Utetezi wa uumbaji kimahesabu na kifizikia: Mathematician's and theoretical physicist appeal to creation

Utetezi wa uumbaji kimahesabu na kifizikia: Mathematician's and theoretical physicist appeal to creation

Hili ngoja nikusaidie, hili haliwezi kutokea na haliwezekani, sababu mmoja amepotosha maandiko kwa maslahi yake na ujinga wake na mwingine anaishi katika maandiko. Hili lipo tangu zama za kale.

Nachoona mimi na ndicho sahihi kila mmona ahudhurishe hoja zake kwa namna iliyo bora.

Kuna mwanazuoni mmoja anasema hivi "Mtume mwenye kutafuta ukweli ushahidi mmoja tu humtosheleza ila mtu asiye tafuta ukweli na mbishani ithibati elfu hazimtoshi" au kama alivyosema.
Kubalianeni kwanza muondoe hiyo sintofahamu kati yenu halafu mkihakikisha kila kitu kiko sawa hakuna utofauti wala mpishano basi mtualike tumjadili huyo Mungu ambaye mmempendekeza kwa pamoja
 
Kubalianeni kwanza muondoe hiyo sintofahamu kati yenu halafu mkihakikisha kila kitu kiko sawa hakuna utofauti wala mpishano basi mtualike tumjadili huyo Mungu ambaye mmempendekeza kwa pamoja
Lhili haliwezekani na sababu nimeshaitoa.

Kingine nyiynyi hamna uwezo wa kujadiliana na sisi sababu mnampinga msiye mjua na hoja hamna.


Kwahiyo kama una hoja iweke mezani.
 
Leta source ya Kuwa everything is made of energy
Sileti source bali naweka fact mezani tu hapa.

Ni kwamba scientifically everything in our visible universe resulted from the big bang

At the big bang there was only energy

Now we have matter and energy, then where did the matter come from?

Jibu lilishatolewa zamani na A. Einstein alipogundua kwamba kumbe matter na energy ni interconvertible, aliposimamisha hii kitu ya E = mcsquare!
 
Kwa mujibu huo inakuwa haileti maana kusema Mungu ni IDEA sababu wazo halimiliki chochote,halina utambuzi, halina matashi, halina malengo, halina maarifa. Bali wazo humilikiwa.
Mawazo yapo aina aina

Hilo uliloelezea ni wazo crystallized fulani lipo fixed - vitu

Kuna mawazo mengine yananyumbuka na yanaweza hata kuzaliana haya ni mawazo hai - viumbe hai

Katika hayo mawazo hai kuna ambayo yameongezea na kujitambua na kuyatambua mawazo mengine hivyo yamepata uwezo wa kujinyumbulisha na kuyanyumbulisha na kuyachanganya mawazo mengine hata kuunda mawazo mapya[mchanganyiko mpya wa mawazo ya zamani] hawa ni - watu na viumbe wengine wanaojitambua........ kwa kusema hivyo sisi ni idea na zaidi

Woooooote hao na vyoote hivyo viko powered na wazo moja wazo la msingi, in Him we live, move, and have our being - Mungu ambaye ni IDEA nzima na zaidi
 
Lhili haliwezekani na sababu nimeshaitoa.

Kingine nyiynyi hamna uwezo wa kujadiliana na sisi sababu mnampinga msiye mjua na hoja hamna.


Kwahiyo kama una hoja iweke mezani.
Sababu ulizozitoa kumbuka zinaweza kutolewa na mkristo kuelezea namna gani isivyowezekana kwa madai hayo hayo kuwa waislamu wamepotosha na kwamba biblia ndio kitabu cha kweli na ukristo ni dini sahihi

Yani hapo wewe ni kama umewawahi wakristo kwa kusema kwamba wakristo wamepotosha kwasababu umekuwa wakwanza kujibu hoja

Ila pengine angewahi kuijibu hiyo hoja mkristo angekuja na maelezo kama hayo hayo kuonesha jinsi gani uislamu sio dini ya kweli na haiabudu Mungu wa kweli.

Kama tumeshaona wenye vitabu vinavyodaiwa kuwa ni vya Mungu bado vitabu vyao vinapingana na kuonesha hali ya kutofautiana mafundisho na maagizo wanayosema yametoka kwa Mungu?

