Ushauri: Nataka kuacha kula wanga kwa mwaka mzima

Ushauri: Nataka kuacha kula wanga kwa mwaka mzima

Ugali na dagaa mchele wa kulumagia😃😃😃
🤣🤣🤣 Yani mkuu unakuta kabakuli ka mboga kadogo ugali hamuonani na mko saba mnachovya humo. Kweli hapo kuna afya zaidi ya kuwa na miraba saba na kufanya kazi kwa kutumia nguvu badala akili.
Yani mpaka karne hii tuko proud kwa kuwork very hard not working smart.
Ulime ekari saba kwa jembe badala ya trekta
 
Lengo lako nini wewe kufanya hivi ?



Acha uongo wewe.

Sukari ndio mzalishaji mkuu wa nishati katika mwili.

Miili yetu inahitaji sukari lakini haihitaji lsdha ya sukari
Ni kweli asiache sukari kabisa, atumie kidogo kwenye chai na matunda ya sukari ale tu Wala hayana shida, ila soda ndo anaweza kuacha Ili kuzuia kujaza mwili sukari ya ziada angekuwa bonge ndo ningemshauri ale nini na hiyo kufunga Ili apungue ila kutokula wanga kabisa simshauli kuacha ila kula kidogo sana na upande wa vegetables ndo uwe sana pamoja na matunda, niliacha sukari kwa muda wa miaka miwili madhara niliyopata bila kujua mpaka Leo najuta hivyo Kila kitu kwenye mwili ni muhimu ila kwa vipimo sahihi na kuzidi au kupungua ndo kunakoleta matatizo kiafya.
 
This is a very good thing. Ni a sort of keto diet. Kweli inasaidia sana kupunguza mwili plus kucontrol blood glucose ambayo inaletanga makisukari. Sio ngumu na sio rahisi pia. Mwili wa binadamu hua una adjust with time. Hapo chakula chako kikuu inabd iwe protein, fats na veggies. So hapo n mwendo wa nyama zote pkus samaki, maziwa, mboga mboga, matunda especially avocado na tango (yale yenye sukari ni kujidanganya.). Ukifanikiwa in one year the results unaeza jikuta unaandika kitabu, na hizi mbususu utapiga sana maana watakua wanakuona kijana tu.
But also kama unaona ni ngumu kuachana na wanga unaeza fanya kitu kinaitwa intermittent fasting, hyo inasaidia zaidi na haina restriction kiviile. With time mwili unazoea
Afanye Mazoezi (running)
And everything will control itself automatically.

#YNWA
 
Haya mambo ya unene na ulaji naonaga labda tu ni asili ya mtu si wengine tunabugia kila kitu na bado hatuwi mabonge.
Digestion ya tumboni ndo uhai mkubwa ulipo, sisi bonge miili yetu Ina digest polepole hivyo inabidi tule kidogo kama hatuna kazi ngumu ila nyie wembamba mfumo unadigest haraka na kutoa makapi haraka.
 
Asubuhi kunywa Maziwa fresh au supu yoyote bila kitafunwa,mchana kula kabage na maharage,jioni matunda yasio na sukari....ukiweza baada ya mwezi kitambi kwisha kbsa.. ila sio kazi rahisi mkuu.
 
Chakula kikuu kuwa protein ni very expensive, kibongo bongo ni kusema unakula mboga peke yake.
Alafu unajua hata hiyo protein hatuli ile yenye faida kama wenzetu labda mayai kidogo sawa ila protein yetu kama wanyama hatuli kama wenzetu hata Nchi jirani, mfano butter mafuta ndo protein nzuri sana kwa mwili lakini inauzwa ghali sana, cheese ambayo pia ni muhimu pia ni ghali sana kitu kinachofanya wengi wale mazao ya mimea au mafuta ya mimea kama vile sisi ni mimea.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]kwa hiyo ugali unaleta umaskini?
Well, to be fair chanzo cha umaskini ni vitu mbalimbali. Lakini hapo kwenye ugali maybe ungesema unbalanced diet ndo inaleta shida because watoto wanapata utapiamlo hivyo brain development inakua haiko fiti. Mahindi ni corn, hata wazungu wanaikula sana tu kwenye vitu kibao kama zile syrup zao wanazoeka kwenye pancakes e.t.c., tofaut ni kwamba hawafinyi tu kama sisi tunavokula ugali.
So shida kuu ni kukosa aina zingine za chakula to go with ugali. Maana ukienda vijijini, ugali ni mlima lakini mboga ni kakisosi kadogo so mostly watu wanakula ugali mwingi na mchuzi

Umaskini >>>>ukosefu wa vyakula mbalimbali>>>utapiamlo>>>poor brain development( plus other factors)>>>>>>>>>>>>Umaskini.

