Ushauri: Nifanyeje juu ya hali hii ya maisha yangu?

Ushauri: Nifanyeje juu ya hali hii ya maisha yangu?

Mkuu umekulia mazingira ya kijijini au mjini?
Nashukuru kwa ushauri wako uwe hodari ila naogopa Kuoa, watoto (Kama Mungu atajalia wakapatikana) wasije kuishi maisha magumu sana. Mimi mwenyewe naishi kwa shida sana na niko peke yangu, sasa nikioa mtoto wa watu mmmmmh na dada yupi huyo anayetaka shida ? ngoja tuu niwe mpole.
 
Wakubwa kwangu shikamoni, wadogo kwangu habari zenu ?

Hongereni kwa majukumu na afya njema, poleni mnaoumwa Mungu akawajaalie mpone.

Ndugu, Nilizaliwa miaka 31 iliyopita. nilipenda sana kuwa mwanajeshi wa jeshi la wananchi, sikufanikiwa kutokana na umri wangu kupita ule unaotakiwa, kukosa fani zinazotakiwa huko, na kutokuwa na mtu wa kunishika mkono kuingia huko. Nina shahada ya sayansi.

Kuna mahala serikalini nimejitolea kwa miaka minne sasa, walivyotoa ajira kupitia utumishi nimebwagwa kwenye usahili nikashindwa ! wakaajiriwa vijana wengine ambao hawakuwa wakijitolea pale. Nimefanya saili nyingi za kuomba kazi utumishi na kwingineko lakini sijafanikiwa kupata kazi.

Hapo Kibaruani wanatoa sh. 15000 kwa siku mtu atakayofanya kazi, (300,000 na kidogo kwa mwezi maana ijumaa pili hatufanyi kazi) hicho kiasi cha fedha kwa mkoa wa Dar es salaam kinaishia kulipa kodi, nauli za kwenda kibaruani, kununua umeme, kula kwa mama ntilie (2000 msosi mmoja), kulipia taka, kulipia ulinzi mtaani, sadaka kanisani, VOCHA na matumizi mengine; sijafanikiwa kuweza kuweka akiba. Sina mchumba, mke wala mtoto maana sina hela za kuniwezesha kuwahudumia, Ukinunua napo magonjwa lukuki .... ila homoni za mwili zenyewe zinafanya kazi yake hazielewi hali yako kiuchumi kwa hiyo ni shida tupu.

Huwa ninatamani sana kwenda jeshini lakini umri, fani na konekisheni ni changamoto

Ninatamani kuoa lakini sina kazi, nikifikiria kurudi kijijini kulima, sawa lakini mtaji wa kulimia na mashamba sina. Nafikiria kusoma 'post graduate diploma in education' ili niwe na taaluma ya ualimu badae niombe kazi serikalini kama mwalimu wa fizikia n.k lakini hela ya kulipia ada (milioni mbili) sina. Huwa ninapenda pia kufanya biashara ya stationery lakini mtaji nao sina !

Ninawaza kurudi chuo kusoma kozi za afya kwa diploma, ada sina ! Nipo njia panda ndugu ninaombeni mnishauri nifanyeje ili kupata hela, niache kujitolea niende chuoni kusoma, niajiriwe serikalini au taasisi binafsi au nifanye miradi hiyo, n.k maisha mengine yaendelee.

Ninatanguliza shukrani kwa ushauri wenu, ninawatakia mda mwema.
Tatizo ni moja kwanza moyo wako bado haujui unataka nin.
Ukiona nyeupe unataka, nyeusi unataka, blue unataka.
Kuacha unajitolea na unapata hata hyo elf kumi na tano wenzio wanajitolea hawapati senti.

Ukijua unataka nin tofauti na hicho kias kidg Cha pesa utajua jinsi au namna gani ya kutengeza pesa nyingine ndogo ndogo nje na hyo sehem ya kujitolea au fursa nyingine hapo hapo kweny hyo ofis unayojitolea.
 
Any way kwa miaka uliyo nayo alafu unalia lia hapa as if huna kipato that is nonesense.

wewe unataka kusema unashindwa kabisa kufikiri utasave vipi 300k, weka 100K assume unalipwa 200K then ndiyo iwe kwenye matumizi iyo 200K.

200K imagine unalipa kodi plus maji na umeme 50K covered, inasalia 150K.

Assume unatumia 100K kila mwezi kwenye food. 50K iliyobaki ni mavazi na sabuni kwa kila mwezi.

Plan kuinvest 100K kwenye issues nyingine.

Unapata alafu unasema hupati.....😅😅
 
Yani mpaka dunia ya leo unawaza kusoma
Ndio maana ni talanta yangu. Mwenyezi Mungu amempatia kila mtu talanta yake hapa duniani, kuna uimbaji mziki wa kidunia, uimbaji nyimbo za injili, uimbaji kaswida, kuna madaktari, wakulima, boda boda madereva, walimu, makuli, mafundi umeme n.k mimi ninapenda kusoma.
 
room yako ya 45-50 Unalipa kodi ya miezi 6 then unaanza ku,make kila siku matumizi ya kula yasizidi 5k.... usafiri jua mwenyewe utacheza vp ila kila siku save 7k kwa week siku sita una 42k ambayo mara mwezi ni 168k ukitoa hayo masula ya umeme,maji na mtakataka yote ya maushuru ya makazi haushindwi kusave 140k ambayo mara mwaka una 1,680,000 then amua nini ufanye maana hiyo hela yatosha.
 
