Ushauri kwa Wakili Mwabukusi kuelekea maandamano ya kitaifa

Ushauri kwa Wakili Mwabukusi kuelekea maandamano ya kitaifa

Tuwe makini sana na fitina za Slaa imekuwaje ghafla Mwabukusi amekuwa na Bifu na CHADEMA yule Babu sio...
 
Mimi kama Mwanachama wa CHADEMA nitasikiliza viongozi wangu wa Chama na msimamo wa Chama bado na hapo hapo ninaweza kutoa ushauri wangu kuwa tusiwe Chama cha Matukio tujikite kwenye Manifesto yetu.

Kwamba mambo yanakwenda kombo:

"Umeme hamna, mafuta bei kama hivyo, ajira hakuna, wizi wa kura kama kazi, katiba subirini kozi ya miaka 3, kodi lipeni na nyongeza za tozo juu, bambikiziweni kesi, uliweni, nk nk ushauri Kwa chama chako: tujikite kwenye manifesto."

Hii ndugu itakuwa akili au matope?
 
Salaam wana jukwaa, nimekutana na interview ya Wakili Mwabukusi na Maria Sarungi probably kutoka Maria spaces/clubhouse. Cha kushangaza Wakili msomi alikua busy kushambulia wapinzani kuwa ni wawaza ubunge, wapenda vyeo n.k. Hivi kweli hajui struggle za lissu hadi kumwagiwa risasi, hajui mbowe alivyofilisiwa na kufungwa kisa kudai katiba mpya na democracia nchi hii?

Pia kalaumu wapinzani kutosupport maandamano yake akiwaita waoga? Hivi siasa za maandamano wapinzani hawajui? Amesahau maandamano ya Arusha 2011 hadi watu wakauwawa? Amesahau maandamano ya pale Kinondoni hadi kina Mbowe wakahukumiwa kifungo na faini ya 300 Million? Yeye Leo ndio anajifanya ni pro-protest kuliko kina Hajji Duni au lissu?

Sio hivyo tu kaongelea suala la wake za viongozi kulipwa posho!! Yes ni kitu cha ajabu lakini Mwabukusi amekiadress kana kwamba tunalipia tendo la ndoa la viongozi yaani "we are paying for that thing.... we are paying for sex". As if wake za viongozi ni vyombo vya ngono tu. Kauli za namna hii ni unnecessary maana badala ya hoja kuwa bandari utaanza kujibu makelele ya feminists na UWT!!

Ushauri naoweza kumpa Mwabukusi ni kwamba atafute PR manager ajue namna ya kujenga mahusiano na umma. Ana hoja nzuri ya Bandari pamoja na katiba mpya ila lazima ajifunze kuwa na shabaha moja kwa wakati. Ni hatari sana kupambana na CCM, CHADEMA na wanawake kwa wakati mmoja utaondoka kwenye limelight in no time....

Kingine kuna haja ya vyama kama CHADEMA au ACT kupitia TCD kuanzisha chuo cha uongozi, diplomacy na political science ili wanasiasa/wanaharakati wote vijana wapitie huko kabla ya kupewa teuzi/uongozi hasa kwenye vyombo vya uwakilishi au kuongoza taasisi/jumuiya ya vyama.

Hili litasaidia kuondoa mihemko, kuleta utulivu wa akili kwenye mijadala, na kuwa na mawasiliano mazuri na jamii. Sasa mtu kawa maarufu juzi tu kaanza kumshambulia Mbowe out of nowhere! haya mambo hayapendezi especially tuliopo opposition maana tukikwaa madaraka si yatajirudia ya sabaya na Makonda!


View: https://youtu.be/78Gi9mXZWwA?si=YMXW0PFJ-jpAesu9

Ni mada uliyotumia muda vizuri.

