USHAURI: Rais Samia suluhisho pekee kwa Bandari Tanzania ni hili

USHAURI: Rais Samia suluhisho pekee kwa Bandari Tanzania ni hili

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Amani iwe nanyi
Leo Rais wa JMT amemtumbua Mkurugenzi wa Bandari Ndug Erick Hamis.

Pamoja na kumtumbua Rais Samia amelalamika juu ya efficiency ya Mamlaka yetu ya Bandari na kusema kuwa Mamlaka hii ingekuwa inafanya kazi vizuri ingeweza kuchangia hata nusu ya mapato ya Bajeti yetu. Ni kweli kabisa naungana na Rais Samia kwenye hili!

Mfupa wa Bandari ni mfupa uliowashinda Marais karibu wote waliowai kutawala Tanzania! Hii imekuwa kawaida kila Rais mpya akiingia au Waziri Mkuu mpya akiteuliwa sehemu ya kwanzq kwenda kulalamika na kutumbua imekuwa Mamlaka ya Bandari Tanzania.

Kwa kumbukumbu zangu kuanzia kwa Mkapa, Kikwete, Magufuli hadi sasa Samia, Bandari hapajawai kupoa.

Hoja yangu kuu kwenye hili ni kwamba inawezekana sana bado hatujajua shida ni nini hasa pale Bandarini na kwa uelewa wangu mdogo napenda leo nimshauri Mhe Rais mambo ya kufanya na naamini kama nilivyoshauri kuhusu Ngorongoro na ikafanyika na sasa imefanikiwa basi nashauri juu ya hili la Bandari na naamini ikifanyika itafanikiwa

1. Lazima tukubali kuwa Bandari ya DSM haiwezi kuwa efficient kwa sababu imekuwa finyu kuhimili idadi ya mizigo, Meli na Magari kiushindani

2. Lazima tukubali kuwa Serikali haiwezi kuendesha bandari kwa ufanisi tunaoutaka katika dunia hii ya ushindani. Bandari kubwa zote duniani na zinazofanya vizuri kwenye soko la ushindani kuanzia Dubai, Hong Kong, Singapore, New York na nyinginezo, zinaendeshwa either kwa sehemu kubwa na private sector au kwa ubia baina ya Serikali na Private Sector

Hivyo ili kufanikiwa kupata ufanisi hapa Tanzania kwenye sekta ya Bandari , Lazima tutake tusitake, tufanye yafuatayo

a. Kwa haraka sana, Ijengwe Bandari ya Bagamoyo ambayo iwe na Gati zisizopungua 40. Bandari hii iendeshwe na Private sector with exception kwenye masuala ya Ulinzi, Usalama na Kodi

b. Sekta binafsi wapewe pia fursa ya kujenga Miundombinu ya Reli na barabara kuunganisha Bandari ya Bagamoyo na Jiji la Dar es Salaam ikiwemo reli ya kati SGR na TAZARA

c. Bandari za DSM, Tanga, Mwanza na Kigoma na Mtwara ziendeshwe kwa ubia na Private sector. Serikali isimamie masuala ya kodi , ulinzi na usalama tu!

d. Barabara ya Mandela Road( dsm) itanuliwe kuwekwa njia 8 kutokea Bandarini hadi Ubungo na utanuzi wa njia 6 uendelee kutoka Kimara hadi Ubungo. Hii ni ili kuleta ufanisi wa usafirishaji mizigo katika Jiji la Dsm. Ikiwezekana Private sector washirikishwe kwenye hili.

e. Kulikuwa na Mpango wa Kujenga Barabara ya Malori kutokea Bandarini hadi Chalinze. Mpango huu ufufuliwe na barabara hii ijengwe hata kwa kutumia Private sector! Fedha zitarudi haraka sana hata kwa toll tax!

Nchi kubwa duniani ziliona hili na wakaamua kufanya! Hata kwa Tanzania Serikali iking'ang'ania kuendesha bandari kila siku mtaishia kushikana uchawi na kutumbuana!

Ni suala la kuamua tu na wakati ni sasa
 
Amani iwe nanyi
Leo Rais wa JMT amemtumbua Mkurugenzi wa Bandari Ndug Erick Hamis.

Pamoja na kumtumbua Rais Samia amelalamika juu ya efficiency ya Mamlaka yetu ya Bandari na kusema kuwa Mamlaka hii ingekuwa inafanya kazi vizuri ingeweza kuchangia hata nusu ya mapato ya Bajeti yetu. Ni kweli kabisa naungana na Rais Samia kwenye hili!