Point hapa ni kuwa, kumbe kitabu au aina fulani ya maandiko yanayodaiwa kuwa yameandikwa na Mungu au kwa muongozo wa Mungu sio uthibitisho wa kuonesha kweli kilichoandikwa humo kimeandikwa na Mungu/kuongozwa na Mungu

Kwa hiyo una suggest nini hapo?

Utumie maelezo ya kitabu kama hoja ya uthibitishi kwa atheist kueleza habari za Mungu wakati kuna theists wenzako hawakubaliani na kitabu chako kuwa ni uthibitisho wa Mungu?

If I were you I would prefer reasonable facts and ignoring text scriptures as evidence.

Uchaguzi ni wako
 
Mawazo yapo aina aina

Hilo uliloelezea ni wazo crystallized fulani lipo fixed - vitu

Kuna mawazo mengine yananyumbuka na yanaweza hata kuzaliana haya ni mawazo hai - viumbe hai

Katika hayo mawazo hai kuna ambayo yameongezea na kujitambua na kuyatambua mawazo mengine hivyo yamepata uwezo wa kujinyumbulisha na kuyanyumbulisha na kuyachanganya mawazo mengine hata kuunda mawazo mapya[mchanganyiko mpya wa mawazo ya zamani] hawa ni - watu na viumbe wengine wanaojitambua........ kwa kusema hivyo sisi ni idea na zaidi

Woooooote hao na vyoote hivyo viko powered na wazo moja wazo la msingi, in Him we live, move, and have our being - Mungu ambaye ni IDEA nzima na zaidi
Hapa bado unarudi kule kule, kama unakiri ya kuwa wazo linatoka kwa Mola maana yake vyote vinarudi kulekule na bado haileti maana kuwa Mola ni wazo.

Nikuulize swali rahisi, wazo ili liwe wazo linatakiwa likidhi vigezo gani ? Au wazo kwa ujumla wake ni nini ?
 
Sababu ulizozitoa kumbuka zinaweza kutolewa na mkristo kuelezea namna gani isivyowezekana kwa madai hayo hayo kuwa waislamu wamepotosha na kwamba biblia ndio kitabu cha kweli na ukristo ni dini sahihi
Hili liko hivyo, ndiyo maana hata wewe japo huna hoja na unadai ya kuwa Mola hayupo. Hata Wakristo nao wanaona wako sahihi wyo wao tu haa Mayahdi kadhalika mpaka Mabudha na watoto wa Mahindu. Kwahiyo kuna kuwa sahihi na kujiona uko sahihi. Maana yake ungekuwa na kichwa chepesi na kufikiria hili hukuoaswa kuliandika sababu liko wazi sana.

Kwahiyo kinachochukua nafasi hapo ni hoja na uhalisia na ubainifu.
 
Kwa hiyo kupitia formula yako ya hesabu ni wazi kwamba njia hiyo inathibitisha Mungu Yehova na habari za utatu mtakatifu ambao haukubaliki na jamii ya kiislamu?

Najua point yako ilikuwa kuweka hoja ku challenge atheists lakini since umemtaja Yesu na utatu umejikuta upo katika nafasi ya kujibu maswali ya waislamu wenye itikadi kali

Kwa hiyo sio atheists tu ambao watapinga kanuni yako, kuna waislamu pia. Hiyo inakupa tafsiri gani?

So unashaurije?

Kwanini tusiwape nafasi nyinyi kwa nyinyi believers mkae chini mfikie muafaka wa pamoja kukubaliana jibu moja ambalo mtasimamia kwa pamoja kwenye mjadala dhidi yetu?
Toka lini waislamu na Wakristo wakakubaliana hoja,
 
Hapa bado unarudi kule kule, kama unakiri ya kuwa wazo linatoka kwa Mola maana yake vyote vinarudi kulekule na bado haileti maana kuwa Mola ni wazo.

Nikuulize swali rahisi, wazo ili liwe wazo linatakiwa likidhi vigezo gani ? Au wazo kwa ujumla wake ni nini ?
Wazo ni kama dhana fulani au nadharia fulani hivi. Wazo sio kitu cha kushikika, kwa hiyo unapolichambua usilifix kama kitu fulani hautalielewa ukifanya hivyo. Wazo latoka kwa Mola na ndiyo Mola havitenganishiki sawa tu na ilivyo wazo-hai la mtu na mtu mwenyewe visivyoachanishika.

