Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Wangefanya hivyo.siku nyingi ningekuwa sauzi.walinipa form zao zile.zina maswali hatari.zikazichoma moto.
Mkuu kupata passport sio kazi kihivyo. Mimi niliwaambia naenda kuwatafuta watoto wa bro wangu hapo nchi jirani kwa M7 wakaniambia kalete living certificates za secondary ili wahakiki background yangu na yale niliyoojiwa na kujaza ktk form. Niliwapatia hizo doc kisha wakanihoji kidogo nikapata pass yangu ndani ya siku chache just 3 - 5 days. Sikutoa rushwa wala nini. Kutoa rushwa ni mapenzi yako tu na mazoea mabaya.
 
Kuna huyu jamaa naye ni mbogo yupo Dar anadai ni agents wa Canada na ulaya. Garama zake visa ya Canada ni 2500usd na ulaya ni 2000 usd.
Weka contact zake na km kuna mtu anamjua vizuri amuelezee km alivyofanya izzo ili watu wasije kutapeliwa.
 
Huyo mkuu ni agent wa visa pamoja na host. Anakutafutia visa then anakulink na mtu aliyepo nchi husika. ...sijafika ofisini kwake lkn
Yupo wapi(anapatikana wapi) ili tumuibukie ofisini kwake au km vipi tuwekee contacts zake.
 
Yah Host ni mbaya sana kama utakuwa ujafanikiwa kabla ya miezi 2 so utabaki kukimbizana na Police ukikamatwa kwaza ni jela ukitoka tu ndege ya kwaza kuja Africa na ww utakuwapo ndani yake Str8 kwa JPM empire

Kuhusu nimejuaje sidhani kama hapa naweza kwambia ila nimekwambia kama unataka utaniambia then nitakutumia

Kuhusu Agent wa kazi za mikono Tanganyika hakuna wapo wa Visa tu kwani ni ukweli usiofichika katika watu 10 waliokuwa na ndoto za kwenda nje kufanya kazi kwa Tanganyika ni 1 au 2 tu lakini toka Mr JPM kuingia na ajira kuwa ni swala la kufikirika ndio mwamko wa watu kukimbia Tanganyika umekuwa ni mkubwa ni juzi tu walikuwa wanaoitwa wabeba box walikuwa wanaonekana vibwengo na kukashifiwa sana lakini leo wao ndio wanaonekana kama wameteka kijiji

Kuhusu Agent msaada wangu unaishia pale niliposema kuwa mm nitakushauri bt siwezi kuingia in 4 Kwenye jambo hili am sorry 4 that dude
Bro naomba uniambie ulijuaje nami kesho au siku nyingine niweze kupima tapeli na Wa kweli mkuu. That's knowledge boss
 
Yah Host ni mbaya sana kama utakuwa ujafanikiwa kabla ya miezi 2 so utabaki kukimbizana na Police ukikamatwa kwaza ni jela ukitoka tu ndege ya kwaza kuja Africa na ww utakuwapo ndani yake Str8 kwa JPM empire

Kuhusu nimejuaje sidhani kama hapa naweza kwambia ila nimekwambia kama unataka utaniambia then nitakutumia

Kuhusu Agent wa kazi za mikono Tanganyika hakuna wapo wa Visa tu kwani ni ukweli usiofichika katika watu 10 waliokuwa na ndoto za kwenda nje kufanya kazi kwa Tanganyika ni 1 au 2 tu lakini toka Mr JPM kuingia na ajira kuwa ni swala la kufikirika ndio mwamko wa watu kukimbia Tanganyika umekuwa ni mkubwa ni juzi tu walikuwa wanaoitwa wabeba box walikuwa wanaonekana vibwengo na kukashifiwa sana lakini leo wao ndio wanaonekana kama wameteka kijiji

Kuhusu Agent msaada wangu unaishia pale niliposema kuwa mm nitakushauri bt siwezi kuingia in 4 Kwenye jambo hili am sorry 4 that dude
Tunaomba utusaidie (ushauri) njia nyepesi tunayoweza tumia kufika Malta au nchi yoyote kuhamia. Na pili hivi hizi visa free countries zilizopo America na Europe utaratibu wake unakuaje kuingia. Unakata tuu tiketi na kwenda au kuna process inabidi ufuate?
 
