Utetezi wa uumbaji kimahesabu na kifizikia: Mathematician's and theoretical physicist appeal to creation

Utetezi wa uumbaji kimahesabu na kifizikia: Mathematician's and theoretical physicist appeal to creation

Philosophy faster definitions: Tafsiri za harakaharaka😂😂
1. the study of the fundamental nature of knowledge, reality, and existence, especially when considered as an academic discipline.
2.a theory or attitude that acts as a guiding principle for behaviour.
Japo kuwa kwenye maana ulizo zitoa hazijazngatia etimolojia ya tamko husika na kuacha maana ya asili, naomba unisaidie kwa kutumia maana hizo ulizo zitoa hapo juu, tuonyeshe zinakusaidia vipi kuujua ukweli ? Hili ndiyo swali langu la msingi.
 
Japo kuwa kwenye maana ulizo zitoa hazijazngatia epitomolojia ya tamko husika na kuacha maana ya asili, naomba unisaidie kwa kutumia maana hizo ulizo zitoa hapo juu, tuonyeshe zinakusaidia vipi kuujua ukweli ? Hili ndiyo swali langu la msingi.
Quite literally, the term "philosophy" means, "love of wisdom." Kupenda hekima, walioanzisha hill neno walikuwa watu waliopenda kujiweka kama watafutaji wa maarifa.

Walijitofautisha na wajuaji wa kina sage na gurus na rabbis. Tena ungejua hii tabia ya 'ujuaji' kujifanya unajua kila kitu. Au umeshikilia maarifa fulani kwamba ndio kila kitu, ndio tabia mahsusi kabisa iliyopelekea kumkataa nabiy Issa kati ya 'wasomi' waliokuwa wengi na kukubalika na watu wa kawaida.

Kuna maandiko katika biblia yanayoweka kheri kwa wahitaji wa maarifa; Heri walio maskini rohoni, maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Na zipo aya kadhaa zinazosifia tabia ya 'ufilosofi': Samahani bandugu nitakopi aya nzima maana sina hakika nikiwapa reference kama kila mmoja ataenda kweli kusoma:

Mithali 8​

1 Je! Hekima halii?
Ufahamu hatoi sauti yake?
2Juu ya mahali palipoinuka karibu na njia,
Penye njia panda, ndipo asimamapo.
3Karibu na malango, mahali pa kuingia mjini,
Mahali pa kuyaingilia malango anapiga kelele.
4Enyi watu, nawaita ninyi;
Na sauti yangu ni kwa wanadamu.
5Enyi wajinga, fahamuni werevu,
Nanyi wapumbavu, mpate moyo wa kufahamu.
6 Sikieni, maana nitasema yaliyo mazuri,
Na kufumbua midomo yangu kutakuwa maadili.
7 Maana kinywa changu kitasema kweli,
Na uovu ni chukizo kwa midomo yangu.
8Maneno yote ya kinywa changu yana haki;
Hapana hata neno lililopotoka au la ukaidi.
9Yote humwelea yule afahamuye,
Yote huelekea mbele yao waliopata maarifa.
10Pokea mafundisho yangu, wala si fedha,
Na maarifa kuliko dhahabu safi.
11 Maana hekima ni bora kuliko marijani;
Wala vyote vinavyotamanika havilingani nayo.
12Mimi, hekima, nimefanya werevu kuwa kao langu;
Natafuta maarifa na busara.
[Watafuta maarifa huitwa filosophers]
13 Kumcha BWANA ni kuchukia uovu;
Kiburi na majivuno, na njia mbovu,
Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.
14 Shauri ni langu, na maarifa yaliyo sahihi;
Mimi ni ufahamu, mimi nina nguvu. [Amenikumbusha hitimisho letu na draga]
15 Kwa msaada wangu wafalme humiliki,
Na wakuu wanahukumu haki.
16Kwa msaada wangu wakuu hutawala,
Na waungwana, naam, waamuzi wote wa dunia.
17 Nawapenda wale wanipendao,
Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
18 Utajiri na heshima ziko kwangu,
Naam, utajiri udumuo, na haki pia.
19 Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi,
Na faida yangu hupita fedha iliyo teule.
20Natembea katika njia ya haki,
Katikati ya mapito ya hukumu.
21Niwarithishe mali wale wanipendao,
Tena nipate kuzijaza hazina zao.

