USHAURI: Nini cha kufanya kama mwenza wako alikuficha kuwa ana mtoto, Ukaja kujua baada ya miaka zaidi ya 10 baadaye?

USHAURI: Nini cha kufanya kama mwenza wako alikuficha kuwa ana mtoto, Ukaja kujua baada ya miaka zaidi ya 10 baadaye?

Mimi nawekaje hasira na mihemko kwenye uzi usionihusu? Hapa tumeitwa tutoe ushauri nakushangaa unapanic kwenye comment yangu,

Unavyosema tusijadili kimazoea ya Kiswahili kwa hiyo tujadili kigeni kwa Kizungu au Kichina? Maana hao hili tukio wakipelekewa ndio kabisaa watazidi kumshangaa huyo Mwanaume,

Umesema mwanzo wa mahusiano mnaulizana moja, mbili, tatu, umejuaje kama hii couple tunayoijadili hapa waliulizana yote hayo!!??

Pia elewa maana ya privacy, kama hajataka jambo lake liwe wazi sio vema kumlazimisha, yule ni mwanae yeye ndie alikua anajua zaidi.
Daah leo ndio nimekuelewa...tukio kama hilo unaweza kuliita privacy?

Je ulizaa kabla ya ndo?
Sio kwa utetezi huu wenye ukakasi kiasi hiki
 
Wakati mwingine tusiongozwe na hisia bali utashi wetu.

Kwani ni kosa mtu kuzaa, ni heri huyo amezaa maana kuna wengine wametoa zaidi ya mimba 7 hadi kuolewa kwao.

Ningekuwa Mimi huyo mtoto ningempokea na kumfanya mmoja ya watoto wangu, kwanza kwa mujibu wa mila zetu mtoto wa mkeo nao ni watoto wako
Excellent kabisa haya ndio maamuzi ya Mwanaume rijali, hakika hapa ndio tunaona tofauti kati ya waliotahiriwa hospital na waliotahiriwa porini.
 
Kwanini nisimuamini?
Jamani kila Mtu ana siri yake kama ameamua kuitunza as long as haikuwahi kuniletea madhara yoyote si basiiiii,

Tena haya mambo ya Mwanamke kuondoka mahali na kuacha mtoto kisha akaja kuolewa sehemu nyingine na kuzaa, mara nyingi huwasahau wale watoto wa mwanzo na kufocus na family mpya, hadi mtoto aje amtafute na hii sio kwa Mwanamke tu hata kwa Wanaume hutokea,

Mimi naona mnakuza vitu ambavyo kimsingi havina mashiko.
Tupe uzoefu wako kama umekutana na kesi kama hio mliisolve kivipi.
Tupe madini.
 
Lazima kuwe na sababu ya yeye kutokusema,

Kuna Mama alipokonywa mtoto na Mwanaume aliyezaa nae, mtoto alikua ana miezi 11, yule Mama alihangaika kuanzia Ustawi wa jamii hadi Mahakamani, kote aligonga mwamba basi akamuachia Mungu na kurudi kwao (Mikoa ilikua tofauti) baada ya miaka kupita, akaja akapata Mwanaume akamuoa hakumwambia kuhusu tukio lile yeye anasema alijaribu kulisahau hakuona sababu ya kulizungumzia tena, Mtoto alikuja kumtafuta Mama yake ameshakua mtu mzima na wajukuu akamletea, Mume ndio kujua hilo sakata lakini hakureact tofauti zaidi ya furaha familia imeungana tena.
Mume bwege huyo ana nyimbo yake kabisa apigwe mawe auawe
 
Huyo ni Mwanaume suruali, halijui jando, hajafudishwa chochote kuhusu ndoa walizoana zoana tu wakaapa basi,

Hakuna jambo kubwa la kuachana hapo unless alikua amemchoka ndio kapata sababu.
Tusijaribu kuhalalisha matakwa/uelewa wetu kuwa uhalisia wa kila mtu.

Huwezi kumuita mtu mwanaume suruali ikiwa kwa kipindi cha miaka 15 ameishi kwa kudanganywa, kuaminishwa kuwa yeye ndie baba watoto wa kwanza kwa mkewe halafu ghafla anaibuka kiumbe na kusemekana ni mtoto wa mkewe.

Haya ni maisha halisi sio tamthilia za Kikorea.

Usaliti katika ndoa sio lazima umvulie mtu mwingine nguo, kitendo cha kuficha jambo ambalo kujulikana kwake kunaweza kuwa na athari katika mahusiano; huo ni usaliti tosha.
 
Habari wana JF.

Kuna Ndoa imevunjika hapa ndoa ya miaka 15.

Mke alizaa kabla ya ndoa, sasa mama huyu alimficha mtoto,

Huyu mtoto alikuwa anaishi na Baba yake.

Mume alijua kwa mawasiliano ya simu.

Mama alipokuwa anaongea na mwanae.

Na mtoto anaumri wa miaka 20.

Mume wa ndoa kazaa nae watoto 4.