Tunaomba utusaidie (ushauri) njia nyepesi tunayoweza tumia kufika Malta au nchi yoyote kuhamia. Na pili hivi hizi visa free countries zilizopo America na Europe utaratibu wake unakuaje kuingia. Unakata tuu tiketi na kwenda au kuna process inabidi ufuate?
Nimesha zungumza sana juu ya Malta so nilichokuwa nategemea ni maswali kutoka kwenu

Kuhusu free visa za EU na US kwa sasa mambo si mazuri zimesitishwa kwa muda kwani mamlaka nchini US inasema kuwa EU ndio limekuwa pango la magaidi kuingia US so wanadplomasia wanashugulikia ikishindikana nayo ulaya kupitia Bunge la Ulaya nao watapiga marufuku kwa free visa kwa raia wa US kuingia EU

Free visa ni kama vile ww unapokwenda S.A au Kenya
 
Maoni yangu kama diaspora wa zaidi ya miaka 10 (Nitazungumzia Ulaya zaidi)

Kuna njia nyingi za kwenda nje lakini njia kuu za kwenda ni njia ya masomo au ndoa.

(i)Masomo

Unatakiwa kutafuta chuo katika nchi uliyoichagua na kuomba udahili katika chuo hicho. Michakato ya kuomba udahili, ada ya masomo na viambatanisho vinavyotakiwa vipo wazi katika wavuti za vyuo vyote. Tumia muda wako kutafiti kama unakidhi vigezo. Nchi nyingi za Ulaya zina wavuti zenye 'database' ya vyuo vyote na kozi zinazopatikana. Nitaorodhesha hapa chini wavuti za kuanza kupitia kama unataka kuja kusoma nje.

Ukifanikiwa kupata udahili utatumiwa 'documents' zote muhimu na chuo kwa ajili ya kuombea 'residence permit'.
Ili kupata kupata 'residence permit', lazima ulipe ada ya masomo na kuwa ni kiasi cha fedha kinachotakiwa na nchi husika kuthibitisha kuwa utaweza kujikimu ukiwa huko. Nchi nyingi za Ulaya hazitoi 'residence permit' kwa masomo chini ya shahada ya kwanza.

Njia hii ni ghali na unahitaji kuwa na uwezo mkubwa maana ada za vyuo vya nje ni kubwa sana na gharama za kuishi ni kubwa mno. Njia mbadala ya hii ni kupata 'scholarship'. Nchi nyingi za Ulaya hazitoi 'residence permit' kwa masomo chini ya shahada ya kwanza.

Kwa shahada ya kwanza, kupata 'scholarship' ni ngumu. Sijawahi kusikia nchi yoyote ya Ulaya ama Marekani wanayotoa 'scholarship' kwa shahada ya kwanza.
Kwa shahada ya uzamili na uzamivu kuna 'scholarships' nyingi, unaweza kupitia wavuti za vyuo mbalimbali kuona ' scholarship' zinazopatikana. Kukumbushana tu, ' scholarship' zinapatikana kwa watu wenye madaraja ya juu ya ufaulu.

Kuhusu mitihani ya kiingereza, karibia vyuo vya nchi zote za Ulaya na Marekani Kaskazini vinahitaji ufaulu mitihani hii kwa alama wanazotaka wao. Mitihani maarufu ya kukidhi vigezo hivi ni TOEFL (TOEFL: Home) na IELTS (IELTS - IELTS Home of the IELTS English Language Test). Angalia wavuti zao kujua gharama na sehemu unazoweza kufanya kwa Tanzania.

Ifuatayo ni orodha ya wavuti zitazoweza kukusaidia kuanza michakato ya kusoma kwa nchi mbalimbali. Utaona vyuo, kozi zinazotolewa na 'scholarships' kama zipo.
Austria (http://www.studienwahl.at/Content.Node/homepage.en.php?fl=en)
Ubelgiji (Home | WBCAMPUS / BELGIUM)
Denmark (Study in Denmark)
Finland (Study in Finland)
Ujerumani (German Academic Exchange Service (DAAD) - DAAD - Deutscher Akademischer Austauschdienst)
Ufaransa (Study in France > CampusFrance)
Uholanzi (Study in Holland)
Ireland (Study in Ireland - Education in Ireland)
Sweden (Study in Sweden)
Uingereza (Study UK | British Council)
Malta (Studying In Malta - Schools, Courses, Education | Study In Malta)
Norway (StudyinNorway / Home - Study in Norway)
Uswisi (swissuniversities - Studying in Switzerland)
Canada (Universities Canada Study Information)
Marekani (Hapa utatumia google kuangalia vyuo kwenye jimbo unalopanga kwenda)
New Zealand (Study Abroad | New Zealand Education | Study in New Zealand)
Australia (Study In Australia)

