Utata: Msanii Roma Mkatoliki na wenzake wakamatwa/tekwa nyara

Utata: Msanii Roma Mkatoliki na wenzake wakamatwa/tekwa nyara

Mimi ni kama maelezo yako yalivyojieleza.
pili, kwann Roma ambea nilikua sijui ni nani mpaka nilipopata maelezo yako kupotea siku mbili Magufuli apewe lawama zote?

kwanini kabla ya kulaumu,tusizipe malamka muda zifanye uchunguzi?

Ni viongozi wangapi wameuwawa katika mazingira yenye utata povu halikuwatoka?
Wenyewe hawana wake na watoto?,mbona jukwaa hatukuona povu likiwatoka?

Acheni double standard kwenye masuala ya msingi.

Kwa taarifa yako ,wajuvi wanaweza tumia nafasi hii kufanya bifu zao kwa kigezo cha mauaji ya kisiasa.
Ili kuipaka matope serikali,na hawata faulu hata kidogo.take my words
 
Akipotea Faru John PM anaunda tume na sampuli zinatumwa nje kuchunguzwa.

Akipotea Ben, Roma au mtu mwingine PM anapiga kimya.

Tuunde tume ya kuchunguza akili za viongozi wetu.


Bandungu wewe uko mbali! Anza kujichunguza wewe mpiga kura!. Faru ni muhimu kuliko binadamu.Mcc mbele kwa mbele!
 
Inabidi sasa kuwe na chanjo ya 'GPS' yaani ku-insert GPS chips kwenye mwili wa binadamu.
 
Wakati mnamtafuta Msanii wa Hip Hop Roma Mkatoliki na Moni Centralzone pamoja na Vijana wengine waliotekwa pale Studio za Tongwe Records, Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana yupo katika mtandao wa kijamii wa Instagram anafanya kazi ya kugonga 'LIKES' katika post za Mange Kimambi.


Umejuaje km ni yeye aliye-LIKE???hata mimi naweza kufungua acc insta kwa jina lako pia mkuu,,,,
 
Habari wakuu nimekuta bandiko katika ukurasa wa Prof. Jay kuhusu kukamatwa kwa msanii ROMA na kuchukuliwa kwa baadhi ya vitu vya studio ya Tongwe record sijui ni kiki au kweli? Mwenye kujua kinachoendelea


=======

View attachment 491832
Baada ya kuzagaa kwa taarifa kuhusu kukamatwa kwa Msanii Roma Mkatoliki akiwa studio na kupelekwa kusiko julikana, Muungwana Blog imefika katika studio za Tongwe Records jijini Dar es salaam ambapo mkasa mzima ulikuwa hivi...

Kwa mujibu wa Mashuhuda (Majina yanahifadhiwa) walio ambao pia wanaishi katika nyumba ambayo inapatikana studio ya Tongwe, wameijuza Muungwana kuwa April 5, 2017 ambayo ilikuwa ni jana, katika majira ya Saa moja jioni ilionekana gari aina ya Noah nyeusi nje ya studio hizo, ambapo walishuka watu zaidi ya Watano na kuingia ndani ya studio hizo.

Watu hao bila ya kujitambulisha walitamka kuwa wanamuhitaji Roma na mwenzake ambapo walimchukua na kutoka nae nje, na baada ya muda kidogo walirejea ndani na kuwachukua wengine watano akiwemo na Prodyuza wa studio hiyo Anayeitwa Moni.

Mbali na kuwachukua watu hao pia mashuhuda hao wemeeleza baadhi ya vifaa vya studio hiyo pia vimebebwa ikiwemo TV, na Computer.

Kwa Mujibu wa Mwanasheria wa Studio hiyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Edin ameiambia Muungwana Blog kuwa nikweli tukio hilo limetokea na mpaka sasa hawajui Roma na wenzake wamepelekwa wapi na hivyo hawezi kuelezea zaidi mpaka atakapojua walipo wakina Roma, ambapo aliongeza kuwa anakwenda kuripoti katika kituo cha polisi cha Oysterbay Jijini humo.

Chanzo: Blogs



Mtu anaweza kushikiliwa kwa masaa 24, badala ya hapo apelekwe kortini ama sivyo wakili wake anaweza kwenda kortini kuuliza state wamproduce kortini ama wamuachie. Jaji ana uwezo wa kuwaamlisha polisi kufanya hivyo. Otherwise serikali itajichafulia jina kwa kushika watu bila ya kuwaelezea makosa yao nini. Vitendo kama hivi vitawaogopesha investors.
 
Roma mshikaji Wangu wewe ndiye umefanya niipende hip hop naomba huko ulipo usife moyo najua una ujasiri sana kaka yangu.
 
Wakati mnamtafuta Msanii wa Hip Hop Roma Mkatoliki na Moni Centralzone pamoja na Vijana wengine waliotekwa pale Studio za Tongwe Records, Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana yupo katika mtandao wa kijamii wa Instagram anafanya kazi ya kugonga 'LIKES' katika post za Mange Kimambi.

[emoji23] [emoji23]
 
Akipotea Faru John PM anaunda tume na sampuli zinatumwa nje kuchunguzwa.

Akipotea Ben, Roma au mtu mwingine PM anapiga kimya.

Tuunde tume ya kuchunguza akili za viongozi wetu.
Faru john na huyo rumi nani mwenye maslahi zaidi kwa nchi hii?
 
Labda hajapotea yumo mikononi mwa serikali sasa tatizo lipo wapi kama kashikwa na serikali?
Ameshikwa kwa sababu gani ?na kwanini kama anakosa wasimfungulie mashitaka.sasa anashikiliwa unataka nyumbani kwake waweke msiba au wafanye nini kama baba wa familia anapotea kama kuku.ukiona hivyo hatuko salama hata kidogo.muda si mrefu tutapuliziwa sumu kama syria.eee mungu tunusuru na haya.mungu uchelewa kutujibu lakini atatenda haki kwa wakati.
 
Akili yako kama matope ya chooni
Huwa mnapenda kufuata mkumbo kwa mambo msioyajua.Mlisumbua humu na hashtag za Saanane,mfalme Mbowe akawapiga stop mkaufyata hata kuhoji hamkuhoji tena
 
Serikali hii inakotupeleka sielewi. Na ifike tutfikiri vema Watanzania. Hiki si kipindi cha kushabikia yanayotokea bila kujali itikadi zetu. Cha kusikitisha serikali iko kimya.
 
Mimi siamini kama hiyo akaunti ni ya mheshimiwa.NOO.
 
Hivi kama simu inaita then haipatikani kwanini wasanii wasiungane kuitrack na kufanya ambush live?
 
Back
Top Bottom