Utata: Msanii Roma Mkatoliki na wenzake wakamatwa/tekwa nyara

Utata: Msanii Roma Mkatoliki na wenzake wakamatwa/tekwa nyara

Akipotea Faru John PM anaunda tume na sampuli zinatumwa nje kuchunguzwa.

Akipotea Ben, Roma au mtu mwingine PM anapiga kimya.

Tuunde tume ya kuchunguza akili za viongozi wetu.
Kwani hao akina Ben na Roma and company nao ni endangered species km faru? Ukisema iundwe tume kwakua hao wamepotea , tutaunda tume ngapi manake watu wanapotea kila siku?
 
Wakati mnamtafuta Msanii wa Hip Hop Roma Mkatoliki na Moni Centralzone pamoja na Vijana wengine waliotekwa pale Studio za Tongwe Records, Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana yupo katika mtandao wa kijamii wa Instagram anafanya kazi ya kugonga 'LIKES' katika post za Mange Kimambi.

mi nashangaa sana taifa hili tunakoelekea.wanachi kutekwa na baadae ukimya kutawala kutoka kwa mamlaka zinazohusika kutulinda.tunalea kitu kibaya sn katika taifa hili kama mamlaka zitaenelea kunyamazia maswala haya ya watu kutekwa na kisha kuchukuliwa ni swala la kawaida.raia wa tanzania ana haki ya kulindwa akiwa kwenye ardhi yake na ndo maana tukawa na vyombo vya ulinzi.kama watu wanapotea tu from no where tunajuaje kama islamic state au alshbaabu wametuingilia.
 
Walianza na tishio la bastola sasa wamehamia kwa wasanii.

...fool oyeeeee
 
amekamatwa au ametekwa
Huko naona ni kutekwa. Anayekamatwa na polisi lazima (inatakiwa) itolewe taarifa anapelekwa wapi na kwa nini. ILA sina hakika kama inakuwa hivyo siku hz maana Ni style ya vamia tishia, beba.
 
hakuna tatizo hapo. it means bashite atashugulikiwa
Binadamu wa nchi hi hawana thamani kama faru john mpaka kifo kinaundiwa tume!!!!! faru fausta kashazeeka ngoja aje ndo utajua kwanini we huna thamani???
 
Hii taarifa haijakamilika inamaswali kibao,. Napata shida kuona watu wanavyoanza kuto povu na kutukana watu na mamlaka hovyo hovyo, hata uhakika wa taarifa yenyewe hawana niyakusadikika tu. Rai yangu tuache majungu na porojo na mihemko tujikite kwanza kupata data za kisayansi kuhusu jambo husika, yaweza kuwa ni mabifu yao, au mamlaka za ulinzi na usalama au ujambazi au vinginevyo, na kama ni mamlaka zetu za ulinzi na usalama tunapaswa pia kujua sababu za kuwakamata ili tujue kama wamefanya kwa masilahi mapana ya Taifa au uonevu.Tukumbuke hata kama ni wasanii Hawana kinga ya kutokamatwa kama kweli wamefanya kosa, tusiunganishe mihemko ya Ney kwenye hili sakata
Tunaomba data, bila shaka utakuwa nazo tayari. Nchi hii Ni ya mihemko. Bahati mbaya mihemko mingi huwa ya kweli
 
ROMA kutekwa imeniuma sana kuna watu wanaonuesha wazi wao ni wababe hakuna wakuwafanya lolote
 
Daah polisi walikosea baada ya kumvamia Ney Wa Mitego wakiwa na Sare ndiyo maana wakamuachia ila la huyu Roma ambaye naskia alikua anajitayarisha Kutoa nyimbo mpya wameamua kuchukua kwa Style nyingine na anaweza asirudi tena kama Ben Saanane.

ece4d7d96f4dda64b55ae5bebfa1bd33.jpg
 
Mwigulu kwa tb joshua alienda kufanya nini malaika mkuu pia alisha enda kwanini wanajificha kwenye mwamvuli wa dini wakati hawa ishi kwa kutenda haki Hakika nabakia kushangaa nchii hii mnyama amekua na thamani kuliko binadamu Faru fausta akipotea anatafutwa kwa nguvu zote ama kweli serikali ya vi-wonder
 
Kwa hiyo ulitaka afanye nini kwa mfano? Hoja za kitoto hizi kujenga grounds za kuporomosha matusi na lawama. JF bila kashfa will never exist
 
Huyo amejiteka tuu kutafuta kiki...ROMA anatekwa kwa sababu gani hasa? ana nini cha kumtisha mtu yeyote nchi hii?
Ni nani aliona Roma akikamatwa? Ni nani aliona Roma akitekwa?
Huu ni uzushi tuu....
kwautaila wako unaweza ona ni uzushi
 
Halafu alivyo mnafiki anajifanya mzalendo sana,muda wote na bendera ya Tanzania kama gari la DC/RC huku huyo huyo wizara yake imetoa arrest warrant kwa Mange akipita mpaka wowote nchi hii!!
Huko mbinguni kuna watu hawastahili kuchomwa moto , mungu anapaswa kuiangalia hii adhabu upya..


Haiwezekani MTU Mwenye dhambi ya kuzini na MTU Mwenye dhambi ya kuua na kuwapoteza wakina beni saa8 au roma waww na adhabu sawa ya kuchomwa moto
 
Back
Top Bottom