Ushauri wa namna ya kutatua changamoto ya kidini kabla ya ndoa

Ushauri wa namna ya kutatua changamoto ya kidini kabla ya ndoa

Katika mahusiano imara mwanamke akiwa na mwanaume anayejitambua hatakiwi kusikiliza sauti nyingine yoyote nje ya mwanaume wake. Kinyume chake ina maananisha mwanamke hajajicommit.

Ni sawa na mwanaume awe na mpenzi wake halafu anasikiliza maelekezo toka kwa mama yake hapo hakutakuwa na mahusiano serious.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nakazia. Kwa msimamo wake huyo mwanamke hamfai mleta uzi.
 
Ninyi ni watu wazima, chapchap ndoa ya serikali, wazazi wataelewa baadae.
 
Huu ni mtihani ambao huwezi kuushinda......dawa pekee ni kuachana na huyo binti.......vipengele vya kidini vina nguvu sana kwenye jamii zetu.......ndoa ya kiserekali ni ya kiserekali lakini kwenye macho ya kidini nyinyi ni wazinifu..........

Achana na huyo binti angali mapema ili uweze kuutibu moyo wako na upate wa kufanana nae......
Kwenye macho ya Mungu?
 
Kuna mmoja alikubali akaslimu ndoa,Watoto watatu now wanaishi kila mtu na dini yake mwanaume anamwambia mke nilibadili gelesha tu hili nikupate[emoji16],
 
UDINI TATIZO SANA MNGEOANAKISERIKALI ISINGEKUWA SHIDA SHIDA NISHASHUHUDIA FAMILIA ZA IVYO NA WAKAISHI VIZURI WATU WANAPENDANA TU TUSIWEKE UDINI MBELE ZAIDI
 
Wakuu nina mchumba wa kiislamu ambae tumeshibana sana na nataka nimuoe lakini imetokea changamoto kwa baba yake anataka nibadili dini na amekomaa kweli kweli.

Baba yake ni mtu wa dini na ni kiongozi kwenye BAKWATA. Binti hana maamuzi sana kwenye swala hilo anamsikiliza mshua wake.

Binti tulishakubaliana tufunge ndoa ya kiserikali (bomani) ili kuondoa huo mkanganyilo wa dini lakini mzee wake hataki.

Nahitaji ushauri wenu wa namna yakutatua hii changamoto.
Hii situation ni Normal sana. Hivi navyoandika miezi miwili nyuma nilitokea kumpata na kumpenda binti wa kiislam huko zenji.

Mimi upande wangu sina shida na Dini. Ni Mkristu niliye safi na kuelewa Ukristu vyema hivyo kuoa binti wa kiislam kwangu isingekuwa shida sababu Uislam umetokea kwa ISHMAIL mtoto wa Abraham kutoka tumbo la kijakazi wake aliyepewa na Sarah mkewe ambaye hakupata mtoto hadi alipofikisha miaka 90+. Hivyo kwa Imani yangu dhabiti ya Ukristo kama Dini Sahihi, kabla ya kurudi kwa Yesu Kristu.


Changamoto ikaa pale manzi hataki mwanaume wa Kikristu sababu ameshakuwa na wanaume wawili wa kikristu na mahusiano hayakwenda vizuri na katika maisha yake ame date mwanaume mmoja tu wa Kiislam.

Hivyo mwanaume baada ya kusoundisha vya kutosha nikaona hapa siwezi kubadili mtazamo wa huyu binti nikaamua kuchapa lapa na kukamata njia mwelekeo kutafuta mwingine wa kutulia nae.

Kijana kama hapo utashindwa kuweka mimba. Nakushauri tembea na beat kutafuta mwingine.
 
Hicho kitu Ni kidogo sana,Mm enz zangu way back 2013 , nilimpata bint wa kipemba,It was same story like you.mzee wake alikomaa nibadili dini tena nilipoenda kumchumbia alimtaarisha na shekh wa wilaya kabisa ili anislimishe,nlikataa ila bahati mbaya mchumba alikuwa na ujauzito, baada ya kushindwa kunislimisha sikurud Tena Hadi leo lakin Hadi sasa bint nipo nae na mtoto yupo class 2, hivo Kama utaweza piga mimba ukishindwa tafuta mwanamke mwingine, OVER.
Unasimulia ujinga unajiona mjanjaaa
 
Umeshaonesha udhaifu.

Unaolewa wewe.

Kama ameshindwa kuiteka Imani yake tafsiri yake hata moyo wake ameshindwa.
Mwanamke akikupenda anaweza fanya lolote Kwa ajili ya Mpenzi wake.

Anachojaribu Kueleza jamaa hapa ni kuwa Huyo Mchumba Ake hampendi.
Ingekuwa ni Mimi napita kushoto.
Wala muda WA kumpiga mimba mtu ambaye hakupendi ni kupoteza muda.
 
Katika mahusiano imara mwanamke akiwa na mwanaume anayejitambua hatakiwi kusikiliza sauti nyingine yoyote nje ya mwanaume wake. Kinyume chake ina maananisha mwanamke hajajicommit.