Tafadhali, tumia muda wako kutafuta na kutafiti vyuo mbalimbali. Hamna dalali wala wakala anayeweza kusaidia mtu kupata 'residence permit'. Uombaji wa 'residence permit/viza' hufanywa na muombaji mwenyewe. Jiepushe na matapeli wanaodai wanaweza kukusaidia kwenda nje ama kupata viza, kila kitu unachohitaji kipo mtandaoni.

(ii) Ndoa
Unaweza kupata 'residence permit' ya UlayaMarekani kwa kufunga ndoa na raia wa nchi husika ama mkaazi yeyote mwenye vibali halali vya kuishi nchi hiyo. Watanzania wengi ninaowajua waliotumia njia hii walikutana na Wazungu wakati Wazungu wakiwa Tanzania hasa kwa ajili ya utalii. Watu wengi wa Arusha na Zanzibar huwa wanachomoka kwa njia hii.

Watanzania wengine huja baada ya kuoa/kuolewa na Watanzania wenzao ambao tayari wana vibali vya kuishi.

Kuhusu kutumia mitandao kutafuta mwenza, unaweza kufanikiwa ila ni kamari. Sina uzoefu na njia ya mtandao, wenye uzoefu wanaweza kuja kujazia.

Nitaendelea kuelezea uzoefu wangu kwenye 'posts' nyingine zitakazofuatia.

USIMPE MTU YEYOTE PESA YAKO AKIDAI KUWA ATAKUSAIDIA KWENDA ULAYA / MAREKANI. HAMNA UWEZEKANO WA MTU YEYOTE KUSHAWISHI UBALOZI WAKUPATIE VIZA , VIZA INAOMBWA NA MUHUSIKA MWENYEWE NA KUNA MAHOJIANO KABLA YA KUPEWA!!!!!
 
Nmepata mchongo wa kwenda japan na mwenyeji wangu kaniambia fursa za kazi kibao na nkifika natafutiwa mwanamke tunafunga ndoa napata kikaratas maisha mengine yataendela. Kwa mwenye uzoefu na inchi hiyo ningependa kujua mengi
kwanini usimuulize huyo mwenyeji wako au naye hana ufahamu na hiyo nchi.
 
Kuhusu kwenda nje na viza ya kutalii halafu usirudi nyumbani

Viza ya kutalii ni viza ya muda mfupi, mara nyingi huwa kati ya miezi 3 hadi 6. Viza hii haikuruhusu kufanya kazi wala kusoma. Unaweza kupata viza hii kwa kuwa na uwezo wa kifedha au kwa kupata mwaliko wa mkaazi halali wa nchi unayotaka kwenda.

Kuna mtindo wa watu kutumia viza hii kama njia ya kuingilia nchi za Ulaya na Marekani halafu baadae 'kujilipua' ama kuishi chini kwa chini.

Zoezi zima la kujilipua polisi na kuomba ukimbizi ni suala la bahati nasibu ambayo kwa asilimia kubwa huwa watu wanarudishwa nyumbani na kupigwa marufuku ya muda mrefu ya kutembelea nchi hiyo. Kutokana na wimbi la wakimbizi la miaka ya karibuni, imekuwa ni vigumu kupata hifadhi kama mkimbizi. Unaweza kuwa Msomali lakini ukanyimwa hifadhi sababu mji ulipotoka Somalia hakuna vita. Mchakato huu huwa unachukua miaka mingi na katika kipindi hiki nchi nyingi haziruhusu ufanye kazi.

