Uzi maalum kwa wale wanaopinga uwepo wa Mungu

Uzi maalum kwa wale wanaopinga uwepo wa Mungu

Huwezi kukataa elimu yenye uthibitisho na inayothibitishika mafundisho yake kwa kuleta uvumbuzi wa shida mbalimbali

Yani ni sawa unataka kuwaambia madaktari wakatae elimu ya kutibu magonjwa kwa vile ni elimu kutoka kwa mzungu.

Au watu wakatae kutumia simu kwa vile ni elimu kutoka mzungu.

Kuna elimu za ukweli na zenye uthibitisho wa matokeo chanya ya mafundisho yake hizo niza kukubaliwa.

Pia kuna elimu za uongo ikiwemo habari za uwepo wa Mungu zisizo na uthibitisho wowote ule zaidi ya hadithi tu, Hizi ni kuzikataa.

Maana hata asilimia kubwa ya wazungu ni Atheists, Hawa amini uwepo wa huyo Mungu.
Kwaiyo siku huyo aliekuletea elimu ya science akianza kuikataa na akakufundisha nawewe utamkubali?
 
Kabla sijaenda kuonesha ni kwa nini naamini Mungu yupo ushaelewa maana ya neno IMAN na misingi ya imani?
Misingi hiyo ya imani imejengwa katika uongo kwa sababu vitu vyote vya kuona, kusikia na kutenda vinafanyika na viungo vya binadamu.

Macho huona, masikio husikia, ubongo huamua na kisha mwili kwa ujumla hutenda.

Hivyo definition yako ya imani ni definition UCHWARA.

Definition yako ni ya MCHONGO.
 
Misingi hiyo ya imani imejengwa katika uongo kwa sababu vitu vyote vya kuona, kusikia na kutenda vinafanyika na viungo vya binadamu.

Macho huona, masikio husikia, ubongo huamua na kisha mwili kwa ujumla hutenda.

Hivyo definition yako ya imani ni definition UCHWARA.

Definition yako ni ya MCHONGO.
Kwaiyo tuseme neno IMANI halipo au lisitumike mfano tusiseme "naamini mtoa mada amepata muongozo"

Hilo neno IMANI lisiwepo maana halina msingi wowote au halina faida
 
we jamaa mbona unarudia swali ni kua huelewi au ni nini, ksoma bandiko upya,

"soma kwa hatua"
Nilisha kufafanulia kwamba akili ya binadamu haipo limited.

Hiyo limit unayo idai ipo ni uongo kwa sababu binadamu hufanya tafiti, uchunguzi na udadisi wa kuvumbua vitu asivyo vijua

Hivyo binadamu kutokujua kitu fulani si kwamba akili yake ipo limited bali ni kwamba bado utafiti na uchunguzi wa kujua kitu hicho hajaufanya hadi kufikia kupata jibu.
 
Nilisha kufafanulia kwamba akili ya binadamu haipo limited.

Hiyo limit unayo idai ipo ni uongo kwa sababu binadamu hufanya tafiti, uchunguzi na udadisi wa kuvumbua vitu asivyo vijua

Hivyo binadamu kutokujua kitu fulani si kwamba akili yake ipo limited bali ni kwamba bado utafiti na uchunguzi wa kujua kitu hicho hajaufanya hadi kufikia kupata jibu.
mambo mangapi yanafanyiwa utafiti na hamna jibu ?
 
Kwaiyo tuseme neno IMANI halipo au lisitumike mfano tusiseme "naamini mtoa mada amepata muongozo"

Hilo neno IMANI lisiwepo maana halina msingi wowote au halina faida
Nilikwambia kwamba, Imani ni kutokuwa na uhakika.

Ndio maana unasema "Naamini mtoa mada amepata muongozo" kwamba huna uhakika kwa asilimia mia kwamba mtoa mada amepata muongozo ila una amini tu, kwamba mtoa mada atakuwa amepata muongozo.

Ungekuwa na uhakika kwa asilimia mia kwamba mtoa mada amepata muongozo, Ungesema
"Najua mtoa mada amepata muongozo"

Na uhakika utakuwa nao kwa vile tayari unajua kwa uhakika zaidi.

Na si kwa imani tena.
 
mambo mangapi yanafanyiwa utafiti na hamna jibu ?
Mambo hayo kukosa majibu si hitimisho(conclusion) ya kusema kwamba majibu hayapo kamwe.

