Usipokuwa makini utajikuta unachangia harusi 5 hadi 6 kwa mwezi

Usipokuwa makini utajikuta unachangia harusi 5 hadi 6 kwa mwezi

Ni rahisi sana. Iko hivi, kama hujawahi kuomba mtu mchango, hakuna mtu anayestahili mchango wako. Hauna deni.

Maana yake mtu anapokuomba mchango, unaweza kumjibu direct kwamba 'samahani sitaweza' na yeye hawezi kuku press kwasababu hakudai - hujawahi kumchangisha.

Ukiwa na msimamo thabiti watu wataliona hili na wataacha kukusumbua. Binafsi kwa mwaka nachangia harusi za mtu mmoja au wawili - ambao ni ndugu nimekuwa nao na tumeshibana.

Sichangii sherehe ya ndugu wa ndugu, rafiki wa ndugu, ndugu wa rafiki na third parties nyingine kama hizi. Hata ndugu ambaye simfahamu (ndugu wa kuambiwa tu - sijawahi kuonana naye) sichangii.

Nimekuwa na msimamo katika hili kiasi cha kwamba siombwi michango wala siaddiwi kwenye magroup.

Ukisema 'hapana' za kutosha, watu wataacha kuomba
Yataka moyo, hongera watu wako ni waelewa sana
 
Hii app ya Whatsapp sioni faida yake kabisaaa imegeuka kausha damu kwangu, imagine nina group tano za michango ya harusi na zote zinadai 50K kwenda juu. Na bado sijui kama kutakucha bila kuongezwa kwenye group jingine.

Yaani kila siku unaungwa kwenye magroup mpya za harusi, watu hata huwajui unaambiwa ni kaka yake Fulani, au ni ndugu wa Fulani then mkeka unawekwa uanze michango, sms usiku na mchana ni michango tu.

Hivi watu hawawezi oa bila kuchangiwa? Uoe wewe tukuchangie sisi? Au ndoa zinakuja kwa kushitukiza? Ka mshahara kenyewe 500K na ndugu wananitazama duh!

HAPANA.
Siku nikuchangia kwenye harusi more than 100k wakiachana watanilipaaa
 
Tatizo ni pale unachangishwa hadi michango ya harusi ya Mjomba wake na rafiki yako duh!

Kama walikuchangia kipindi cha harusi yako na wewe wachangie kipindi cha harusi zao .

Kama hawakukuchangia katika harusi yako na wewe usichange harusi zao...........

Mwisho kabisa katika maisha jifunze kuwa na msimamo sio leo hii unawakataa watu wa karibu alafu kesho kutwa unawahitaji kipindi una jambo lako
 
Hii app ya Whatsapp sioni faida yake kabisaaa imegeuka kausha damu kwangu, imagine nina group tano za michango ya harusi na zote zinadai 50K kwenda juu. Na bado sijui kama kutakucha bila kuongezwa kwenye group jingine.

Yaani kila siku unaungwa kwenye magroup mpya za harusi, watu hata huwajui unaambiwa ni kaka yake Fulani, au ni ndugu wa Fulani then mkeka unawekwa uanze michango, sms usiku na mchana ni michango tu.

Hivi watu hawawezi oa bila kuchangiwa? Uoe wewe tukuchangie sisi? Au ndoa zinakuja kwa kushitukiza? Ka mshahara kenyewe 500K na ndugu wananitazama duh!

HAPANA.
Bwana wee nashangaa sana sasa burudani upate wewe kero tupate sie...haya basi tukichanga na sie tumuonje bibi harusi na bwana harusi 🤣🤣🤣🤣
Ila michango inakera kweli kweli. Wacha tuu.
 
Watu wa kaskazini muache harusi za showoff maana marafiki zangu wanaotokea kaskazini na wahaya ndio wanapenda sherehe za kuchangiwa .

Oeni kimya kimya , kuchangiwa ni ushamba , unakaa unapigia simu usiku missed call hata 6 ili uombe mchango .

Hata iwe vip lakini kuomba michango ni aibu kubwa , kila siku ni nyie kuomba pesa .
 
Inakuwaje mtu unachangisha mchango wa harusi?, ina maana unataka jambo kubwa kuliko uwezo wako kwa gharama za watu wengine. Hii haipo sawa.

Wewe fanya jambo lako kwa usawa wa uwezo.
Watu wa kaskazini ili wafanye showoff ndiowanapenda sana , kwa kweli ni aibu kuomba michango harusi ni private tena kimya kimya kishkaji unamaliza kazi .

Unakuta mtu anatuma kwa kila mtu meseji hiyo hiyo mpaka kero .
 
Hivi inakuwaje mtu furaha yake binafsi aliyo ipanga kwa muda mrefu anataka watu wamchangie pesa ?
Mnamchangia mtu akale mbususu.
Unatoa 50 000,unapewa vipilau vimepwayapwaya na kibawa na tubia tuwili baasi.
Hapo,safari za kanisani ukumbini li program lireefu.
Then mnapigiwa wimbo wa aurlus mabele mnaagwa.
Mbaya zaidi mwaka tu wanakuja kuomba ushauri.
Pumbavu sifanyi ujinga huo.
 
Kuna jamaa mmoja aliwaingiza mkenge wachangiaji wa harusi yake. Ilipofika siku ya kufunga ndoa akaenda kufungia bomani bila kufanya sherehe na hakufungia ndoa kanisani kama alivyopanga awali. Fedha za michango akazigeuza mtaji wa kufungua duka.
 
Kuna jamaa mmoja aliwaingiza mkenge wachangiaji wa harusi yake. Ilipofika siku ya kufunga ndoa akaenda kufungia bomani bila kufanya sherehe na hakufungia ndoa kanisani kama alivyopanga awali. Fedha za michango akazigeuza mtaji wa kufungua duka.
😂😂😂naunga mkono hoja
 
Ni zaidi ya ushamba mkuu
Watu wa kaskazini muache harusi za showoff maana marafiki zangu wanaotokea kaskazini na wahaya ndio wanapenda sherehe za kuchangiwa .

Oeni kimya kimya , kuchangiwa ni ushamba , unakaa unapigia simu usiku missed call hata 6 ili uombe mchango .

Hata iwe vip lakini kuomba michango ni aibu kubwa , kila siku ni nyie kuomba pesa .
 
Back
Top Bottom