Mfupa wa Bandari ni mfupa uliowashinda Marais karibu wote waliowai kutawala Tanzania! Hii imekuwa kawaida kila Rais mpya akiingia au Waziri Mkuu mpya akiteuliwa sehemu ya kwanzq kwenda kulalamika na kutumbua imekuwa Mamlaka ya Bandari Tanzania.

Kwa kumbukumbu zangu kuanzia kwa Mkapa, Kikwete, Magufuli hadi sasa Samia, Bandari hapajawai kupoa.

Hoja yangu kuu kwenye hili ni kwamba inawezekana sana bado hatujajua shida ni nini hasa pale Bandarini na kwa uelewa wangu mdogo napenda leo nimshauri Mhe Rais mambo ya kufanya na naamini kama nilivyoshauri kuhusu Ngorongoro na ikafanyika na sasa imefanikiwa basi nashauri juu ya hili la Bandari na naamini ikifanyika itafanikiwa

1. Lazima tukubali kuwa Bandari ya DSM haiwezi kuwa efficient kwa sababu imekuwa finyu kuhimili idadi ya mizigo, Meli na Magari kiushindani

2. Lazima tukubali kuwa Serikali haiwezi kuendesha bandari kwq ufanisi tunaoutaka katika dunia hii ya ushindani. Bandari kubwa zote duniani na zinazofanya vizuri kwenye soko la ushindani kuanzia Dubai, Hong Kong, Singapore, New York na nyinginezo, zinaendeshwa either kwa sehemu kubwa na private sector au kwa ubia baina ya Serikali na Private Sector

Hivyo ili kufanikiwa kupata ufanisi hapa Tanzania kwenye sekta ya Bandari , Lazima tutake tusitake, tufanye yafuatayo

a. Kwa haraka sana, Ijengwe Bandari ya Bagamoyo ambayo iwe na Gati zisizopungua 40. Bandari hii iendeshwe na Private sector with exception kwenye masuala ya Ulinzi, Usalama na Kodi

b. Sekta binafsi wapewe pia fursa ya kujenga Miundombinu ya Reli na barabara kuunganisha Bandari ya Bagamoyo na Jiji la Dar es Salaam ikiwemo reli ya kati SGR na TAZARA

c. Bandari za DSM, Tanga, Mwanza na Kigoma na Mtwara ziendeshwe kwa ubia na Private sector. Serikali isimamie masuala ya kodi , ulinzi na usalama tu!

d. Barabara ya Mandela Road( dsm) itanuliwe kuwekwa njia 8 kutokea Bandarini hadi Ubungo na utanuzi wa njia 6 uendelee kutoka Kimara hadi Ubungo. Hii ni ili kuleta ufanisi wa usafirishaji mizigo katika Jiji la Dsm. Ikiwezekana Private sector washirikishwe kwenye hili.

e. Kulikuwa na Mpango wa Kujenga Barabara ya Malori kutokea Bandarini hadi Chalinze. Mpango huu ufufuliwe na barabara hii ijengwe hata kwa kutumia Private sector! Fedha zitarudi haraka sana hata kwa toll tax!

Nchi kubwa duniani ziliona hili na wakaamua kufanya! Hata kwa Tanzania Serikali iking'ang'ania kuendesha bandari kila siku mtaishia kushikana uchawi na kutumbuana!

Ni suala la kuamua tu na wakati ni sasa
Wajenge bandari kubwa ya Bagamoyo hakuna cha njia ya mkato,kila siku mtatumbua.
 
Naomba kuuliza, tulifanya PPP na TICS, tukabinafsisha baadhi ya Mageti, Je ufaninisi uliongezeka?je mapato yaliongezeka? Je tumejifunza nn kutokana na mkataba huo?
Solution niionayo mimi.

1. Tukamilishe upanuzi wa bandari ya Tanga - Uganda, Rwanda na Burudi ile ndo iwe destionation port yao.- hii sio tu itapunguza msongamao Dar bali pia itafufua uchumi wa Tanga.

2. Tukamilishe upanuzi wa Bandari ya Mtwara - Mizigo ya Zambia na Malawi ipitie huko. Hii nayo itapunguza msogamano Dar na kukuza mji wa Mtwara.

3. Dar ibaki na mizigo ya Congo na Mizigo ya Ndani tu.

4. Tujenge highway kwenda mikoa yote inayopakana na inchi jirani.

5. Tuwajengee uwezo watanzania waweze kuziendesha bandari zao..kuwalaumu na kuwatumbua kwakua tu hawaperfom km bandari za nje ni km kuwatumbua viongozi Simba na Yanga kwakua tu hawaendeshi vilabu vyao km na team za ulaya, uarabuni or asia...by theway kwann serikali haijalaumu kwa kutojiendesha km serikali za ng'ambo?
These people need exposure, resouces, support and political will.

