Uzuri wa Paul Makonda ni kiongozi mwenye Mamlaka popote anafiti kundi kubwa la watu litahamia Arusha sasa

Bado tunahitaji likes 1000+ kwa Mh. Paul Makonda. Huku tukiendelea kusubiri hotuba yake ya kwanza katika jiji letu la ARUSHA
 
Watu wa dini wanasema "ana kibali".

Hii Huwa inatokea tu kwa baadhi ya watu kukubalika hata wakifanya mabaya. Mfano kwenye music tuna Nyandu Toz na Juma nature.

Kwangu Mimi,Makonda ni kiongozi wa hovyo.Jamaa ana mdomo mchafu kama Manara.
Mdomo uliochongoka umemponza. Mama amemuweka pale yeye anasifia marehemu. Eti anasema anatamani angekua mwenezi enzi za marehem ndio watu wangemkoma. Matusi,dharau kiburi na kejeli
 
Bado tunahitaji likes 1000+ kwa Mh. Paul Makonda. Huku tukiendelea kusubiri hotuba yake ya kwanza katika jiji letu la ARUSHA
Sasa anamhutubia nani badala ya kutatua kero za wananchi? Akihutubia hutubia utenguzi utamhusu huo ndio ukweli
 
Utoto raha sana, eti gonga like
 
Chuki ya mtu mmoja haiwezi kuharibu kukubalika kwa Makonda.
Kumbuka hapo alipo anaondolewa na mtu mmoja pasipo hata kikao wala ushauri wa mtu mwingine.
Abadilike bado umri mdogo abadilike sana anahitaji marafiki kuliko maadui,anahitaji amani kuliko karaha,anahitaji kwenda mbali kuliko alipotokea
 
Uzuri wa Paul Makonda ni kiongozi mwenye Mamlaka popote anafiti.

Utabiri wangu ni kwamba kundi kubwa la watanzania litahamia Arusha sasa.

Anajua kucheza na nafasi yake.

Tunao subiri hotuba ya kwanza ya Paul Makonda akiwa Arusha gonga like.
Naunga mkono hoja, ila naomba nikurekebishe kidogo, sio kweli kuwa Paul Makonda ni kiongozi mwenye Mamlaka popote anafiti, ukweli ni kuwa Paul Makonda hana mamlaka yoyote, kwasababu mamlaka ya kweli ni kutoka juu!, Paul Makonda ni mpakwa mafuta, hivyo ana kitu kinachoitwa "kibali", mbele ya macho ya mamlaka ya kweli, ni kutokana na kibali hicho, kinamuwezesha kukubalika popote!, Lema na Gambo wote wawili watashika adabu zao!, na wale machalii wa Arusha, watanyooka!. Arusha itakuwa kama pepo fulani, itachanua, itang'aa kutokana na kibali cha Makonda!.

Paul Makonda ni mpakwa mafuta wa Bwana mwenye kibali machoni pake.


Wanabodi, kwenye bandiko hili Ndugu, Jamaa na Marafiki, Njooni Tumtetee Makonda Dhidi ya Mapapa Wauza Unga Wanaomzushia... nilishauri
Hata baada ya kuteuliwa kuwa RC wa Arusha, Paul Makonda bado anapigwa vita na wasiomtakia mema, wasioitakia mema CCM na wasio itakia mema Tanzania.

Hongera sana Mkuu mpya wa mkoa wa Arusha, Paul Makonda, kuiheshimisha Arusha, endelea kunyoosha kama JPM.

Kiukweli ninamkubali sana Paul Makonda!, Tangu nilipoanza kumkubali Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam
He has never let me down!. Tena niliwahi kushauri Baada ya Magufuli, 2025 Makonda atatufaa sana, kwasababu ana uthubutu kuliko hata JPM!. Apunguze... ushauri huu still stands, kwasababu miaka hii 4 ya Mama ni kumalizia awamu ya Magufuli, awamu ya baada ya Magufuli inaanza 2025, ila Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke hivyo you never know with politics, everything is possible!.

Paul Makonda kanyaga mwendo, chapa kazi hapo RChuga, panyooshe, machalii wa Arusha wanyooshe!, kazi iendelee!.
Paskali.
 
Hakika watanzania ni watu wenye chuki sana kwa watu wanaojituma watu wazalendo kwa taifa Lao. Naomba Mungu watanzania waendelee kutawaliwa tu na watu wenye akili.

Makonda anatatizo gani mtu anajituma kwa moyo wote.
Walimu wa AR wajiandae kutolipa nauli...😛😛😛🙄🙄🙄
 
Katika kipindi ambacho comrade anatakiwa awe makini sana ni hapo Arusha kwenye wadhifa wake mpya!

Akikosea TU atapotea!!

Nadhani baada ya kupata Ile ajali alipoa sana,sijui ni nini kilimtokea !mi nadhani ni yeye mwenyewe aliomba atolewe kwenye cheo kile baada ya kuona anakua target!!

Alianza kuongea hadharani kabisa eti ananusurika kutegewa sumu!nilishtuka nikajua Kuna tatizo!

Namtakia Kila la kheri comrade makonda!
 
Jamaa ana vita kubwa sana , kiufupi ana vita kubwa ila kwa kuwa ni Mpakwa Mafuta atashida , akifika Arusha nitaenda kumnong'oneza jambo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vipi hapa "mpakwa mafuta" alikuwa anafuata "wauza unga" studio ya Radio na Tv saa 4:46 usiku??
 
Hakika watanzania ni watu wenye chuki sana kwa watu wanaojituma watu wazalendo kwa taifa Lao. Naomba Mungu watanzania waendelee kutawaliwa tu na watu wenye akili.

Makonda anatatizo gani mtu anajituma kwa moyo wote.
Wewe binti, mara nyingi waigizaji huwa na wafuasi. Uzalendo wa Makonda ni upi? Unasubiri hotuba au drama zake? Uko Arusha sijuhi ataingia kwa ungo, maana sarakasi za mikokoteni, punda na baiskeli keshazifanya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…