Vibanda vilivyowekwa kando ya barabara Jijini Dar es Salaam kuondolewa

Vibanda vilivyowekwa kando ya barabara Jijini Dar es Salaam kuondolewa

Hakika Mwendazake kaondoka na yake...
Watu waliofanya kazina Magufuli walipata shida sana, mwishowe wanakubali tu sababu yeye ndio muamuzi wa mwisho, Kiongozi hafuati taratibu za miji, sasa hawa watumishi wa manispaa wanatekelezaje sheria za mipango miji wakati Mkuu wa nchi anazivunja hizo kanuni?
 
ni jambo la busara sababu ni sehemu ya mipango mji.....dunia ya sasa miji lazima ipangike na sio kuishi tu kiholera holera.

hata hivyo, natamani mama angesubiri kwanza kidogo 'awapange' hawa jamaa kidogo halafu wangejiongeza wao wenyewe baada ya muda wa maangalizi. katika kuwapanga huko, angetumia hata siku yake moja (kama anavyoitumia leo kuongea na wazee) kuongea na hawa jamaa kupitia vyombo vya habari ili ujumbe umfikie kila machinga kutoka kila pembe ya nchi. siku hiyo angeitumia kuwaelimisha ni namna gani dunia inavyotakiwa kuwa kulingana na maendeleo ya nchi (tena ikiwezekana siku hiyo angegeuka km mwalimu au tv presenter pale tbc kwa kuonyesha na picha kabisa za miji iliyopangika vema) na nini wafanye sasa!

ingependeza sana na vile mama alivyo mueleweshaji mzuri nina uhakika wangeelewa haswaa na nguvu ndogo sana hatimaye ingetumika hapo baadae!
 
Wenye nguvu ya fedha washafanya Yao tena,

Ndiyo tunajua, kila kitu lazima kiende Kwa utaratibu, Labda niulize Kwa Mleta uzi, Je Hilo gari linalotangaza halisemi mbadala wa hao wenye vibanda wanapaswa wapelekwe wapi?

Kama ndivyo, tayari hili ni kosa lingine kubwa baada ya lile la Kwanza la makampuni ya kigeni yanayokuja kuwekeza nchini hayatakiwi kuwekewa limiti ya wafanyakazi wanaotakiwa kuja nao kutoka makwao ili kufanya kazi kwenye kampuni hizo za kigeni!!

Hilo ndilo kosa kubwa kuliko mengine yote ambayo yameendelea kuwepo Wakati huu,

Watanzania mtegemee kukosa ajira kwenye makampuni yote ya kigeni na hata ysliyowekeza tayari mtaanza kutimuliwa mdogomdogo na wageni kuletwa kufanya kazi hizo

Yetu macho
Kama mimi ni mtanzania nimeajiriwa kama marketing manager kwenye kampuni ya kigeni na ninafanya kazi yangu vizurii na kampuni inapata wateja wengi na kupata faida kwanini wanitimue? Yaani watanitimua tu kisa mtanzania au kuna sababu nyingne unaificha?
 
Hakuna marefu yasiyo na ncha.Hatimaye mda wao umefika...Ule uhuru wa kijinga umeisha,wacha waende hayo maeneo rasmi yaliyopangwa.Mbona tutawafuata tu kulikoni kutughasi watembea kwa miguu.
 
Asante kwa kuwa wasikivu

 
Wamachinga huwa wanapenda kukaa sehem zenye mkusanyiko wa watu wengi hasa wale ambao wapo katika movement kubwa ya kutoka sehem moja kwenda nyingine.

Kwa jiji la Dar es Salaam sasa hivi jinsi lilivyo inahitajika kubuni stendi kubwa nyingi sanaa na kuhakikisha daladala za kwenda sehem mbalimbali zinakutana katika hizo stendi.

Mfano stendi kama Kariakoo, Mnazi Mmoja, Posta(Bandarini na Stesheni), Makumbusho, Mwenge, Mbagala rangi 3, Ubungo, Tabata, Buguruni, Temeke, Tandika, Kigamboni, Gongo la mboto, Tegeta, Mbezi na maeneo mengi ambayo yanakuwa na movements ya watu wengi.

Stendi zijengwe kwa kuwezesha daladala ziwe zinalazimika kuwamwaga watu hapo na hapo wanatakiwa kuunganisha safari zao bila ya kutembea tena umbali mwingine kufuata daladala zingine.

Hii itasaidia sana kuwaondoa wale wamachinga wanao jipanga kando ya barabara kuvizia hizo movements za watu.

Kingine mfano wa stendi ya makumbusho pale hakuna wamachinga wengi wamejipanga kando kando ya barabara za kuingia kuelekea stendi sababu hawana huo ulazima. Wamachinga wengi wapo ndani mule stendi wamejibana.

Mtu hawezi kushuka ndani ya gari huku mwanzoni mwa zile barabara zinazotumiwa na daladala kuingia stendi ya makumbusho kisa tu anunue kitu ambacho akifika ndani mule stendi anaweza kukipata na akaunga Safari yake bila usumbufu.

