Ushawahi Kupokea muujiza gani ukaamini kuwa Mungu yupo?

Ushawahi Kupokea muujiza gani ukaamini kuwa Mungu yupo?

Nililipwa kiasi kikubwa cha hela kwa ajili ya shughuli fulani,ila nikazifanyia shughuli tofauti,tajiri yangu akanisakama sana hadi niliposikia amefariki nikajua Mungu yupo.
Mweeeh mweeh!
 
Muujiza hautoshi kuthibitisha uwepo wa M-ngu,even devils can do miracles.

Kinacho thibitisha uwepo wa M-ngu ni personal divine encounter,yaani M-ngu mwenyewe anajifunua kwako kibinafsi,hakuna dini wala sayansi inatosha kuthibitisha uwepo wa M-ngu,it must be your personal divine experience,binafsi nimeshakutana na malaika 2 times na nime encounter na Mwana wa M-ngu 1 time,sihitaji mtu wa kunithibitishia,Mimi mwenyewe nimethibitisha.
Unajuaje hii ni personal divine enconter na si ugonjwa wa akili tu unakufanya uone maruweruwe?
 
Wakuu,
mimi ni muajiliwa katika moja ya duka kubwa jirani kwangu,nimeajiliwa tangu 2021,mwaka 2023 mwajili wangu alinifuta kazi kutokana na sababu za hapa na pale,ilikuwa ni mchana,nikajiondokea kwenda nyumbani nikiwa sina matumaini tena,asubuhi yake akanipigia simu kuwa niendelee na kazi,tena kwa kuniomba msamaha,nikarudi,baadae anijengea nyumba ya bati nyumbani manake mwanzo zilikuwa nyumba za makuti, na mpaka leo,nipo dukani kwake,katika miradi yake hasa ya ujenzi,na usimamizi wa nyumba za kupanga nasimamia mimi,na mwezi wa nne ananilipia mahari nioe,kama sio Mungu aliyetenda ni nani/nini?
 
Nililipwa kiasi kikubwa cha hela kwa ajili ya shughuli fulani,ila nikazifanyia shughuli tofauti,tajiri yangu akanisakama sana hadi niliposikia amefariki nikajua Mungu yupo.
haaah[emoji32][emoji46]
 
Nimejua kulingana na upeo wangu.
Huo upeo wako unauhakiki vipi?

Unajuaje kuwa huna ugonjwa wa akili tu unaokufanya ufikiri Mungu yupo na kuona hayo mauzauza unayosema Mungu kakutokea wewe mwenyewe?

Hujajibu swali hili.
 
Moja ya jibu dhaifu sana mkuu, huna hoja upuuzwe Kiranga
Si unaona mkuu?

Yani mtu anashusha viwango vya mazungumzo mpaka unatamani usimjibu tu.

Sasa mtu anayekujibu kama guluguja asiye na ubongo wala uti wa mgongo ukimbeza utakuwa umekosea?
 
Si unaona mkuu?

Yani mtu anashusha viwango vya mazungumzo mpaka unatamani usimjibu tu.

Sasa mtu anayekujibu kama guluguja asiye na ubongo wala uti wa mgongo ukimbeza utakuwa umekosea?
Huyo atakuwa anaburuzwa asijue anaabudu nini,amejaribu kuleta utetezi wake kutetea asichokijua,ila amepigwa maswali ameshindwa atetee vipi, watu wa namna hii tunao katika jamii,na ukute katika mtaa wao yeye ndiye mwenyekiti,wanamwamini kuwa mzee wenye hekima na maarifa, ila humu tunamwona kana kwamba ni mmoja wa member asiye na mchango wowote jukwaani. Kiranga Tanzanian Dream
 
Vip mdogo wako naye?

Mdogo wangu naye alipona.

Magari baada ya kugongana, kabla ya kushika moto, basi liliendelea kubiringida mpaka kwenda kutulia nje ya barabara ambako kulikuwa na moto unawaka kwenye nyasi. Mimi na jamaa mmoja tulikuwa wa kwanza kutoka, tukipitia upande wa juu kwenye dirisha lilivunjika. Mara baada ya kutoka, nilikazana kuzima moto kwenye nyasi kwa kutumia matawi, lengo nikitaka niingie kumtafuta mdogo wangu. Mara kwa mbali, tulikotokea nikamwona mdogo wangu anakuja. Kumbe yeye alirushwa nje ya basi kupitia nyuma ambako kulikuwa kumebomoka. Yeye hakufika nasi kule mwishoni.