Sehemu ya Busara katika Uumbaji [READ THIS PART CAREFULLY, imebeba madini ya uzi huu. Kama yeyote utang'amua sehemu nilipopingana na maandiko tafadhari nirekebishe]
22 BWANA alikuwa nami katika mwanzo wa njia yake,
Kabla ya matendo yake ya kale.
23 Nalitukuka tokea milele, tangu awali,
Kabla haijawako dunia.
24Wakati visipokuwako vilindi nalizaliwa,
Wakati zisipokuwako chemchemi zilizojaa maji.
25 Kabla milima haijawekwa imara,
Kabla ya vilima nalizaliwa.
26Alipokuwa hajaiumba dunia, wala makonde
Wala chanzo cha mavumbi ya dunia;
27Alipozithibitisha mbingu nalikuwako;
Alipopiga duara katika uso wa bahari;
28Alipofanya imara mawingu yaliyo juu;
Chemchemi za bahari zilipopata nguvu;
29 Alipoipa bahari mpaka wake,
Kwamba maji yake yasiasi amri yake;
Alipoiagiza misingi ya nchi;
30 Ndipo nilipokuwa pamoja naye, kama stadi wa kazi; [Umeona!!]
Nikawa furaha yake kila siku;
Nikifurahi daima mbele zake;
31 Nikiifurahia dunia inayokaliwa na watu;
Na furaha yangu ilikuwa pamoja na wanadamu.
32 Basi, wanangu, nisikilizeni sasa;
Maana heri hao wazishikao amri zangu.
33Sikieni mafundisho, mpate hekima,
Wala msiikatae.
34Ana heri mtu yule anisikilizaye,
Akisubiri sikuzote malangoni pangu,
Akingoja penye vizingiti vya milango yangu.
35 Maana yeye anionaye mimi aona uzima,
Naye atapata kibali kwa BWANA. [Njia, kweli, uzima ]
36 Bali anikosaye hujidhuru nafsi yake mwenyewe,
Na wao wanichukiao hupenda mauti. [Malipo ya ukaidi, uongo ni mauti]
 
Naanzia hapa kwa sababu hili umelileta kwa ufupi. Mahubiri ni nini ? Je mahubiri hayawezi kuwa uhalisia au lini mahubiri hayajawahi kuwa uhalisia ?

Mfano naposema acheni zinaa, lini zinaa ilikuwa nzuri ? Kuacha zinaa ni uhalisia au ni kinyume chake ?

Sasa naomba unionyeshe wapi nimeleta mahubiri.

Jaribuni kuchambua hoja na msikimbie hoja. Mfano kuna sehemu nimekuomba uelezee maana ya tamko "wazo" matokeo yake hukufanya hivyo ukaanza kuongelea mambo mengine yasiyo husiana na swali nililo kuuliza, huku ni kutokuwa makini na hoja ya aliye dhidi yako.
Nikiri kwamba hilo la kusema 'unaleta mahubiri' nimelikopi toka kwa wadau kadhaa humu JF tu.

Nikachukulia tafsiri yake ni: kuleta maneno au dhana fulani kutokea katika imani yako /kitabu chako na kusisitiza kuwa huo ndio uhalisia bila kujali kingine. Hasa kwa watu wasioamini unachokiamini in the first place.

Kuhusu maana ya wazo, pia labda niseme kuna namna fulani unaubishi tu, nilishaitafsiri vile ambavyo nimeiconceive kichwani. Basi nikiri sikutafuta maneno sahihi. Maana kama ningetafuta maneno sahihi hata kabla ya kuandika huu uzi hiyo sehemu ya neno MANTIKI ningeweka neno BUSARA. Kuendana na biblia ilivyotumia. Lakini kama nilivyosemaga; Let us not get caught up in semantics broh.
 
Quite literally, the term "philosophy" means, "love of wisdom." Kupenda hekima, walioanzisha hill neno walikuwa watu waliopenda kujiweka kama watafutaji wa maarifa.

Walijitofautisha na wajuaji wa kina sage na gurus na rabbis. Tena ungejua hii tabia ya 'ujuaji' kujifanya unajua kila kitu. Au umeshikilia maarifa fulani kwamba ndio kila kitu, ndio tabia mahsusi kabisa iliyopelekea kumkataa nabiy Issa kati ya 'wasomi' waliokuwa wengi na kukubalika na watu wa kawaida.

Kuna maandiko katika biblia yanayoweka kheri kwa wahitaji wa maarifa; Heri walio maskini rohoni, maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Na zipo aya kadhaa zinazosifia tabia ya 'ufilosofi': Samahani bandugu nitakopi aya nzima maana sina hakika nikiwapa reference kama kila mmoja ataenda kweli kusoma:

