kuwashawishi watu baki kujizuia kumhimiza mtu yeyote kujenga nia ya kutenda uhalifu wa kiuchaguzi na hivyo kumfanya mtu baki asifikirie kutekeleza uhalifu wa kiuchaguzi; au

(d) Kufichua taarifa muhimu zinazohitajika kwa ajili ya ama kuzuia uhalifu wa kiuchaguzi kutendeka au zinazoweza kusaidia kuwatia hatiani watu waliotenda uhalifu wa kiuchaguzi.

6. Kwa hakika, tunao wajibu wa kisheria na kimaadili wa kupigania ujio wa serikali halali, jambo linalomaanisha kwamba tunao wajibu wa kisheria na kimaadili wa kuzuia ujio wa serikali haramu, kwa sababu zifuatazo:

(a) Kisheria, ibara ya 28(1) ya Katiba ya Tanzania (1977) inampa kila raia “wajibu wa kulinda, kuhifadhi na kudumisha uhuru, mamlaka, ardhi na umoja wa taifa.”

(b) Kimaadili, sheria ya maadili asilia inatupa jukumu la kutekeleza matendo mema na kuzuia matendo maovu, kwa kuhakikisha kwamba, kisiasa, inasimikwa serikali iliyotokana na wapiga kura halali, inayofanya kazi kwa niaba ya watu wote, na yenye kutekeleza majukumu yake kwa faida ya watu wote.

7. Kwa hiyo, raia wa Tanzania tunao wajibu wa kupigania uchaguzi utakaofanikisha ujio wa serikali halali na kupinga uchaguzi utakaofanikisha ujio wa serikali haramu. Hii ndio mantiki ya kaulimbiu isemayo kwamba “Bila Kufanya Mageuzi Kwanza Hakuna Kufanya Uchaguzi,” yaani “No Reforms, No Elections.”

Kwa ujumla, ni wazi kwamba hitimisho hili lisemalo linawaweka njiapanda baadhi ya wanachama wa Chadema wanaotaka kugombea Udiwani, Ubunge na Urais kwa tiketi ya Chadema.

Pia, ni wazi kwamba vyama vingine vinaweza kuendelea na maandalizi ya uchaguzi, maana hii sio sera yao. Na wanachadema wanaopinga sera hii wanayo hiari ya kutafuta jukwaa jingine la kisiasa lisilotambua sera hii ili wapewe fursa ya udhamini wanaoutaka.

Milima, mabonde na makorongo ya kisiasa

Tuhuma kwamba chaguzi zote za 2010, 2015, 2019, 2020 na 2024 unaonyesha kuwa tunayo mifumo ya kikatiba na kisheria inayowapatia wanasiasa matapeli fursa ya kufanya uhalifu wa kiuchaguzi kwenye chaguzi zetu, kiasi kwamba, kwa kipindi cha miaka 15, tumekuwa tukiongozwa na serikali haramu zilizotokana na mbinu haramu, nazi zinao ushahidi wa kuziunga mkono kama ifuatavyo:

(a) Uchaguzi unaosimamiwa na ma-WEO, ma-DED, ma-DC, ma-DAS, na ma-RAS unakosa uhuru, uwazi na ushindani wa kweli, kwa sababu wao ni watumishi wa serikali ya chama tawala, na hivyo kufanya uhalifu wa kiuchaguzi kwa faida ya chama tawala.

(b) Sheria za uchaguzi zinawaruhusu Watumishi wa umma kuvaa kofia za Watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakati w auchaguzi na hivyo kufungua milango ya uhalifu wa kiuchaguzi.

(c) Tume ya Taifa ya Uchaguzi imo kwapani mwa Rais wa nchi, ambaye ndiye huteua wajumbe wake, na hivyo kushindwa kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria pekee kwa sababu ya kuyumbishwa na maagizo kutoka Ikulu.

(d) Tume ya Taifa ya Uchaguzi haina uwezo wa kisheria wala kifedha wa kusimika watumishi wake kwenye kila jimbo la uchaguzi kwa mujibu wa sheria.

(e) Katiba inamruhusu Rais wa nchi aliye madarakani na ambaye ni mgombea kuendelea kutekeleza majukumu yake ya Urais wakati wa kampeni za uchaguzi ilihali yeye ni Amiri Jeshi Mkuu, Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, na Msimamizi Mkuu wa Jeshi la Polisi.

Jambo hili linafungua mianya kwa baadhi ya vyombo vya ulinzi na usalama, kama vile Jeshi la Polisi na TISS, kufanya uhalifu wa kiuchaguzi ili kumsaidia “bosi” wao kushinda.

