Utafiti Wangu: Watoto wengi hupenda zaidi ndugu upande wa mama kuliko upande wa baba

Utafiti Wangu: Watoto wengi hupenda zaidi ndugu upande wa mama kuliko upande wa baba

Niliwahi kuhudhuria send off ya rafiki yangu mmoja. Eti wakati wa mawaidha mama wa mke anasimama na kusema, "baba tumekupa huyu binti hana alama yoyote ya kipigo mwilini mwake. Ikitokea amekushinda au mmeishana tafadhali usimguse, mrudishe tu nyumbani kama ulivyomchukua." Huu ni ujinga mkubwa na ni pigo kuu kwa ndoa. Mwanamke huingia kwenye ndoa mguu mmoja ndani mmoja nje. Hana cha kupoteza kwenye ndoa no matter what happens.

Sasa mimi nilimwambia jamaa yangu, "ingekuwa mimi ndio naoa, ndoa hii ingeishia hatua hii hii ya send off, basi!!" Jamaa hakunielewa kabisa. Usithubutu kuoa mwanamke ambaye wazazi wake hawako radhi kumwacha huru. Huwezi kamwe kujenga familia imara badala yake itakupasa wewe ndio uwe nafasi ya mke kusudi ndoa idumu. Matokeo yake upande wa mwanamke utakuwa na nguvu kwenye ndoa yenu kwa, sababu bila hivyo mke hakai.

Mke bora kabisa ni yule ambaye maisha yake ameyatoa asilimia 100 kujenga ndoa yake. Mwanzoni roho yake iliambatana na wazazi wake, lakini tangu mwanamume alipomwingilia akamtoa bikra, alipanda ndani yake roho mpya ambayo inakwenda kuziba gap lililokuwa likijazwa na wazazi. Sasa amefungamana na mtu mpya, ndio maana binti kabla ya kufanya mapenzi kwa mara ya kwanza huripoti kwa wazazi kila tukio linalohusu mapenzi. Ila siku akiingiliwa tu, huanza kuficha kila tendo wazazi wasijue, hakuna tena muunganiko. Anaweza hata kubanwa gheto kwa msela kwa siku kadhaa huku wazazi wakihaha kumtafuta.

Sasa ukioa mwanamke wa aina hii, hawezi kuwa na muunganiko wa kweli na mumewe, achilia mbali ukoo wa mume. Kwake yeye wazazi ni kimbilio pale anapoharibu, kwa sababu rohovyake ishavurugwa na wanaume wengi, hivyo ana emotional blur. HAJUI KUPENDA, anategemea mashosti wa Instagram na semina za akina mauki wamfundishe mapenzi ni nini. Amesahau kuwa alitoroka darasani pale wazazi wake walipokuwa wakifundisha kwa mtaala halisi wa malezi, akakimbilia ukahaba. Sasa akiingia kwenye ndoa ataishi kwa experience ya hao wanaume walio tangulia kuwa naye, atamchukukia mume wa ndoa kama WANAUME WENGINE TU. Kwa mtindo huu kwa nini asiimarishe ukoo wake ndani ya ndoa?

Kosea yote, lakini usikosee kuoa, majuto yake ni makuu.

Asante
umeongea ukweli unaouma, wengi wataukimbia huu mchango wako.
 
Wazazi wa, binti wanamfundisha kuwa aishi kwa ujanja ndani ya ndoa. Yaani anapoingia tu aanze kujiandaa kutoka kwani tayari wanamjua binti yao kuwa tabia zake si za mke wa ndoa. Mke anawafanya wazazi wake kuwa ndio wasiri wake, anawasikiliza wao zaidi kuliko mume wake.

Wazazi wa mume wanamfundisha kuwa usithubutu kumwamini mke kwani wengi wamewaangamiza waume zao. Mume anakuwa na mahusiano zaidi na ndugu kuliko mkewe hasa kwenye mambo ya kuijenga familia yake mwenyewe.

Sass ukitazama ujinga huu unajiuliza, kuna sababu gani ya kuingia kwenye ndoa? Sababu pekee inayobaki hapo ni kutaka kumiliki sekta ya ngono, basi. Katika hayo hapo juu hakuna mpango wa malezi bora kwani hakujalenga kuwaandalia watoto mazingira bora kwa siku zijazo. Faida pekee ni ngono tu. Watoto watakuwa kero badala ya baraka, lakini tutataka tuzae kwa sababu tu watu hawawezi kutuelewa tusipokuwa na watoto. Tutasimangwa na kuchekwa, hivyo tunazaa ili kuwaridhisha watazamaji wala si kwa sababu ya kujenga familia.

Kwa mazingira haya TANGU AWALI NDOA HAIKUWAPO. Ni malaya wawili wameamua kuishi ndani ya nyumba moja bila muunganiko halisi wa mke na mume. Tena basi wazazi wao wanajua fika kwamba hapo hakuna ndoa ndio maana wamewaandaa siku wakikorofishana wagawane mapato ya hicho kikoba, kila mtu aendelee na maisha yake binafsi.
ukweli mtupu.
 
