Uzi maalum kwa wale wanaopinga uwepo wa Mungu

Uzi maalum kwa wale wanaopinga uwepo wa Mungu

Kwa sababu hakuna aliyethibitisha uwepo wa Mungu.
Ila kisayansi, inawezekana ukajua umri wa kitu Fulani kwa vipimo, na njia maalumu kama CARBON 14. so vitu vyote ivi vimethibitishwa kisayansi
Unasubiri atokee wa kuthibishia.. unadhani ni kwanini awepo mtu wa kukuthibitishia uwepo wa Mungu.. jaribu kutafta haya mwenyewe.. kila tunacholishwa kina kuwa ni kwa benefit ya anaetulisha sio yetu.. dunia haipo hivyo unavyoitazama wewe
 
Matendo ya Mitume 17:24.,25.,26.,27.,28.,29.


24. Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo, yeye, kwa kuwa ni Bwana wa mbingu na nchi, hakai katika hekalu zilizojengwa kwa mikono;

25. wala hatumikiwi kwa mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji kitu cho chote; kwa maana ndiye anayewapa wote uzima na pumzi na vitu vyote.

26. Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao;

27. ili wamtafute Mungu, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu.

28. Kwa maana ndani yake yeye tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu. Kama vile mmoja wenu, mtunga mashairi alivyosema, Maana sisi sote tu wazao wake.

29. Basi, kwa kuwa sisi tu wazao wa Mungu, haitupasi kudhani ya kuwa Uungu ni mfano wa dhahabu au fedha au jiwe, vitu vilivyochongwa kwa ustadi na akili za wanadamu.



Mind you hapo Paulo alikuwa ameenda kwa wagiriki wenye shule zao mababa wa kisomo wakawa wameandika kwa Mungu asiyejulikana..
Hizi zote ni nadharia mkuu, ndo maana mna dini nyingi mara uhindu, uislamu, ukristo, ushinto .. we una uhakika kama dini Yako ndo ya kweli?
 
Ukishasema MUNGU inatosha kukueleza kwamba ni mwanzo na mwisho..



Yohana 1:1.,2.,3.,4.
1. Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.


2. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.

3. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.
Hizi ni stori tu kaka, kama hadithi ya sungura na fisi
 
Hizi zote ni nadharia mkuu, ndo maana mna dini nyingi mara uhindu, uislamu, ukristo, ushinto .. we una uhakika kama dini Yako ndo ya kweli?
Achana na mambo ya dini.. Tunazungumzia imani ya kwamba Mungu yupo nadhanj hata paulo ndo alichozungumzia hakuna mahali kwenye hizo mistari amesema dini..

Alafu ndio tuzungumze huyo Mungu unamuaminije
 
Kabla sijaanza kukuuliza, Umewahi kuhakiki kuchukua DNA ya bibadamu na nyani ili ujithibitishie wewe mwenyewe ?
Sijawahi sababu Mimi sio daktari, ila wenye taaluma yao wamepima DNA na wamefanya utafiti, na wamekubali, evolution theory ni uhalisia
 
Achana na mambo ya dini.. Tunazungumzia imani ya kwamba Mungu yupo nadhanj hata paulo ndo alichozungumzia hakuna mahali kwenye hizo mistari amesema dini..

Alafu ndio tuzungumze huyo Mungu unamuaminije
Huwezi kunipa stori kwamba Mungu yupo, na Mimi nikaiamini,
Naomba uthibitisho nione kweli Mungu yupo, usilete hadithi za kwenye biblia
 
Dini ni kusanyiko la watu wanakuwa na wanachoamini na taratibu zao katika kumuabudu Mungu.. Mungu hataki tuwe wanadani anatutaka tuwe kama alivyotukusudia.. hajatuumba tusumbuliwe na hali ya dunia hii hajatuumba tutawaliwe na dunia bali tuitawale..

Kitu ambacho hatukifanyi.. Anataka ufate kile anachokwambia ili uwe bora sio vinginevyo
Hizi zote ni nadharia mkuu, ndo maana mna dini nyingi mara uhindu, uislamu, ukristo, ushinto .. we una uhakika kama dini Yako ndo ya kweli?
 
Dini ni kusanyiko la watu wanakuwa na wanachoamini na taratibu zao katika kumuabudu Mungu.. Mungu hataki tuwe wanadani anatutaka tuwe kama alivyotukusudia.. hajatuumba tusumbuliwe na hali ya dunia hii hajatuumba tutawaliwe na dunia bali tuitawale..

Kitu ambacho hatukifanyi.. Anataka ufate kile anachokwambia ili uwe bora sio vinginevyo
Yote ayo umejuje, ushawah kukutana na Mungu, mkaongea, akakwambia hayo?
 
