Utakatishaji Fedha, Biashara inayoendelea kwa Siri kubwa

Utakatishaji Fedha, Biashara inayoendelea kwa Siri kubwa

Watu wa Sembe wameguswa hapa ..eti hawaelewi alichoandika mtoa mada.
 
Habari wadau!

Naenda kwenye hoja moja kwa moja kwenye hoja.

Ki ukweli utakatishaji fedha ni biashara ambayo ipo kwa siri sana.

Usione mtu anajipost na rundo la hela na hana kazi yeyote akasema yeye ni free mason ukaamini we ni mjinga hata serikali ina ujinga flani.

Kuna watu wana hela Dunian hapa hela chafu ambayo inahitaji kuwa katika system sehemu sahihi ya kutakatisha ni Africa.

Usione msanii analipwa milioni 300 ya kibongo kwa shoo ya watu 20 uko nje ukasema amepata bingo.

Leo hii kuna companies wanakopesha hela kisa una Nida Number siamini kama kweli wanapata faida.

Wachungaji feki wa kutosha wana hela hatari. Ukiuliza wanauza maji na mafuta au baraka ndo wanapata hizo hela.

Jichanganye ukiamini utatoboa kama hamna source ya hizo hela.

Watakatishaji fedha wakubwa duniani ni

1. Drug dealers.
2. Wanasiasa
3. Wafanyabiashara.
4. Wanamichezo.
5. Wasanii. (wanamuziki na wacheza filamu.)
6. Kamali.

Ongeza yako unayoyajua katika hili!!!!!!
Wewe umeshawahi kutakatisha?
WIVU TU
fanya kazi.....acha porojo
 
Hivi unajua vizuri Money laundering? (Utakatishaji wa pesa) uko je au unadhani kila mwenye pesa nyingi ni mtakatishaji fedha.......unajua watanzania tuna pewa misamihati mikubwa wakati elimu yetu na uelewa wetu uko chini, kisa tuna kipaji cha kuongea hata taka taka.
Wewe umethibitisha ulichoongea maana pia umeandika taka taka na jinsi gani kichwa chako kilivyo na akili mbovu kuwahi kutokea.
 
Mtoa post unaonekana hujui maana ya Utakatishaji fenda ni Kuitoa pesa chafu ambayo ilipatikana visivyo halali eg wizi uwe wa serikalini au ujambazi au hela uliyoipata visivyo halali na kwa vile ni nyingi unataka isikae mkononi mwako iwe kwenye mzunguko ili ufaidike baada ukiwa nayo watu wajue uliipata kwa biashara isionekane kuwa uliipata kwa njia isiyo halali serikali ijue kuws chanzo cha mapato yako ni ile biashara na sio vinginevyo.
Umesema vyema ila kuna watu leo hii nchini wanatumika kutakatisha fedha na serikali ipo kimya. Mtu anaonyesha hela kwenye mtandao akidanganya watu yeye ni free madon
 
Mimi nimekuja kufahamu hapa bongo mtu mwenye hela nyingi au mwenye cheo kikubwa hawapendwi bila kusahau watu wenye elimu kubwa nao wanaambiwa elimu yao nifeki na haina maana hawasaidii nchi n.k.
 
Na hivi ndivyo nijuavyo kwamba pesa yoyote ambayo inapatikana katika shughuli zilizo nnje ya sheria za nchi na pengine kidunia ndio huwekwa kwenye huo upande wa kuwa pesa haramu ila wahusika mara nyingi huwa wanazitafutia sababu ya kuzitakasa ili zionekane safi.

Sasa kitu ambacho kidogo kimeniyumbisha kwenye hilo bandiko ni kwamba mfano wa watu wa makanisa kwamba kwa mujibu wa andiko kile wanachokifanya sicho kinachowaingizia pesa ila wanatumia hiyo njia ili iwe ya utakaso wa hizo fedha walizo nazo.

Hapa ndio amenichanganya mimi kwa sababu hadi sasa kuna pastor alikua na kanisa lake huko buza na alikua anaombea watu kwa laki tano na watu wanakiri kwamba walikua wanatoa hizo fedha na bado kuna mmoja alijaza ule uwanja wa pale kawe na akauza sana maji na mafuta plus sadaka na mengine yote ambayo yaliyofanyika usiku ule kuhamisha pesa kutoka kwenye mifuko ya watu kwenda kwakwe.

