Uteuzi: Rais Samia amteua Humphrey Polepole kuwa Balozi Malawi, Mchechu arudishwa NHC

Uteuzi: Rais Samia amteua Humphrey Polepole kuwa Balozi Malawi, Mchechu arudishwa NHC

Polepole kamuenzi JPM,kabaki na ulimi mmoja mpaka sasa,na hatimaye kaula.
Mkuu, hapo jamaa kazimwa aachane na wahuni, kama ni suala la ulaji hata ubunge ulikuwa na pesa tu
 
Polepole kamuenzi JPM,kabaki na ulimi mmoja mpaka sasa,na hatimaye kaula.
Kwa akili yako wewe unaona kaula? Bora ungeishia kusoma tu bila kukomenti chochote. Ona sasa unavyoonekana mpumbavu kwa vitu vya kujitakia.
 
Inaonesha kabisa Mama hataki mtu yeyote wa Magufuli na kwa hesabu yao wanaona Pole pole atawapa challenge! Sasa kwa kifupi katumbuliwa huko ni kumpeleka tu akajinyonge mwenyewe! Kama anajiamini amtake Rais asichukue nafasi yake! Ila tofauti na Hapo ndo kashapotea huyo!
tatizo ukikataa unaonekana huna maslahi na nchi bali ni tumbo lako binafsi, kwani hata huko Malawi unawakilisha maslahi ya Taifa lako
 
Hivi inakuwaje mstaafu anarudishwa kazini?

Huku ndio kupeana mashavu sasa. Huku watoto wa maskini waliojikongoja kusoma wanaambiwa waende veta au wajiajiri..

Recycling bad, old, broken, tired people, with nothing new to offer. Uwezo mdogo wa kuchagua watu sahihi kuongoza na kusimamia Taasisi, idara na wizara nyeti kwa maslahi ya Tanzania unaligharimu na utaligharimu sana hili taifa.
 
Juzi waliidhinisha mkopo wa kibiashara tsh 164 billioni with government guarantee NHC wamalizie miradi yao iliyokwamia kati washapewa first payment tsh 40 billion.

NHC ilikopa zaidi ya tsh 1 trillion zama za J.K miradi ambayo aikulipa. Kwakuwa mkopo ulikuwa na government guarantee sasa hivi deni linalipwa na walipa kodi.

Nehemia alipotaka tena government guarantee kwa miradi ambayo keshaikopea ilihali madeni ya awali serikali inamlipia for poor investment decision and poor management of costs za miradi ndio JPM alipoona upuuzi na kumtimua.

Mama shida, hiyo kazi sio size yake ni wazi nani anaongoza nchi kwa sasa. Inaonekana anawaza kuendelea baada 2025 come whatever na kufanya ivyo inabidi amfurahishe mwafulani akiamini anaweza mudu mikiki ya 2025.

Kumalizia miradi sio shida but does it have to be the same people who caused the problems in the first place.
 
Mbona Malawi karibu ni bora angepelekwa Ukraine huko kungemfaa zaidi
 
Nehemia Mchechu NHC tena? Ni sababu zipi zilipelekea kutumbuliwa? Hazikuwa genuine?Hivi hakuna watanzania wengine?
Kizazi cha mchwa kilianza kurudi mapema tu baada ya mama kushika usukani.
 
Akikataa Uteuzi wa Rais kesho kutwa yule Muandishi wa Barua ya Mnyika ya kuteua Kina Halima Mdee na ya kujiuzulu Ndugai anaingia Jikoni na huwa hakosei mapishi
Nimecheka sana hii coment
 
Rais Samia Suluhu amemteua Humphrey Polepole kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi.

Sambamba na hilo Rais Samia Suluhu amemteua Shamsi Vuai Nahodha kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Pia Rais Samia Suluhu amemteua Waziri Kindamba kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe.

Kindamba alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa TTCL na anachukua nafasi ya Mhandisi Marwa Rubirya ambaye amestaafu kwa umri.

Polepole na Kindamba wanatarajiwa kuapishwa kesho Jumanne tarehe 15 Machi 2022 Ikulu ya Chamwino Dodoma saa 04:00 Asubuhi.

Katika hatua nyingine Rais Samia Suluhu amemteua Nehemia Mchechu kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

Mchechu ambaye amewahi kuhudumu kwenye wadhifa huo, anachukua nafasi ya Dkt. Maulid Banyani ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Pia amemteua Balozi na Mkuu wa Jeshi la Polisi (Mstaafu) Ernest Jumbe Mangu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Mamlaka ya Bandari (Tanzania Port Authority).

Na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Peter Ulanga kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL).

Ulanga ni Mkurugenzi Mstaafu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF).

Na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Meja Jenerali John Julius Mbungo, Mkurugenzi Mstaafu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuwa Mwenyekiti wa Bodi wa Shirika la Meli Tanzania (MSCL).

View attachment 2150380
View attachment 2150479
WAZIRI NAPE NNAUYE ALIVYOTANGAZA UTEUZI WA HUMPHREY POLEPOLE
Kashika kidevu
 
Nauliza tu sio kwa ubaya.
Hivi Polepole Ana mke na watoto?
Maana kila Mara namuona anapika au amehifadhi KY.
 
Back
Top Bottom