Utumwa katika picha: Hivi iliwezekana vipi? Mbona Waarabu, Wahindi, Wachina hawakufanywa slaves?


unayajua mateso wanayoyapata?
 
Wakuu,

Mwelekeo tu wa thread hii,unaonyesha wazi kuwa WAAFRIKA TUNA MATATIZO ndani ya vichwa vyetu!
Hapa mleta hoja alikuwa anatuamsha na tuone jinsi hawa wakoloni walivyotufanya wanyama na kutushawishi tujitambue!!

Cha ajabu eti badala ya KUUNGANA na kupeana moyo na kuzikataa hila zote za kikoloni dhidi yetu kuwa sisi si watu,eti tunagombanana sisi kwa sisi tukitetea MABWANA ZETU waliowafanya babu zetu watumwa!!!!#!

Hivi kama dini zao zinatufanya tuwe hivi,kwa nini hatujiulizi UOVU wote waliouleta chini ya mwamvuli wa dini zao!!?

Mie nawaomba sana,linapokuja suala la UAFRICA wetu tuvue dini zetu pembeni na tupiganie utu wetu kama waafrika!!

May God bless AFRICA!
 

Jee, huelewi kuwa hao hao babu zako ndio walikuwa wakiuzana wenyewe kwa wenyewe kwa kubadilishana na shanga na vioo? soma historia.

Naona ni ujuha kuanza kulaumu mtu aliyekuja kununua biashara ambayo ameuziwa na babu yako ukaanza kumlaumu.

Kwanini tunataka kuficha historia ya ukweli?

Siamini kuwa Mwaarabu au Mzungu mmoja aje peke yake akamate watu na wao wanamuangalia tu. Historia ya ukweli haipo hivyo, tunaelewa kuwa Waafrika walikuwa mashujaa, tunaelewa kuhusu akina Kimweri, Milambo, Mkwawa, Songea na wengineo waliopigana vita kukataa kudhadhalishwa na wazungu.

Ukweli ni kuwa Waafrika wenyewe walikuwa wakifanya biashara hii na wanunuzi walikuwa wakija kutoka ndani na nje ya Afrika. Tena kwa thamani ya shanga na vioo tu, usishangae, shanga na vioo enzi hizo vilikuwa ni vitu vya thamani kubwa kwa kuwa walikuwa hawavijui na ni vya ajabu sana kwao. Kam vile sasa noti, Waafrika leo hii tunauzana wenyewe kwa noti, kwani thamni yetu ndio imefikia hapo.

Naona bora mababu walikuwa na akili kwa kuuza wenzao kwa vioo na shanga kuliko sasa tunauzana kwa noti aka makaratasi.
 
niliona ile movie 12 years a slave ......

yaani mtu anapigwa halafu analazimishwa kusema jina lake la kiutumwa.
(Brain washed ) baada ya muda mtu anajiita mtumwa na anaamini alizaliwa kuwa mtumwa.

Ni kitu ambacho bado nakitafakari .
 

Mkuu,
Biashara bila soko haifanyiki!
Hao babu zetu waliwauza hao wenzao kutokana na nguvu wakoloni waliyokuwa nayo!
Na si kwamba ni babu zetu wote walihusika na biashara hiyo ,ni baadhi tu ambao walikuwa vibaraka wa hao wageni!!
Kwa hiyo suala la utumwa lilikuwa ni baya kwani lilikuwa linafanyika kwa kutumia nguvu na bila ya ridhaa ya yule anayefanywa mtumwa!

Na kushiriki kwa waafrika wenzetu kwenye biashara hiyo mbaya hakuifanyi biashara hiyo kuwa ilikuwa nzuri!

AFRICA kwanza!
 
Hao waliuawa na walihasiwa pia wanawake hawakupelekwa huko uarabuni.

Hapana sio kweli hata wanawake walipelekwa pia na ushahidi upo mwingi tu na huko Kuwait kulikuwa na mfalme mwafrika ambae mama yake alikuwa ni mtumwa na baba yake mwarabu
 
Sina agenda yoyote..., ila kiukweli ni kwamba waafrika bado ni watumwa..., waulize CCM watakuambia ni kweli au sio...

​jikomboe kifikra kwanza maana inaonekana bado! sikiliza wimbo mmoja wa bob Marley uitwao Redemption Song, kuna ka kipengee kanasema ....emancipate yourself from mental slavery....
 
Sidhani kama ni busara kuanzisha uzi mpya lakini kuna kitu kinafanana na hiki nimekikuta sehemu.
Naomba kama kuna mtu mwenye taarifa haya maonyesho yako wapi atujulishe ili baadhi watakaoweza waende kuweza 'kufungua' vichwa vyao.
 
Cha kusikitisha ni kuwa haya mambo yanatokea sasa kwa kiwango cha kusikitisha zaidi.
wale walio wasomi wanawaumiza zaidi wasiosoma lakini cha kujiuliza ni kwa nini hakuna ukataaji wa makusudi ili haya yasitokee!?
Hivi siasa za Al-Shaabab, Boko Haram, LRA ni matokeo ya haya!?
 

