Acheni ubahili na ujuaji.
Tafuta Wakili, mlipe akufanyie "conveyancing".
Ukishamlipa wakili atahakikisha unanua kiwanja/nyumba ambayo iko salama kwa kuanza kukufanyia 'official search' (upekuzi wa usalama wa ardhi hiyo kwenye masijala ya ardhi katika eneo husika), mpaka kukuandikia mkataba wa mauziano (au kuhakiki mkataba wa mauziano utakaoletewa).
Wengi wenu kwa ubahili au ujuaji, mnajikuta mnanunua ardhi/nyumba ambazo sio mali halali za wauzaji, au ardhi/nyumba ambazo zimekopewa benki n.k
Nikupe mfano, marafiki wawili waliosoma pamoja walitaka kununua nyumba za ghorofa karibu karibu. Nyumba zikapatikana. Mmoja akatafuta wakili akamlipa amfanyie "conveyancing" from stage A to Z, akamlipa 2M.
Wa pili akaona ile 2M ni pesa nyingi, akaenda kununua hivyohivyo. Baada ya kusaini mkataba na kuhamia, akagundua kwamba ule mkataba wa mauziano alioletewa ulikuwa na "exclusion clause", this is a clause limiting liability to the drawer (drafter of the contract).
Baada ya kuhamiwa akaletewa bili ya maji na umeme jumla 3.2M. Alipomfata muuzaji ili alipe akakataa, akasema haikuwa sehemu ya makubaliano. Kwenda kwa Mwanasheria akaambiwa hivyohivyo, kwasababu mkataba uliandikwa "nyumba inauzwa kama ilivyo". Lakini angemlipa Wakili basi angeongeza clause kwamba "madeni yote yanayohusu nyumba hiyo kabla ya mauziano yalipwe na muuzaji".
Kwahiyo acheni ubahili na ujuaji muepuke hasara zisizo za lazima [emoji28]