Kuishi chini kwa chini. Hapa watu huwa wanaishi nchi fulani bila vibali (hawana makaratasi). Kutokana na nchi zote zilizoendelea kuwa na namba za utambulisho, huwezi kupata ajira rasmi wala kusafiri ukiwa katika hali hii. Unaweza ukapata kazi (maarufu kama black job) lakini mwajiri wako atakulipa mshahara mdogo mno ambao haukidhi mahitaji ya kila siku. Ukifanya kazi hizi, hulipi kodi, huchangii pensheni wala huna haki zozote kama wafanyakazi wengine halali. Watu wa aina hii ndio mara nyingi inapita miaka mingi bila kurudi nyumbani maana hawawezi kusafiri.

Katika kipindi hiki cha miezi 3 au 6 ya viza ya utalii, unaweza ukabahatika kupata mwanamke akakusaidia kupata makaratasi kwa njia ya ndoa. Pia, ni ngumu kwa mwajiri yeyote kukuajiri kama ukiwa na viza ya utalii, usitegemee kupata kazi ukiwa na viza hii.

Viza ya utalii ya Schengen

Hii viza inakuwezesha kutembelea nchi yoyote kati ya nchi wanachama wa makubaliano hayo. Viza hii haikuruhusu kufanya kazi wala kusoma. Unaweza ukaangalia orodha ya nchi za Schengen hapa Schengen Area Countries List - Schengen Zone
 
Nimesha zungumza sana juu ya Malta so nilichokuwa nategemea ni maswali kutoka kwenu

Kuhusu free visa za EU na US kwa sasa mambo si mazuri zimesitishwa kwa muda kwani mamlaka nchini US inasema kuwa EU ndio limekuwa pango la magaidi kuingia US so wanadplomasia wanashugulikia ikishindikana nayo ulaya kupitia Bunge la Ulaya nao watapiga marufuku kwa free visa kwa raia wa US kuingia EU

Free visa ni kama vile ww unapokwenda S.A au Kenya
Sasa brother hapo kwenye kuingia Malta hapo, maana nimetafuta kila possible way napaona kugumu. Mpaka najihisi sina swali kwakweli.
 
  • Thanks
Reactions: Qj_
Kuhusu kwenda nje na viza ya kutalii halafu usirudi nyumbani

Viza ya kutalii ni viza ya muda mfupi, mara nyingi huwa kati ya miezi 3 hadi 6. Viza hii haikuruhusu kufanya kazi wala kusoma. Unaweza kupata viza hii kwa kuwa na uwezo wa kifedha au kwa kupata mwaliko wa mkaazi halali wa nchi unayotaka kwenda.

Kuna mtindo wa watu kutumia viza hii kama njia ya kuingilia nchi za Ulaya na Marekani halafu baadae 'kujilipua' ama kuishi chini kwa chini.

Zoezi zima la kujilipua polisi na kuomba ukimbizi ni suala la bahati nasibu ambayo kwa asilimia kubwa huwa watu wanarudishwa nyumbani na kupigwa marufuku ya muda mrefu ya kutembelea nchi hiyo. Kutokana na wimbi la wakimbizi la miaka ya karibuni, imekuwa ni vigumu kupata hifadhi kama mkimbizi. Unaweza kuwa Msomali lakini ukanyimwa hifadhi sababu mji ulipotoka Somalia hakuna vita. Mchakato huu huwa unachukua miaka mingi na katika kipindi hiki nchi nyingi haziruhusu ufanye kazi.

Kuishi chini kwa chini. Hapa watu huwa wanaishi nchi fulani bila vibali (hawana makaratasi). Kutokana na nchi zote zilizoendelea kuwa na namba za utambulisho, huwezi kupata ajira rasmi wala kusafiri ukiwa katika hali hii. Unaweza ukapata kazi (maarufu kama black job) lakini mwajiri wako atakulipa mshahara mdogo mno ambao haukidhi mahitaji ya kila siku. Ukifanya kazi hizi, hulipi kodi, huchangii pensheni wala huna haki zozote kama wafanyakazi wengine halali. Watu wa aina hii ndio mara nyingi inapita miaka mingi bila kurudi nyumbani maana hawawezi kusafiri.

Katika kipindi hiki cha miezi 3 au 6 ya viza ya utalii, unaweza ukabahatika kupata mwanamke akakusaidia kupata makaratasi kwa njia ya ndoa. Pia, ni ngumu kwa mwajiri yeyote kukuajiri kama ukiwa na viza ya utalii, usitegemee kupata kazi ukiwa na viza hii.