Mithali 8​

1 Je! Hekima halii?
Ufahamu hatoi sauti yake?
2Juu ya mahali palipoinuka karibu na njia,
Penye njia panda, ndipo asimamapo.
3Karibu na malango, mahali pa kuingia mjini,
Mahali pa kuyaingilia malango anapiga kelele.
4Enyi watu, nawaita ninyi;
Na sauti yangu ni kwa wanadamu.
5Enyi wajinga, fahamuni werevu,
Nanyi wapumbavu, mpate moyo wa kufahamu.
6 Sikieni, maana nitasema yaliyo mazuri,
Na kufumbua midomo yangu kutakuwa maadili.
7 Maana kinywa changu kitasema kweli,
Na uovu ni chukizo kwa midomo yangu.
8Maneno yote ya kinywa changu yana haki;
Hapana hata neno lililopotoka au la ukaidi.
9Yote humwelea yule afahamuye,
Yote huelekea mbele yao waliopata maarifa.
10Pokea mafundisho yangu, wala si fedha,
Na maarifa kuliko dhahabu safi.
11 Maana hekima ni bora kuliko marijani;
Wala vyote vinavyotamanika havilingani nayo.
12Mimi, hekima, nimefanya werevu kuwa kao langu;
Natafuta maarifa na busara.
[Watafuta maarifa huitwa filosophers]
13 Kumcha BWANA ni kuchukia uovu;
Kiburi na majivuno, na njia mbovu,
Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.
14 Shauri ni langu, na maarifa yaliyo sahihi;
Mimi ni ufahamu, mimi nina nguvu. [Amenikumbusha hitimisho letu na draga]
15 Kwa msaada wangu wafalme humiliki,
Na wakuu wanahukumu haki.
16Kwa msaada wangu wakuu hutawala,
Na waungwana, naam, waamuzi wote wa dunia.
17 Nawapenda wale wanipendao,
Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
18 Utajiri na heshima ziko kwangu,
Naam, utajiri udumuo, na haki pia.
19 Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi,
Na faida yangu hupita fedha iliyo teule.
20Natembea katika njia ya haki,
Katikati ya mapito ya hukumu.
21Niwarithishe mali wale wanipendao,
Tena nipate kuzijaza hazina zao.

Sehemu ya Busara katika Uumbaji [READ THIS PART CAREFULLY, imebeba madini ya uzi huu. Kama yeyote utang'amua sehemu nilipopingana na maandiko tafadhari nirekebishe]
22 BWANA alikuwa nami katika mwanzo wa njia yake,
Kabla ya matendo yake ya kale.
23 Nalitukuka tokea milele, tangu awali,
Kabla haijawako dunia.
24Wakati visipokuwako vilindi nalizaliwa,
Wakati zisipokuwako chemchemi zilizojaa maji.
25 Kabla milima haijawekwa imara,
Kabla ya vilima nalizaliwa.
26Alipokuwa hajaiumba dunia, wala makonde
Wala chanzo cha mavumbi ya dunia;
27Alipozithibitisha mbingu nalikuwako;
Alipopiga duara katika uso wa bahari;
28Alipofanya imara mawingu yaliyo juu;
Chemchemi za bahari zilipopata nguvu;
29 Alipoipa bahari mpaka wake,
Kwamba maji yake yasiasi amri yake;
Alipoiagiza misingi ya nchi;
30 Ndipo nilipokuwa pamoja naye, kama stadi wa kazi; [Umeona!!]
Nikawa furaha yake kila siku;
Nikifurahi daima mbele zake;
31 Nikiifurahia dunia inayokaliwa na watu;
Na furaha yangu ilikuwa pamoja na wanadamu.
32 Basi, wanangu, nisikilizeni sasa;
Maana heri hao wazishikao amri zangu.
33Sikieni mafundisho, mpate hekima,
Wala msiikatae.
34Ana heri mtu yule anisikilizaye,
Akisubiri sikuzote malangoni pangu,
Akmngoja penye vizingiti vya milango yangu.
35 Maana yeye anionaye mimi aona uzima,
Nayafe aaftapata kibali kwa BWANA. [Njia, kweli, uzima ]
36 Bali anikosaye hujidhuru nafsi yake mwenyewe,
Na wao wanichukiao hupenda mauti. [Malipo ya ukaidi, uongo ni mauti]
Unajua mpaka najiuliza kwanini hujui swali langu. Swali langu ulisema ya kuwa Falsafa inamsaidia mtu kuujua ukweli, nikakuuliza swali tuonyeshe ni kwa namna gani Falsafa inamsaidia vipi mtu kuujua ukweli ? Hili ndiyo swali langu la msingi. Lakini nashangaa kwanini hulijibu.
 
Nikiri kwamba hilo la kusema 'unaleta mahubiri' nimelikopi toka kwa wadau kada aa humu JF tu.

Nikachukulia tafsiri yake ni: kuleta maneno au dhana fulani kutokea katika imani yako /kitabu chako na kusisitiza kuwa huao ndio uhalisia bila kujaliko kingine. Hasa kwa watu wasioamini unachokiamini in the
Sasa hili tatizo mko nalo wengi humu ndani, ndiyo maana ghuwa hamjibu maswali na mnakimbia hoja na mnakuwa mnakosea kosea sana. Sasa kwanini unakili jambo pasi na kulitafakari na kulihakiki ?

