#COVID19 UVCCM: CCM imchukulie hatua Askofu Gwajima kwa kuhamasisha Watanzania kukataa chanjo ya Uviko-19
Askofu Rashid Gwajima ameishika CCM na Serikali yake pabaya wamebakia kubweka bweka tu lakini hawana cha kumfanya. Gwajima ana'watu'.
 

NUKUU ZA KATIBU MKUU WA UMOJA WA VIJANA WA CCM (UVCCM) NDUGU. KENANI LABAN KIHONGOSI AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI LEO 27/07/2021

"Tunapenda kumpongeza Mhe Rais Samia Suluhu Hassan na Mwenyekiti wa Chama chetu Kwa namna ambavyo ameendelea Kufanya Kazi bila kuchoka na kuendelea kulinda Amani ya Nchi yetu, na sisi Vijana tupo pamoja naye kuhakikisha adhma ya serikali ya Awamu ya 6 inaenda kutimia"...

2710220_1615278746701.png
 
Nadhani kama kweli katiba ya sasa inapigia chapuo uhuru wa maoni na kusikilizwa Gwajima ametumia haki yake kabisa. Na alikuwa ndani ya kanisa lake madhabahuni. Waliomchukua video na kusambaza ndio wazandiki.

Ccm hapa wanaigiza kama wanavyoigiza mengine mengi ya ugaidi, kamati za tozo, kamati ya chanjo yote maigizo, Tunajenga barabara. Hakuna dalili ya kulinda pesa zinazokusanywa na zitakazokusanywa kuna kila dalili ya upigaji na uwajibikaji imetoweka kabisa toka JPM katwaliwa na mola.

Na gwajima wote hata mwendazake alikuwa anamgwaya simply yuko well estblished kupitia imani yake, fitina anazijua, na ni sukuma original ni kariba mungu amempa. Na atawasumbua kama ilivyokua mtikila wakfanikiwa kumtoa ataanzisha hoja ya mgombea binafsi na ana ushawishi sana ndani ya imani ya pentecostal or revival churches hapa tanzania. Huyu aliwahi mpaka kumchamba Kardinal Pengo on public church session. Hili lijitu liko very bold n sio muoga
 
Dodoma. Umoja wa Vijana wa CCM ( UVCCM) umekitaka chama chao kumchukulia hatua Mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima kwa kitendo chake cha kuhamasisha watanzania wakatae chanjo ya Uviko-19...
Ila Ma CCM ni Manafiki Jaman sijawahi kuona, kutoka kutukana watu wanaovaa Barakoa Mpaka na menyewe kuanza kuvaa
CCM naamini hata wakiwekewa Taahira pale Juu atawageuzageuza atakavyo
 
Alikua anaongea KANISANI KWAKE SHIDA IKO WAPI ndio madhara ya kuweka VIJANA WAJINGA uvccm
 
Manufaa ya kugawa ubunge hadi kwa mitume na manabii. Hao wanaishi kwa Neno: Mathayo 4:4.

Itikadi, sera, mipango, ukada, protokali za chama, caucus ya wabunge, n.k., hayo ni mambo ya ulimwengu huu; yatatoweka. Kazi kwenu, mtimueni kabla hajawageuza misukule kisha kuwafufua upya!
 
Aliongelea jimboni au kanisani?

Tusichanganye dini na siasa!
Mkuu, zote kazi zake. Anaweza kuzipiga mix bila kero. Ni kama kemia na siasa, tiba mbadala na siasa, muziki na siasa; tumeshazoea kumixiwa.
 
MATAGA hili swala la gwajima msilifanye agenda kiufupi ujinga ni wakati wa kwenda kurudi kila mtu anaijua njia kwa kifupi hatuchanji
 
MH.GWAJIMA NA TUHUMA NZITO MNO......

Ukimsikiliza vyema katika ile CLIP yake kuna sehemu amerudia mara mbili kumtaja Hayati JPM...."kuwa ni kwanini Sasa chanjo ije baada ya JPM kuaga dunia....alipoaga dunia tu,chanjo zimekuja"...
Hivi nyie si ndo mlikuwa mnasema hakuna corona enzi za mwendazake leo imekuaje
JamiiForums-1797793390.jpg
 
Legacy isiyoyumba ya mwendazake ni pamoja na hiyo ya kukataa chanjo ambayo Gwajima anailinda na kuitetea.
MH.GWAJIMA NA TUHUMA NZITO MNO......

Ukimsikiliza vyema katika ile CLIP yake kuna sehemu amerudia mara mbili kumtaja Hayati JPM...."kuwa ni kwanini Sasa chanjo ije baada ya JPM kuaga dunia....alipoaga dunia tu,chanjo zimekuja".....

Kauli hii ni ya hovyo kupindukia.....

Anataka AMCHAFUE RAIS SSH kwa "kumdogosha na kumfanya mwepesi kiuongozi" kwa kuwa HAYATI JPM ameacha LEGACY ya misimamo ISIYOYUMBA.....

MANENO HAYA NI MANENO MABOVU MNO KUTOLEWA NA MBUNGE TU DHIDI YA AMIRI JESHI WA MAJESHI YA ULINZI NA USALAMA

#GwajimaAfukuzweCCM
#KaziIendelee
#TujiandaeKuchanjwa
#JMTMilele
 
Pumbavu zenu mlivosema tupige nyungu korona itaondoka yenyewe..hamna msimamo nyie
 
Habari!

Niliandika uzi kuwa mbunge wa Kawe ana nia ya kugombea Urais 2025. Na kwa mujibu wa mifumo ya CCM 2025 ni zamu yako tena Mh. Samia Suluhu kugombea Urais.

Huyu Gwajima mtu mwenye nguvu na mjanja sana, kavipiga vita vingi na kushinda. Usipojifunga kiume umdhibiti mapema huyu Askofu Gwajima atakuharibia njia na kukimegamega chama chenu nasi wapinzani tutashangilia maana huwenda tukapata mpenyo.
 
Mshauri na njia ya kutumia ili kumdhibiti.

Binadamu tunaishi kisharishari tu, yaani kila kitu tunawaza kukomoana na kushindana kila wakati.

Matokeo yake watu kunyanyaswa bila sababu na kupoteza future za watu huku familia na watu wengine kuumia zaidi.

Hii ndiyo maana Tanzania hatuendelei kabisa.

Ubinafsi mwingi usio na wala sababu za msingi.
 
Back
Top Bottom