Tafiti nyingi zilishindwa sana mpaka pale majaribio mengi zaidi na zaidi yalipo endelea kufanyika ndipo majibu yakapatikana.

Mfano, waliojaribu kwenda mwezini walirusha vyomba vingi sana angani bila mafanikio lakini mwishowe walifanikiwa kufika mwezini kwa kuendelea kufanya tafiti zaidi na zaidi.

Hivyo jambo fulani kukosa jibu si hitimisho la moja kwa moja kwamba jambo hilo halina jibu na halitakaa lipate jibu.
 
Ukipinga uwepo wa Mungu au shetani inabidi usiamini katika dhana ya ubaya wa jambo lolote au uzuri wa jambo lolote kwa sababu kama uwepo wa Mungu na shetani ni myth basi kudhani jambo fulani ni baya au zuri ni myth, kudhani kwamba ukiua mtu ni jambo baya hiyo ni upotofu maana sababu inayotufanya tusiuane na kama nikileta sababu zangu za kuua inabidi zikubaliwe na ukipinga hizo ni shida zako sio zangu kwa kuwa siamini kama kuua ni jambo baya regardless sababu au bila sababu
This logical fallacy is called non sequitur.

Kitu cha kwanza inachotakiwa kufanya ni kuthibitisha Mungu yupo.

Kabla ya kusema Mungu kaumba hiki au Mungu kaleta hiki, thibitisha Mungu yupo kwanza.
 
Mambo hayo kukosa majibu si hitimisho(conclusion) ya kusema kwamba majibu hayapo kamwe.

Tafiti nyingi zilishindwa sana mpaka pale majaribio mengi zaidi na zaidi yalipo endelea kufanyika ndipo majibu yakapatikana.

Mfano, waliojaribu kwenda mwezini walirusha vyomba vingi sana angani bila mafanikio lakini mwishowe walifanikiwa kufika mwezini kwa kuendelea kufanya tafiti zaidi na zaidi.

Hivyo jambo fulani kukosa jibu si hitimisho la moja kwa moja kwamba jambo hilo halina jibu na halitakaa lipate jibu.
je kuhusu uwepo wa Mungu mbona wewe umeshaweka conclusion kwamba hayupo,

wakati sanansi yenyewe haina majibu na hai conclude kua hayupo
 
This logical fallacy is called non sequitur.

Kitu cha kwanza inachotakiwa kufanya ni kuthibitisha Mungu yupo.

Kabla ya kusema Mungu kaumba hiki au Mungu kaleta hiki, thibitisha Mungu yupo kwanza.
mfano umekuta nyumba imejengwa, lakini hujawakuta mafundi hapo au umekuta tu vifaa vyao wenyewe hawapo

hauta tumia uwepo wa vifaa walivyoacha au jengo walilojenga, kuthibitisha kua mafundi wapo arround ?
 
je kuhusu uwepo wa Mungu mbona wewe umeshaweka conclusion kwamba hayupo,
Kwa sababu mimi sidai kwamba Mungu yupo.

Mnaodai Mungu yupo ni ninyi na inabidi mthibitishe madai yenu.
wakati sanansi yenyewe haina majibu na hai conclude kua hayupo
Sayansi haisemi Mungu yupo.

Sayansi ina kanusha madai yenu ninyi mnaosema Mungu yupo halafu hamna uthibitisho.

Sayansi inasema Mungu hayupo kwa vile hakuna uthibitisho wowote ule wa uwepo wa Mungu huyo.

Hivyo ukiweza kuthibitisha Mungu yupo utai prove wrong sayansi kwa kusema Mungu hayupo.

Na sayansi ita conclude Mungu yupo kutokana na uthibitisho wako.

Lakini cha ajabu ni kwamba mpaka sasa mmeshindwa kuithibitishia sayansi kwamba Mungu yupo.

Ila mnafosi imani zenu uchwara ziwe ukweli bila kuleta uthibitisho.
 
Kwa sababu mimi sidai kwamba Mungu yupo.

Mnaodai Mungu yupo ni ninyi na inabidi mthibitishe madai yenu.

Sayansi haisemi Mungu yupo.

Sayansi ina kanusha madai yenu ninyi mnaosema Mungu yupo halafu hamna uthibitisho.

Sayansi inasema Mungu hayupo kwa vile hakuna uthibitisho wowote ule wa uwepo wa Mungu huyo.