Sasa swali la msingi ni je ninayo yaweka humu ya uongo siyo uhalisia ? Kama ya uongo na si uhalisia kazi ni rahisi sana onyesheni uongo wake na kutokuwa kwake na uhalisia. Ili kuonekana mimi siko sahihi, sasa kama mnashindwa kufanya kimoja tu kati ya hivyo viwili, tatizo mko nalo nyinyi na elimu zenu ni ndogo, na mnakuwa mmekaa kibishi na mijadala ya kielimu haiendi hivyo. Lazima ukosoe hoja na kuinakishi hoja siyo kuikimbia hoja na kujaza tuhuma.
 
Kivipi ?

Nani haja tafsiri vizuri tamko hili ? Kwangu mimi ni kinyume nimeshaelezea zaidi ya mara mbili maana ya tamko "AKILI" tena kwa maana yenyekujitosheleza.

Nipe maana ya neno wazo na utupe msingi wake.
Mfano nimetazama mahala wazo wamesema ni 'tukio la akilini'. Sasa akili yenyewe ndio nisaidie uliitafsiri vipi tuendelee kujenga.
Mlitumia marejeo gani katika huo uchambuzi wenu huo ? Hiyo nishati mliijuaje na inaitwaje au ina sifa gani ? Sababu maelezo yako haya. yameishia juu juu.
Sio kila wakati mareference, kwani sisi hatuwezi kufikiri. Huu uwezo tumepewa wanadamu wote tuutumie. Usitake kuwapa credit bure na ushahidi wale wanaodai kwamba ukiwa mtu wa dini basi umeshikiwa akili. Basi chukulia kama ni nadharia katika ukuzi wake [a theory in development]
Nafsi ni roho na mwili. Roho ni kitu kisocho onekana chenye mafungamano ya moja kwa moja mwili na kuufanya mwili kuwa hai.

Hili ni kosa sababu umeandika ya uongo na kinyume na uhalisia.
Nimeomba ile 'hali' yaani roho ipojepoje kikwako. Wote tunakubaliana ni kisichoonekana ndio. Tunachotaka sasa ni maelezo ya hiyo 'entity' ya roho ilivyo ikiwa umekataa kuwa haipo kiwazowazo. Lete maelezo yako sasa.
 
Sasa hili tatizo mko nalo wengi humu ndani, ndiyo maana ghuwa hamjibu maswali na mnakimbia hoja na mnakuwa mnakosea kosea sana. Sasa kwanini unakili jambo pasi na kulitafakari na kulihakiki ?
Mbona nimeuona ukweli wake pia, kwani suala la wewe kung'angana na uhalisia wako binafsi, kuufanya ndio universal hufanyi? Hata Scars alijaribu kukuonesha hilo pale alipoamua kuchukua upande wa biblia kwa muda lakini sijui kama hataulimuelewa alichokuwa anakionesha. Je uliielewa maana pana ya alichokionesha achana na alichokitype tu?
Sasa swali la msingi ni je ninayo yaweka humu ya uongo siyo uhalisia ? Kama ya uongo na si uhalisia kazi ni rahisi sana onyesheni uongo wake na kutokuwa kwake na uhalisia. Ili kuonekana mimi siko sahihi, sasa kama mnashindwa kufanya kimoja tu kati ya hivyo viwili, tatizo mko nalo nyinyi na elimu zenu ni ndogo, na mnakuwa mmekaa kibishi na mijadala ya kielimu haiendi hivyo. Lazima ukosoe hoja na kuinakishi hoja siyo kuikimbia hoja na kujaza tuhuma.
Moja kati ya watu wanapenda mijadadala iwe ya kielimu ni mimi, rest assured

Lakini mda mwingine unatupa wakati mgumu maana hata tukijibu tunaonekana hatujajibu tu mfano hii tafsiri ya falsafa👇 bado tu turudi palepale kisa hatujagusia kijitafsiri ulichonacho wewe kichwani? Hakuna aliyekimbia hoja, sema kuna wanaokataa hoja wengi tu.
 
Unajua mpaka najiuliza kwanini hujui swali langu. Swali langu ulisema ya kuwa Falsafa inamsaidia mtu kuujua ukweli, nikakuuliza swali tuonyeshe ni kwa namna gani Falsafa inamsaidia vipi mtu kuujua ukweli ? Hili ndiyo swali langu la msingi. Lakini nashangaa kwanini hulijibu.
Okay okay nitajaribu tena mara ya tatu kama sikosei;

Kupenda busara/hekima kutampelekea mtu kuwa mtafutaji wa maarifa. I aaa.. h kutafuta maarifa pia hupelekea mtu kupenda busara [sijui kuku na yai mwingine IDK]

Kadri anavyotafuta maarifa atazidi kuwa mwerevu, na ndio atazidi kufahamu kuwa yapo maarifa zaidi na atayatafuta zaidi maana anakipenda hicho kitu. Atakuwa Philosopher.

