UVCCM wagonjwa hawahitaji picha ya Rais, acheni hizi propaganda

UVCCM wagonjwa hawahitaji picha ya Rais, acheni hizi propaganda

Nchi ngumu sana hii... Kwamba picha ya rais ndo inafanyaje Kwa wagonjwa sasa?
 
Jana nilikuwa naongea na jirani zangu wana ccm wa kutegemewa na chama chao.

Lkn kwa sasa wanasema kabisa kuwa wapo tayari kukipigia kura chama cha upinzani kuliko kuipigia ccm kura kisa Hangaya.
Waongo hao.
WanaCCM wote wanaishi kwa CCM kuwa madarakani.
CCM ikitoka madarakani watakufa njaa hao, na hill wanalijua.
Wanajua hasira walizo nazo wananchi juu yao. Hivyo wapo tayari hata jina liwepo tu, kulinda usalama wao.
 
UVCCM na BAVICHA ni aibu za taifa. Kuna mwaka UVCCM walitaka kufanya maandamano ya kupongeza hotuba ya Rais Kikwete. Wakati huohuo kipindi Kikwete anakaribia kumaliza awamu yake aliwatimua kwenye event ambayo ilikuwa na ulazima wao kuwepo. Yaani Kikwete alishtuka majitu haya hapa na mavazi ya kijani kwenye shughuli isiyohitaji hayo mambo, akawaambia waondoke. Matukio ya UVCCM yenye kutia hasira ni mengi. BAVICHA wao tatizo lao ni kukabidhi akili zao zote kwa Sultani Mbowe. Walichobaki nacho ni matusi tu.
 
Jana nilikuwa naongea na jirani zangu wana ccm wa kutegemewa na chama chao.

Lkn kwa sasa wanasema kabisa kuwa wapo tayari kukipigia kura chama cha upinzani kuliko kuipigia ccm kura kisa Hangaya.
Jirani yako ana kura moja tuu, [emoji1] na anakupima tuu hapo uchaguzi ukifika CCM huwa inakuwa na ajenda moja tuu ya USHINDI.
 
UVCCM na BAVICHA ni aibu za taifa. Kuna mwaka UVCCM walitaka kufanya maandamano ya kupongeza hotuba ya Rais Kikwete. Wakati huohuo kipindi Kikwete anakaribia kumaliza awamu yake aliwatimua kwenye event ambayo ilikuwa na ulazima wao kuwepo. Yaani Kikwete alishtuka majitu haya hapa na mavazi ya kijani kwenye shughuli isiyohitaji hayo mambo, akawaambia waondoke. Matukio ya UVCCM yenye kutia hasira ni mengi. BAVICHA wao tatizo lao ni kukabidhi akili zao zote kwa Sultani Mbowe. Walichobaki nacho ni matusi tu.
Hata hivyo,BAVICHA hawapalilii teuzi serikakini!
 
Unaweza kusema umeona kila hadi sasa, Ila ukweli ni kuwa vingi bado hujaviona na pengine ndio mwanzo wa kuviona.

Vijana wa CCM wamepita kwenye hospital na fremu ya picha ya Rais wakiwaonyesha wagonjwa.

Sasa hapa unajiuliza Hawa wagonjwa wakiona picha wanapona au? Lakini ni kwamba hao wagonjwa hawamjui Raisi Mama Samia?

Ni vitu vyakushangaza sana, nchi yetu hii ina vijana wa hivi je kesho tutatoa akina Elon Musk wetu?

Rais anapaswa kukataa hizi mambo maana hazina faifa yoyote kwa wananchi na huenda wanaofanya hivi hawana mapenzi nae bali ni namna tu ya kujipendekeza.

Au tupo kwenye kampeni za uchaguzi mkuu?

Walking and sleeping at the same time.
 
1643726107569.png
 
CCM haitegemei kura.
Vyombo vya dola vina tumika.
Nyie mna washabiki na CCM ina wafuasi, nilifanya utafiti mdogo 28 October 2020, wale waliokuwa wanamshabikia TAL sikuwaona kituoni licha ya kuwahimiza twende tukapige kura, matokeo yakitoka mnalalamika.
 
Jirani yako ana kura moja tuu, [emoji1] na anakupima tuu hapo uchaguzi ukifika CCM huwa inakuwa na ajenda moja tuu ya USHINDI.
Kwa Avatar yako sioni sababu ya kujichosha na wewe
 
Waongo hao.
WanaCCM wote wanaishi kwa CCM kuwa madarakani.
CCM ikitoka madarakani watakufa njaa hao, na hill wanalijua.
Wanajua hasira walizo nazo wananchi juu yao. Hivyo wapo tayari hata jina liwepo tu, kulinda usalama wao.
Sasa hapo walikuwa wananiongopea mimi au walikuwa wanaziongopea nafsi zao?
 
Nyie mna washabiki na CCM ina wafuasi, nilifanya utafiti mdogo 28 October 2020, wale waliokuwa wanamshabikia TAL sikuwaona kituoni licha ya kuwahimiza twende tukapige kura, matokeo yakitoka mnalalamika.
Katiba mpya ndio jibu
 
Back
Top Bottom