Utofauti wa Mwafrika na watu wengine hauko kwenye rangi tu, hata akili. Mtu mweusi kapunjwa akili

Utofauti wa Mwafrika na watu wengine hauko kwenye rangi tu, hata akili. Mtu mweusi kapunjwa akili

Hakuna kabisa kinachotesa, ila hali tuliyo nayo inafikirisha! Kaa hapo ulipo na kuanza kutafakari, bila mzungu ungekua umevaa magome ya miti, hauna umeme, hauna simu ya mkononi, TV,hauna usafiri, orodha ni ndefu mno!
Ukiwa unamaanisha nini haswa? Wacha ulimbukeni. Kwani kuvaa magome ya miti ni dhambi? Kiuhalisia sio lazima mtu kuishi uwe na umeme, sio lazima kuwasiliana na simu ya mkononi, Usafiri....unajuwa horsepower?
Usionyeshe ulimbukeni namna hiyo ndugu yangu.
Bibi ya kuke kijijini, nilipokuja toka shuleni na kumwambia mzungu mbaya,nusura achukue mwiko anipigie nao!
Aliniuliza leo unanisomea barua toka kwa baba yako,( baba yangu alikua Dar sisi tuko mkoani) aliniuliza lini uliona karatasi linaweka maneno,au linakuambia kitu.Akaniambia enzi zao mtu akiwa mbali hujui amekufa au mzima!
Baadaye nimemwelewa Marehemu bibi yangu!
Irrelevant. Sorry for your loss.
 
Usimkufuru Muumba wako, na wala usimdhihaki Mungu......
Lakini pia usiangalie historia ya dunia katika kurunzi ya karne za 17-21, huwezi kupata majibu sahihi.
Nina mengi sana ya kusema, lakini nadhani hatutaelewana kwasababu umeshaamini kwamba wewe ni duni.
Nataka kukuambia namwamini Mungu, na kwa upande wangu naona wazi Mungu Ali create races mbalimbali, na maybe alizitaka zi function tofauti! Maana hata katika uumbji wake,kuna wenye IQ kubwa na wengine ndogo!

Wengine hata umpeleke shule gani na umpe kila nyenzo! Uwezo wake wa kuelewa ni mdogo! Hata ufanyaje!

Hivyo sio mbaya ukiliangalia tatizo la Waafrika that way! Sisemi huo ni mtamo wangu 100%..
Lakini nao nauangalia napo tazama tatizo la mwafrika.
 
Hizo Mwene Mutapa, Songhai, Mali Empire n.k kuzilinganisha na British Empire, Spanish au Mongol Empire ni sawa na kulinganisha kichuguu na mlima Kilimanjaro.
Angalia Legacy ya British na Spanish Empire duniani; Kingereza ni Lugha ya Kwanza, ikifuatia na Kihispania kuzungumzwa na jamii nyingi zaidi tofauti duniani. Wamesambaza dini ya Ukristo kote duniani, Wamesambaza mfumo wa sheria, uongozi, mavazi, mazao.

Nitajie hata legasi moja ya hizo himaya za Ki Africa hata kwetu watu weusi wenyewe.

Legacy itokee wapi brother wakati ilifutwa na nchi zilizozitawala kiasi kwamba mtu hata akifua chuma anakatwa mkono

Na pia Africa katika kiwangi kikubwa haikuwa imepiga hatua ya kuifikia imperialism kiasi cha kuanza kutawala sehemu nyinginezo za nje ya Africa

Ila kwa teknolojia baadhi za north Africa kama calender, kuhesabu, majira na misimu ya mwaka. Yalivumbuliwa misri ya zamani 🙏🙏
 
Sidhani hata kama viongozi na walimu wengi wana ufahamu au uelewa wa umuhimu wa mlo bora kwa wanafunzi mashuleni. Wao watakuwa wanafahamu wanafunzi wanatakiwa wale wajaze tumbo tu.
Nilisikitika sana. Nilimpa solution ndogo lakini matokeo yake yangekuwa makubwa. Awali bajeti ya kununua mboga kila jumanne ilikuwa inawapa tabu. Lakini nasikitika sana na wenzangu walikuwa ready kwamba sisi wenyewe wanafunzi tujilimie na kutunza bustani.
Poor us!
 
