Ushauri: Nataka kuacha kula wanga kwa mwaka mzima

Ushauri: Nataka kuacha kula wanga kwa mwaka mzima

Niko wiki ya nne sasa bila ya kutumia chakula chochote cha wanga. Naomba nikupatie ratiba yangu ya chakula kwa siku.
Naamka saa 11, napata maji ya uvuguvugu yaliyotiwa ndimu. Napiga pushup kidogo kisha najiandaa kwenda ofcn.
Kwa kuwa nina usafiri wangu, mrs anakuwa ananifungashia juice ya kutosha anayotengeneza mwenyewe. Juice hii inakuwa ya mchanganyiko wa matunda mbalimbali na mboga mboga kama karoti, nyanya, parachichi, embe, apple, nk. Epuka matunda yanayotoka South Africa, mengi ni GMO.
Nakunywa juice hiyo around saa 2 asb na saa 4 asb.
Saa tano napata dafu.
Saa saba napata mboga za majani na matunda kama ndizi na parachichi.
Saa tisa napata tena juice (huwa nabeba ya kutosha na nahifadhi kwenye friji ofcn.
Naweza pia kuwa na snacks kama karanga au tende
Nikirudi nyumbani saa kumi na mbili napata juice au saladi ya mchanganyiko wa matunda na mboga mboga.
Wakati mwingine hiyo inakuwa imetosha kabisa na nakuwa sihitaji kupata kitu kingine zaidi ya chai ya mchanganyiko wa viungo iliyotiwa asali.
Siku nyingine naweza kula maboga yaliyochemshwa pamoja na vitu kama njugu mawe, choroko au kunde.
By the way mimi nimeamua kupunguza sana matumizi ya nyama ili kupunguza asidi mwilini.
Ongeza na samaki wa kuchoma, nyama choma
 
Mkuu jaribu kula miwa ya kukaanga & maji ya kupondwapondwa kwenye kinu
 
Huwezi pungua kupitia kuacha kula peke yake.

Naona wadau wengi wanasema wameacha wanga na mwili umepungua.

Mwili unapungua kwa mawili ama ufanyiwe operation au ufanye mazoezi. Intentional starvation itabackfire na ulcers na magonjwa mengine.

Halafu mazoezi ni ishu ndogo sana. Yaani wewe unayeruka kichura chura mara tano kila siku you are better off kuliko mimi ninayekesha nacheza PS.
Mawatu yanjitesa hadi naamua kuyashangaa tu badala ya kuyaonea huruma [emoji28]

Ama kweli akili nyingi huondoa maarifa [emoji38]
 
Kwani kitambi kinauma?kwa Nini mateso yote hayo?mbinguni hamna wanga utaukumbuka!
Kisukari ni kibaya sana...
Presha ya mishipa ni hatari sana...

Anyway mtu akishindwa kula vaykula bora vya mpangilio .. ajiunge na BIMA YA AFYA kujiandaa kadri mri unavyokwenda.
Kuokaoa ghrama wakti akipambana na maumivu ya matibabu
 
Kuna mtu namfahamu yeye kila siku jan to December anakula wali ,hana kitambi ana mwili mzuri tu.

Ndugu yangu jilie tu mbinguni hakuna hotel, kule ni kuimba mapambio tu.
 
Ni kweli asiache sukari kabisa, atumie kidogo kwenye chai na matunda ya sukari ale tu Wala hayana shida, ila soda ndo anaweza kuacha Ili kuzuia kujaza mwili sukari ya ziada angekuwa bonge ndo ningemshauri ale nini na hiyo kufunga Ili apungue ila kutokula wanga kabisa simshauli kuacha ila kula kidogo sana na upande wa vegetables ndo uwe sana pamoja na matunda, niliacha sukari kwa muda wa miaka miwili madhara niliyopata bila kujua mpaka Leo najuta hivyo Kila kitu kwenye mwili ni muhimu ila kwa vipimo sahihi na kuzidi au kupungua ndo kunakoleta matatizo kiafya.
Soda, nyama nyekundu, nyama za kwenye makopo/beef sausage,kuku wa kizungu na mayai ya kizungu, sembe, ngano iliyokobolewa, maziwa ya ng'ombe wa kisasa, chipsi mayai feki, piza, baga, chai ya rangi ni hasara na ujinga mtupu wa Mtu kujitakia [emoji6]

Na bado tutaheshimiana tu, kama akili tumejaliwa afu hatuzitumii zaidi ya kujidai tuna uzungu mwiiingi kumbe ni pumba tupu [emoji4]
 
