Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

sio wewe tu... kupoteza nafasi mzee alafu kuja kuipata tena mziki...
God bless him,
Nimefurahi sana kuona Kaveli amekamilisha,
manake alivyokuwa anachelewa na izzo analalamika basi roho ilikuwa inanidunda kwa kuhofia kuipoteza nafasi,
Mungu mkubwa amekamilisha,
and now nina amani
 
mimi najua ulaya marekani hata asia wapo wa tz wengi mno lakini hata kutuonesha njia kwa kutafuta taasisi zitakazo saidia wandugu bongo, kutusaidia wale tunaopenda kuandika maandiko ya miradi na hii ni kutuunganisha na taasisi husika kama kuna ugumu tujadiliane katika baadhi ya mambo ikiwezekana iundwe taasisi na kusajiliwa kisheria ili wanachama wake waweze kutambulika na kuwa rahisi hata kuwapata pale watendapo mambo kinyume na taratibu... hapa ni kufanya mambo yaende kwa kurasimishwa na sio kienyeji ndio maaana naisi mliopo majuu mnakuwa na hofu... na hata katika hili la kuhost kwanini kusisajiliwe taasisi ya kulink tz na wakina [HASHTAG]#izzo[/HASHTAG] ili mlio abroad mjue mnafanya kazi na watu wa aina gani

ni mawazo tu wadau... dunia inabadilika sio mmoja mmoja tena ni kushirikiana, tuelekee kale umoja ni nguvu...
 

Mkuu Kupata host mbona ni easy tu jaribu kujiunga na hii site Help Exchange: free volunteer work exchange abroad Australia New Zealand Canada Europe utajiunga na account ya bure then baadae uta upgrade account yako kuwa premium kwa gharama ya kama Tsh 50K(20€)
Ukiwa na premium account utaweza kuwasiliana na hosts pamoja na kusoma reviews za hao hosts.

Kwenye hiyo site Australia kuna zaidi ya hosts 5K. Naamini itakuwa kazi rahisi kwako kupata host Australia kuliko Bashite kuonesha vyeti.

So far nimeona hii site ni bora kuliko Meet and Stay with Locals All Over the World ni mtazamo wangu lakini. Ningependekeza na wale wote ambao tunataka kufanya mission 1 kutoka kwa mkuu izzo ingekuwa vema tutafute hosts tufanye kweli... muda mzuri wa kuingia Malta ni summer time coz kunakuwa na tourists wengi so I hope kutakuwa na deiwaka za kutosha kwa hiyo tunaweza kutumia hosts wetu kama work placement.

I wish you Goodluck!
#Malengo#TukutaneMalta
 
mkuu Mimi Nina bahati sana ya kupata wapenzi wa kizungu na nimeshawalia pesa zao japo sio nyingi ila 200$ kawaida sana tatizo linakuja nikimuomba pesa nyingi ya kwenda ndo ananipiga calendar

ninao wawili mmoja yupo Tennessee mwingine yupo Michigan ni nurse Ila huyu wa Michigan ndo amenishikilia kupita kiasi mwingine wa tatu niliamua kumuacha sababu ya wivu huyu yupo Virginia ana wivu hadi kero me mwenyewe kapuku tu sina pesa ya kufika huko USA

Sasa naomba msaada nifanye nini ili nifanikiwe kufika huko Nipitie njia ipi ipi nijilipue huko USA
 
Unawapatia wap
 
Mkuu tunasubir mrejesho wako kutoka ubaloz wa Italy

Nashukuru chief
nimefika isipokua hawaruhusu mtu kuingia mpaka ndani, pana mlizi ana information zote. siku ya kuingia ndani ni kwenda kuchukua visa tu! siku za kuchukua visa ni jumatatu, ijumaa na jumatano. wamenipatia website ambayo ina form za kudownload na kila kitu, so vitu vyako vyote unavifanyia huko, then wamenipa na e-mail yao ukimaliza unawatumia huko. lakini pia ukikwama kuna namba ya maulizo unawapigia wanakusaidia (amesisitiza simu zikipigwa basi yawe mambo ya msingi)

Website; www.ambdaressalaam.esteri.it
E-mail; dar.visti@esteri.it
Tel 0222115935-6
 
[emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji120]
 

Mkuu ubarikiwe sana. Ngoja ni review nitatoa mrejesho.
 