Kuchomoka kwenye hii Cycle sio rahisi.
 
Nashukuru hawa wanakubali kuniuzia mboga tu, bila wali au ugali.
Bahati mbaya sana jamii tunayoishi imekariri kuwa chakula ni wali, ugali au ndizi. Lakini inafaa watu wenye restaurant watambue kuwa mahitaji ya watu yanayofautiana. Mimi ningelifurahi kupata watu wanaotengeneza saladi tu na kuiuza hivyo hivyo
Mimi nina sehemu moja ambayo wameniambia niwe nanunua mboga ninazotaka wananipkia na kisha wananiuzia tena nusu bei ya chakula wanayouzia wengine.

Nimekubali nafanya hivyo japo si kila siku ila sasa hivi nina uhakika nikiamua siku flani mchana nakula salad basi kweli nauhakika wakupata.
 
Karibu jamii zote amabzo ugali ni chakula chao kikuu zimejaa umaskn. Na hii ni afrika kusini mwa jangwa la sahara
Mbona mimi ni tajiri sana lakini kama kawa nabamiza sana dona tena lililosheheni nafaka zaidi ya 6 zisizokobolewa?

Pia Baba zangu wana ukwasi wa kutosha na wameshatoboa zaidi ya miaka 90 na hawana ugonjwa wowote wa kisukari, TB, kansa, BP, UKIMWI.

Kisukari ni mifumo mibovu ya kimaisha Kwa Binadamu yeyote sababu huwezikosa kisukari kwa kuendekeza kujishindilia mivyakula isiyo na mpangilio(hakuna virutubisho) na ukashinda vijiweni kutwa nzima ukiwa umekaa tu kupiga stori bila ya mwili wako kufanya kazi au kufanya mazoezi maana sukari uliyoiingiza mwilini itakosa namna ya kufanya kazi ili itoke mwilini kupitia inshu kama jasho, mkojo na haja kubwa.

Gonga vyakula vya wanga visivyokobolewa, mboga mboga za majani, vyakula vya protini hasa hasa samaki wabichi, kunde, soya, dengu, maharagwe mekundu halisi, njugu mawe, mbaazi, njegere, choroko, korosho, karanga, matunda, maziwa, asali na maji mengi sana ya kunywa.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]kwa hiyo ugali unaleta umaskini?
Well, to be fair chanzo cha umaskini ni vitu mbalimbali. Lakini hapo kwenye ugali maybe ungesema unbalanced diet ndo inaleta shida because watoto wanapata utapiamlo hivyo brain development inakua haiko fiti. Mahindi ni corn, hata wazungu wanaikula sana tu kwenye vitu kibao kama zile syrup zao wanazoeka kwenye pancakes e.t.c., tofaut ni kwamba hawafinyi tu kama sisi tunavokula ugali.
So shida kuu ni kukosa aina zingine za chakula to go with ugali. Maana ukienda vijijini, ugali ni mlima lakini mboga ni kakisosi kadogo so mostly watu wanakula ugali mwingi na mchuzi
Jamaa halioni hata aibu kudanganya Watu wanaoishi maisha hayo, wanaotafakari na kufanya maamuzi thabiti hapa JF [emoji848][emoji1787]
 
Mbona mimi ni tajiri sana lakini kama kawa nabamiza sana dona tena lililosheheni nafaka zaidi ya 6 zisizokobolewa?

Pia Baba zangu wana ukwasi wa kutosha na wameshatoboa zaidi ya miaka 90 na hawana ugonjwa wowote wa kisukari, TB, kansa, BP, UKIMWI.

Kisukari ni mifumo mibovu ya kimaisha Kwa Binadamu yeyote sababu huwezikosa kisukari kwa kuendekeza kujishindilia mivyakula isiyo na mpangilio(hakuna virutubisho) na ukashinda vijiweni kutwa nzima ukiwa umekaa tu kupiga stori bila ya mwili wako kufanya kazi au kufanya mazoezi maana sukari uliyoiingiza mwilini itakosa namna ya kufanya kazi ili itoke mwilini kupitia inshu kama jasho, mkojo na haja kubwa.

Gonga vyakula vya wanga visivyokobolewa, mboga mboga za majani, vyakula vya protini hasa hasa samaki wabichi, matunda, maziwa, asali na maji mengi sana ya kunywa.
We unakula vyenye rutuba majority wanakula sembe iliyokobolewa yani sembe debe mboga kisoda
 
Niliacha kula wanga( mara mmoja mmoja nakula) nimepungua sana sana. Nakunywa capuchino asubuhi, mchana salads tofauti, nazitia Thunfisch, kuku au beef, yogurt matunda na maji mengi.
Hiyo capuchino ina aslilimia ngapi ya carbs?
 