Nitajisema mimi halafu tutatengeneza analojia, maana Mola haelezeki moja kwamoja

Mimi ni wazo la umimi, wazo la mimi lipo katika kila seli inayoniunda mimi na lipo zaidi ya hizo seli tu, so mimi nipo na seli zangu zipo. Seli za mwili wangu hazina uwepo nje ya mimi..... ila mimi nipo zaidi ya hizo. Wazo la mimi kuwepo huku haliondoi kwamba nipo pia katika hizo seli. Mwanzo wake ni mimi na mwisho wake ni mimi - Wazo hai

Kwa kizungu wazo hai naona linaendana na hii kitu inaitwa 'consciousness' 'kitu' fulani hivii ambacho hakiwekwi sehemu moja ili useme ufahamu huu hapa. Kwa hiyo wacha tu nifanye kosa la kurudia msamiati niseme; Wazo ni wazo 😏 na kinachowaza wazo nacho ni wazo, wazo lililo hai na mara nyingi linalojitambua pia. Wazo linalojitambua laongoza mawazo mengine yoote chini yake. Na yote ni sehemu ya wazo moja.
 
Hili ngoja nikusaidie, hili haliwezi kutokea na haliwezekani, sababu mmoja amepotosha maandiko kwa maslahi yake na ujinga wake na mwingine anaishi katika maandiko. Hili lipo tangu zama za kale.

Nachoona mimi na ndicho sahihi kila mmona ahudhurishe hoja zake kwa namna iliyo bora.

Kuna mwanazuoni mmoja anasema hivi "Mtume mwenye kutafuta ukweli ushahidi mmoja tu humtosheleza ila mtu asiye tafuta ukweli na mbishani ithibati elfu hazimtoshi" au kama alivyosema.
Ubishan upo Kati ya ukwel na uongo coz hiz nguvu huwa mara nyingi hukinzana, unataka kuwe na kimoja tu unachoona wewe ni ukwel , huoni unamkufuru huyo MUNGU wako aliyeruhusu huo unaoita ukweli ukae pamoja na uongo?
 
Msingi wa swali lako ni kwamba wanaowaza ni sisi binadamu peke yetu au?

Binafsi ninaposema wazo nina picha kuuubwa sana ya hilo wazo. In summary niseme ni wazo la Mungu Mwenyezi linalosustain uwepo wa huu ulimwengu wetu na zaidi ya huu ulimwengu wetu, yanayoonekana kwetu, yasiyoonekana kwetu na hata yasiyowezekanika kuonekana yoooooote yapo kwenye wazo lake Mungu.

Kwa upande wetu sisi mawazo yetu yanaathiri viumbe walio chini yetu na walio karibu yetu na walio ndani yetu;
Walio karibu yetu: Ngombe, mwenzi, majani, bakteria, fangasi
Walio chini yetu: Almost wote
Walio ndani yetu: mitochondria, seli hai nyeupe/nyekundu, mikono,miguu....
Ukiangalia hata walio juu yetu kwa kiasi fulani, itoshe kusema tunaathiriana wote.
Hilo neno wazo unaweza ukaliita pia super intelligence.
 
Kwa mujibu huo inakuwa haileti maana kusema Mungu ni IDEA sababu wazo halimiliki chochote,halina utambuzi, halina matashi, halina malengo, halina maarifa. Bali wazo humilikiwa.
Mbona wazo lina hivyo vyote
 
Hili liko hivyo, ndiyo maana hata wewe japo huna hoja na unadai ya kuwa Mola hayupo. Hata Wakristo nao wanaona wako sahihi wyo wao tu haa Mayahdi kadhalika mpaka Mabudha na watoto wa Mahindu. Kwahiyo kuna kuwa sahihi na kujiona uko sahihi. Maana yake ungekuwa na kichwa chepesi na kufikiria hili hukuoaswa kuliandika sababu liko wazi sana.

Kwahiyo kinachochukua nafasi hapo ni hoja na uhalisia na ubainifu.
Hoja kila mtu anazo utofauti ni kipimo cha kuangalia authenticity ya hizo hoja kama zime qualify

Ukitumia Quran kama ndio kipimo wa madai yako ambayo unasema ni sahihi kumbuka unaweza kukosolewa na mkristo kupitia biblia yake

Sasa mjadala unaohusisha hoja za vitabu ni infinite kwakua hakuna aliyetayari kukubali kitabu chake ni uwongo na kitabu cha mwingine ndio cha kweli.