Hakika Mkuu wangu. Umenena.

Tafakari bora na yenye kuleta tija kwetu haipaswi KUFUNGWA na misimamo ya aidha mazoea yetu, imani zetu, vyama vyetu, serikali, mila, elimu, ndugu, mama, mzazi, mtoto, urafiki, n.k. Kuwa huru kwanza, USIFUNGWE na chochote, JIKATAE/JIKANE, kuwa mweupe kabisa, ulichobaki nacho kiwe Uwezo wa kutafakari tu!

HAKUNA LILILOGUMU KWA MTU MWEUSI KAMA KUKANA UKRISTO AU UISLAMU WAKE, JAPO NI KATIKA TAFAKARI TU! Na hayo ndio mafanikio makubwa ya mzungu kwa Mtu mweusi. Hapo hatukuchanganya ushabiki wa mpira, muziki, vyama, mavazi, n.k. ni TOTAL BRAINWASHING!

Lakini Bob alitutaka tujumuike nae katika kuimba the song of revolution "Redemption Song" pia akatutaka bila kuchoka wala kusita kila raia kila kona into battle "War" nonestop, till we "Chase dem Crazy Boldheads"

So 'Won't u help to sing, Anothe song of freedom'

Mungu wetu yu tayari kutupigania vitani. Anaita sasa!
 
Yaliyopita si ndwele, tugange yaliyopo na yajayo.

Kama hujui ulikotoka, huwezi kujua ulipo na uendako. Kwa kutokupenda kujishughulisha na historia ya tulikotoka kantu hatuwezi kujua tuendako.

Kwa hayo mawazo yako ndio maana mpaka leo bara la Afrika bado tu watumwa na tutaendelea kuwa watumwa.
 
Swali lako zuri sana! Hata mimi nikiwa mdogo nilishawahi kumuuliza babu yangu kua ni kwanini huku kanisani picha ninazoziona ukutani na mazabahuni kama vile zile picha za Mitume/Malaika/Yesu na Bikira Maria ni wazungu tu na picha ya Shetani ni kiumbe cheusi???
 
tena yapasa kujiuliza hao watumwa kibao kutoka EAST AFRICA na kusafirishwa kwa majahaz kwenda kwa majini magaidi KIZAZI CHAO KIPO WAPI??? mbona wa west africa kizazi chao kipo america?? historians naomba mnijibu

walikua wakiwaas kama mabeberu...wazungu hawakua na uo ukatil thats y leo tun ma negros....
 
Dah! Hizi picha zinasikitisha na uko sahihi, yaani utadhani ni kitu cha kufikirika tu. Ili uwe mtumwa wa mtu lazima akutawale kifikra, ili akutawale kifikra lazima eidha awe na 'akili' zaidi yako au uwe kimeo zaidi yake. Sasa kwa hawa watumwa ni kwamba walikuwa vimeo na hao mabosi wao walikuwa na 'akili' zaidi yao. Mabubu yetu ya Afrika weusi ilikuwaga mijinga sana.
 

Usiwasingizie wakoloni, biashara ya utumwa Afrika haikuanzia kwa wakoloni. Hivi umeshasoma kuhusu Ma chief waliokuwa na watumwa hapa hapa Afrika au bahati mbaya kwenye kiwango hicho hukufika?

Jee, hujasoma kuhusu ma Pyramid ambayo yapo Afrika yalijengwa na akina nani?

Jee, hujasoma kwenye vitbu vya dini kuwa hata Mtume Yusuf (Josef son of Jacob in the Bible) kuwa alikuchukuliwa utumwa Misr, ambayo ni Afrika?

Utakuta utumwa haukuanzia kwa mkoloni ulikuwepo hata hapa kwetu karne na karne kabla ya kutawaliwa na wageni.

Nnachokisema ni hiki, tatizo si biashara ya utumwa aliifanya nani au kwanini, ukianza kutafuta hayo utajikuta hata babu yako aliuza watumwa kwani kama hakuuza watumwa basi na wewe kwanini saa hizi usiwepo utumwani? Tatizo ni pale Waafrika tunapobaki na kukubali kuwa historia yetu imeanzia na kuishia utumwani, kutawaliwa na uhuru. La hasha, tuna historia kubwa na ndefu zaidi ya hiyo, tufunguke kuutafuta ukweli.

Walioiandika hii historia tunayojifunza hadi hii leo walikuwa na malengo yao, na malengo yao ni kuwafanya watu weusi kuwa ni duni daima milele. Mfano mzuri ni pale wanapomchora "Mungu" humfanya mweupe na ni mzungu na pale wanapomchora shetani humfanya mweusi. Hata malaika basi hakuna mweusi!

Fikiri.
 
naomba unitajie tafadhali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…