Utapeli wa kuagiza gari Japan

Hai sio Nigerians...wabongo wenzetu
Wabongo sasa wamekuwa nuksi sana hata hao wanaojinadi mawakala wao wa hapa bongo gari grade 3.0 au 3.5 wao wanaipaisha grade 4.0, sio wakweli kabisa bora kuingia kwenye secure website zao na kuchati nao moja kwa moja na hata au wanaojiita Sbteyo ukiwasiliana nao moja kwa moja gari kama grade R wao hawakuambii wanakupa sound za kihindu.
 
Wewe mat*k kweli! 🤣🤣🤣
😄😄😄😄😄. Leo Bimkubwa umenichekesha kweli umeifanya siku yangu iwe mukide. Man Filandu Nipo njiani natoka kwa Chalamila nakuja huko nisubiri hapo stendi karibu na Lodge ya vancouver.
 
Umetapeliwa ndugu, kampuni haiwezi kufanya mawasiliano ya hovyo kama haya, hao ni wabongo wenzako wanakuzungusha na kingereza

Namna ya kukusaidia tuma website yao na sio email
 
Pole Sana, sasa, wadau wekeni kampuni za ukweli, ambao tunaweza kuagiza magari,maana bongo mataperi wengi, sasa hv tumekuwa "dog eats dogs society"
 
😄😄😄😄😄. Leo Bimkubwa umenichekesha kweli umeifanya siku yangu iwe mukide. Man Filandu Nipo njiani natoka kwa Chalamila nakuja huko nisubiri hapo stendi karibu na Lodge ya vancouver.
Mtu mwenyew umejunga JF juzi tu, ushamba tu..usije ukaniharibia CV humu nikaonekana wa hovyo hovyo..!watu tupo kitambo humu.Kuwa na heshima kijana
 
Makampuni mengi sana wanawatumia real motors

Sheria za japan ni kali sana hauwezi kufungua kqmpuni ya kitapeli japan

Fikiri kwamba gari yako tu usipofanya ukaguzi wa mwaka japan kifungo miaka 5.je ukiharibu image ya japan kwa kumtapeli mtu ?
 
Asante ndugu kwa mawazo kesho naenda police kufatilia maana leo hata job sijaweza kwenda sikuwa na nguvu kabisa.
 

Nilishiriki pia kumtahadharisha mnunuzi
Tukamwambia asijaribu kutuma pesa

Jamani unapata wapi ujasiri kununua gari huko
-nunue sbt,beforward,trust na enhance
 

Kaka humu watu hawasomi lakini kesi ya REAL MOTORS sio mara ya kwanza watu kulalamika na walishauriwa

Usiagize gari kama huna uhakika na iyo website

Mwenyewe nmeagiza gari SBT imefika
Tena bila kupitia agent wala ofisi yeyote


So sehemu pekee naweza reccomend ni
1.SBT
2.SBT
3.Befoward
4.Enhance
5.Japanessevehicles(Trust)

Hawa huihitaji kwenda ofisini wala agent[emoji845]
 
Mtu mwenyew umejunga JF juzi tu, ushamba tu..usije ukaniharibia CV humu nikaonekana wa hovyo hovyo..!watu tupo kitambo humu.Kuwa na heshima kijana
😃😃😃😃😃😃😃😃😃😃😃😃Yaaaaani unazidi kunichekesha Bimkubwa, hapa nilipo nacheka mpaka nataka nikuangukie nyuma, mimi ndio Man Filandu AkA mzee wa juzi kati lakini mwenye ID tofautitofauti, mwenye kuzishibisha server za JF
 
Pole mkuu ila real motors hawa ninaowafahamu hawako ivo, nimeagiza gari mpya kabisa grade 5 millieage 20400km, one owner nimetumiwa documents mpaka certificate ya jamaa alokua anamiliki. Maybe haukupita kwenye trusted site yao. Ila jamaa wako real kama jina lao
 
Saa ingine hikers wanaibaga email address ya kampuni halafu wanaibadilisha kidogo tuu Hata utajua , unakuta una chat na matapeli ukifikiria ni company
 

Real Motors wako vizuri Sana kwenye quality ya gari kuliko hata kampuni tajwa hapo juu. Mimi mteja wao Sana. Tatizo mtu akifatwa whatsapp na namba ya Japan anaingia mtego, ni vizuri watu kufahamu aina za utapeli mtandaoni.
 
Unapoagiza chochote , tukia muagizaji mwenye reputation kubwa na nzuri, na ufike ofisini kwao, tena uliazia kwa wengine waliogiza ofisi halisi zilipo, maana wapo wanafungua ofisi feki na kuandika jina la SBT au Beforward, ukienda kesho yake hukuti kitu.

Ila Binafsi ni bora niongeze milioni 1 au 2 nikanunue Showroom, gari naikagua, nalipa pesa naondoka nayo hapo hapo, nasubiri kadi tu ya gari.
 
Pole sana mpambanaji.Mungu akutie nguvu kipindi hiki kigumu. Pesa zinatafutwa tu utajaaliwa
Hii ni comment Bora Sana kuzidi zote , Kwa wote wanaoloose pesa wasiumie Sana , pesa zinatafutwa , nimegundua mtu akikutapli au kukudhurumu pesa yako uliyopata Kwa uhalali kabisa , milango mingi hufunguka ya kuingiza kipato , hii ishanikuta mi mwenyewe , cha msingi ni kuongeza juhudi kwenye michakato yako tuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…