Wamachinga wateja wao ni watu ambao wananunua vitu kwa kushtukiza yaani, ameona bidhaa rahisi kubebeka na akaona kule nyumbani sina hiko kitu basi ananunua na kuendelea na safari yake.

Tofuati na hayo ma Mall na Supermarket ambapo mteja huwa anajipanga kabisa kuwa naenda kufanya shopping sehemu fulani.

Kwahiyo kusema wamachinga wakusanyike sehemu sijui kama machinga Complex pale hakuna movement ya watu ya kueleweka ni kama kuwafanya wajiwekee kishopping Mall chao na kamwe hawawezi kupata wateja wao wa siku zote ambao ni watu wapita njia tu.
 
Kama mimi ni mtanzania nimeajiriwa kama marketing manager kwenye kampuni ya kigeni na ninafanya kazi yangu vizurii na kampuni inapata wateja wengi na kupata faida kwanini wanitimue? Yaani watanitimua tu kisa mtanzania au kuna sababu nyingne unaificha?
Si unayo tayari, Lkn ujue pia damu ni nzito kuliko maji
 
Swala la machinga waondoke tu mjini wanaua biashara watengewe maeneo yao Magufuli alibugi sana


Kwanza hawalipi kodi na wanaponunua bidhaa hawaombi risiti kwenye maduka makubwa so serikali inapata hasara ya kodi.

Vile vile wengi mjini ni wafanya biashara wakubwa wanafanya kutoa pesa kwenye mfuko wa suluali na kuweka kwenye mfuko wa shati.


Ndio maana ukwepaji kodi unaongezeka kwa sababu watu wenye address za kulipa kodi biashara zao wanachukua machinga.

Halafu machinga wenyewe wanauza sana halafu hawana leseni za biashara za kufanyia kazi wengine unakuta ndio wale waliofunga maduka kipindi cha Magufuli unakuta machinga ameweka bidhaa za milio 10 nje hii sio haki hata kidogo.

Watafutiwe maeneo maalumu kama Tandika tegeta, Ubungo mbagala wawe na shopping mail zao na walipe kodi ili tuone kama watauza tens bidhaa ovyo na kuhatarisha hata maisha ya wanunuzi.

Unakuta mtu anauza nyanya kariakoo katikati ya barabara seriously sehemu ambayo mnasema ni soko la kimataifa.?
We jamaa una roho mbaya, vaa viatu vya hao machinga ili uone maisha wanayoishi na namna wanavyoendesha maisha yao na familia zao ukizingatia humo barabarani ndipo wateja wengi walipo kwa wingi

Sema wangewekewa utaratibu sio kuwaondoa pasipo kujua wanapoelekea uo ni kama unyanyasaji na udhalilishaji
 
Wamachinga huwa wanapenda kukaa sehem zenye mkusanyiko wa watu wengi hasa wale ambao wapo katika movement kubwa ya kutoka sehem moja kwenda nyingine.

Kwa jiji la Dar es Salaam sasa hivi jinsi lilivyo inahitajika kubuni stendi kubwa nyingi sanaa na kuhakikisha daladala za kwenda sehem mbalimbali zinakutana katika hizo stendi.

Mfano stendi kama Kariakoo, Mnazi Mmoja, Posta (Bandarini na Stesheni), Makumbusho, Mwenge, Mbagala rangi 3, Ubungo, Tabata, Buguruni, Temeke, Tandika, Kigamboni, Gongo la mboto, Tegeta, Mbezi na maeneo mengi ambayo yanakuwa na movements ya watu wengi.

Stendi zijengwe kwa kuwezesha daladala ziwe zinalazimika kuwamwaga watu hapo na hapo wanatakiwa kuunganisha safari zao bila ya kutembea tena umbali mwingine kufuata daladala zingine.

Hii itasaidia sana kuwaondoa wale wamachinga wanao jipanga kando ya barabara kuvizia hizo movements za watu.

Kingine mfano wa stendi ya makumbusho pale hakuna wamachinga wengi wamejipanga kando kando ya barabara za kuingia kuelekea stendi sababu hawana huo ulazima. Wamachinga wengi wapo ndani mule stendi wamejibana.

Mtu hawezi kushuka ndani ya gari huku mwanzoni mwa zile barabara zinazotumiwa na daladala kuingia stendi ya makumbusho kisa tu anunue kitu ambacho akifika ndani mule stendi anaweza kukipata na akaunga Safari yake bila usumbufu.

Wamachinga wateja wao ni watu ambao wananunua vitu kwa kushtukiza yaani, ameona bidhaa rahisi kubebeka na akaona kule nyumbani sina hiko kitu basi ananunua na kuendelea na safari yake.

Tofuati na hayo ma Mall na Supermarket ambapo mteja huwa anajipanga kabisa kuwa naenda kufanya shopping sehemu fulani.

Kwahiyo kusema wamachinga wakusanyike sehemu sijui kama machinga Complex pale hakuna movement ya watu ya kueleweka ni kama kuwafanya wajiwekee kishopping Mall chao na kamwe hawawezi kupata wateja wao wa siku zote ambao ni watu wapita njia tu.
 
Back
Top Bottom