Ni sawa na mwanaume awe na mpenzi wake halafu anasikiliza maelekezo toka kwa mama yake hapo hakutakuwa na mahusiano serious.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huyu binti ana upendo wa dhati kabisa, ishu ni hapo tu kwa mshua wake.
 
UDINI TATIZO SANA MNGEOANAKISERIKALI ISINGEKUWA SHIDA SHIDA NISHASHUHUDIA FAMILIA ZA IVYO NA WAKAISHI VIZURI WATU WANAPENDANA TU TUSIWEKE UDINI MBELE ZAIDI

Waislamu ndio shida.. wanawake wao hawataki waolewe na wakristo.. huku wao wenyewe hawawezi kuwatunza hao wanawake zao
 
Badili dini,oa,mzalishe halafu rudi kwenye dini yako pamoja naye.

Uzuri uislamu hauna mambo mengi,unasilimishwa na kuoa papo kwa papo bila hata mafundisho.
Hapo ni swala la imani mkuu, siwezi kubadili dini sababu ya ndoa. Solution ni kiwa neutral kwa maana ya kufunga ndoa ya kiserikali then maisha yaendelee. Tutabariki mbele ya safari
 
Ushauri wa humu wengi wanapotosha.

Palipo na upendo Kuna maelewano mkuu. Usikubali kumpoteza huyo mama watoto

Ndoa inaongozwa na mambo makuu mawili
1. Upendo
2. Sheria

Unapounda familia/serikali lazima kuwe na SHERIA ambazo hufuata baada ya Upendo.

Sheria za familia lazima ziwe na kitabu cha Muongozo, ambayo ndio Katiba.
Anayeongoza familia/Baba ndiye hutoa sheria ili kudhibiti Mabadiliko yoyote ya kitabia, kihisia na kiakili yatakayotokea ndani ya familia.

Kama Mwanamke amekataa tafsiri yake hataki kuongozwa na Mshikaji hiyo ndio maana. Yaani huyo Manzi yey ndiye anataka kuongoza hiyo serikali.
 
Unasimulia ujinga unajiona mjanjaaa
Acha ujuaji wew,upi ujinga wangu?au ulitaka niache dini yangu kwa ajil ya mwanamke!?huwa mnapenda sana watu wafuate dini yenu,ndio Tena najisifu nimemuwin mpemba kabadili yeye mwenyewe na kakil ameenda sehem sahihi.
 
Mkuu tulishakubaliana kuwa watoto watakuwa upande wa imani yangu. Hilo halina ubishi, changamoto ni hapo kwa mshua wake tu, tukivuka hapo tumetoboa.

Watoto ni wamama ndugu YANGU.
Malezi yanatoka Kwa Mama.

Sasa utaoaje mwanamke ambaye hatawafundisha watoto wako kile unachotaka awafundishe.
Anyway kila mtu ananamna yake ya kuunda Familia.
Ila weka akilini watoto wadogo hujifunza tabia za Mama Kwa urahisi zaidi kutokana na ukaribu wao na Mama Yao.

Ushauri, Kwanza hukupaswa kujadiliana Naye mambo ya Dini Bali ungemfundisha indirect way mpaka auone Ukristo ni mzuri Kwa matendo zaidi kuliko maneno.
Unachotakiwa kukifanya ni kumbadilisha huyo Shemeji yetu awe vile utakavyo ndipo umuoe.

Vinginevyo unajipa kazi huko mbeleni.
Zingatia, tofauti za Kidini ni moja ya sababu za kisheria za kuvunja Ndoa
 
Hicho kitu Ni kidogo sana,Mm enz zangu way back 2013 , nilimpata bint wa kipemba,It was same story like you.mzee wake alikomaa nibadili dini tena nilipoenda kumchumbia alimtaarisha na shekh wa wilaya kabisa ili anislimishe,nlikataa ila bahati mbaya mchumba alikuwa na ujauzito, baada ya kushindwa kunislimisha sikurud Tena Hadi leo lakin Hadi sasa bint nipo nae na mtoto yupo class 2, hivo Kama utaweza piga mimba ukishindwa tafuta mwanamke mwingine, OVER.
Wala sio kitu cha kujisifia hiki
 
Mkuu tulishakubaliana kuwa watoto watakuwa upande wa imani yangu. Hilo halina ubishi, changamoto ni hapo kwa mshua wake tu, tukivuka hapo tumetoboa.
Mkuu tafuta mwana mke mwingine huyo amesha kushinda.

Siku zote wazazi wa mchumba wako wakikukataa usilazimishe maana undani wa familia yao huijui ukirazimisha unaweza kufungua mlango wa matatizo makubwa katika maisha yako.

Wanawake wapo wengi sana wanahitaji kuolewa tena wa dini yako.

Na kusisitiza achana na huyo binti ,hao wanao kumshauri sijui umpe mimba sijui umtoroshe wana kupotosha maana hujui huyo mzee ni jinsi gani anampenda binti yake anaweza kukufanyia kitu kibaya.
 
Back
Top Bottom