Dawati la suruhisho walijaribu kuweka sawa ili wasiachana ila ilishindika. Hata wachungaji walishauri kuwa asamee tuu kwani hata mtoto kashakuwa mkubwa hakuna shida yoyote lkn ndo hivyo ndoa imevunjwa jana na mahakama.

Huyu mama alizaa kipindi anaumri wa miaka 21.

Sasa wanajamii hivi vitu vinatokana na nini mpk mmoja anaamua kuficha mtoto?

NI NINI CHA KUFANYA BAADA YA KUJUA HATA KWA MUME KAMA ALIFICHA KUWA ALIKUWA ANAMTOTO.
Mimi nashauri kwa mwanamke kama mumeo anasimamia majukumu yake vizuri bila shida yoyote ukiletewa mtoto pokea. Ila kwa Mwanaume mkeo akijifungua mtoto sio wa kwako achana nae. Hakuna heshima hapo na ukiangalia wanaume tunapitia changamoto kubwa sana kwenye utafutaji. Yaani mtu unatumia hela zako kwake halafu anakupa shida. Ni sawa sawa mtu atumie hela zake anazotafuta kwa tabu na shida kununua matatizo.
 
Daah leo ndio nimekuelewa...tukio kama hilo unaweza kuliita privacy?

Je ulizaa kabla ya ndo?
Sio kwa utetezi huu wenye ukakasi kiasi hiki
Umekosa hoja unakimbilia personal attack, lol kama hujala nenda kale kwanza hii mada ni kubwa sana kwako sio kila kitu cha kuchangia,

Btw, Nimezaa nikiwa kwenye Ndoa, watoto watano (mapacha mara mbili na mmoja) wote kwa baba mmoja, nipo kwenye ndoa mwaka wa 11 huu, tunaposhauri masuala ya ndoa hatushauri kwa mihemko na hasira bali kwa kujenga kwani Ndoa ya halali ikivunjika ni dhambi kubwa sana pia tunawafikiria na watoto ambao hata hatujui ni umri gani,

Narudia tena, kula ushibe hii mada kwako ni kubwa sana ukizingatia hata ndoa huijui.
 
Alafu kuna kisa kimoja kimemtokea mwenzetu wa ofisini kimenishangaza kwa alivyo react ila nikasema acha nije nishirikishe na wanajamvi huku.

Huyu dada kakaa kwenye ndoa kama miaka mitatu hivi. Sasa anakuja kugundua mume wake aliwahi kuchepuka na ex wake tena sio mara moja kipindi wapo kwenye mahusiano. Yaani kabla ya ndoa. Yani wame date miaka saba, mwaka wa nne mwanaume akawa na mahusiano na ex wake wameenda kama miaka miwili na ex malavidavi kama yote ila huyu dada anasema hakuwahi kuhisi. Sasa mke mtu kaja kujua wakati wameshaoana. Anasema ye bado kinamuuma kwasababu alimuamini sana mme wake inakuwaje alimsaliti kipindi ambacho alimpenda na kumuamini.

Wengi tukamshauri aache yaliyopita wagange yajayo. Akauliza ingekua nyinyi mngesahau na kusamehe? Nikasema wanajamvi mpo kibao mna majibu em mshaurini na nyinyi.
Watakuwa wanaendelea na mahusiano still.
Huyo mume ni msaliti tuu.

Haya mambo watu wanachukulia simple sana.
 
Alafu kuna kisa kimoja kimemtokea mwenzetu wa ofisini kimenishangaza kwa alivyo react ila nikasema acha nije nishirikishe na wanajamvi huku.

Huyu dada kakaa kwenye ndoa kama miaka mitatu hivi. Sasa anakuja kugundua mume wake aliwahi kuchepuka na ex wake tena sio mara moja kipindi wapo kwenye mahusiano. Yaani kabla ya ndoa. Yani wame date miaka saba, mwaka wa nne mwanaume akawa na mahusiano na ex wake wameenda kama miaka miwili na ex malavidavi kama yote ila huyu dada anasema hakuwahi kuhisi. Sasa mke mtu kaja kujua wakati wameshaoana. Anasema ye bado kinamuuma kwasababu alimuamini sana mme wake inakuwaje alimsaliti kipindi ambacho alimpenda na kumuamini.

Wengi tukamshauri aache yaliyopita wagange yajayo. Akauliza ingekua nyinyi mngesahau na kusamehe? Nikasema wanajamvi mpo kibao mna majibu em mshaurini na nyinyi.
Mume wake anasemaje??
 
Mimi nashauri kwa mwanamke kama mumeo anasimamia majukumu yake vizuri bila shida yoyote ukiletewa mtoto pokea. Ila kwa Mwanaume mkeo akijifungua mtoto sio wa kwako achana nae. Hakuna heshima hapo na ukiangalia wanaume tunapitia changamoto kubwa sana kwenye utafutaji. Yaani mtu unatumia hela zako kwake halafu anakupa shida. Ni sawa sawa mtu atumie hela zake anazotafuta kwa tabu na shida kununua matatizo.
Wengine nao, hata mada hajaielewa maskini anaweka kachumbari na maharage,

Nacheka kama mazuri
 
Back
Top Bottom