Uwezo wa kuongea na wafu: Elimu Iliyoshindikana duniani

Uwezo wa kuongea na wafu: Elimu Iliyoshindikana duniani

Kuna tofauti ya roho na nafsi? nilijua ni kitu kimoja...., hizo habari za marehemu kukataa au kutii kuvaa ni porojo..., peleka sokoni

Usikimbilie kupost kuwa na kituo fuata mtiririko wa habari nzima ili uje na hoja yenye mashiko
 
Iko hivi sikuwa anakataa live bali wakati wa kumvisha kama ni koti shati au hata suruali kuna kiungo kimoja hukakamaa kwa mfano kama ni mkono haunyanyuki au haukunjiki, kama ni mguu unajipinda au unakuwa mzito kunyanyua
Hivi vitu vinafanyika kwa namna ya ajabu na ya kipekee kabisa

Vilevile kuna kukosea vifungo au zipu kujichanganya! Yani mnaanza kufunga kifungo cha kwanza vizuri kabisa mkifika mwisho aidha vimepishana au mmeruka matundu, tulishawahi kukosea vifungo Mara SABA
Ni mpaka nilipotumia elimu niliyojifunza kuongea na marehemu kwa upole na kwa kumbembeleza ndio mambo yakawa sawa, na pia ndani ya chumba husika kama yupo mtu alikuwa na ugomvi na marehemu hakuna kitakachokwenda sawa hapo mpaka yule mtu atoke

Mi niliwahi kumuona mmoja mtu wa KIGOMA sasa alishaeleza akifariki akazikwe kigoma, watoto baada ya baba yao kufa wakaandaa mazishi Dar..basi maiti alikuwa anapimwa vizuri, mkitengeneza Jeneza anaongezeka inabidi kurudi kwa fundi mwisho wakubwa wakasema tusilazimishe marehemu alishakataa kuzikwa Dar
 
Hiyo sio tafsiri yake na hapa unazungumzia neno wakati mimi nazungumzia nilichokutana nacho katika uhalisia wake
Kama ulizungumza na maiti ujue uliongea na kitu kingine sio marehemu. Shetani huyo aisee.
 
Itakuwa poa sana, nita ku Pm halafu twende utagundua ulicho kiandika hakipo.

Nilichokiandika kipo kwakuwa kilinihusu mimi mwenyewe binafsi na si maramoja rafiki, kule naenda kukuonyesha kingine kabisa
 
Iko hivi sikuwa anakataa live bali wakati wa kumvisha kama ni koti shati au hata suruali kuna kiungo kimoja hukakamaa kwa mfano kama ni mkono haunyanyuki au haukunjiki, kama ni mguu unajipinda au unakuwa mzito kunyanyua
Hivi vitu vinafanyika kwa namna ya ajabu na ya kipekee kabisa

Vilevile kuna kukosea vifungo au zipu kujichanganya! Yani mnaanza kufunga kifungo cha kwanza vizuri kabisa mkifika mwisho aidha vimepishana au mmeruka matundu, tulishawahi kukosea vifungo Mara SABA
Ni mpaka nilipotumia elimu niliyojifunza kuongea na marehemu kwa upole na kwa kumbembeleza ndio mambo yakawa sawa, na pia ndani ya chumba husika kama yupo mtu alikuwa na ugomvi na marehemu hakuna kitakachokwenda sawa hapo mpaka yule mtu atoke


We jamaa ni muongo kuliko hata CCM
 
We jamaa ni muongo kuliko hata CCM
Njaa hoja hujibiwa kwa hoja, kukimbilia tu kutoa conclusion ya uongo bila hoja ni uvivu wa kufikiri au kukwepa ukweli
Hapa kuna vitu vitatu, uhalisia wa nilichoandika, ukweli wa maneno yangu na Kongo uliouona katika post yangu
Labda tu nikwambie kwa upole kwamba hapa si jukwaa la siasa wala mapenzi, hapa kilichopo kipo na kitakuwepo, nimeandika uhalisi wa kile kilichotokea si mara moja au mbili sasa suala la kuamini au kutoamini sio jukumu langu, huo utakuwa mtazamo wako

Haya mambo ni ngumu sana kuwa na ithibati za kisayansi ndio maana wengi wetu tusiopenda kufikirisha bongo zetu, na kufikiri zaidi ya kufikiri huku tukiutazama ulimwengu kwa namna nyingine isiyozoeleka na wengi huja na maneno kama haya ya kwako
Njaa hii dunia ni zaidi ya unavyoiona na kuisoma kwenye zile elimu za kawaida mashuleni, kuna zaidi ya hapo kuna ulimwenguni mwingine kabisa ambao hufanya kazi kwa namna ya tofauti kabisa na ni ulimwengu huo unaofanya maisha yasonge,sio huu ulimwengu wa 1+1=2 THINK BIG rafiki soma elimu ya utambuzi utaona dunia katika mwanga tofauti
 
Last edited by a moderator:
Hili somo linahitaji utulivu wa hali ya juu, asilimia kubwa kwenye umma kama hivi hawatakubaliana na wewe au kukuelewa kiurahisi.
 