Huwezi kunipa stori kwamba Mungu yupo, na Mimi nikaiamini,
Naomba uthibitisho nione kweli Mungu yupo, usilete hadithi za kwenye biblia
Eeh! Mimi nimekupa story Mungu yupo.. nimekwambia uthibisho ni wewe basi niongeze na mimj na kila anaesoma.. kwasababu tupo hai tuna kitu ambacho sayansi haiwezi kutupa.. uhai.. sasa kama wewe haupo hai uniambie
 
A
Hawaamini uwepo wa Mungu kwasababu hawamuoni, ila wanaamini wana akili lakini hawazioni
Akili unaweza kuipima, hata hospital unaweza kuipima akili, sababu ni kitu ambacho kipo.
Ila Mungu hayupo, sababu hajawah kuonekana, kuskika Wala kujitokeza popote.
 
Yote ayo umejuje, ushawah kukutana na Mungu, mkaongea, akakwambia hayo?
Kwani unadhani Mungu anaongeaje.. au unadhani kwamba Mungu hawezi kuongea na wewe..

Kile kitu mnachokiita machale huo ni mfano wa Mungu anaongea na wewe.. na hata ukitaka bado atataka kujihusisha zaidi na maisha yako zaidi ya unavyowaza
 
Eeh! Mimi nimekupa story Mungu yupo.. nimekwambia uthibisho ni wewe basi niongeze na mimj na kila anaesoma.. kwasababu tupo hai tuna kitu ambacho sayansi haiwezi kutupa.. uhai.. sasa kama wewe haupo hai uniambie
Bado unaongea nadharia za kikristo ulizo fundishwa kanisan. Lakin hujathibitisha uwepo wa Mungu
 
Kwa sababu dunia haijaumbwa.

Dunia ipo tu, kwa sababu haijaumbwa.

Usicho elewa ni nini?

Na wewe toa sababu.

Onyesha ni wakati gani huyo Mungu aliumba Dunia?

Uni prove wrong kwamba dunia ilikuwepo tu.

Na unionyeshe kwa uthibitisho Mungu huyo alivyoumba dunia na kwamba dunia haikuwepo tu bali iliumbwa.

Uli elewa niliyokwambia mwanzo,

Sababu ni hii..👇

Kama kila kitu kilichopo lazima kiwe kimeumbwa Hata Muumbaji wa kila kitu lazima awe ameumbwa.

Na kama si lazima kila kitu kilichopo kiwe kimeumbwa, Hata Dunia haihitaji iwe imeumbwa.

Usicho elewa ni nini?

Au unakaza fuvu tu!!

Kwa nini unadhani si hali ya kawaida?

Kwani ni lazima isiwe hali ya kawaida?

Kwa nini hudhani ni hali ya kawaida?

Hiyo extraordinary power ndio Dunia yenyewe.

Labda wewe umeamua kuita na kuipachika hiyo Extraordinary power jina Mungu.
kumbe una amini kwenye uwepo wa extra-ordinary power,

Hongera !, sasa upo one step away kuja kwenye concept yetu sisi Theists !
 
Kwani unadhani Mungu anaongeaje.. au unadhani kwamba Mungu hawezi kuongea na wewe..

Kile kitu mnachokiita machale huo ni mfano wa Mungu anaongea na wewe.. na hata ukitaka bado atataka kujihusisha zaidi na maisha yako zaidi ya unavyowaza
Hizo ni fikra zako tu, wengine watasema wanaongea na Allah wengine Zeus wengine Warumbe, wengine Vishnu. Sasa Mungu gani ni WA kweli kati ya hao
 
Yote ayo umejuje, ushawah kukutana na Mungu, mkaongea, akakwambia hayo?
Nimejuaje?

Dini inafata namna au taratibu ni logic tu.. angalia waislamu wanataratibu zao katika kumuabudu Mungu, angalia walokole. Angali wakatoliki ni vikundi tofauti maslai tofauti ila mpango ni Mungu..
 
Kwa sababu hakuna aliyethibitisha uwepo wa Mungu.
Ila kisayansi, inawezekana ukajua umri wa kitu Fulani kwa vipimo, na njia maalumu kama CARBON 14. so vitu vyote ivi vimethibitishwa kisayansi
mkuu carbon 14 isotope sio accurate hata kidogo. Wanasayansi wanalitambua hili. Kuna sintofahamu nyingi kwenye kipimo cha carbon 14 isotope
 
Nimejuaje?

Dini inafata namna au taratibu ni logic tu.. angalia waislamu wanataratibu zao katika kumuabudu Mungu, angalia walokole. Angali wakatoliki ni vikundi tofauti maslai tofauti ila mpango ni Mungu..
Ndo nimekwambia unithibishie uwepo wa Mungu nimuone, umeshindwa
 
mkuu carbon 14 isotope sio accurate hata kidogo. Wanasayansi wanalitambua hili. Kuna sintofahamu nyingi kwenye kipimo cha carbon 14 isotope
Kwa asilimia mbili tu kati ya mia ndo inaweza ikawa sio accurate, napo n mara chache sana.
Lakini Kuna njia nyingine za kupima umri wa vtu kama vile RADIOMETRIC DATING METHOD.
 
Back
Top Bottom