Kuna mambo mazuri uliyoongelea, na kuna mengine huko mbali sana na hisia kama zinazomsukuma Wakili kuziwasilisha kama anavyofanya.
Wakili hayupo mbali sana na ukweli, anaposema hayo juu ya vyama vya upinzani, pamoja na kwamba umetoamifano ya akina Mbowe na wengine walivyo dhurika juu ya misimamo yao. Hiyo haiwezi kuondoa sura nyingine inayojitokeza kwa viongozi hao wanapoonekana kugeuka nyuma na kuwa kama zigo la chumvi.
Inaeleweka sana kwa mtu kama wewe kuleta mada hii hapa, kwani ni sampuli nzuri sana ya watu wanaogeuka sura kila mara hali inaporuhusu kuonyesha uhalisia wao ulipo.

Ninakubaliana nawe kuhusu 'moderation' anayotakiwa kuwa nayo Wakili katika kuwasilisha mambo.

Naomba niseme, sijachambua kiundani hoja zako ulizowasilisha humo moja baada ya nyingine. Huu ni muono wangu tu wa jumlajumla baada ya kupitia andiko haraka.
 
Kwamba mambo yanakwenda kombo:

"Umeme hamna, mafuta bei kama hivyo, ajira hakuna, wizi wa kura kama kazi, katiba subirini kozi ya miaka 3, kodi lipeni na nyongeza za tozo juu, bambikiziweni kesi, uliweni, nk nk ushauri Kwa chama chako: tujikite kwenye manifesto."

Hii ndugu itakuwa akili au matope?
Siku Wananchi wakichoka hakuna cha Mwabukusi wala Slaa wenyewe wataingia Mabarabarani so far wako bize na YANGA SIMBA mchana usiku VIGODORO.


Hebu tazama maandamano ya YANGA
Screenshot_20210722-115138.jpg
 
Dunia hiyo haioni huko Cameroon, Rwanda, Uganda, Russia, Ivory coast, n.k. Macho ya dunia yanaona Tanzania tu??
Kizazi hiki Cha maovu hakitogharikishwa Kwa mvua ,moto au upepo ila viongozi madhalimu ndio itakuwa adhabu Yao.
Badala ya maandamano labda National Istighfar day.
 
Mbowe, Lissu tunawapa pole za kupigwa risasi na kufilisiwa lakini hii struggle siyo ya watu binafsi sababu kuna watu wamekufa kabisa kwa ajili ya mapambano ya kuitoa CCM. Je hao utawambia nini familia zao? Viongozi wa sasa hawana mbinu, ari wala mikakati ya kiuhalisia wakuitoa CCM. Wakina Mwakubusi wanajaribu kuratibu maandamano na civil disobedience na hiyo ndio lugha CCM wanaelewa na kuogopa. Hivi nyie mnawezaje kuwa waastarabu kwa watu wanaoiba kura mchana kweupe huko Zanzibar na mkaamini watabadilika na kuwa waastarabu? Eti unaongelea vyuo vya Uongozi, Diplomacy una akili kweli wewe? Unapambana na mhuni wa Mbagala kwa technique za Oysterbay.
Kufa wakati huu kwa ajili ya maandamano ya Chama cha siasa Chenye lengo moja tu la KUSHIKA DOLA ni kuikosea NAFSI YAKO, FAMILIA YAKO NA JAMII KWA UJUMLA!!!!

Hakuna guarantee that CHADEMA will be better off kuliko hawa waliopo....

Tunayaona KENYA na kwingineko.....

Tupinge maovu lakini lazima tutambue CHARITY BEGINS AT HOME
 
Dunia hiyo haioni huko Cameroon, Rwanda, Uganda, Russia, Ivory coast, n.k. Macho ya dunia yanaona Tanzania tu??
Wanajua kuwa Tanzania ikiingia kwenye Vita vya sisi kwa sisi hao wanyama pori waliojaa Serengeti Selou na Burigi wote watachomwa mishikaki.
 
Siku Wananchi wakichoka hakuna cha Mwabukusi wala Slaa wenyewe wataingia Mabarabarani so far wako bize na YANGA SIMBA mchana usiku VIGODORO.