Mara baada ya kumwona, nikaishiwa nguvu, nikaa chini, moto ukalifikia basi, likashika moto. Moto ukawa mkubwa kiasi cha kuzuia mtu yeyote kulusogelea. Mdogo wangu sijui aligongwa na kitu gani, alikuwa amevimba kwenye paja, lakini alikuwa anatembea kwa kuchechemea. Mimi nilijaa damu maeneo mengi lakini siyo kutoka kwenye mwili wangu, ni za watu wengine. Sikuwa na jeraha lolote la kuonekana, japo nilikuwa nasikia maumivu ya wastani kwenye kifua. Vipimo vyote vilionesha sikuvunjika sehemu yoyote.
 
Mdogo wangu naye alipona.

Magari baada ya kugongana, kabla ya kushika moto, basi liliendelea kubiringida mpaka kwenda kutulia nje ya barabara ambako kulikuwa na moto unawaka kwenye nyasi. Mimi na jamaa mmoja tulikuwa wa kwanza kutoka, tukipitia upande wa juu kwenye dirisha lilivunjika. Mara baada ya kutoka, nilikazana kuzima moto kwenye nyasi kwa kutumia matawi, lengo nikitaka niingie kumtafuta mdogo wangu. Mara kwa mbali, tulikotokea nikamwona mdogo wangu anakuja. Kumbe yeye alirushwa nje ya basi kupitia nyuma ambako kulikuwa kumebomoka. Yeye hakufika nasi kule mwishoni.

Mara baada ya kumwona, nikaishiwa nguvu, nikaa chini, moto ukalifikia basi, likashika moto. Moto ukawa mkubwa kiasi cha kuzuia mtu yeyote kulusogelea. Mdogo wangu sijui aligongwa na kitu gani, alikuwa amevimba kwenye paja, lakini alikuwa anatembea kwa kuchechemea. Mimi nilijaa dakuwa na jeraha lolote la kuonekana,
Mungu ni mkuu sana.
 
Mpaka sasa hakuna mtu aliyethibitisha Mungu yupo.

Miujiza siyo uthibitisho pekee wa uwepo wa Mungu. Uwepo wa Mungu na yale anayotuagiza kwa njia ya manabii wa kale ni masuala ya imani. Jambo lolote la kiimani halithibitishwi kwa majaribio ya kisayansi.

Kutoamini kuwa Mungu yupo, wewe huwezi kuwa wa kwanza, hata hapo kale walikuwepo, na inathibitishwa kwenye biblia:

Zaburi 53:1​

Mpumbavu anasema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa, hakuna hata mmoja atendaye mema.

NB: Kuanzia pale uwezo wa mwanadamu unapoishia, ndipo ukuu wa Mungu unapoanzia.

Mwanasayansi mmoja alikuwa akidai kuwa Mungu hayupo. Akaambiwa aeleze mwanzo wa mwanadamu ni nini? Akasema mwanadamu alitokana na wazazi wa kale. Akaulizwa na hao walitokana na nini? Akasema hao watakuwa walitokana na cells zilizo-undergo evolution ya muda mrefu. Akaulizwa na hizo cells zilitoka wapi? Akasema, there must be a power without which nothing can be done. Wanateolojia wakamwambia, hiyo POWER ndiyo MUNGU mwenyewe.

"aheri anayeamini bila kuona'
 
Mungu ni mkuu sana.

Amina. Na kamwe sitaacha kuukumbuka ukuu wake na wema wake kwangu. Kuna mengi aliyonitendea ambayo wengine watasema ni ya kawaida, lakini mimi naamini ni kwa neema zake.
 
  • Thanks
Reactions: K11
Miujiza siyo uthibitisho pekee wa uwepo wa Mungu. Uwepo wa Mungu na yale anayotuagiza kwa njia ya manabii wa kale ni masuala ya imani. Jambo lolote la kiimani halithibitishwi kwa majaribio ya kisayansi.

Kutoamini kuwa Mungu yupo, wewe huwezi kuwa wa kwanza, hata hapo kale walikuwepo, na inathibitishwa kwenye biblia:

Zaburi 53:1​

Mpumbavu anasema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa, hakuna hata mmoja atendaye mema.

NB: Kuanzia pale uwezo wa mwanadamu unapoishia, ndipo ukuu wa Mungu unapoanzia.

Mwanasayansi mmoja alikuwa akidai kuwa Mungu hayupo. Akaambiwa aeleze mwanzo wa mwanadamu ni nini? Akasema mwanadamu alitokana na wazazi wa kale. Akaulizwa na hao walitokana na nini? Akasema hao watakuwa walitokana na cells zilizo-undergo evolution ya muda mrefu. Akaulizwa na hizo cells zilitoka wapi? Akasema, there must be a power without which nothing can be done. Wanateolojia wakamwambia, hiyo POWER ndiyo MUNGU mwenyewe.

"aheri anayeamini bila kuona'
Imani si uthibitisho.

Imani ni haki ya kikatiba na kiutu ambayo haihitaji uthibitisho.

Usichanganye madawa.
 
Back
Top Bottom