Basi katika utafutaji wake huo atatumia mbinu nyingi, atachunguza asili, atasoma wanazuoni wengine, atatengeneza nadharia, atapima ukweli, atatumia mantiki, atabahatisha etc etc atatumia mbinu zote awezazo kuutafuta ukweli.

Kutokana na ukomo wa uwezo wake, na akili yake kuna msaada toka juu utamsaidia pia, haya huitwa mafunuo. Mfalsafa atayachukua na atayaharmonize na kuyasynchronize na anayoyafahamu. Atayatupilia mbali yaliyoonekana kuwa ni uongo[error] na ataukumbatia ukweli mpya anaoendelea kuufanyia kazi.
 
Mbona nimeuona ukweli wake pia, kwani suala la wewe kung'angana na uhalisia wako binafsi, kuufanya ndio universal hufanyi? Hata @Scars alijaribu kukuonesha hilo pale alipoamua kuchukua upande wa biblia kwa muda lakini sijui kama hataulimuelewa alichokuwa anakionesha. Je uliielewa maana pana ya alichokionesha achana na alichokitype tu?
Napenda watu wa kweli na napenda sana ukweli. Ukweli ni kwamba alichokiandika huyo uliye mtaja, hakiluodhi vigezo kutokana na maswali niliyo muuliza. Yeyw alimilo katika katika misingi ya wakristo mimi nilimili katika kuutafuta huo ukweli, ni vitu viwili tofauti, ndiyo maana mwisho wa siku akahitimisha ya kuwa tukubaliane katika kutofautiana. Watu hamuutaki ukweli na kuutafuta kadhalika, kingine siyo waadilifu.

Uzuri katika kitabu kiitwacho "adabu al Bahth wa al Munadhara (The etiquette of research and debate)" cha Imam Shanqiity anasema hakikisha unamjua vizuri yule unaye jadiliana na kusoma kwa umakini hoja zake, hili nyinyi mmelikosa.


Sasa kutokana na kutohakiki kwenu mambo yenu kumefanya muandike yale mnayo yataka na si kuandika ule ukweli.
Moja kati ya watu wanapenda mijadadala iwe ya kielimu ni mimi, rest assured
Kama hali iko hivyo, mbona hufati adabu za mijadala ys kielimu ? Sasa usiishie kupenda tu bali uifanyie kazi elimu na ujifunze kadhalika.
Lakini mda mwingine unatupa wakati mgumu maana hata tukijibu tunaonekana hatujajibu tu mfano hii tafsiri ya falsafa👇 bado tu turudi palepale kisa hatujagusia kijitafsiri ulichonacho wewe kichwani? Hakuna aliyekimbia hoja, sema kuna wanaokataa hoja wengi tu.
Wala mimi sikukuuliza maana ya Falsafa, mimi nilikuomba unionyeshe ni kwa namna gani Falsafa inakusaidia kuujua ukweli, nilikuuliza swali la maana ya wazo. Sasa wewe ukaanza kutoa maana ya Falsafa na kuacha kuelezea vipi Falsafa inakusaidia kuujua ukweli. Mfano nikusaidie tu, labda ungesema Falsafa imenisaidia mimi kujua Dunia imeumbwa na Mola kwa hivi na hivi, sasa ukitoa maana tu ya Falsafa unakuwa hujajibu swali nililo kuuliza.

Sasa msiwe mnawatuhumu watu kwa uongo, lazima muwe wasdilifu na kufanya insafu. Kinyume chake hatamfaidika na hii mijadala na mtakuwa mnapoteza muda.

Mimi niko tofauti sana na nyinyi sababu mimi nimekuzwa ba dini yangu katika kuutafuta ukweli na kuufanyia kazi, na si kuwa kama "Sponji" kuzoa kila kinachokuja mbele yangu.

Badilikeni vijana, na mkiyasoma hayo mnayoyasoma hakikisheni mnayaelewa.
 
Ila unatakiwa utambue kwanza unaishi Kwenye matrix umepangiwa cha kufanya na cha kuamua na watu wachache wenye nia ya mtu asijitambue , ukiona nembo ya jicho la tatu kwenye hao wanaoitwa secret society , ujue wao wamejitambua na ndo wao walituweka kwenye matrix fo the purpose. Ili mtu ujitambue na ujue ukweli wote from univesal memory unatakiwa uwe true seeker wa meditation ya spiritual.
😃. Secret society.....Mfano Mmasai na secret society anakuwa programmed saa ngapi huko umasaini alikozaliwa? ukiachana na tecknology, life of a human haina tofauti na viumbe wengine. Ts just eating, pooping, sleeping and sex ili kuzaana. Hata tukienda mars, mwisho wa siku ts all about eating, pooping and sex. Secret society nao mwisho wa siku they will eat, poop, sleep and have sex Kama ng'ombe tu.

