UTAFITI: Dhana ya Mfumo Kristu Tanzania na Ukweli wake

Status
Not open for further replies.
Ndugu yangu Yeriko, kama kweli ulizunguka mikoa uliyotaja, ni wazi kuwa ulitumia gharama si kidogo bali ni kubwa kwa misingi ya kiuchumi na muda pia. Lakini nasikitika kukueleza kuwa, matokeo ya utafiti wako yamebeba ujumbe ufuatao:

(a) Huna uzoefu na masuala mazima ya utafiti kwa sababu hukuaddress swali la utafiti (Hypothesis) na hivyo kutoka nje ya swali.
(b) Huenda ulifanya vizuri kwenye utafiti lakini, aliyekufadhili amekulazimisha kutoa matokeo ya aina hii.
(c) Umefanya utafiti huku ukiwa na majibu kichwani ambayo ndo unataka tuyaamini.

Kwa ufupi ni kwamba ulichokieleza siyo utafiti uliyokusudia kujibu swali la Je ni kweli kwamba kuna mfumo kristo katika uendeshaji wa Serikali?

Pengine ningekuona kuwa umefanya utafiti iwapo ungekuja na matokeo yanayojibu masuala na sio idadi ya waumini ambayo kwa kawaida ilitakiwa iwe sample tu na siyo conclussion ya issues. Mathalani badala ya kutuorodheshea idadi ya waumini wanaoshiriki kwenye hizo shughjuli ulizozitumia katika utafiti wako, sample hiyo ungeitumia kupata maoni yao yanayokanusha au kuthibitisha hypothesis yako.

Pia utafiti wako umepotoka kwa sababu hukujipa shida ya kujiuza nini maana ya mfumo kristo ambapo baada ya kutupatia tafsiri, ungetumia sample yako kukanusha au kuthibisha hypothesis yako.

Ni kutokana na ukweli huo, tafadhali naomba utupatie majibu ya kweli ya utafiti wako la sivyo tutaamini kuwa wewe ni miongoni mwa wasomi wengi wa kibongo ambao hawakuelimka na hawataki kuelimika licha ya kusomeshwa na raslimali za nchi kwa niaba ya wengi.
 

Huyu hata sijamuelewa mantiki ya uzi wake nini. Anasema amefanya research kuhusu mfumo kristo halafu anahoji mfumo kristo nini na unaendeshwaje?. Yericko hebu pitia shule za sekondari advanced level uangalie ratio ya waislamu nawakristo ikoje na ujiulize f1 walianza wangapi na wameishia wapi na ni kwanini?, pitia vyuo vikuu na colleges nako uje na ratio yake then utuambie nini tatizo waonekane wakristo weng kuliko waislamu. Jiulize why private hospital kama Bugando madaktar wanalipwa na serikali pamoja na ruzuku wanayopata kutoka serikalini lakini sio Hospital kama Alhudaa pale tanga et al?
Jiulize viongozi wangapi bungeni, wizarani, mashuleni, na kwingineko ni wakristo weng kuliko waislamu halafu uniambie tatizo nini?
Few to mention.
 
Hongera sana Yeriko. Kila anapoijua KWELI, mwanadamu huzidi kuwa huru. Kweli huweka watu huru. Ni hatua kubwa kufungua baadhi ya watanza from beliefs and attitudes.
Nakushuru sana mkuu,
 

Sijakutukana na situkani.
Post zako na wengine zina maneno ya vijembe kwa Wakristo na Ukristo, unafikri mimi nitaita hayo maneno ya vijembe nini zaidi ya chuki???
Nilipo unganisha na Somalia ni kukutaka wewe na wote wenye mtazamo wako watafakari maneno yao yao dhidi ya neno MFUMO KROSTO TANZANIA kwani Somalia ni nje ya Tanzania.

Mwisho mimi sikuangalia Bhangi kwa Bob Marley badala yake nilisoma au kusikiza mistari yake yenye ujumbe mzuri. Naupenda Ukristo ndio mana sijamhukumu Bob Marley badala yake nimemuachia MUNGU yeye ndie ahukumu kwa kua yeye huhukumu kwa haki.
 

Acha Upotoshaji, Serikali ni Party to Contract sio Observer au Agent wewe, Sasa hivi hatua ya kukanusha imeshavuka, ni hatua ya kutaka kujua matumizi halisi! Ulianza kufanya Reserch kabla ya kujua maana na hatua pamoja na Mbinu zake , Wakongwe wa Reserch wanasema ' Reserch is not All about Abundancy of Data but ACCURACY OF it'. Umenifurahisha sana kusoma '...Utafiti wa Mikoa kadhaa juu ya Mfumo Kristo...' Usiku mwema Kamanda!
 