Mkuu

Kazi unayo sema unaodharau TU!

Bana matumizi weka akiba usijiachie Sana!!

We oa usiogope MAISHA hela ya kula unayo!sema usioe golikipa oa hata muuza nyanya au mpishi wa hoteli au hata mhudumu wa hoteli!

Mafanikio hayana kanuni FULANI zaidi ya kuchapa kazi Sana!

Haimaanishi ukioa au usipooa ndio utafanikiwa au hautofanikiwa!

Chapa kazi Buni biashara hata ndogo ya 200000/= anzia hapo Mkuu!!
 
Tatizo ni moja kwanza moyo wako bado haujui unataka nin.
Ukiona nyeupe unataka, nyeusi unataka, blue unataka.
Kuacha unajitolea na unapata hata hyo elf kumi na tano wenzio wanajitolea hawapati senti.

Ukijua unataka nin tofauti na hicho kias kidg Cha pesa utajua jinsi au namna gani ya kutengeza pesa nyingine ndogo ndogo nje na hyo sehem ya kujitolea au fursa nyingine hapo hapo kweny hyo ofis unayojitolea.
Ninataka nipate hela ya kutosha kufanyia biashara au kufanya mambo hayo mengine. Namna ya kupata kiasi kingine cha fedha ndio nipo njia panda sasa. Kitu cha kufanya siyo shida, shida ni jinsi ya kupata hela ya kukifanyia hicho kitu
 
Any way kwa miaka uliyo nayo alafu unalia lia hapa as if huna kipato that is nonesense.

wewe unataka kusema unashindwa kabisa kufikiri utasave vipi 300k, weka 100K assume unalipwa 200K then ndiyo iwe kwenye matumizi iyo 200K.

200K imagine unalipa kodi plus maji na umeme 50K covered, inasalia 150K.

Assume unatumia 100K kila mwezi kwenye food. 50K iliyobaki ni mavazi na sabuni kwa kila mwezi.

Plan kuinvest 100K kwenye issues nyingine.

Unapata alafu unasema hupati.....😅😅
Gharama za maisha haziko hivyo ndugu. Ziko juu sana, kwa huu mpangilio wa matumizi siwezi kuishi hili eneo. Ningependa niweke akiba lakini ni ngumu.
 
Gharama za maisha haziko hivyo ndugu. Ziko juu sana, kwa huu mpangilio wa matumizi siwezi kuishi hili eneo. Ningependa niweke akiba lakini ni ngumu.
Sasa mkuu wewe acha kazi uone ilivo kazi kupata kazi, acha kazi ukiwa na plans, mkuu wewe pambana sana, maisha siyo marahisi kiivo.
 
Futa mawazo ya kurudi chuo.Futa mawazo ya kuajiriwa.Futa mawazo ya mshahara mdogo.Weka wazo la Je leo ukisimamishwa happy utaishi vipi???
Cha kufanya,chukulia Kila mwezi unalipwa laki 2.Laki moja week akiba.
Kwanza hamia kwenye chumba Cha Bei nafuu,au tafuta mtu mwaminifu mchangie chumba.
Pili,sadaka ni muhimu Je huwa unaiombea kabla ya kutoa???Kama huiombei basi Bora uache kutoa sadaka.
Tatu,Huwa unatumia vocha ya kiasi gani kwa mwezi???Mfano,vocha ya buku unajiunga kifurushi Cha meseji mwezi mzima.
Je kazini Huwa unatoka saa ngapi???Kama ni mapema,basi tafuta kitu Cha kujiongezea kipato baada ya masaa ya kazi.Mfano unaweza kuanzisha biashara ya kuuza mchele hapo mtaani kwako.
Au unaweza kutafuta goli la kuuza kuku jioni.
 
Ninataka nipate hela ya kutosha kufanyia biashara au kufanya mambo hayo mengine. Namna ya kupata kiasi kingine cha fedha ndio nipo njia panda sasa. Kitu cha kufanya siyo shida, shida ni jinsi ya kupata hela ya kukifanyia hicho kitu
Pesa haiji kimazingara.
Jipange ni namna gani hyo elf kumi na tano utaibana ufanye kitu chchte kitakachokuingizia elf 5 kwa siku ukifika hatua hyo utawaza kikubwa kwa sabb tayali kuna kidg unapata
 
Hatua ta kwanza acha kujilinganisha na wengine, hapo utajiona wewe na utajielewa zaidi.

Hatua ya pili, leo usiku ule muda wa kwenda kulala kabla hujapata usingizi, anza kuzitatafakari ndoto zako zote ulizo nazo. Kisha kuna kitu utakipata.

Hatua ta tatu, ili ufanikishe ndoto zako inakupasa uamke usingizini. Mafanikio hukaa kwenye akili ya mhusika na hakuna kanuni kwamba ukifanya hivi na hivi lazima ufanikiwe kimaisha, hivyo cha msingi kuwa makini na intuitions zako mwenyewe hapo ndipo kuna siri za mafanikio yako.
 
Back
Top Bottom