Hapa ndipo nnapohitaji connection ya hilo andiko na utakatishaji.

Yaani anawezaje kuprove kwamba hawa watu hawapati pesa kupitia hizo njia ila zipo njia haram za upatikanaji wa pesa zao hasa ukizingatia uwingi wa wafuasi ambao wamejizolea kwenye hayo maeneo yao ya kazi.
Sasa unahitaji taaluma ya ujasusi kweli hapo kubaini kuwa kuna mianya ya kutakatisha pesa za watu wengine? Au hata zake alizotengeneza kwenye Illegal business zake nyingine?
Au hukumuelewa anyway sio wote tunafaa kuchunguza matukio.
Yeye alipowataja tu hao watu nikaona ni kwa namna gani wanatekeleza hilo jambo iwe ni pesa zao au wamepewa !!
 
Mnaosema hamjamuelewa mtoa mada..mko serious kweli au mnatanua mbona hata hahitaji akili kubwa sana:
1.Mtu anajifanya mtumishi wa Mungu: Anasema anapaka pes kwenye sadaka na kuuza maji - na huwezi verify - kumbe anauza madawa ya kulevya..pesa yake ndo anaitaja kama kaipata kwenye sadaka - bila kuwa na kanisa angeshindwa kuhalalisha matumizi makubwa..mfano apeleke bank nillion 3 watamuuliza source ya hizo pesa anasema sadaka na watu wanaona kanisa lipo na watu wanajaa wanakubali.
2.Wafanyabishara: Mtu anakiduka smart cha level ya kawaida mfano anauza simu lkn matumizi yake siyo ya mchezo ukimuuliza anakujibu si ninauza simu..kumbe ile gelesha tu..kipato kinatoka kwingine kabisa.
3.Msanii: Show chache mapesa mengi..kumbe gelesha tu...anajilipa kwa pesa haramu na anaweza kwenda kuzitumbukiza bank -kumbe kapush mzigo...
N.K
 
Kwa lugha rahisi, Unakuta mtu kafungua fremu Mwenge anaweza akagonga mwezi asiingie mteja hata mmoja ndani, Faida 0% ila nyuma ya pazia ni kupoteza maboya tu ana bizness nyengine chafu ili ile ya frem ionekane kama ndo chanzo cha kwanza cha mapato.
 
Drug dealer hatakiwi kuwepo hapa
Bank moja ulaya Hongkong and Shanghai Banking Corporation Limited walipigwa fain ya 1.9 b usd kwa kusindwa kuwazuia CARTEL WAKUBWA WA COLOMBIA NA MEXICO ku launder hela kupitia hiyo benk, KIMSING WAUZA MADAWA WANAONGOZA KWA SHUGHULI YA KUTAKATISHA FEDHA, mleta mada hajakosea wakuu, Top ten money laundering scheme in histori ina Wauza Ngada wengi kuliko watu wengine wowote.
 
Kutakatisha pesa ni kitendo cha kuchukua pesa iliyopatikana kwa njia haramu(madawa, wizi,utapeli etc)kisha kuiingiza kwenye mfumo,biashara halali inayotambulika kisheria.

Mfano labda tuseme mimi ninafanya biashara ya madawa ya kulevya, pesa nitakayoipata baada ya kufanya biashara ya madawa ya kulevya niende nikafungue showroom ya kuuza magari, so kila ninapouza madawa nachukua pesa naenda kuongeza magari huo ndio utakatishaji. Wengine ongezeeni
Umepata hela chafu unaenda kuinunua nyumba alafu unakaa after sometime unaiuza tena ile nyumba then hii hela inakuwa justifiable hata ukiulizwa umepata wapi pesa unasema uliuza nyumba ilokuwa yako, kuna stail nyingi za kutakatisha fedha. Nakumbuka kuna jamaa alikujaga hapa jukwaani kuuliza namba ya kuvusha dolla laki 9 kama sio M1 kuja tanzania kutoka marekan sababu hawez weka hiyo hela benk na hawez kusafiri nayo akawa anataka apewe mawazo ya namna gani hiyo fedha ataifikisha bongo land kwa namna yeyote, ukisoma ule uzi ndio utajua watu wanavyosafisha fedha aisee
 
Back
Top Bottom