  • Thanks
Reactions: len
Well ni mfumo wa kula kwa baadhi ya masaa na ku-fast a.k.a kufunga kwa masaa yaliyobaki katika masaa 24. The one ambayo nimeitumia mara kwa mara ni ya 16/8 hrs. Yaani kwa masaa 16 nafunga, alaf masaa 8 nakula. So in essence mlo wangu wa kwanza unaanzia saa sita mchana na wa mwisho unatakiwa uwe by saa mbili usiku. Then after hapo hakuna ninachokula zaidi ya maji na kahawa (bila sukari), pia kahawa sio lazima. Kwenye hayo masaa 8 unaruhusiwa kula chochote (lakini kwa kiasi, sio unafukia kama unaenda kuchinjwa). Hvyo mlo wa kwanza unaeza kua a light meal, japo sio lazima kutegemeana na kipato. Personally hua huo mlo wa kwanza ni lunch. After hapo, jioni kama saa kumi na mbili unaeza pata dinner. After hapo hata ukipata maziwa before saa mbili n sawa pia. Hakuna rwstrictions. Do what works for you lakini tu muhimu iwe katika hiyo timeframe. Mwanzon itakua ngumu kucover hizo 16hrs but in 2 to 3 weeks mwili unazoea na unasahau kabisa suala la njaa.
Angalizo. Huo muda wa kuanza kula (the 8 hour block) sio lazima uanze saa sita kamili mchana, ni mapendeleo yako na shughuli zako. Cha muhimu uwe unakula in 8 hrs block na unafunga hozo nyingine.
Bila shaka kwa ratiba hii huna kitambi. Mwenye vidonda vya tumbo hii ratiba haiwezi.

Miili ya watu inatofautiana sana. Kuna mtu anakula sana yaani huwezi kumkuta hali labda kama kalala, ila cga ajabu hana tumbo liko flat.
 
Habari wana jamvi.

Kijana wenu nikiwa na umri wangu wa miaka 33 kamili, nimedhamiria kwa hiyari yangu mwenyewe, bila kushurutishwa wala kushawishiwa na mtu yeyote; kuacha kula kabisa vyakula vyenge wanga. Vyakula vyenye wanga kwa wingi ni kama mahindi, mpunga, mihogo, viazi, magimbi, ngano, mtama n.k

Inaaminika kisayansi vyakula hivi vikitumika kwa wingi vinasababisha sana kitambi na unene, kisukari na magonjwa ya moyo.

Juzi Jumatatu, 21.03.22 nikaanza movement yangu bila kuwa na mpango maalum. Asubuhi sikujua ntakula nini...mpaka imefika saa 5 sijala kitu. Sehemu za kula zote zina vitafunwa tulivyovizoea maandazi, chapati, vitumbua, mikate, viazi, mihogo and the likes. Ikafika saa 7 njaa inauma vibaya sana mpaka nikahisi kutetemeka mwili.

Nikajisemea cha kufia nini? Nikala zangu dona safi, nyama, maharage na spinach. Baadae nikawa nakunywa tu maji.

Sasa najiona kabisa sina plan na sielewi hii game inachezwaje. Najua humu kuna wazoefu wa haya mambo. Naomba mnisaidie wenzangu msiokula wanga ama heavy meals mnafanyaje?

Mnakula nini hasa? Na mliishindaje njaa hizi siku za mwanzo mpaka tumbo lizoee? Maana ile juzi nilihisi mpaka kizungu zungu.
Mimi napenda sana nyama iwe ya kuku, ng'ombe, mbuzi, kuku n.k. Ndio udhaifu wangu mkubwa.

Nipeni ushauri wadau. Hili ndio lengo la uzi.
Asanteni.
NB: sina ugonjwa wowote unaonizuia kula chochote.
Welcome to the club mkuu..

Mie huu mwezi wa pili sasa... Naona naendelea vizuri tu. Huwa nabeba kila kitu asubuhi nahakikisha nina lunch na breakfast. Mie hupendelea zaidi karoti, matango, mayai ya kuchemsha, parachichi na white meat na wakati mwingine maharage kiasi etc. So ni rahisi tu wala huwezi pata njaa.
 
Jiandae Financialy uwe sawa sawa pia, Watumiaji wanga wengi pia Sababu kuu ni "saving" akitandika chapati na supu hapo mnakutana jioni kwenye ubwabwa. AU kama n familia Marage robo mahindi nusu,Makande haya hapa siku nzima na kesho yake chai yapo...

Ku replace wanga yakubidi kamfuko kakae vizuri maana kula mpk ushibie protini usipojipanga utalalamika mara 5 kuwa maisha n magumu,wakat ugali wa buku upo tena na mboga kama zoteeee.
Yeah ni kweli inagharimu sio sawa na kula wanga
 
Maisha yetu ya kitanzania wanga ndio main dish kuanzia asubuhi mpaka jioni. Ukiacha wanga labda uwe unajipikia mwenyewe maana ni ngumu sana kupata chakula kisicho na wanga mtaani.
Ni kweli mkuu.. Na ajipange kubeba otherwise ni changamoto
 
Bila shaka kwa ratiba hii huna kitambi. Mwenye vidonda vya tumbo hii ratiba haiwezi.

Miili ya watu inatofautiana sana. Kuna mtu anakula sana yaani huwezi kumkuta hali labda kama kalala, ila cga ajabu hana tumbo liko flat.
Well ni kweli, kimeisha. Nilikua obese plus plus, but kimeisha. Sema shida ni kwamba kila nikijisahau kidogo (especially on vacations) kinarudi. Na ukigain weight unanotice kabisa mwili umekua mzembemzembe
 
Back
Top Bottom