Haya mawazo mengine ni matokeo ya kukua kwa tecknology na kujua kugoogle na ni ziada baada ya kula, kunya, kufanya ngono ili kuzaana.
 
Mfano nimetazama mahala wazo wamesema ni 'tukio la akilini'. Sasa akili yenyewe ndio nisaidie uliitafsiri vipi tuendelee kujenga.
Akili ni tamko lenye asili ya kiarabu, lenye maana ya kuzuia jambo lisiende nje ya mpaka wake, hii ni maana ya kilugha, na kama ya mkufungia mnyama kwa waarabu iliitwa "'aqli". Kiistilahi ni uwezo au kizuizi kinachomfanya mtu asikosea katika maamuzi na kufanya jambo.
Sio kila wakati mareference, kwani sisi hatuwezi kufikiri. Huu uwezo tumepewa wanadamu wote tuutumie. Usitake kuwapa credit bure na ushahidi wale wanaodai kwamba ukiwa mtu wa dini basi umeshikiwa akili. Basi chukulia kama ni nadharia katika ukuzi wake [a theory in development]
Kufikiri lazima tufikiri swali unafikiri kwenye au juu ya nini, na kipi unatumia iki usikosee kwenye kufikiri kwako ? Lazima hili uliangalie.

Mimi ni mtu wa dini na nimechagua dini sababu huku ndiko salama ilipo, hatuongei kwa kujisifu ila sisi huwa tunafikiria mambo kwa usahihi kuzidi wasio kuwa watu wa dini. Kadhalika akili zetu hazijashikiliwa na mawazo ya watu kama ilivyo kwa Wanafalsafa na Wakana Mungu.
Nimeomba ile 'hali' yaani roho ipojepoje kikwako. Wote tunakubaliana ni kisichoonekana ndio. Tunachotaka sasa ni maelezo ya hiyo 'entity' ya roho ilivyo ikiwa umekataa kuwa haipo kiwazowazo. Lete maelezo yako sasa.
Sasa tumeshakubaliana ya kuwa ni kisicho onekana, unataka vipi ujue kipoje kipoje na hakionekani ? Ishara ya kuwepo roho ni uhai na ndiyo roho humfanya mja kuwa hai na hii hupulizwa. Kama ilivyo njaa, njaa haionekani ila ina ishara kuonyesha uwepo wake ila huwezi kusema njaa ipo hivi na hivi bali unaweza kuelezea viashiria vya njaa, na ndivyo ilivyo kwenye roho.
 
Uzuri katika kitabu kiitwacho "adabu al Bahth wa al Munadhara (The etiquette of research and debate)" cha Imam Shanqiity anasema hakikisha unamjua vizuri yule unaye jadiliana na kusoma kwa umakini hoja zake, hili nyinyi mmelikosa.
Amini kwamba, karibu wote humu ndani tunafanya hivyo. Tunasoma hoja na kujitahidi kuwajua tunaojadiliana nao. Na wengi hoja ndio msingi na sio mtu. Siwezi kuikataa pointi ya ukweli ya mtu kisa tu nafahamu ni wa dini nyingine, au ni mkana Mungu. No.
Mimi niko tofauti sana na nyinyi sababu mimi nimekuzwa ba dini yangu katika kuutafuta ukweli na kuufanyia kazi, na si kuwa kama "Sponji" kuzoa kila kinachokuja mbele yangu.
Kuna tofauti fulani kati ya aliyekuzwa na dini kuutafuta ukweli, na aliyekuzwa na ukweli kuitafuta dini. Weka akilini hii kitu. Basi hayo yameshatokea ombea tu hiyo dini yako [jitihada zako za kumtafuta Mungu] iwe ni ya KWELI.
Badilikeni vijana, na mkiyasoma hayo mnayoyasoma hakikisheni mnayaelewa.
Ushauri mzuri kwa wote sisi tukianza na wewe. Na hivi kweli unafikiri kuna mtu katika hili jukwaa hafanyi jitihada hizo? Unaichukuliaje JF intel?
 
😃. Secret society.....Mfano Mmasai na secret society anakuwa programmed saa ngapi huko umasaini alikozaliwa? ukiachana na tecknology, life of a human haina tofauti na viumbe wengine. Ts just eating, pooping, sleeping and sex ili kuzaana. Hata tukienda mars, mwisho wa siku ts all about eating, pooping and sex. Secret society nao mwisho wa siku they will eat, poop, sleep and have sex Kama ng'ombe tu. Haya mawazo mengine ni matokeo ya kukua kwa tecknology na kujua kugoogle na ni ziada baada ya kula, kunya, kufanya ngono ili kuzaana.
Daah! umewapunguza sana wanaadamu.

