Uzi maalumu kwaajili ya maombi ya Alfajiri

Asante Mungu muumba wa mbingu na nchi kwa siku mpya tena, tunashukulu kwa kutupatia nafasi nyingine ya kurekebisha njia zetu, tunaomba nguvu zako zikatulinde tukaimalize siku salama, kwa upendo wako ukatujalie mahitaji yetu, tunasema asante kwa kutupigania vita vyetu, tumeuona mkono wako na matendo yako bwana ni makuu mno, kwa uchache wa maneno yetu tunaomba wingi wa neema zako,.
amen
 
.
Amkeni katika maombi. Mstari wa kusimamia "jaribu halikuwapata ninyi isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu,ila Mungu ni mwaminifu ambaye hata waacha mjaribiwe kupita muwezavyo, lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea ili muweze kustahimili"
1 wakorintho 10:13.
Tukumbuke Bwana mwenyewe ametuagiza tuombe "usitutie majaribuni Bali utuokoe na yule muovu"
Nawakaribisha tuombe juu ya majaribu. Ubarikiwe
 
Habari za kwenu wapendwa
Mwanzo nilikuwa nafikiri tuwe na ratiba ya kufanya maombi nimetafakari sana naona jambo hili litatubana sana kama sasa tunaelekea kipindi Cha uchaguzi inatubidi Tuombee sana amani na utulivu uendelee kudumu
Sasa tukishakuwa na ratiba itatulazimu tufuate ratiba na sio mambo mengine
 
Nazani kwa sasa siku hizi mbili m Tuombee sana taifa letu amani,utulivu na mamlaka zote kwa ajili ya kipindi hichi ambacho tunaelekea kipindi uchaguzi Tuombee ulinzi wa taifa lote Mungu anapendezwa na maombi haya na huwa yanajibiwa kwa haraka
 
2 Nyakati 7:14
Ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekeza, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.


1 Timotheo 2:1-2
1. Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote

2. Kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, tuishi maisha ya amani na utulivu katika utauwa wote na ustahivu.
 
Bwana, tafadhali uwe kati yetu tunapokusanyika kama chombo chako kuinua nchi yetu na viongozi wetu. Tafadhali linda nchi yetu dhidi ya mgawanyiko unaotia changamoto uwezo wetu wa kuishi maisha yanayokupendeza. Tetea walio hatarini na wasio na sauti, na ulete haki kwa wale ambao wamedhulumiwa.

Mithali 14:34
Haki huinua taifa;
Bali dhambi ni aibu ya watu wo wote.
 
Kila ukiwa unasikia Allah ahkbaru asubuhi au muda wowote jua ni kauli inayomtukuza Mungu kuwa Mungu Mkubwa na iwe sauti ya kwanza kuisikia kila uanzapo siku mpya aameen
 
Amina Mungu wa upendo atatenda
 
Q
Waislam tuna sala 5 za faradhi (lazima) kila siku, maombi (dua) ndiyo usiseme.

Tokeni kizani Muingie kwenye Nuru.

Hiyo mnayoiita "zaburi" hamsemi kweli, siyo "zaburi" hiyo.

Kwanini hamsemi kweli?
 
Leo ni siku nyingine tunaendelea na maombi ya taifa Letu ili tuishi maisha ya amani na utulivu kipindi hichi ambacho tunaelekea kwenye uchaguzi
 
Amkeni katika maombi Leo, Maombi yenye majibu juu ya mahitaji yako,
Waebrania 4:16"Basi na tukaribie kiti Cha neema Kwa ujasiri ili tupewe rehema na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji"
Ndugu Asubuhi ya Leo tunaalikwa kwenye kiti Cha enzi Kwa Ujasiri basi twende Kwa imani tukiamini yupo baba ambaye anasikia maombi yetu. Tuendelee na maombi mwana wa Mungu.


Your browser is not able to play this audio.
 
Maombi ya kuombea taifa ni maombi yenye nguvu sana haya ni maombi yenye kufungua mlango wako wa mafanikio na utajiri

Ukiamka usiku usisahau kuombea sana mambo haya kila siku

Ombea amani na utulivu
Ombea viongozi Mungu awape afya njema na hekima ya kuongoza
Ombea watu wote wenye mamlaka wafanye kazi kwa kutoa haki
Ombea rasilimali zilizopo katika taifa hili zinufaishe watanzania wote kwa usawa

Ndani ya kipindi kifupi tu utaanza kuona neema za Bwana Kuna mabadiliko utaanza kuyapata katika kazi au ajira uliyonayo
 
Q

Waislam tuna sala 5 za faradhi (lazima) kila siku, maombi (dua) ndiyo usiseme.

Tokeni kizani Muingie kwenye Nuru.

Hiyo mnayoiita "zaburi" hamsemi kweli, siyo "zaburi" hiyo.

Kwanini hamsemi kweli?
Haya hiyo ni nini? Ni uenda wazimu kubishania imani ya mapokeo, dini ziko nyingi sio uislamu na ukristo au Uyahudi tuu bali kuna zingine kama Budha na huwasikii wakileta mabishano.
Kila mtu aamini atakacho tusilazimishane maana mwishowe ni kuchakazwa kama kule Gaza bure!
 
Kesho tena Mungu akitupa kibali tutakutana hapa kwaajili ya kufanya maombi naomba muongozo

Tuombee Nini wapendwa ?
Nawakaribisha

Nataka kila siku tunapopata kibali jukwaa hili tuwe na ombi la pamoja kila siku
 
Dinikwa Mwenyezi Mungu ni moja tu, zingine zote ni imani zilizobeba majina au vyeo vya watu.

Wagawe uwatawale.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…