Utapeli wa Dawa ya 'HIT' katika kuua Mbu

Utapeli wa Dawa ya 'HIT' katika kuua Mbu

Auntie tena hizi za kuchoma unaona kabisa mbu walivyokufa yaani auntie hit bado haijaisha kila siku naipuliza ukikaa kidogo unasikia mbu wanalia

Rungu afadhali napuliza kwa week mara mbili ila hit hapana kwakweli
HIT hamna kitu mle Auntie...
Wakati naanza kuitumia nilikuwaga nasema Dawa ya Mbu si ndiyo hii....Ile harufu yao...

Ila ukiipuliza Lisaa limoja likiisha Mbu hao...

Rungu kiboko yao
 
ukitaka mbu afe ni umshike umpulizie usoni😂😂😂
Mkuu hawa Mbu wa kizazi hiki ni mbu wa siku za mwisho hawasikii dawa. Pia hawana adabu hata kidogo usipokua makini wanawezakuwa wanageuza kichwa chako lodge wanamaliza mambo yao hapo
 
Mkuu kuhusu hit ni kweli jamani inalevya mbu sio kuua mpaka nilijiuliza au hii ni fake bora rungu mara 100 kuliko hit
I wish ningekuwa na Mamlaka huko TBS hii dawa ingebaki historia.
 
Tanzania tuna kiwanda kipo Kibaha. Kinatengeneza dawa za kuua mazalia ya mbu. Kipo kibaha, mkoa wa Pwani.
Dawa zao ni nzuri sana unanyunyizia kwenye mazalia ya mbu, mbu kwako wanakuwa historia.

Inauzwa 30mls kwa 1000, lita moja kwa 13000. Nakushauri utumie hiyo


Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
Ahsante sana kwa ushauri.

Eneo nilipo nipo na shughul za ufugaji pia nafuga mifugo mbalimbali ikiwemo na Samaki, sasa matumizi ya dawa kwa njia ya Fumigation ni risk mno. Natamani kutumia dawa za aina hiyo.
 
Hizi dawa zilikuwa vizuri miaka minne iliyopita ila hali ya sasa kwa kweli ni UTAPELI wa wazi.

1. Haiui MBU kwa kiwango kinachopaswa yaani katika Mbu 50 watakufa watatu (3).

Yaani mpk mbu afe ni umloweshe na hiyo dawa ndio atakufa ila ukipuliza kama inavyoelekezwa upulize ktk mazingira ya eneo waliopo, hakika hatokufa Mbu hata mmoja, ukitaka mbu afe ni umshike umpulizie usoni.

2. Hata Mbu kuzimia kidogo hakuna! Sana sana watajificha tu kwa muda wa lisaa limoja baada ya kupuliza ila watarudi na wakirudi wanarudi na NJAA ya kufa mtu. (Inawezekana hii Dawa ina wapa Appetite zaidi)

Si kwa HIT tu nimetumia dawa ya RUNGU pia haina matokeo mazuri ktk kuangamiza MBU.

Je wana JF mmekutana na hii changamoto?

Je mnapendekeza dawa ipi bora ya kuangamiza hawa viumbe?

NB: Nimezungumzia kwa upande wa Mdudu aina ya MBU tu kwa kuwa ndio mdudu anayenisumbua mahala nilipo, hakuna Mende wala wadudu wengine, hivyo ufanisi wa dawa hii kwa kuua viumbe wengine sijaupima.

Nawasilisha.
Tanzania kila kitu ni feki.Hao TBS wenyewe nadhani ni feki pia
 
ukitaka mbu afe ni umshike umpulizie usoni😂😂😂
Mkuu hawa Mbu wa kizazi hiki ni mbu wa siku za mwisho hawasikii dawa. Pia hawana adabu hata kidogo usipokua makini wanawezakuwa wanageuza kichwa chako lodge wanamaliza mambo yao hapo
Mbu wa sahivi wapo very technical kwanza wanakuuma kwanza alafu maumivu unapata tyr ameshaondoka eneo la tukio yaan wapo stealthy..... .

Kingine hawaonekani kirahisi/kijingajinga.

Pia ni wabishi kufa au kuzimia.

Nahis hawa mbu ni laboratory modified species..
 
Ni kweli kabisa,mbu hawafi na hata rungu ni harufu tu inabaki muda mrefu lakini haziui.
Nimeamua kujibana narumia x pel bei sio poa Sana imesimama
Biadhaa Tanzania ni utapeli Mtupu hata maji ya Kopo haya tunayonunua ukifatilia kwa makini utaona ni maji feki.

Sema walishapewa nembo za kubandika za Mamlaka husika basi haya maji ya nomba wanatuwekea tu
 
KDR.... knock down resistance mechanism ndani ya mbu ndio kitu kinawasaidia kupambana na sumu mnazo-wapulizia.
 
Mbu wa sahivi wapo very technical kwanza wanakuuma kwanza alafu maumivu unapata tyr ameshaondoka eneo la tukio yaan wapo stealthy..... .

Kingine hawaonekani kirahisi/kijingajinga.

Pia ni wabishi kufa au kuzimia.

Nahis hawa mbu ni laboratory modified species..
Watakua wale wa jangwani
 
Hii dawa ya HIT haifai hata kuwa air freshner, nilishawahi kuitumia nilijuta kununua...
Kwanza ina harufu mbaya utadhani kitu kilichooza,
PIli, haiui mbu hata sisimizi haiui.

Ni dawa isiyofaa hata ukipewa bure
Huu uzi unatakiwa uwe viral hadi social media zote.
Tunaibiwa sana Nchi nzima
 
leo nimempata kunguni mmoja nikamuweka sehemu open nakachukua HIT kuona kama wanaosema ni kweli? nikampulizia yule kunguni nikaona bado anatembea tena fasta nikasubiri dakika moja nikampulizia tena HIT nikaona bado anatembea tu, nikahakikisha yanayosemwa ni ukweli, HIT NI OVYOOO SINUNUI TENA
 
Back
Top Bottom