Hata saizi ukiwa na hoja ya ku challenge bible ambayo hoja biyo wewe unaona iko sahihi kuonesha kasora ya bible ni lazima kwa namna moja uwe umeipitisha katika misingi ya Quran

Yani utasema jambo fulani wakristo mmepotosha kwa kuzingatia sababu ambazo hilo jambo lilivyoelezwa kwenye Quran

Yani by default umejitengenezea msimamo kuwa Quran ndio msingi sahihi muda wote

Lakini ukumbuke hayo yote unayoweza kuyafanya, pia hata wakristo ndio hivyo hivyo.

Na ndio maana nasema hoja ya kusema Mungu hivi Mungu vile kwasababu kitabu kimesema haipaswi kutumiwa kwa watu rational ilihali miongoni mwenu tu mnaomini Mungu hamkubaliani na viatabu vya nyinyi kwa nyinyi
 
Wazo ni kama dhana fulani au nadharia fulani hivi. Wazo sio kitu cha kushikika, kwa hiyo unapolichambua usilifix kama kitu fulani hautalielewa ukifanya hivyo. Wazo latoka kwa Mola na ndiyo Mola havitenganishiki sawa tu na ilivyo wazo-hai la mtu na mtu mwenyewe visivyoachanishika.

Siyo kisichoshikika hakiitwi kitu. Wazo nalo ni kitu chenye sifa anuai zake. Lakini hata tukijaalia wazo likawa si kitu. Wapi linatoka wazo ? Wazo halimiliki wazo halina utambuzi, vipi ulipe sifa ambayo si yake. Mfano wazo la kujenga, vipi ulipe sifa ya kujenga hali ya kuwa lenyewe halijafanyiwa kazi ?

Maana yake wazo haliwezi kuwa Mola. Ni sawa na sisi tumetoka kwa Mola kwahiyo sisi hatuwezi kuwa Mola sababu hatuna sifa alizo nazo Mola kwa dhati yake.

Uhai siyo wazo, wazo haliwi wazo mpaka liwe limewaziwa na kuwasilishwa.

Haya mambo unapokosea wewe unayaongelea kifalsafa zaidi ndiyo maana ynakuwa mbali na jambo husika, yaani huligusi jambo husika.

Jaribu kuyaelezea haya mambo kiuhalisia, shida ya falsafa ni kama kuuzunguka mbuyu. Yaani unakuwa unazunguka tu pasi na kuugusa mbuyu husika, ndicho unachokifanya wewe.
Kama tumeshaona wenye vitabu vinavyodaiwa kuwa ni vya Mungu bado vitabu vyao vinapingana na kuonesha hali ya kutofautiana mafundisho na maagizo wanayosema yametoka kwa Mungu?
Ndiyo maana kila siku huwa nawakosoa kwa kutokuwa kwenu watafiti na kufatilia mambo. Usome Ukristo katika misingi yake, kadhalika Uislamu na sini nyingine. Mtu mwenye akili timamu huuliza kama Mola ni mmoja kwanini kuna dini nyingi ? Jibu sahihi ni kuwa Mola ni mmoja na dini lazima iwe moja. Jalia Mola wangekuwa zaidi ya mmona hii dunia ingeendeshwaje ? Lazima kungekuwa na vuta ni kuvute huu ndiyo uhakika wa mambo.

Kwahiyo wenye akili timamu lazima watataka kujua nani yuko sahihi na nani ni kinyume chake. Vipi utajua nani mkweli na nani si mkweli, haoa lazima uweke nia ya kutaka kujua mambo na si kama mnavyo fanya nyinyi, kutaka kujitutumua na hamna mnachokijua.

Sisi huwa tunasema hivi "Kila mmona ana dai Laila ni mpenzi wake, lakini tukimuuliza Laila juu ya hilo ana kana ya kuwa hakua mpenzi wake hata mmoja katika hao ." Hii na maanisha ya kwamba lazima mambo uyajue ndiyo uhitimishe.