Mimi si Biblia ama kuruwani,

Wala sio alfa na omega,

Nimefungua milango ya wengine, sasa njia ni nyeupe!

Na ukweli uje
 

Usiogope Vijembe hata nyie Mnarusha, Ni sawa kupiga Bikra halafu ukaogopa kuchafuka Damu, hivi unasubiri hukumu ya Mungu kusema Bob Marley alikuwa Mvuta bhangi? Kusema Waislam ni wakorofi kwa kuwa kila walipo kuna Vurugu ni sawa na kusema miaka ile ya 1960 eti Watu weusi ni wakorofi kwa kuwa kila walipo kuna fujo, Africa,Ulaya na Marekani kote walikuwa wakipambana kwa hiyo useme, Akina Mandela,Kwame,mondlane,Malcom X,Martin Luther ni watu wakorofi! Usiku mwema, hatuna Chuki nnyi tunachuki na Dhulma!
 
Takwimu zilizopo humu hazina ukweli kwa kiwango kikubwa. Wanasiasa 521,000 Dar unamaanusha wanachama WA vyama vya siasa au viongozi? Sidhani kama kuwa mwanachama WA chama cha siasa automatically unakuwa mwanasiasa. Na kama Ni viongozi, uongozi WA kisiasa unaanzia ngazi ya mtaa, sidhani kama Dar Ina mitaa laki tano, no way...

Hope kwenye ajira umeongelea sekta zote na sio public peke yake kama watu wanavyodhani.

Pia napata shida Sana kuamini kuwa mtafiti anaweza kutembelea maduka 489,000. Ina maana hii Ni sensa, yaani umetembelea entire population. Je ulikuwa na maswali unauliza au checklist? Nijuavyo researcher makini anaweza kuwafikia watu 10 kwa siku maximum, kwa hiyo kama ulikuwa na watafiti 1000 wangetumia siku 48 kutembelea maduka ya kariakoo na hata kama ulikuwa unawalipa 10,000 kwa siku maana yake ungetumia shs 480,000,000. Sina hakika unafanya biashara gani lakini siamini kama unaweza kutumia hela yote hii kwa tafiti ya kuangalia mfumo kristo. Unless ulete Raw data, sisi researchers hatuwezi hata robo kukubaliana na wewe
 

Jisomee hapa kwa kupanua ufahamu wako kidogo ewe ndugu uliyeharibiwa na ngano za akina Ilunga na Mohamed Said

http://bit.ly/19SFYet
 
Mkuu wangu,

Nikujuze tu kuwa mpaka mwezi uliopita yani mwezi wa nane, Dar es Salaam ilikuwa inakadiriwa kuwa na wakaazi 5.1 milioni,

Sasa ukiona watumishi wa umma laki 8 ni maajabu basi mimi nitakuona wewe ndio wa maajabu zaidi,
watumishi wote wa umma nchi nzima hawazidi laki 6.
 

NAKUUNGA MKONO. hUYU JAMAA ALITAKA KUWASISHA MESEJI YAKE TU NA SIYO UTAFITI KAMA ANAVYODAI.
 

Kuna wakati ni vema kuruhusu mshangao akilini na moyoni mwako,
 

kwa mtazamo huu wa kujidharau mtaendelea kuwa wa nyuma milele! Badilikeni.
 
MOU ni mkataba kati ya serikali na kanisa ili serikali itoe ruzuku kwa shughuli za kijamii kama mahospital na mashule yaliyoko chini ya kanisa.kwahiyo MOU haiwahusu huduma za kijamii nje na zile za kanisa.
 
watumishi wote wa umma nchi nzima hawazidi laki 6.

Mkuu acha kufikiri kwa karibu hivyo ndugu,

Nikuulize swali dogo tu,

Mtumishi wa umma ni yupi?

Kwaarifa yako ndugu,

Vyombo vya ulinzi na usalama JWTZ, JKT,JKU, KmKM,Polisi, Zimamoto,Wanyamapori, na Mageza idadi yao wanafika 3.6 milioni, hapo idara ya usalama wa taifa haijahusishwa,

Hao wote ni watumishi wa umma,

Sasa kwa akili yako fupi unadhani watumishi wa umma ni wale masekretari pale utumishi tu???
 
MOU ni mkataba kati ya serikali na kanisa ili serikali itoe ruzuku kwa shughuli za kijamii kama mahospital na mashule yaliyoko chini ya kanisa.kwahiyo MOU haiwahusu huduma za kijamii nje na zile za kanisa.

Nimeweka hapo juu link ya MOU hebu nenda isome usipoteshe jamii hapa,
 
tatizo huweki hata link za kusapoti maneno yako,na unataka watu waamini,sikubaliani na hiyo hesabu.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…