Hivyo ukiweza kuthibitisha Mungu yupo utai prove wrong sayansi kwa kusema Mungu hayupo.

Na sayansi ita conclude Mungu yupo kutokana na uthibitisho wako.

Lakini cha ajabu ni kwamba mpaka sasa mmeshindwa kuithibitishia sayansi kwamba Mungu yupo.

Ila mnafosi imani zenu uchwara ziwe ukweli bila kuleta uthibitisho.
wewe mwenyewe umetoka kusema kwamba sayansi ikishindwa ku prove kitu saivi sio kwamba hakipo, inawezekawa ikafanikiwa kuprove baadae,

kwa mantiki hiyo, uta conclude vipi Mungu hayupo kwasababu Sayansi imeshindwa ku prove Yupo ?
 
mfano umekuta nyumba imejengwa, lakini hujawakuta mafundi hapo au umekuta tu vifaa vyao wenyewe hawapo

hauta tumia uwepo wa vifaa walivyoacha au jengo walilojenga, kuthibitisha kua mafundi wapo arround ?
Ukiuchukua mfano huu, ukasema kwamba kilicho complex hakiwezi kuwapo bila kuumbwa, kimantiki, unaweza kukubali kuwa nyumba haiwezi kuwepo bila kujengwa na mtu.

Na unaweza hata kukubali kuwa mtu hawezi kuwepo bila kuumbwa na Mungu.

Na mantiki hiyo hiyo itakutaka ukubali kwamba Mungu hawezi kuwapo bila kuumbwa na yeye, na aliyemuumba naye kaumbwa, hivyo hivyo, bila mwisho.

Katika ulimwengu huo, hakuna Mungu.

Umeitoa hoja yako kama uthibitisho kuwa Mungu ni lazima awepo.

Lakini, ukiiangalia kwa undani hiyo hoja, kiukweli inaonesha Mungu hayupo na hawezi kuwepo.
 
Sitatumia maandiko ya Dini Quran wala Bible, labda wataelewa kidogo, maana humu JF nimegundua wapo wengi, unaweza ukajikuta una chati hata na shetani directly, anapotosha

Tuanzie kwenye Civilization na Level ya akili na kufikiri viumbe mbalimbali wapo kwenye level tofauti za civilization na akili. Inaweza kuonekana kupitia namna yao ya maisha.

Mfano Simba wana territory yao wanaweka alama kabisa iwe kuacha kinyesi n.k ila wana mipaka ya utawala na kuna utawala wa simba dume eneo hilo ambapo akiingiliwa na Simba mwingine ambae hakua hapo lazima wapigane vibaya sana hadi moja akubali show.

Tembo pia vilevile kiasi kwamba mwenzao akifa wanahizunika na kuonyesha kuomboleza...

Mchwa pia, wapo wana utawala wao, wana malkia, kuna walinzi kuna wajenzi, na wanajenga haswa, kichuguu kimejengwa kwa ustadi haswa inaonyesha kabisa wana mawasiliano mazuri sana na wanajua wanachokifanya.

Nyuki pia vile vile, wana jenga nyumba yao, sehemu ya kuwekea asali, kuna malkia, kuna wanaolinda eneo, nknk.

Yaani hadi wanavyotengeneza asali kumlinda malkia na kulinda eneo lao, lina onyesha wazi level yao ya kujielewa na level ya mawasiliano ni kubwa kabisa.

wanyama ni wengi ambao tunaweza kuwa tumia kama reference, Sokwe etc.

Hawa viumbe wote, kila mmoja kwa nafasi yake mfano tuchukulie nyuki, wanajiona wana akili(ni kweli wanayo),
wanajiona wanajua mambo mengi na kufikiri logically kwamba huyu ametuchokoza kwaiyo tuji-oganize kushambulia na kujilinda, wanajua kujenga, wanamuheshimu malkia na kumlinda...

ila pia kuna mambo hawajui na hawajui kama hawajui na hawawezi kukuelewa hata ukijaribu kuwaelewesha,
na hautakua hata na intrest ya kuwaelewesha...

Mfano: Je binadamu anaweza kua na interest ya kutaka kumuonyesha nyuki ni jinsi gani binadamu wameendelea kiteknolojia?