Point hapa ni kuwa, kumbe kitabu au aina fulani ya maandiko yanayodaiwa kuwa yameandikwa na Mungu au kwa muongozo wa Mungu sio uthibitisho wa kuonesha kweli kilichoandikwa humo kimeandikwa
Sahihi kabisa hali iko hivyo.
Kwa hiyo una suggest nini hapo?
Kila mtu mwenye hoja zake aruhusu kuhojiwa na kuthibitisha hoja zake na kujibu kila anachoulizwa. Sababu hali ilivyo ni kiwa mchana wake ni sawa na usiku wake hapitei humo ila mwenye kutaka apotee. Mambo yako wazi mno.
Utumie maelezo ya kitabu kama hoja ya uthibitishi kwa atheist kueleza habari za Mungu wakati kuna theists wenzako hawakubaliani na kitabu chako kuwa ni uthibitisho wa Mungu?
Hili nalo siyo hoja, ndiyo maana sisi huwa tunasema hivi leteni hoja zenu kama nyinyi mnasema kweli. Kwahiyo kila mtu ataleta hoja zake. Sababu ukweli uko wazi lazima atajulikana nani mkweli na nani muongo, sababu sote tumejaaliwa neema ya akili na kutafakari.

Kuna vitu huwa havipingani na akili kabisa, hili wengi hawalijui na kama wanalijua basi wana kaidi. Mfano tu suala la kwamba Mola yupo, hili jambo halipingani kabisa na akili, yeyote apingaye jambo hilo, aidha :

1. Ni mjinga hajui anachokipinga
2. Au ni mpumbavu
3. Au anavyo vyote viwili.


If I were you I would prefer reasonable facts and ignoring text scriptures as evidence.
Maandiko ndiyo uhalisia wenyewe. Mola wetu baada ya kufunga mlango wa utume na akatupa ishara, aliyaacha mambo wazi mno. Watu siyo kwamba wanaukataa ukweli kwamba unakasoro la hasha wapo wanao kataa ukweli kwa ajili ya malsahi yao. Hili kwanza liweke akilini.

Kingine ufunuo haupingani na ufunuo, ukiona akili yako inapingana na ufunuo kuna moja kati ya mawili au una yote, aidha umjinga au mpumbavu au una vyote.

Sababu uhalisia ndiyo facts yenyewe, mfano wa fact hii je kwamba hii dunia imejiumba au imetikana pasi na chochote ? Hii ni facts yaani uhalisia, huwezi kupinga jambo hili, majibu yake huonyesha ya kuwa hii dunia haiwezi kutokea pasi na chochote au kujiumba sababu singi wa wa ujenzi unajulikana, ni ufinyu wenu tu wa kutofikiria mambo katika uhalisia wake, ndiyo maana hili wakana mungu wote hamjawi kutuambia ya kuwa sis imekuwaje mpaka tukawepo hapa duniani ?
Uchaguzi ni wako
Mola wetu ametuumba sote na kitu kiitwacho "Fitrah (Inert disposition)" hichi kitu kinamfanya mtu asipinge uwepo wa Mola endapo atafikiria kwa undani zaidi na lazima atakiri ya kuwa hii dunia imeumbwa. Hii hali anayo kila mtu.

Leo hii wakana mungu ukiwauliza kwanini tunaishi ? Hawana jibu sahihi, je tunaishi na kufa tu, halafu basi ? Maana yake haya maisha hayana maana. Sasa akili iliyo salama inakataa hili, inakwambia lazima kuna lengo maalumu la kutufanya sisi tuishi na kuwepo hapa, sasa kuanzia hapa akili yako itaonekana inafanya kazi vizuri. Sasa wakana Mungu akili hii hawana, wao ni kukaririshana mawazo ya wajinga fulani na wao wanayabeba kama yalivyo.
 
Ubishan upo Kati ya ukwel na uongo coz hiz nguvu huwa mara nyingi hukinzana, unataka kuwe na kimoja tu unachoona wewe ni ukwel , huoni unamkufuru huyo MUNGU wako aliyeruhusu huo unaoita ukweli ukae pamoja na uongo?
Ndiyo maana akaweka wazi uongo na ukweli. Ikabaki kwako kuchagua, kwahiyo ukiamua kufata uongo na ukweli uko wazi tutakuuliza kwanini unafata uongo na ukweli uko wazi. Hii ndiyo maana ya uhuru wa kuchagua, na akatuoa akili ya utambuzi yaani ya kujua mambo hayo.
 