Mimi niko karibu sana ndugu zangu upande wa baba na si mama. Ila hata kwa baba watoto wa mashangazi ndio tuko nao karibu mno. Tunaweza ongea kwa simu hata masaa 2. Ila kimbembe kiko kwa watoto wa bamkubwa na mdogo hao huwa tunaonana siku ya matukio tu.
Ukweli ni kwamba ni rahisi kuwa karibu na familia ambayo mwanamke ndio ndugu yako, kwasababu mara nyingi mwanamke ndio mfalme wa nyumbani, ndio anaangalia welfare za nyumbani zote. Hivyo in most cases ndugu upande wa baba utakaokuwa nao karibu ni watoto wa shangazi zako na sio baba wadogo/wakubwa. Upande wa mama ndugu utakaokuwa nao karibu ni upande wa mama zako wakubwa na wadogo, wajomba haiwezi kuwa Sana.
 
Ukweli ni kwamba ni rahisi kuwa karibu na familia ambayo mwanamke ndio ndugu yako, kwasababu mara nyingi mwanamke ndio mfalme wa nyumbani, ndio anaangalia welfare za nyumbani zote. Hivyo in most cases ndugu upande wa baba utakaokuwa nao karibu ni watoto wa shangazi zako na sio baba wadogo/wakubwa. Upande wa mama ndugu utakaokuwa nao karibu ni upande wa mama zako wakubwa na wadogo, wajomba haiwezi kuwa Sana.
Kina mama wakiolewa wanapasua sana koo za watu.
 
Not really, sijui hata niiwekeje hii...mimi ni mwanamke, ninapoenda kwenye nyumbani yoyote inategemewa nitakuwa na connection zaidi na mwanamke, likifanikiwa hili ndio nitakuwa na uhuru kwenye hiyo nyumba maana lazima tukubali kuwa mwenye nyumba ni mwanamke. Sasa nikienda kwa sister nakuwa tayari tuna connection na tumezoeana ila nikienda kwa bro mtu ambaye nimemzoea ni bro kuliko mkewe ambaye ndio mwenye nyumba hapo kwa hivyo siwezi kuwa comfortable maana mtu niliyemzoea na yeye ni 'mgeni'katika hiyo nyumba. Sijui kama nimeeleweka
Umeeleza vizuri sana, mahali popote pale utakapokwenda, jua mwenye nyumba ni mwanamke, huo ndio ukweli, ama unapenda au hupendi. Hivyo ni rahisi kujenga ukaribu mahali ambapo ndugu yako ni mwanamke (ndio mama mwenye nyumba)
 
Shida iko kwa akina Baba. Unakuta baba hakuna hata siku moja anachukua watoto wako wakasalimie ndugu zako na hiyo inafanya siku wakikutana wanakuwa kama strangers hawana relationship yoyote. Kingine kama mume una uwezo ukioa ndugu za mume sometimes wanamchukia mke hivyo kufanya uhusiano wa watoto na ndugu zao uwe mbaya
Mara nyingi huwa hivi, ndugu wa kaka anayejiweza kwenye ukoo huwa hawapatani na mke wake na saingine unakuta ni mke anakuwa na mashauzi na kutaka kuonekana Special kwenye ukoo!

Kwamba yeye ndio kaolewa na mume mwenye hela kwenye ukoo mzima na hili hulipasisha mpaka kwa watoto wake kuwa wajione wakishua! Hapa lazma unakuta kuna kuwa na daraja
 
Mara nyingi huwa hivi, ndugu wa kaka anayejiweza kwenye ukoo huwa hawapatani na mke wake na saingine unakuta ni mke anakuwa na mashauzi na kutaka kuonekana Special kwenye ukoo!

Kwamba yeye ndio kaolewa na mume mwenye hela kwenye ukoo mzima na hili hulipasisha mpaka kwa watoto wake kuwa wajione wakishua! Hapa lazma unakuta kuna kuwa na daraja
Tena daraja refu sana mkuu. Unakuta kwa baba mdogo/mkubwa wamejaa ndugu wa mkewe tu ila ndugu wa mume hakuna kabisa na mama mwenye nyumba hawataki waende.
 
Tena daraja refu sana mkuu. Unakuta kwa baba mdogo/mkubwa wamejaa ndugu wa mkewe tu ila ndugu wa mume hakuna kabisa na mama mwenye nyumba hawataki waende.
Anakuwa anawa discourage kwenda kutokana na tabia zake za ajabu! Watoto wa ndugu wa mume don’t feel at home kama wale wa mke!
 
Anakuwa anawa discourage kwenda kutokana na tabia zake za ajabu! Watoto wa ndugu wa mume don’t feel at home kama wale wa mke!
Alafu wengi wao baade hao hao watoto wa ndugu wa mume wakifanikiwa anaanza kuwaita "watoto wangu". Mimi nimeapa siji kumpa mtoto wangu jina la mke wa baba mdogo/mkubwa.
 
Back
Top Bottom