6. Mimi sio muumini wa Bagamoyo. Sababu kuu ni kua tukiijenga hii bandari za Tanga na Mtwara ndo bai bai..no one will want to go there, 2nd ipo karibu sana na Dar which doesnt make sense...
 
Wajenge bandari kubwa ya Bagamoyo hakuna cha njia ya mkato,kila siku mtatumbua.
Bandari ya Bagamoyo haiepukiki! Ukipita barabara ya sea view upanga hadi masaki unaona meli nyingi ziko kwenye foleni! Zile meli zinakaa foleni hadi two weeks!

Kwa mendoza ule hatuwezi pata ufanisi kwenye bandari kamwe
 
Naomba kuuliza, tulifanya PPP na TICS, tukabinafsisha baadhi ya Mageti, Je ufaninisi uliongezeka?je mapato yaliongezeka? Je tumejifunza nn kutokana na mkataba huo?
Kama kuna makosa tunaweza kujifunza na kurekebisha! Tumefanya kwenye madini imewezekana hatuwezi kushindwa kwenye Bandari
 
Hili ndo suluhisho pekee! Tukiendelea kuwa wabishi kila siku tutaishia kufukuzana
... mnakumbuka stori za NetGroup Solutions? Mnakumbuka jinsi ilivyosifiwa? Kwamba siangalii rangi ya paka, muhimu akamate panya? Mnakumbuka jinsi ilivyoiacha taasisi ile mahututi hadi kesho? Private sector is one thing ila kuna tatizo la msingi zaidi! Bila kutatua kiini cha tatizo mtaleta kila aina ya private sector ila nchi itaendelea kubaki mahututi!
 
Kuna wale Waarabu wa DP World wako vizuri sana hata huo upanuaji wa Barabara wanaweza kuwekeza wenyewe.
Sio lazima DP World! kuna wawekezaji wengi sana tunaweza India nao ubia na wakafanyq uwekezaji wao pale na tukapata mapato makubwa sana
 
... mnakumbuka stori za NetGroup Solutions? Mnakumbuka jinsi ilivyosifiwa? Kwamba siangalii rangi ya paka, muhimu akamate panya? Mnakumbuka jinsi ilivyoiacha taasisi ile mahututi hadi kesho? Private sector is one thing ila kuna tatizo la msingi zaidi! Bila kutatua kiini cha tatizo mtaleta kila aina ya private sector ila nchi itaendelea kubaki mahututi!
Hata NMB inaendeshwa kwa ubia, puma energy inaesheshwa kwa ubia na zinafanya vizuri kwenye kuingizia nchi mapato makubwa
 
Ndo tunapoelekea TASAC kashaporwa mamlaka kibao kwa Sheria mpya ile Sheria yao imefanyiwa amendment
 
Na suala la utitiri wa Clearing and forwarding agents uangaliziwe.
Siku hizi kumekuwa na utitiri wa Clearing and forwarding agency companies na zingine ni za mifukoni kabisa kwa sababu ya urahisi wa kuzìanzisha na huku kukiwa na uchache wa mizigo inayokuja na kupitishwa nchini matokeo yake ma agents wengi siku hizi ni kama vishoka tu,watu wanalizwa sana na hao hao ma agent ndio wamekuwa kama ndio wanasaidia kukwepa sana kodi wakishirikiana na watumishi wa mamlaka za ukusanyaji mapato(TRA)
Bandari haina ufanisi na hata mamlaka zingine kama TRA,TMDA,TBS,GCA wamekuwa na ufanisi mdogo sana.
Napendekeza hizi Clearing agents ziwe chache zenye sifa ya kimtaji na kiuweledi na hizo ndio zitoe ajira kwa agents wengi ufanisi utapatikana tu.

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
 
Hata NMB inaendeshwa kwa ubia, puma energy inaesheshwa kwa ubia na zinafanya vizuri kwenye kuingizia nchi mapato makubwa
... unalinganisha madali wa fedha (NMB) na mission critical infrastructure za nchi - Tanesco, TRC, TPA?
 
... unalinganisha madali wa fedha (NMB) na mission critical infrastructure za nchi - Tanesco, TRC?
Inawezekana! Singapore wanafanya kwa nini isiwezekane Tanzania?
 
Back
Top Bottom