ukisoma historia ya gunduzi muhimu katika hisabati na sayansi utakuta jamii zingine zote duniani zimehusika kasoro mtu mweusi tu
Mansa Musa alienda America before ya Columbus na akafanya biashara na wenyeji. Ivi hii Koo yake bado Ni tajiri na ule utajiri kweli inabidi tufuatilie
 
Waarabu walifanya haya yafuatayo katika historia yao:
1. Walianzisha hesabu za Algebra (Uniting broken parts)
2. Wao ndiyo walianzisha namba hasi (Negative Numbers), mtafute Omar Khayyam.
3. Wao ndiyo walianzisha mfumo wa tumia desimali kurekodi Sehemu (Decimal in recording fractions)
4. Wao ndiyo walianzisha hesabu za mchemraba (Cubic Equations), mtafute Omar Khayyam.
5. Wao ndiyo walifanikiwa kurekodi jamii 200 za mazao (Classification), mtafute Ibin Bassal.

Lakini nikuulize, hivi leo hii hawa waarabu ambao wameisaidia dunia hivi, wameweza kutengeneza hata gari au ndege yoyote ile zaidi ya kuuana ??? Tatizo ni nini ??? Utasema hawana akili ???
Sasa unasemaje Mkuu? Nini kilitokea kikatufanya tuwe hapa? It seems mzungu alichukua hiyo knowledge akatupiga nayo usoni!
Sasa hiyo knowledge yote kwa nini tuliipoteza! Kwa nini mzungu anaitumia against us!
Kuna mahali tulizidiwa kete!
 
naumga mkono hoja yako ila kuna maeneo nakupinga kwakua sote ni sawa ila mfumo wa kidunia ndio unakandamiza zaidi waafrika

chanjo madawa na bidhaa nyingi zinazokuja afrika sio salama sana kwa afya ya akili zetu na hii yote inasababishwa na uchumi mdogo tulio nao hivyo kutegemea zaid kutoka nje ndio maana watajiri wanapeleka wake zao kujifungulia nje wakijua kabisa mtt atapata chanjo za nje na atakua amekwepa machanjo takataka tunayoletewa ambayo yanavinasaba vinavyoharibu mfumo wa fahamu kwa asilimia kubwa
 
Sijui ni kwamba hata kusoma hatupendi au hata uwezo wetu wa ku focus/attention bila kulazimika nao ni mdogo. Waafrika wengi wanasoma ili wapate vyeti na kazi tu.
Unaweza ukasafiri mwaka mzima kwa bus, meli, treni au ndege usikutane kabisa na mtu mweusi akiwa hata ameshika tu kitabu.
Hapa bando wanalitumia insta kucheki mademu na tiktok. Kiukweli inauma mno Basi. Mtu hajui anaweza akajifunza skills nyingi mno online ama kwa vitabu vipo vingi na Ni bure Ni bando lako tu.
 
Nataka kukuambia namwamini Mungu, na kwa upande wangu naona wazi Mungu Ali create races mbalimbali, na maybe alizitaka zi function tofauti! Maana hata katika uumbji wake,kuna wenye IQ kubwa na wengine ndogo!
Wengine hata umpeleke shule gani na umpe kila nyenzo! Uwezo wake wa kuelewa ni mdogo! Hata ufanyaje!
Hivyo sio mbaya ukiliangalia tatizo la Waafrika that way! Sisemi huo ni mtamo wangu 100%..
Lakini nao nauangalia napo tazama tatizo la mwafrika.
Mkuu, unapozungumzia akili ya binadamu (Human Intelligence) unazungumzia kitu kikubwa ambacho kina sura nyingi. Mpaka sasa wanasayansi wa masomo ya saikolojia wanaanza kukubaliana kwamba akili ya binadamu ina nyanja zaidi ya tano (Facets of Intelligence). Hivyo hakuna mwanadamu ambaye anaishi halafu asiwe mzuri kwenye nyanja hata moja. Prof. Howard Gardener anazigawanya human intelligence katika nyanja kuu hizi zifuatazo:

  1. Logic-Mathematics Intelligence
  2. Visual- Spatial Intelligence
  3. Musical Intelligence
  4. Bodily - Kinesthetic Intelligence
  5. Linguistic - Verbal Intelligence
  6. Intrapersonal Intelligence
  7. Interpersonal Intelligence
  8. Naturalistic Intelligence
Sasa leo, hii ukitaka kumpima Lionel Messi akili kwa kumlinganisha na Elon Musk nadhani utakuwa unakosea sana. Hili ndiyo tatizo kubwa la mifumo ya elimu zetu ambazo zimeanzia Ulaya. Hivi unadhani mtu kama Diamond Platnumz na Mbwana Samatta wangeendelea kukaa darasani wangefanikiwa kama ambayo wamefanikiwa leo hii ??? Hili hadi Albert Einstein aliwahi kulisema......