Toka lini waislamu na Wakristo wakakubaliana hoja,
Nacho shangaa ni oale wanapotaka kutushawishi sisi tusio amini Mungu kwa nja ya vitabu

Ya i vitabu ambavyo wao kwa wao hwakubaliani kama ni vya kweli, vitabu hivyo hivyo wanataka kuvitumia kama uthibitisho kwetu

Hiyo hatukubali, kama wataona vitabu ni hoja za msingi kwenye uthibitisho basi wafanye makubaliano wampitishe

Mungu mmoja: Mwenye sifa moja, eidha yehova ambaye kasema kwenda peponi ni lazima umkubali Yesu na kuoa mke zaidi ya mmoja ni uzinzi

Au Allah ambaye yuko mbingu ya 7 kasema watu wasali swala tano, kufunga kula, uoe wake wa 4 na kutakuwa na adhabu ya kaburi kwa waovu nk.

Hapo inatakiwa achaguliwe Mungu mkoja na mmoja atemwe.

Kitabu kimoja: Maana yake kuna kitabu hapo kinatakiwa kipitishwe kua ni batili ili hicho kimoja kiwe cha kweli),

Pepo moja: Maana yake hapa wakubaliane ni either wakubaliane pepo yenye kuimba na kusifu au yenye bikra 72. Hapa pia linahitajika jibu moja tu

Kama wao watashindwa kuafikiana jibu moja basi itakuwa ni ujinga kutumia vitabu hivyo kama hoja ya uthibitisho kumthibitishia mtu asiyeamini katika Mungu.
 
Mungu mmoja: Mwenye sifa moja, eidha yehova ambaye kasema kwenda peponi ni lazima umkubali Yesu na kuoa mke zaidi ya mmoja ni uzinzi

Au Allah ambaye yuko mbingu ya 7 kasema watu wasali swala tano, kufunga kula, uoe wake wa 4 na kutakuwa na adhabu ya kaburi kwa waovu nk.
Tatizo lipo kwenye watu kutaka kutumia mila na desturi zao kama sheria ya kufuatwa na wote duniani, ego,nationalism etc

Sasa ili wafanikishe hilo jambo wanaamua kusema ni maagizo ya Mungu

Lakini sijui kwa waamini wengine lakini binafsi naona Mungu ni mkuuuuubwa mno kuanza kufuatilia eti tuoaneje, au tutumie siasa zipi. Cha msingi tu je hivyo vitu vinaijenga jamii au vinaibomoa amueni kama jamii ilostaarabika.

Maamuzi ya haki yanayofanywa duniani Mungu huwa anayapitisha wala haina ubaaaabe. No.

So katika jamii ya wakulima ni sahihi kusali mara moja kwa wiki na usiku labda. Ila kwa wanaovuna mafuta ni sahihi kwao kusali kila baada ya masaa matano.

Jamii yenye almost idafi sawa ya jinsia ni sahihi mke mmoja mme mmoja na jamii ambayo wanaume wamepotezwa vitani ni sahihi mme mmoja wake wawili-wanne.

Hakuna cha dhambi wala nini kama hilo jambo ni jema kwa 'afya' ya jamii husika bro
 
Mbona wazo lina hivyo vyote
Wazo halina hivyo vyote. shida yenu haya mambo mnayajadili kifalsafa zaidi na si kiuhalisia. Katika sifa za Falsafa kutokana na msingi wake dhaifu huwa hawaifati hoja na kujua msingi wa mambo na kuyahusianisha mambo moja kwa moja.

Nakuuliza swali rahisi hapa, wazo linaweza vipi kuamua jambo au kupanga mambo ?
 
Wazo halina hivyo vyote. shida yenu haya mambo mnayajadili kifalsafa zaidi na si kiuhalisia. Katika sifa za Falsafa kutokana na msingi wake dhaifu huwa hawaifati hoja na kujua msingi wa mambo na kuyahusianisha mambo moja kwa moja.

Nakuuliza swali rahisi hapa, wazo linaweza vipi kuamua jambo au kupanga mambo ?
Mbona umekimbia darsa nilikuwa nakupa , muhammad anasema mbwa wote weusi ni mashetani
 
Back
Top Bottom