Vibanda vilivyowekwa kando ya barabara Jijini Dar es Salaam kuondolewa

Vibanda vilivyowekwa kando ya barabara Jijini Dar es Salaam kuondolewa

[emoji348]Watafutiwe sehemu kwani wao ni akina nani?

[emoji348]Wale vijana wenzao vijijini wanatafutiwa mashamba ya kulima na nani?

[emoji348]Wale waliomaliza vyuo na shule mbalimbali wanatafutiwa kazi na nani?

[emoji348]Kuna watu wana mamitji makubwa hawataki kukodi frem ati wao ni machinga watfutiwe eneo

[emoji348] Utaratibu wa mipango mji uheshmiwe na kila anayekuja mjini ajue anakuja kuishi vipi na sio kuanza kulalamika na kujiona wao ni kundi flani vulnerable ambalo linahitaji kutokufuata sheria lihurumiwe na kila mtu na liwe mzigo kwa serikali enyi WAMACHINGA na BODADODA ninyi ni akina nani?
Bodaboda na machinga walilelewa vibaya,watoto vitinda mimba wa mwendazake
 
Kama pale ilala boma kutokea kigogo mwisho ni kero tupu!wamehodhi eneo lote lile,soko la mchikichini kulikua na parking kubwa tu upande breweries lakini sasa hivi vimejaa vibanda hamna parking tena!
Yote yamesababishwa na kufa kwa uchumi wa nchi.Mfano korosho, mbaazi, ufuta,mifugo bei ikiwa nzuri kilimo kikilipa nani awe machinga hali wanunuzi ukufuata shamba.
Kabla ya mwendazake Wakenya walijaa hadi vijijini wakichumbia mazao yaani unapewa advance mazao yakikomaa unamaliziwa cash yako wanavuna mazao yao we unabakia na pesa.Walijaa Mbeya,njombe,iringa, kilimanjaro kwenye ndizi,viazi mviringo,walijaa dodoma iringa rukwa ruvuma kwenye mahindi walijaa pwani tanga kwenye matikitiki,nyanya,mboga nk.Huku wacongo,wazambia wakijaa kanda ya ziwa hadi visiwani wakinunua dagaa, samaki,mabondo,Wasudani Wakenya wakinunua vitunguu,nk Wacomoro, zimbabwe, zambia wakijaa kariakoo kuleta pesa hii ilisaidia Sana watu kubakia sehemu moja kuzalisha.Baada ya sera chakavu za kuwafanya matajiri wawe masikini,na kufunga mipaka,bifu zisizo kichwa majirani zetu wote walipotea hali ikawa ngumu vijijini ikapelekea wimbi la machinga mijini.Pesa zilijaa toka KILA nchi jirani ikapelekea kushamiri kwa bureau de change mijini,thus uliona nyumba za nyasi zikipotea kwa kasi ya 5G nchi nzima Bati zikienea kwa kasi vijijini sababu ya mzunguko mzuri wa pesa kabla ya sera chakavu.
Tukivutia Wawekezaji ajira zitakuwepo,tukifungua mipaka wakulima na wafugaji watauza nje uzalishaji utarejea na idadi ya machinga itapungua mijini.
 
Zinaheshimika biashara za machinga. Wenye maduka na biashara kubwa walikuwa wahanga wa TRA. Uchumi gani unajengwa na wamachinga??? Hawa wapangiwe maeneo maalumu. Sio kila eneo ni la kufanya biashara. Mji uwe safi na wao waishi kama wananchi wa Tanzania.
Tukiwa hatufuati sheria na taratibu tujue tunajukomoa wenyewe
Wanasiasa uchwara ndio zao la wimbi la machinga mijini
 