Hili somo linahitaji utulivu wa hali ya juu, asilimia kubwa kwenye umma kama hivi hawatakubaliana na wewe au kukuelewa kiurahisi.

Nafikiri shida kubwa ni hizi elimu tulizoletewa toka nje na kutufundisha kuwa chao ni bora na chetu ni upuuzi mtupu, tumekuwa brainwashed vibaya sana na hii kitu

Kuna mtu anacoment hapa unaona kabisa huyu ni tatizo la umri, kazaliwa ocean rd(wenyewe wanaona sifa) kasomea bunge na kazini posta ambako hana hata miaka 10,

Kuna wengine wametekwa kabisa na dini ukimwambia lolote nje ya hapo atakurukia tu na majibu rahisi, tena saa nyingine na kejeli, bila kufahamu kuwa hata hicho anachoamini hakijui vema na kwamba kimezungumzia jambo husika tena kwa mapana
 
Nilitegemea ungetoa ufafanuzi zaidi juu ya maswali niliuliza hapo. Sjui ni ujuaji au umbumbumbu tu!!!! Anyway, How could you know babu yangu alikuwa na hizo mila?

hata ukifafanuliwa hutaelewa, wengi wenu ni walemavu wa fikra, how could you know babu yako HAkuwa na hizo mila?
 
someni 1 samwel 28:7

7 Ndipo Sauli akawaambia watumishi wake, Nitafutieni mwanamke mwenye pepo wa utambuzi, nipate kumwendea na kuuliza kwake. Watumishi wake wakamwambia, Tazama, yuko mwanamke mwenye pepo wa utambuzi huko Endori.
8 Basi Sauli akajigeuza, na kuvaa mavazi mengine, kisha akaenda, yeye na watu wawili pamoja naye, wakamfikilia yule mwanamke usiku; akasema, Tafadhali unibashirie kwa utambuzi, ukanipandishie yeye nitakayemtaja kwako.
9 Yule mwanamke akamwambia, Angalia, unajua alivyofanya Sauli, jinsi alivyowakatilia mbali hao wenye pepo wa utambuzi na wachawi katika nchi; mbona basi wanitegea tanzi uhai wangu, ili kuniua?
10 Naye Sauli akamwapia kwa Bwana, akasema, Aishivyo Bwana, haitakupata adhabu yo yote kwa jambo hili.
11 Ndipo yule mwanamke aliposema, Je! Ni nani nitakayekupandishia? Naye akasema, Nipandishie Samweli.
12 Hata yule mwanamke alipomwona Samweli alilia kwa sauti kuu; na yule mwanamke akamwambia Sauli, akasema, Mbona umenidanganya? Kwa kuwa wewe ndiwe Sauli.
13 Mfalme akamwambia Usiogope; waona nini? Yule mwanamke akamwambia Sauli, Naona mungu anatoka katika nchi.
14 Naye akamwuliza, Ni mfano wa nini? Akajibu, Ni mzee anazuka; naye amefunikwa vazi. Basi Sauli akatambua ya kwamba ndiye Samweli mwenyewe, akainama uso wake mpaka nchi, akasujudia.
15 Ndipo Samweli akamwambia Sauli, Mbona umenitaabisha mimi, hata kunipandisha juu? Sauli akajibu, Mimi nimetaabika sana; kwa kuwa hao Wafilisti wananifanyia vita, naye Mungu ameniacha; hanijibu tena, wala kwa manabii, wala kwa ndoto; kwa hiyo nimekuita wewe, ili wewe unijulishe nifanyeje.
16 Samweli akasema, Kwa nini kuniuliza mimi, akiwa Bwana amekuacha, naye amekuwa adui yako?
17 Yeye Bwana amekutendea kama alivyosema kwa kinywa changu; Bwana amekurarulia ufalme mkononi mwako, na kumpa jirani yako, yaani, Daudi.
18 Kwa sababu wewe hukuitii sauti ya Bwana, wala hukumtimilizia hasira yake kali juu ya Amaleki; kwa sababu hii Bwana amekutendea hili leo.
19 Tena pamoja na wewe Bwana atawatia Israeli mikononi mwa Wafilisti; hata na kesho wewe na wanao mtakuwapo pamoja nami; tena Bwana atawatia jeshi la Israeli pia mikononi mwa Wafilisti.
20 Mara Sauli akaanguka chini kifulifuli, akaingiwa na hofu kuu kwa sababu ya maneno hayo ya Samweli, wala hakuwa na nguvu yo yote; kwa maana hakula chakula mchana kutwa, wala usiku kucha.
 
hata ukifafanuliwa hutaelewa, wengi wenu ni walemavu wa fikra, how could you know babu yako HAkuwa na hizo mila?
images
 
Back
Top Bottom