Ni kweli tunafanya sex, eating, sleeping, and pooping lakini tumeenda mbali pia na KUJIULIZA kwa nini hayo mambo yapo vile yalivyo? Tumechunguza na tunaendelea kuchunguza kupata majibu.
 
Kuna tofauti fulani kati ya aliyekuzwa na dini kuutafuta ukweli, na aliyekuzwa na ukweli kuitafuta dini. Weka akilini hii kitu. Basi hayo yameshatokea ombea tu hiyo dini yako [jitihada zako za kumtafuta Mungu] iwe ni ya KWELI.
Ukweli unamkuza vipi mtu ? Ukweli upo ila dini ni mfumo wa maisha na ukweli si mfumo, vipi umkuze mtu. Jifunzeni maana za maneno ili mjue kuyatumia.
Ushauri mzuri kwa wote sisi tukianza na wewe. Na hivi kweli unafikiri kuna mtu katika hili jukwaa hafan
Wapo wengi sana na vitendo vyao ndiyo vinathibitisha hilo na si utetezi kama unao ufanya hapa.

Na kama wanafanya basi hawana misingi ya kuijua elimu yoyote wanayo jifunza ndiyo maana elimu hizo zinawapiteza na hawanufaiki kwazo.
 
Daah! umewapunguza sana wanaadamu.

Ni kweli tunafanya sex, eating, sleeping, and pooping lakini tumeenda mbali pia na KUJIULIZA kwa nini hayo mambo yapo vile yalivyo? Tumechunguza na tunaendelea kuchunguza kupata majibu.
Tunachunguza tukiwa na Objective ya kuendelea kuwepo ili tufanye yale yale vizazi na vizazi. Au kuna objective nyingine zaidi ya uwepo wetu? kuendelea kuwepo ndio sababu ya uchunguzi, na tukiwepo ni kuendeleza kula poop, sleep and sex. Hayo ndo maisha, mengine yoote ni ili hayo yaendelezwe.
 
Akili ni tamko lenye asili ya kiarabu, lenye maana ya kuzuia jambo lisiende nje ya mpaka wake, hii ni maana ya kilugha, na kama ya mkufungia mnyama kwa waarabu iliitwa "'aqli". Kiistilahi ni uwezo au kizuizi kinachomfanya mtu asikosea katika maamuzi na kufanya jambo.
Onaa sasa hii inavyosadifu kujifunga wewe mwenyewe. Yaani kama umetafsiri kitu kuwa ni mipaka wakati kiasili ni kitu kisicho na mipaka na umeona ni fine kabisa basi kuna tatizo. Ndio maana wanasema lugha ni chombo cha kutawala leo nimejionea. Basi tukubaliane kwamba mimi nikisikia neno 'akili' nina maana tofauti maana hata huyo anayeenda nje ya mipaka kwangu ni ametumia 'akili' yake.
Mimi ni mtu wa dini na nimechagua dini sababu huku ndiko salama ilipo, hatuongei kwa kujisifu ila sisi huwa tunafikiria mambo kwa usahihi kuzidi wasio kuwa watu wa dini. Kadhalika akili zetu hazijashikiliwa na mawazo ya watu kama ilivyo kwa Wanafalsafa na Wakana Mungu.
Hata mimi ni mtu wa dini kwa maana ya kutafuta, kumjua Mungu na kuwa na uhusiano naye.
Kuhusu ufikiri ni wote tunafikiri sahihi kulingana na uelekeo binafsi, kujumuisha wakana dini na wa dini nyingine labda kinachotutofautisha ni ile premise/msingi tuliouweka mwanzo tu. Asiyefikiri sahihi ni kichaa na humu hakuna kichaa.
Sasa tumeshakubaliana ya kuwa ni kisicho onekana, unataka vipi ujue kipoje kipoje na hakionekani ? Ishara ya kuwepo roho ni uhai na ndiyo roho humfanya mja kuwa hai na hii hupulizwa. Kama ilivyo njaa, njaa haionekani ila ina ishara kuonyesha uwepo wake ila huwezi kusema njaa ipo hivi na hivi bali unaweza kuelezea viashiria vya njaa, na ndivyo ilivyo kwenye roho.
Basi sasa kwangu nikisema hali ya kiwazowazo hata hiyo njaa ipo humo, ni kama dhana fulani/concept fulani inayoitwa na kuwa njaa. WAZO.
 