NB: Kwamba mkuu ni lazima mtu afaulu darasani ili kupima uwezo wake kiakili ???
 
watu wanajua USA sheria zipo tofauti kati ya White people na Black people... na serikali imehakikisha there is no family structure among Black people in USA sababu wanajua strong society haiwezi kupatikana kama hakuna family structure
Samahani mkuu nakuomba unielezee hili nilielewe tafadhali hata pm nakuomba mno japo nijue dunia yangu ilivyo
 
Inavyodaiwa, sehemu muhimu sana ya ubongo wa Binadamu inayojulikana kama "Modula Oblangata" ya Waafrika waliyo wengi (siyo wote) ni duni ukilinganisha na Wazungu na Watu wa ngozi nyeupe.
 
Hapa bando wanalitumia insta kucheki mademu na tiktok. Kiukweli inauma mno Basi. Mtu hajui anaweza akajifunza skills nyingi mno online ama kwa vitabu vipo vingi na Ni bure Ni bando lako tu.
Elimu iliyoko leo Mitandaoni,mzungu hakuwa nayo huko nyuma.Waafrika tuna desa la bure! Unaweza kujua hata Nuclear inatengenezwaje!

Lakini mitandao ya pono ndio inayoongozwa kutazamwa! Mtu anakuuliza swali,tena graduate, kitu ambacho angepata tu kwa kutumia siju yake!
Iko kazi mkuu!
 
Hapa tunaangalia facts nyingi sana usi depend na fact moja ok tunaweza kusema upo sahihi lakini upande mwingine haupo tuangalia fact mbili utamaduni na life style huwezi ukasema utamaduni wa mzungu ukawa sawa na mwafrika hata siku moja haiwezekani kitu kama tutoea mfano mzuri kuitwa boss kama ulivyo tangulia kusemaa hapo lakin wale haki sawa na hawaruhusu kuonekana mtu boraa zaidi huko kwao na wale maisha yao hawana hofu na nidhamu yao ya kawaida kulinganisha na waafrika wafrika wengi ni waoga na pia tunaheshimaa ndo maan kila mtu mwenye wadhifa wake anapewa heshima lakini wenzetu hawana hivyo vitu sis tamaduni zetu na desturi ni tofauti na wao na life style yao na ya kwetu ni tofauti na wote tumeumbwaa sawa akunaa Aliyependelewaa sisi ishu uwajibikaji nakutumia fursaa
 
Tutabalishaje hiyo mind set? Tunakua na Rais mwenye PHD, anaongoza serikali nzima, na wananchi kwenda kupokea ndege airport karne ya leo! Wasted hours, wengine wanatoka Dodoma na magari ya serikali just kuja pokea ndege! Sasa huoni tu kuna vichwani mwetu haviko sawa!
Sikupingi hata kidogo. Kuna vitu haviko sawa vichwani mwetu. Na tunafanya haya yote wakati sisi ni maskini wa kutupwa. Hata hii tozo ni kielelezi kingine cha kushindwa kwetu. Maskini anatozwa fedha leo, kesho yake Mwingulu anaichukuwa na kwenda kuitumbua yote na msafara wake.
 
Africa ina vituko sana, kuanzia juu mpaka chini
Vituko ni vingi mno! Kuna Rais West Afrika alijenga kijijini kwake kanisa kubwa kushinda la Vatican! Hata kijijini chake kizima kingeingia kanisa labda lisingejaa!
Mobutu alifanya nini kijijini kwake! Hebu tukubali kidonge kichungu! Tuna matatizo makubwa!
 
Sikupingi hata kidogo. Kuna vitu haviko sawa vichwani mwetu. Na tunafanya haya yote wakati sisi ni maskini wa kutupwa. Hata hii tozo ni kielelezi kingine cha kushindwa kwetu. Maskini anatozwa fedha leo, kesho yake Mwingulu anaichukuwa na kwenda kuitumbua yote na msafara wake.
Sio hivyo tu,kijiji kizima kinatoka kumpokea! Kesho akichukua madaraka ataanza wimbo...mabeberu ...
mabeberu ndio wametufikisha hapa!
 