(f) Katiba inaruhusu Rais wa nchi kushika nafasi ya mwenyekiti wa chama cha siasa, kabla na wakati wa uchaguzi, na hivyo, kufungua mlango wa Rais huyu kuvitumia vyombo vya ulinzi na usalama kwa faida ya chama tawala.

(g) Katiba na sheria zetu vinazuia matokeo ya uchaguzi wa Rais yanayobishaniwa kupingwa mahakamani kisheria. Hivyo, uhalifu wa kiuchaguzi kuhusiana na kura za urais hauwezi kukosolewa kimahakama.

(h) Sheria na Katiba havijapiga marufuku tabia ya uhalifu wa kiuchaguzi wa kugeuza mchakato wa uchaguzi kuwa mashindano ya kujaza fomu za wagombea, jambo ambalo linazalisha wagombea wa kupigiwa “kura za ndio au Hapana,” na hivyo kukiuka kanuni ya uchaguzi wenye ushindani.

Kwa sababu hizi zote, hitimisho la kimantiki ni kwamba ma-WEO, ma-DC, ma-DAS, ma-DED, ma-DSO, ma-OCD, ma-RSO, ma-RAS na ma-RC walioshiriki kwenye uhalifu wa kiuchaguzi ni wanasiasa matapeli waliotenda jinai na kuachiwa watembee huru mitaani kana kwamba hakuna kosa la kisheria wametenda.

Lakini baadaye kidogo watu hawa hawa ndio wanaonekana kusimamia amani na utulivu ("law and order") kwa kuhakikisha kuwa watenda jinai wanaadhibiwa kwa mujibu wa sheria.

Undumila kuwili huu umeleta dharau kubwa kwa serikali tulizo wahi kuwa nazo tangu 2010.

Madhara ya milima, mabonde na makorongo haya

Makorongo haya kwenye uwanja wa siasa za vyama vingi yamekuwa na madhara ya kisiasa tangu zamani, hata kabla ya hayati Magufuli hajakanyaga Ikulu. Mfano:

(a) Mwaka 2010 na 2015 enzi za Kikwete

Katika zama hizi kulikwa na “vikosi kazi” vya kukomboa majimbo yaliyo hatarini.

Kwa kila jimbo ambalo tayari lilithibitika kuanguka mikononi mwa wapinzani, vikosi hivi vilikuwa vinashirikiana na baadhi ya ma-WEO, ma-DC, ma-DAS, ma-DED, ma-DSO, ma-OCD, ma-RSO, ma-RAS na ma-RC kufanya “ukombozi.”

Mfano mmoja ni ule wa Jimbo la Karagwe mwaka 2010. Mgombea wa CCM, Gosbert Blandes Begumisa, alipoteza jimbo hilo kwa tofauti ya kura zipatazo 500. Mgombea wa Chadema alishinda.

Kikosi kazi kikafika Karagwe haraka. Kiongozi wa kikosi kazi kile alikuwa ni Afisa Usalama aliyeitwa “Haule.” Wakachakachua takwimu Blandes akatangazwa mshindi.

Niliambiwa kuwa, Kila kikosi kilikuwa kinapewa magari, fedha taslimu na wakati mwingine helikopta. Na kwa kila jimbo lililokuwa linakombolewa “malipo ya kazi maalumn” yalikuwa fedha ipatayo TZS 100,000,000 (soma milioni mia moja).

Hivyo, wajumbe wa “vikosi kazi” hivi enzi za Kikwete walifanikiwa kujenga majumba, kununua magari, na kuanzisha biashara kubwa. Kwao, wakati wa msimu wa uchaguzi wajibu wao ulikuwa ni kuiba majimbo na ulikuwa ni msimu wa “mavuno” makubwa.

View attachment 3242827
Gosbert Blandes Begumisa, Mbunge wa zamani wa Karagwe

(b) Mwaka 2019 na 2020 enzi za Magufuli

Wakati wa JPM idadi ya “vikosi kazi” iliongezeka, kiasi kwamba uhalifu wa kiuchaguzi ikawa sera rasmi ya kila jimbo la uchaguzi. Ma-WEO, ma-DC, ma-DAS, ma-DED, ma-DSO, ma-OCD, ma-RSO, ma-RAS na ma-RC wote walipewa maagizo rasmi ya kusimamia ushindi wa wagombea wa CCM.