Tunachunguza tukiwa na Objective ya kuendelea kuwepo ili tufanye yale yale vizazi na vizazi. Au kuna objective nyingine zaidi ya uwepo wetu? kuendelea kuwepo ndio sababu ya uchunguzi, na tukiwepo ni kuendeleza kula poop, sleep and sex. Hayo ndo maisha, mengine yoote ni ili hayo yaendelezwe.
Basi hata mambo ya dini na kadhalika ni muendelezo wa kutaka kuendelea kuwepo - maisha ya milele so they say. Lengo ni moja ila kwa kina zaidi
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Basi hata mambo ya dini na kadhalika ni muendelezo wa kutaka kuendelea kuwepo - maisha ya milele so they say. Lengo ni moja ila kwa kina zaidi
Ndio mkuu. Watu tunataka kuendelea kuishi. Na kuendlea kuwa na matumaini ya kuishi, Yaani to keep on eating, pooping, having sex. Kutokuwepo na vizazi kupotea ndio hofu tuliyonayo binadamu na ndio kichocheo cha mambo mengine yote.

Muulize muumini, ukishaenda mbinguni then what? Muulize mwanasayansi ukishagundua chanzo cha uhai then what? Muulize yoyote swali lolote mwisho unarudi pale pale, kuendelea kula, kunywa na kuishi kama wafanyavyo wanyama wengine.
 
Onaa sasa hii inavyosadifu kujifunga wewe mwenyewe. Yaani kama umetafsiri kitu kuwa ni mipaka wakati kiasili ni kitu kisicho na mipaka na umeona ni fine kabisa basi kuna tatizo. Ndio maana wanasema lugha ni chombo cha kutawala leo nimejionea. Basi tukubaliane kwamba mimi nikisikia neno 'akili' nina maana tofauti maana hata huyo anayeenda nje ya mipaka kwangu ni ametumia 'akili' yake.
Nimefurahi kuona nilichokiandika hujakielewa na huu ni muendelezo wa kuonyesha udhaifu wenu na kutoshughulika na dhati ya mambo.

Naam akili ina mipaka, ndiyo maana hakuna anae ijua kesho yake. Akili inaishia pale ambapo ufunuo unapo endelea.

Ndiyo maana hata Wanafalsafa wa kale wa Magharibi kwa kutumia kwao akili zao walitafuta chanzo cha maisha na kila kitu lakini wakakosea, hii ilionyesha mpaka wa akili. Wapo waliosema chanzo cha maisha ni moshi,wengine wakasema moto, wengine wakasema hewa, wengine wakasema Atomu na wengine wakasema ukamilifu upo kwenye namba kumi hapa namuongelea Pytahgoras, bali wengine wakasema kisicho mpaka na wengine na wengine.

Kwahiyo huwezi kuonyesha wapi nimejifunga. Ndiyo maana umeishia kuandika tu na kuondoka zako bila kulsoa nilicho kiandika.
Hata mimi ni mtu wa dini kwa maana ya kutafuta, kumjua Mungu na kuwa na uhusiano naye.
Kuhusu ufikiri ni wote tunafikiri sahihi kulingana na uelekeo binafsi, kujumuisha wakana dini na wa dini nyingine labda kinachotutofautisha ni ile premise/msingi tuliouweka mwanzo tu. Asiyefikiri sahihi
Hii sahihi sababu ukweli upo kinyume chake. Huwezi ukawa mtu wa dini ukaitanguliza falsafa, wakati msingi wa falsafa tunaujua ya kuwa ni akili pekee.

Kuna jibu lako ulilitoa nikalipuuza kwa kutoa kwako jibu hilo kwa kulazimisha maana ya kupenda hekima kama imekusaidia kuujua ukweli. Wakati muda huo Falsafa inajioambanua kama elimu na fani yenye matawi kadha wa kadha.
Basi sasa kwangu nikisema hali ya kiwazowazo hata hiyo njaa ipo humo, ni kama dhana fulani/concept fulani inayoitwa na kuwa njaa. WAZO.
Ushawahi kujiuliza kwanini unashindwa kutoa maana ya tamko wazo na kuliweka katika uhalisia ? Wewe huwa una wazo, jiangalie tu wewe wazo la kujenga nyumba fulani linakuwa vipi na ufahamu au kujitambua ? Hili kwa kukusaidia hutoweza.
 
Ushawahi kujiuliza kwanini unashindwa kutoa maana ya tamko wazo na kuliweka katika uhalisia ? Wewe huwa una wazo, jiangalie tu wewe wazo la kujenga nyumba fulani linakuwa vipi na ufahamu au kujitambua ? Hili kwa kukusaidia hutoweza.
Hapana, wazo la kujenga halina utambuzi lipo kundi la mawazo fixed ambayo baadaye tutayacrystallize kuwa nyumba.

Yanayojitambua ni kama hivyo nafsi za watu na roho zao. Yanayojitambua ni yana nguvu fulani inayoyapower. So yana kitu kama will yaani utashi.
 
Back
Top Bottom