Hao wanaotolewa maeneo hayo wanatarajiwa kuhamishiwa wapi?. Mtihani mpya kwa wale waliochukua mikopo haswa kina mama wanaotegemea vikoba na pesa za aina hiyo.
Mzee kuchukuwa mkopo ukaweka kibanda barabarani nisawa kweli! Mimi nashauri hata leo viondolewe,kwanza nikelo kubwa kwa watembea kwa mguu na vilevile ikija kutokea hajari ya gari kuacha njia ndo unaweza kuelewa.Viondolewe safi kabisa
 
Yote yamesababishwa na kufa kwa uchumi wa nchi.Mfano korosho, mbaazi, ufuta,mifugo bei ikiwa nzuri kilimo kikilipa nani awe machinga hali wanunuzi ukufuata shamba.
Kabla ya mwendazake Wakenya walijaa hadi vijijini wakichumbia mazao yaani unapewa advance mazao yakikomaa unamaliziwa cash yako wanavuna mazao yao we unabakia na pesa.Walijaa Mbeya,njombe,iringa, kilimanjaro kwenye ndizi,viazi mviringo,walijaa dodoma iringa rukwa ruvuma kwenye mahindi walijaa pwani tanga kwenye matikitiki,nyanya,mboga nk.Huku wabongo,wazambia wakijaa kanda ya ziwa hadi visiwani wakinunua dagaa, samaki,mabondo, Wacomoro, zimbabwe, zambia wakijaa kariakoo kuleta pesa hii ilisaidia Sana watu kubakia sehemu moja kuzalisha.Baada ya sera chakavu za kuwafanya matajiri wawe masikini,na kufunga mipaka,bifu zisizo kichwa majirani zetu wote walipotea hali ikawa ngumu vijijini ikapelekea wimbi la machinga mijini.
Tukivutia Wawekezaji ajira zitakuwepo,tukifungua mipaka wakulima na wafugaji watauza nje uzalishaji utarejea na idadi ya machinga itapungua mijini.
Kariakoo pale walijaa wacomoro kama wapo moroni vile,walianza kufika mpaka kondoa huko nishawahi kuwakuta,wazambia na wakongo nao awakua nyuma
 
wakati linajengewa stand na batabara za maaana mkasema mwendazake anakurupula[emoji16][emoji16][emoji16]

mtanzania ni kama nzi,uchafu anapenda na usafi anapenda pia.
Ingependeza umtuhumu muhusika wa hiki ulichoandika.
Kimsingi mimi huwa sipingi kila kitu na huwa sikubali kila kitu.
 
Uchafu uliokuwa unaonekana katika jiji la dar es salaam huwezi kukuta katika majiji makubwa kama Johannesburg ama pretoria.

Hongereni sana serikali ya awamu ya sita kwa kuliona hili.
 
.... Tutegemee chadema kuanza kutetea wamachinga?
Hapana, hilo ni CCM, waliliendekeza na walinywe wenyewe, iwe kwa kubadili gia au kwa kupingana wenyewe kwa wenyewe. ukumbuke ile kauli ya mwanaCCM mwenye mamlaka, kwamba msiwasumbue hawa kwa kuwa walinipigia kura! Sasa usiiingize CHADEMA, hilo ni la walioipigia kura CCM
 
Hilo tangazo sijalielewa vizuri, sababu kuna vibanda kando kando ya barabara na kuna machinga wanaotandaza chini, hapo ni vibanda vinaondolewa ama tangazo linatangaza kuwaondoa machinga wote barabarani? Nifahamishe!
 
Umewahi kufanya kazi katika kampuni za wahindi?. toka zamani wao wanaleta wahindi wenzao kufanya kazi hata ya ulinzi. Kuleta wafanyakazi haijaanza leo. je unafikiri watanzania hawana sifa, wavivu au hawaaminiki?
Kwa hiyo ni bora iwe rasmi sasa, embu umefikiri Kwamba, Ikiwa itakuwa hivyo, na Kwa sifa mbaya tuliyonayo Watanzania kuwa,Sisi ni wavivu, waizi maofisini ingawa sio wote, Je, ni Watanzania wangapi watapoteza ajira zao baada ya tangazo Hilo??
 
Back
Top Bottom