Uliotegemewa kuwa uchaguzi haali uligubikwa na uhalifu wa kiuchaguzi wenye sura zifuatazo:
  • Kutoandikisha wapiga kura kwenye ngome za wapinzani,
  • Kuwaengua wagombea wao wengi,
  • Kutowaruhusu mawakala wa vyama vya upinzani
  • Kuingiza kura feki (premarked ballots) kwenye sanduku la kura, na
  • Kutowatangaza wapinzani hata pale walipoonekana kushinda.
Hatimaye wapinzani hawakuambulia kitu.

(c) Mwaka 2024 enzi za Samia Suluhu Hasan

Wakati wa SSH utaratbu wa hayati Magufuli ulifufuliwa na kutekelezwa kikamilifu. Ma-WEO, ma-DC, ma-DAS, ma-DED, ma-DSO, ma-OCD, ma-RSO, ma-RAS na ma-RC wote walipewa maagizo rasmi ya kusimamia ushind wa wagombea wa CCM. Wapinzani hawakuambulia kitu pia.

Kwa mara nyingine tena, uliotegemewa kuwa uchaguzi haali uligubikwa na uhalifu wa kiuchaguzi wenye sura zifuatazo:
  • Kutoandikisha wapiga kura kwenye ngome za wapinzani,
  • Kuwaengua wagombea wao wengi,
  • Kutowaruhusu mawakala wa vyama vya upinzani
  • Kuingiza kura feki (premarked ballots) kwenye sanduku la kura, na
  • Kutowatangaza wapinzani hata pale walipoonekana kushinda.
Kwa mara nyingine tena wapinzani hawakuambulia kitu.

View attachment 3242833
Jakaya Mrisho Kikwete

Ni katika mazingira haya, kijana Afisa Usalama mmoja ambaye kwa sasa bado anafanya shahada yake ya kwanza ya Sheria katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania alibuni falsafa ya "R" nne, yaani "4Rs philosophy."

Hii ni falsafa yenye kumaanisha "Reconciliation, Resilience, Reforms and Rebuilding." Yaani, "Upatanisho, Ustahimilivu, Ukarabati wa mifumo, na Ujenzi wa Mifumo mipya," kwa maana ya "4U" kwa Kiswahili.

Katika falsafa ya "4R/4U" maneno "Upatanisho" na "Ukarabati wa mifumo" yanahusika zaidi kwenye changamoto za uchaguzi tulizoshuhudia kwa miaka 15 sasa.

Kunahitajika "Upatanisho" kati ya watu waliotangazwa washindi isivyo halali na washindi halali ambao hawakutangazwa na kisha wakadhulumiwa ushindi wao, wakapoyeza fedha zao za kampeni, na wakati mwingine kufulisika kabisa mara tu baada ya dhuluma hizo.

Aidha kunahitajika "ukarabati wa mifumo" ya uchaguzi ili kuziba mianya ya uhalifu wa kiuchaguzi unaofanywa na vyombo vya dola kama vile ma-WEO, ma-DC, Ma-DED, ma-DAS, ma-RAS na ma-RC.

Nje ya hatua hizi za kimakusudi, "falsafa ya 4R" au tuseme "falsafa ya 4U" itabaki ni ukasuku mtupu.

Na bahati mbaya kijana aliyeibuni hana uwezo wa kuidadavua zaidi maana bado ni "denti" na wakubwa zake wanampuuza kwa sababu hiyo.

Na kubwa zaidi ni kwamba wale wakubwa zake walioipokea hawaielewi vema maana wao hawajui vema mwasisi wa wazo alikuwa anafkiria nini.

View attachment 3243761
Albert Chalamia, RC wa Dar es Salaam, rafiki yake Joseph Selasini wa NCCR Mageuzi

V. MAPENDEKEZO YA HATUA ZINAZOPASWA KUCHUKULIWA

Kutokana na yaliyojadiliwa hapo juu, napenda kutoa wito na mapendekezo yafuatayo kwa Serikali, Bunge, Makanisa, Misikiti, Azaki, Wanazuoni wa Vyuo Vikuu na watu wote wenye mapenzi mema kwa Tanzania:

1. Kwa kuwa Tanzania sio dola ya Kiimla, wala Himaya ya Kifamle wala Taifa la Kijeshi, bali ni Dola ambayo ni Jamhuri ya Kikatiba na Kidemokrasia, inayofuata demokrasia ya vyama vingi vya siasa tangu mwaka 1992;

2. Kwa kuwa, sifa kuu ya dola ambayo ni Jamhuri ya Kikatiba na Kidemokrasia ni uchaguzi unaofanyika kwa uhuru, uchaguzi unaofanyika kwa uwazi, uchaguzi unaofanyika kwa haki na uchaguzi unaofanyika kwa ushindani wa hoja za kisera;