Unaifahamu historia ya kemet/Misri , amabayo hapo kabla ilijulikana land of blacks Ambayo haijachakachuliwa na hao white supremacists?

Unafaham kemet/Misri ilitawala Dunia Kwa miaka mingi uko nyuma? Unafaham wa Arabu ni Wafamizi North Africa na Egypt ya Leo?

Unafam pyramids zilizopo Misri, Sudani, na Ethiopia zimejengwa na watu weusi, na Hadi Leo hawana jibu zilijengwa vipi, na unafaham hesabu ilitumika kujenga hizo pyramids?

Unafaham Kemet/Misri ilistarabika mapema zaidi ya Ulaya? Unafaham wana Filosofia wa Magharibi walikua wakisafiri kuja kujifunza Kemet/misri?


Unakifahamu kitabu Cha the book of the coming forth by day/ book of the dead , Kiliandikwa na watu weusi?

Unafaham maktaba ya Alexandria iliyochomwa moto na wazungu wakishirikiana na ndugu zao wa arabu, kupoteza asili ya mtu mweusi na yote aliyo yafanya hapo kabla, na wakaiba vitabu vyote vilivyokua vinaelezea sayansi na teknolojia wanayotumia hivi sasa kufanya uvumbuzi, na vilivyobaki wakavitia moto?
Unafaham kuanguka kwa kemet/ misri ndio ulikua mwanzo wa Afrika kutawaliwa na kuchukuliwa watumwa?

Unafaham wazungu wanavyotumia nguvu kubwa kupindisha historia ya Mtu mweusi Ili aendelee kujiona Duni, na awatawale milele?

Unafaham gunduzi zinazofanyika Misri ya Leo kwenye pyramid of Giza hazitoki hadharani Hadi ziwe white washed?

Usijidharau ndugu, hapo kabla tulitawala kuanzia Afrika, Amerika Hadi Ulaya,

tawala zinainuka na kuanguka, zama za hao westerners zinaenda kufika ukingoni, Afrika inanyanyuka tena.
Kwani mkuu hii maabara ya Alexandria si alikuwa mtawala wa ottoman empire. Si alikuwa anatokea sijui gani akaja akapiga kambi hata misri Kuna bandari Ina jina lake. Na Ni kweli wale Roman empire walikuwa wanakuja kujifunza huko Egypt vitu.


Sema na Roman empire ilitapakaa ujue mpaka Sahara desert pia.
Kuna dola zilitawala hapo.
Mansa Musa alienda America around 1340 Kama sio kijana wake aliyeitwa aboubakar akafanya biashara na hao wahindi wekundu hakujisema kuwa Aligundua Bata Ilo Mana lilikuwepo.


History ya mweusi Ni Kama imefichwa huwa kidogo Patrice lumumba anawaamsha watu sema hawaamki.



Huyo Alexandria the great Kuna namna alikuja huko misri hakuwa mturuki kweli Ila alikuwa Ni mtu wa Taifa sio ndani ya afrika.
Naomba uni update na Kama una off naomba unisaidie plz
 
Chanzo cha yote hayo ni hii elimu yetu 😁
Elimu yetu ina mapungufu yanayo hitaji kazi ya ziada kuyarekebisha!
Na hii nikuanzia chini kabisa (Nasari) na kuendelea; Inapima mtu anayeweza kukariri kuliko wengine.
Hivyo anayeweza kukariri eti ndiye mwenye akili; maana yake Elimu yetu imetengenezwa kwa mfumo wa kuandaa wafanyakazi/waajiriwa (labour). Anayeweza kukariri ukimtuma kazi hasahau ila hana ubunifu/Creativity
Namaanisha; Elimu yetu haiandai watu Kufikiria. Vipaji mbalimbali, ubunifu nk havina nafasi kabisa kwenye mfumo wetu wa Elimu

Kwa upande wa weupe (Wazungu) hutumia muda na nguvu kubwa kujua kipaji cha mtoto na anaelekezwa kusoma hicho hicho; kama ni kuimba, kuogelea, michezo, ufundi wa magari/ujenzi/mitambo nk, mahesabu, viumbe hai, historia nk
Na ndio sababu unakuta mzungu anachokijua anakijua kweli kweli. Huku Bongo unafundishwa mambo mengi na karibia 50% hayana application kwenye kitu chochote...badala yake ni kupima mtu anayeweza kuya kariri. nk nk nk nk nk
 
Back
Top Bottom