Hebu tazama maandamano ya YANGA
View attachment 2769566

Lissu hasubiri miaka 1000 wananchi watakapochoka. Kuchoka wananchi hakutoki kwa mungu ndugu. Kulikoni kutaka kuvuna mahali bila Kupanda?

Kwani Kenya maandamano Yale ni spontaneous? Mbona leo au Jana hayapo? Kama wako ndiyo msimamo wa chadema huo umekaa kufukuzia ruzuku tu hauna lolote.

Msimamo kama huo lazima kuungwa mkono na ma CCM na WA aina ya kina johnthebaptist
 
Lissu hasubiri miaka 1000 wananchi watakapochoka. Kuchoka wananchi hakutoki kwa mungu ndugu. Kulikoni kutaka kuvuna mahali bila Kupanda?

Kwani Kenya maandamano Yale ni spontaneous? Mbona leo au Jana hayapo? Kama wako ndiyo msimamo wa chadema huo umekaa kufukuzia ruzuku tu hauna lolote.

Msimamo kama huo lazima kuungwa mkono na ma CCM na WA aina ya kina johnthebaptist
Chadema na Ruzuku ni kama Wali na Maharage
 
Kwani Kenya maandamano Yale ni spontaneous? Mbona leo au Jana hayapo? Kama wako ndiyo msimamo wa chadema huo umekaa kufukuzia ruzuku tu hauna lolote.
Nimeishi na kusomea Kenya mindset ya Mtanzania iko tofauti sana na Mkenya mpaka huwa najiuliza Artificial Borders zinawezaje kubadilisha tabia za watu kiasi hicho Mkenya anajitambua zaidi na yuko active kwenye mambo yanayomhusu iwe kwenye kabila lake au jamii yake.

Mtanzania wa Kilimanjaro Arusha Manyara anaweza kufanana kidogo na Mkenya hata CCM wenyewe hupata tabu sana kwenye maeneo hayo.

Mkenya aneweza kuingia barabarani hata wakiwa watano.
 
Wanajua kuwa Tanzania ikiingia kwenye Vita vya sisi kwa sisi hao wanyama pori waliojaa Serengeti Selou na Burigi wote watachomwa mishikaki.
Unataka kusema dunia Ina uchungu sana na rasilimali zilizopo Tanzania kuliko zilizopo DRC na kwingineko??
 
Ndio, hao wazanzibar mbona waliandamana wakafa Mamia walipata nini? Wamekuja kupewa serikali ya Umoja wa kitaifa mezani. Same to CHADEMA kama ni maandamano tulifanya sana ila mchakato wa katiba enzi za JK na Sasa zimepatikana mezani wala sio kwa maandamano.

Nimeongelea uwasilishaji mada kwa wananchi, mbona Mbowe au Mbatia au Zitto wapo composed kwanini mpaka uanze matusi weeee hadi kwa wapinzani wenzako waliokutoa gerezani?

Kwa nchi kama Kenya ni kweli ila waTanzania wengi bado wajinga na hawaamini katika nguvu ya umma. Ndio maana kuna mgao ila wanacheka cheka tu na simba na yanga.

Mbinu waliotumia ni ya diplomatic na ndio imeleta mikutano kuruhusiwa, na sheria mbovu za uchaguzi zinaenda futwa, tume huru inaanza na mchakato wa katiba mpya umekuja. Ukipata tume huru na katiba mpya ni step ya kwanza kuitoa ccm sasa unadhani ccm itatoka kwa NEC au maandamano? Zaidi watamtoa Samia watamweka Mpango na watendelea kutawala miaka 60 mingine kama Zimbabwe!!
Kwa hiyo sababu watu wanakufa hivyo wasiandamane ?

Una miaka mingapi dogo ?
 
Huyo Mzee huenda katumwa na CCM kwa sababu aliwahi kusema kwamba hajarudisha kadi ya uanachama wa CCM.

Hatuwezi kufanya siasa kwa hisia. Ndiyo maana CCM wanatutaka tuwe hivyo. Kama yeye anaweza kuwa katumwa kwanini usiwe na wewe pia hapo ulipo?
 
Back
Top Bottom