Upo sahihi.
Acha kula wanga, sukari, mafuta na ikitokea sasa umekula wanga jitahidi iwe mchana na kiasi kidogo.
Kula sana mbogamboga, protein, matunda.
Mie binafsi huwa nanenepa sana nikila wanga, sukari, na ma vya kula ya mafuta.
Lakini nikiacha kula hayo mavyakula napungua ninakula mcharooo na ninakuwa mwepesi sana.
Kama ujuavyo sisi wamama ndo wapishi wa familia, kwa kiasi fulani ni ngumu kucontrol mfano mchana ukiwa unalisha mtoto anataka mle wote(watoto wangu huwa wanataka tule wote, na wakiona nakula mboga mboga tu na wao eti wanagoma kula) usiku mume nae anataka mle wote au akulishe, wageni nao wakija ni noma kuanza kujieleza umewapikia eti wewe huli inabidi uzuge ule, ukienda ugenini napo changamoto maana kama mnajua sisi ni watanzania.
Changamoto ni nyingi sana kufikia malengo.

Ila all in all ni kupambana na hizo challenge, mfano sasa hivi nina mwezi wa 2 nimeacha mno kula wanga inatokea mara chache sana nikadokoa wali maharage vijiko 2, pilau kijiko 1, chapati robo(hivi vyote haizidi mara 1 kwa wiki)
Hii ni ratiba yangu.
Asubuhi nachemsha maji moto yakiwa na tangawizi, mchaichai abdalasini, kisha naweka limao.
Masaa 2 baadae nakunywa kikombe cha maziwa fresh labda mayai 2 kuchemsha, au maziwa matupu.
Mchana nakula parachichi, mchemsho wa mboga za majani, kama nikipata kitoweo iwe kuku, samaki au nyama choma au mchemsho poa(ni lazima kimojawapo nipate)
Usiku mara nyingi nakunywa mtindi, au smoothie ya mtindi&parachichi&,passion.
Uko sahihi lakini , usicomplicate mambo jaribu kuwaelewesha tu kuwa sili chakula fulani kwasababu ya sukari, uzito n.k basi, usifanye kila jambo kumridhisha
 
Huwezi pungua kupitia kuacha kula peke yake.

Naona wadau wengi wanasema wameacha wanga na mwili umepungua.

Mwili unapungua kwa mawili ama ufanyiwe operation au ufanye mazoezi. Intentional starvation itabackfire na ulcers na magonjwa mengine.

Halafu mazoezi ni ishu ndogo sana. Yaani wewe unayeruka kichura chura mara tano kila siku you are better off kuliko mimi ninayekesha nacheza PS.
Mkuu naona unachanganya kati ya watu wanaoshinda njaa, ili wapungue.

Na walioacha kula wanga haimaanishi kuwa unatakiwa kushinda njaa.

Mtu akiacha kula vyakula vya wanga kabisa lazima uzito upungue.

Kiasi cha sukari kinapungua..
Mwili utakuwa ni rahisi ku butn calories, sababu kwa kuacha wanga Energy nyingi itatoka katika vyakula vya healthy fat..na protein pamoja vitamins
 
Ningekuwa na mamlaka ningezuia uuzaji wa unga wa mahindi iwe dona au sembe bila kuwa na mchanganyiko mwingine. Kuna wakat inabid uvuke mstari wa utash wa weng wajinga kuwasaidia wenyewe. Tatzo la utapiamlo mkoa wa iringa kuwa juu ni la kiufaham zaid kuliko ukosef wa nini kiliwe! Ndo mana nchi zinazohangaikia afya za akili za watu wao wako makin na ingredients za bidhaa kuliko uchu wa kodi. Hadi maji yanawekwa virutubisho vya IQ!

Unakuta mtu aba kipato lakin hajali familia inakula kwa malengo gan na bado anatumia bajet kubwa kula ovyo!
Elim ya afya na lishe ianzie chekechea mtoto ajue kila mlo anatakiwa mboga za majan nying kuliko chakula chenyewe!

Mtoto awe na kibustan chake hata kidogo, akuhudumie akitoka skuli, atajiongeza anavokua!
Mtu ana li eneo litoto halifanyag kitu had mchaichai ananunua! Wazaz wa sasa vijana kwa wazee ni wabinafs, hawatak uzao wao kujitegemea hata kifikra utadhan wanaish wakiwa wa mwisho!
True
 
Back
Top Bottom