Nyuki anaweza kuelewa kwamba binadamu anaweza kuongea na mtu wa marekani kupitia iternet kwamba binadamu anaweza kuwasiliana hivi Jamii Forums kwa id fulani na hawajawai kuonana wala kua na namba ya simu wala kukutana?

Nyuki anaweza kuelewa kwamba hilo bomba linalotoa maji au hiyo taa inayowaka usiku barabarani au nyumbani imetengenezwa na binadamu na sio kwamba ipo tuu... inakazi na bili zinalipwa?

Hayo ni baadhi ya maendeleo ya binadamu na kujaribi kulinganisha uwezo wa akili wa nyuki na binadamu,

Ni dhahiri kwamba hai make sense kwa nyuki, na hatuna interest ya kutaka kumuelewesha

Tumetofautiana kiakili na nyuki kiasi cha kua sisi tunaweza kumuelewa nyuki ila yeye hawezi kutuelewa

Nyuki nae usipo mlinganisha na binadamu, ana akili kubwa tuu na huenda anajiona vilevile binadamu anavyojiona kiakili, na anakiamini kile akili yake inachowaza kumbe ndo akili yake ilipoishia.

Vile vile kwa binadamu anajiona yupo advanced kiakili ambayo ni kweli pia kwa nafasi yake lakini pia na yeye ana limit ambayo akili yake inaishia.

Tunaona tu dunia, jua mwezi, maporomoko na vingine, ni kama tuu nyuki akikutana na taa, bomba la maji, kweli anaona taa inatoa mwanga, bomba linatoa maji...

Ila hajui hasa lile bomba imekuaje lipo pale, au taa imekuaje ipo pale, imewekwa na nani?

Anachojua inatoa mwanga, mechanism nyuma yake je inakuaje inawaka usiku mchana haiwaki? Inakazi gani haswa? Hajui na hana uwezo wa kufatilia kujua.

probably akiona gari anajua ni mojawapo ya viumbe wengine, hajui kama binadamu ndo yupo ndani anaendesha. au anaweza kua analichukulia kwa namna tofauti kabisa. au hata haelewi chochote.

Hiyo ni relation tu ya kuonyesha jinsi akili ya viumbe mbalimbali ina limit yake

Binadamu pia limit ya akili yetu ina limit inapoishia

Mfano ndo unakutana na Mtu anayesema "Mungu Hayupo kwasababu Huwezi kumuona wala kumgusa wala kusikia sauti yake"

Hiyo ni moja wapo ya limit ya akili yetu, ina depend moja kwa moja na milango ya fahamu, masikio macho, pua, ulimi, ngozi...

Anakwambia "jua lili kwepo tuu, na dunia ilikwepo tuu, kwamba kama jua au dunia haiwezekani kuwepo tuu, basi na Mungu hawezekani kuwepo"

Inaonyesha ni jinsi gani akili yetu inafikia limit, kuyaelewa mambo mengine..

Mambo ambayo hatuyajui bado ni mengi ni infinity ♾️, na ningumu hata kuingia akilini haya make sense kwasababu yapo beyond uwezo wa akili.

Kama vilevile tulivyoona kwa mfano wa nyuki, kwamba kumuelezea hata teknolojia yetu hai make sense, kwaajili ya limit yao ya akili.

Kwa ufupi wanakataa uwepo wa Mungu ambao wanauwezo mdogo sana wa kufikiri,hwafikirii katika uhalisia zaidi ya nadharia za walio watangulia.
 
wewe mwenyewe umetoka kusema kwamba sayansi ikishindwa ku prove kitu saivi sio kwamba hakipo, inawezekawa ikafanikiwa kuprove baadae,

kwa mantiki hiyo, uta conclude vipi Mungu hayupo kwasababu Sayansi imeshindwa ku prove Yupo ?
Kwa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, pingamizi si kwamba hajathibitishwa tu.

Pingamizi ni kwamba hoja ya kuwepo kwake ina internal contradiction.

Ni kama useme kuwa katika Euclidean geometry, pembetatu ina nyuzi 180 na duara lina nyuzi 360, halafu kuna pembetatu ambalo hapohapo ni duara.

Obviously pembetatu ambayo hapohapo ni duara haiwezekani kuwapo, kuwapo kwake kunashindikana kwa sababu sifa ya pembetatu, nyuzi 180, inapingana na sifa ya duara, nyuzi 360.

Unaelewa hilo jambo?
 
Back
Top Bottom