3. Kwa kuwa chaguzi za 2019, 2020 na 2024 zilifanyika kwa njia ya udanganyifu ulioratibiwa na matapeli wa kisiasa waliokuwa wanafuata nyayo za Hayati JMP;

4. Kwa kuwa udanganyifu wa kisiasa katika chaguzi za 2019, 2020 na 2024 ulitekelezwa na ma-WEO, ma-DED, ma-DC, ma-DAS, ma-DAS na Wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya sasa;

5. Kwa kuwa udanganyifu wa kisiasa ulifanikiwa kwa sababu ya uwepo wa mifumo mibovu ya kikatiba na kisheria;

6. Kwa kuwa sheria na Katiba ya sasa vinasabaisha kuwepo kwa uwanja wa uchaguzi usio tambarare bali uwanja wenye milima, mabonde na makorongo yanayowakandamiza wagombea wa vyama vya upinzani;

7. Na kwa kuwa serikali inayoingia madarakani kwa njia za udanganyifu inakuwa haina uhalali ikiwa ni sawa na serikali zilizokuwepo enzi wa ukoloni chini ya wazungu na serikali zilizokuwepo enzi za utumwa chini ya waarabu;

8. Hivyo basi, natoa wito kwamba, Serikali na Bunge vinapaswa kuandaa vikao maalum vya Bunge kwa ajili ya kupitisha Mabadiliko ya 15 ya Katiba ya Tanzania (1977) pamoja na marekebisho stahiki ya sheria za uchaguzi ili mambo yafuatayo yawezekane kabla ya uchaguzi mkuu wa 2025:

(a) Sheria na Katiba vikataze ma-WEO, ma-DED, ma-DC, ma-DAS, ma-RAS kusimamia chaguzi.

(b) Sheria na Katiba vitamke kuwa chaguzi zote nchini zitasimamiwa na Watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi iliyo huru.

(c) Tume ya Taifa ya Uchaguzi iondolewe kwapani mwa Rais wa nchi kusudi iweze kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria pekee bila kuyumbishwa na maagizo kutoka Ikulu.

(d) Tume ya Taifa ya Uchaguzi iweke watumishi wake kwenye kila jimbo la uchaguzi kwa mujibu wa sheria.

(e) Katiba ikataze Rais wa nchi aliye madarakani na ambaye ni mgombea kuendelea kutekeleza majukumu yake ya Urais wakati wa maandalizi na uendeshaji wa kampeni za uchaguzi.

(f) Katiba ikataze Rais wa nchi kushika nafasi ya mwenyekiti wa chama cha siasa.

(g) Katiba na sheria zetu viruhusu matokeo ya uchaguzi wa Rais yanayobishaniwa kupingwa mahakamani kisheria.

(h) Sheria na Katiba vipige marufuku tabia ya udanganyifu wa kugeuza mchakato wa uchaguzi kugeuzwa mashindano ya kujaza fomu za wagombea.

(i) Rais Mstaafu wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, anayejua vizuri sana haya "mambo mambo" alisaidie Taifa kuondokana na hii Kero Sugu ya Uhalifu wa Kiuchaguzi, hata kama chama chake cha CCM kitangoka madarakani kwa sababu hiyo. Tanzania ni kubwa kuliko vyama vya siasa.

(j) Wanasheria wa Tanganyika Law Society watusaidie kuandaa miswada ya sheria zinazopaswa kuwasilishwa Bungeni muda wowote kwa ajili ya kutekeleza mapendekezo hapo juu. Washirikiane na Wizara ya Sheria na Katiba. Tumechelewa sana, hivyo inabidi tukimbie.

(k) Padre Charles Kitima akae na muumini wake mmoja Joseph Selasini ili kumkanya na kumwongoza kwenye sala ya toba. Huyu jamaa alikuwa Mwenyekiti wa Baraza la Walei Taifa, chini ya Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC).

Lakini anayoyafanya sasa hivi sio sawa kabisa. Anahujumu jitihada za kuimarisha siasa za vyama vingi nchini Tanzania. Tangu ampindue James Mbati wa NCCR-Mageuzi kazi yake ni kuhakikisha NCCR-Mageuzi wanatekeleza sera za CCM kwa moyo mkunjufu.

Mara nyingi vikao vyake na RC Chalamila vinafanyika pale Kisuma Hotel Magomeni. Kwa sasa Selasini amekuwa kama Lyatonga Mrem katika siku zake za mwisho. Anajikomba CCM hadi inatisha.