Mkuu Kaveli nimekusoma nimekupata and your write ups are very very interesting my bro.

I can deduce strong ambitiousness and potentiality in you that should never be wasted in whatever case.

I do salute this kinda spirit ambayo inaamsha mzuka hata wa mtu aliyekuwa kajisahau na kumkumbusha he has to keep his plans alive. Now what I can insist to you, is to keep fucused on your plans and never mind the distractions for the sake Of your endeavors.

Kihusu kusaka za madafu kupitia kilimo cha vitunguu hata usiwaze mkuu karibu sana, tutafanya hata fundraising ya kiujanja ujanja kama alivyofanya baba jeska kwenye maafa ya tetemeko na kwenda kujenga uwanja wa bombardier kijijini kwake chato...lol.
 
Wakuu Ni vyema tunaopewa ushauri tuutumie ikiwezekana haraka mafanikio yake yaonekane kwa haraka ili wanaotushauri wapate moyo na wajue watu wapo serious.
Swala la kuzingatia hili mkuu ila kwa sababu uzii utaendelea kuwepo swala la mrejesho haliitaji haraka sana.
 

Mkuu, asee nimekuwa nikiskia Australia ni ngumu sana kuingia kwa raia wa kigeni hasa kutoka kwenye hizi nchi zetu za giza sasa kupitia hili bandiko lako ndio nimepata sababu.

Kwanza imavyonekama kuingia kama raia tu job seeker ni ngumu hatari na kuingia kama mwanafunzi ndio hivyo INA hitaji uwe na mpunga wa maana sana kwa account yako kana kwamba ni ngumu kwa mbongo mwenye hiyo hela kushawishika kwenda kumake life pande hiyo...!!

Nataka kufahamu vipi kwa anaejitoa kutaka kuingia huko kama asylum seeker, kuna resistance gan!?
 
Mkuu tupo vijana wako hata wakija zaidi ya kumi uwezo wa kuwahost upo pls tuunganishee tuu kwa hilo usijali nipe hata kesho nipo tayari kufanya kazi hiyoo
 
MAXCENCE MELLO/INVISIBLE

NGOJA NIKURAHISISHIE KAZI KUHUSU JUKWAA LA DIASPORA (WENGINE MNAWEZA KUMTUMIA PM NA HII POST ILI ATUWEKEE SUBFORUM YETU)


Ndani yake kutakuwa na subforums 3 hivi

1. LIVING/MOVING ABROAD (sasa hiumu ndio kila mtu ataangalia wapi anaishi au anataka kwenda kujilipua etc then ataanzisha thread yake) at later stage tutakuwa na sticky ili maswali yasijirudie rudie

AUSTRALIA & NEW ZELAND

CANADA

EUROPE

FAR EAST & ASIA

MIDDLE EAST

USA

LATIN AMERICA

2. WORKING ABROAD
Hii itakuwa ni self explanatory na kutakuwa na sticky threads mbali mbali za profession hivyo hakutokuwa na haja ya kuchanganya maswali ya kazi sticky zitakuwepo za kazi za Accountants, Electricians, Information Technology, Nurses, Doctors, and other Medical/Healthcare occupations, Plumbers, Police, Teaching, Trucking Electrician

Pia kutakuwa na threads za Job offers

na thread maalum kwa watafutaji kazi yaani jobs wanted

3. THE LOUNGE GENERAL DISCUSSIONS
Hapa kutakuwa na threads za kinachoendelea ulipo kuanzia issue za kuoa ili kupata makaratasi, kesi za kuacha mke, kuficha pesa,meet up, connections za wana diaspora na bila kusahau kutakuwa na special thread ya KURUDI NYUMBANI NA CHALLENGES, diaspora wanauza bidhaa zao, nk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…