Viza ya utalii ya Schengen

Hii viza inakuwezesha kutembelea nchi yoyote kati ya nchi wanachama wa makubaliano hayo. Viza hii haikuruhusu kufanya kazi wala kusoma. Unaweza ukaangalia orodha ya nchi za Schengen hapa Schengen Area Countries List - Schengen Zone
Bro nyie mlio njee tayari mnatusaidia vipi? Maana km vile njia zote msala
 
Nchi ipi ya kwenda ipi si ya kwenda

Tofauti ya fikra za watu kuwa Ulaya ni Ulaya, kuna nchi za Ulaya ambazo hazifai kwenda kama unatafuta maisha. Jiepushe na nchi za Ulaya mashariki kama Czech, Estonia, Hungary, Latvia, Lithuania, Poland, Slovakia, Slovenia, Bulgaria, Croatia, Romania, Ukraine na Urusi. Nchi hizi hamna kazi na mishahara yake ni midogo mno ambayo haitaweza kukusaidia kwa lolote. Watu wengi wa nchi hizi huwa wanakimbilia nchi za Ulaya magharibi. Pia ubaguzi umekithiri sana Ulaya mashariki.

Nchi nyingine za kujiepusha nazo ni nchi ambazo zilikuwa na uchumi mkubwa lakini zimeanguka kiuchumi. Nchi hizi ni Ugiriki, Italia, Ureno na Hispania. Waafrika wengi katika nchi hizi ni wauza unga au wamachinga. Raia wa nchi hizo pia wanakimbilia nchi nyingine za Ulaya.

Pia, ukienda nchi wasiyotumia Kiingereza jiepushe na kuishi miji midogo. Kwa wale wanaotaka kuja nchi za Nordic (Sweden, Denmark, Finland, Norway na Iceland) mjiepushe na kwenda kuishi miji midogo mbali na miji mikuu. Ukiishi mji mkubwa angalau unaweza ukasukuma maisha kwa Kiingereza na kazi pia zipo. Ukienda vijijini huko hamna kazi na kuishi bila kuongea lugha ya hapo ni ngumu. Vijijini pia ubaguzi upo kwa kiwango cha juu ukilinganisha na mijini.
 
Nimefanya utafiti ni kwamba huyu jamaa ndio alikuwa ni Agent lakin mtu wa mwisho kumpeleka ilikuwa mwaka 2015 na aliyempeleka anaitwa Hassan Baswale ambae alimfanyia mpango wa kwenda Spain bt jamaa hakufanikiwa kuingia alirudishwa airport palepale so toka mwaka huo jamaa ajapeleka mtu tena na leseni yake inaonyesha ameshapeleka watu 136 ni watu 56 tu ndo walifanikiwa kuingia wengi walirudishwa aidha airport au walikamatwa na kurudishwa na jamaa anamtandao Uturuki si nchi za ulaya sana na kumbuka Uturuki si mwanachama wa EU lakini pia kuna ukaribu sana na huyu jamaa na mtu aliyeanzisha thread hapa ambae anatumia id hizi


Britanicca ,DR RWEYENDERA, Katelelo so uamuzi ni wako Good luck kwa ushaidi au kujua kama ninachokisema ninauhakika nacho ukitaka ninaweza kukupatia kama utaiji coz siwez kuweka hapa jukwaani
Duh! Thumbs up, you are the best.
Huyu Britanicca nadhani kuna watu hawa hamu hata ya kumsikia. Asante kwa yote unayoshare na waTz wenzako. Bless you
 
Nimesha zungumza sana juu ya Malta so nilichokuwa nategemea ni maswali kutoka kwenu

Kuhusu free visa za EU na US kwa sasa mambo si mazuri zimesitishwa kwa muda kwani mamlaka nchini US inasema kuwa EU ndio limekuwa pango la magaidi kuingia US so wanadplomasia wanashugulikia ikishindikana nayo ulaya kupitia Bunge la Ulaya nao watapiga marufuku kwa free visa kwa raia wa US kuingia EU

Free visa ni kama vile ww unapokwenda S.A au Kenya
Mkuu US ilikataa free visa kwa baadhi ya nchi tu za EU ikiwemo Romania na Poland.... Sababu kuu ni hali ya uchumi kwa nchi hizo....
 
Back
Top Bottom