Joseph Selasini akiw anaongea na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa

View attachment 3243765
Padre Kitima wa TEC ambaye ni Mlezi wa kiroho wa Joseph Selasini wa NNCR-Mageuzi

VI. MAPINGAMIZI NA MAJIBU YAKE

Mapendekezo yangu hapo juu yanaweza kupingwa na watu kadhaa kwa njia mbalimbali. Baada ya mapingamizi ninayoyatarajia na ambayo nataka kuyajibu kabla hayajaibuka ni kama ifuatavyo:

Pingamizi: “Hoja ni nzuri, utafiti mzuri, ila sio realistic, kwa maana kuwa hayana uhalisia kama tukiangalia muda uliobaki. Tuachane na utopian politics”

Majibu: Naamini kuwa hoja yangu inatekelezeka kwa kuwa kazi ya kuandaa miswada kwa hati ya dharula inawezekana. Bajeti ya kuitisha Bunge maalum kwa ajili ya kupitisha miswada hiyo iko ndani ya uwezo wa serikali. Wabunge bado wapo maana Bunge halijavunjwa.

Pingamizi: “Uchaguzi is a process inayosimamiwa na serikali. Hakuuna siku serikali iliwahi kuahirisha uchaguzi mkuu kwa kuusogeza mbele kwa sababu ya kurekebisha jambo lolote.”

Majibu: Ukweli kwamba huko nyuma hatujawahi kufanya jambo Fulani hakumaanishi kuwa leo au kesho hatuwezi kufanya jambo hilo. Tukumbuke kuwa uchaguzi upo kwa ajili ya watu na sio watu kuwepo kwa ajili ya uchaguzi. Pia, ratiba ya uchaguzi sio msahafu.

Pingamizi: Tundu Lissu na Chadema yake hawana uwezo wala mamlaka ya kusema “no reforms no election” na kauli yake ikatekelezwa na serikali. Kwa hiyo, hakuna mageuzi yoyote na uchaguzi utafanyika.

Majibu: Mawazo hayo yana-personalise hoja yangu. Lissu ameanzisha hoja. Mie nimejielekeza kwenye hoja na kumweka pembeni. Tujiepushe na tatizo hilo la ARGUMENTUM AD HOMINEM. Yaani tutofautishe hoja na mleta hoja. Tufikirie juu ya uwezekano kwamba hoja ni nzuri, serikali itaweza kuipenda, Bunge litaweza kuichagamkia. Let us think positively. Namna hiyo, tutakuwa na mchango ambao sio biased sana.

Pingamizi: Tukifanya mageuzi ya kimfumo kwa ajili ya kuondoa mabonde, milima, makorongo na miiba kwenye uwanja wa siasa, Wapinzani wa Chadema watapata fursa ya kukiangusha chama tawala cha CCM, wakati bila CCM nchi inaweza kuyumbishwa na Chadema kwa sababu ya ukabila wao.

Majibu: Tulipoanzisha mfumo wa vyama vingi tulikubaliana kwamba uchaguzi wa chama kimoja dhidi ya vyama baki ndio mtindo wa maisha yetu ya kisiasa. Hiyo maana yake ni kwamba tulikubali kwamba, kwa kuwa sauti ya wengi ni kama sauti ya Mungu, basi chama kitakachopata kura nyingi ndicho kinapaswa kuongoza nchi.

Chama hicho kinaweza kuwa Chadema au chama kingine. Na kuhusu tuhuma kwamba Chadema inaumwa ugonjwa wa ukabila wa kichaga, tuhuma hiyo sasa umepatiwa tiba.

Ujio wa Timu Lissu umekivua chama cha Chadema gamba la ukabila wa kichaga uliokuwa unaelezwa kwa njia ya maneno kwamba "CHADEMA maana yake ni Chagga Development Manifesto."

Nawasilisha.

View attachment 3243764
James Mbatia wa NCCR Mageuzi aliyepinduliwa na Joseph Selasini
Bara la Afrika ni mahali pekee kabisa hapa duniani ambako kuna Watu na Watawala wengi zaidi ambao hawajastaarabika kabisa katika maisha yao. That's why unaona kwamba sauti za milio ya risasi au milio ya mitutu ya bunduki haikomi kusikika barani Afrika.

The only suitable method of dealing with African Regimes is by means of Guns. Ndio maana unaona kwamba Wazungu wamewekeza pakubwa Sana katika masuala ya kutoa Misaada ya silaha za kupigania Vita ndani ya Ardhi iliyopo katika nchi za bara hili la Afrika.

So you are wasting your time and resources for nothing
 
Back
Top Bottom