Vibarua viwandani au part time job kwa hapa Dar es Salaam zinapatikana wapi?

Vibarua viwandani au part time job kwa hapa Dar es Salaam zinapatikana wapi?

Asante Sana umenena vyema haya ndio mawazo ambayo alietoa unajua kabsa amewah au ndo yupo kwenye gari moja nawewe
Kabisa bro tupo behewa moja (graduate 2017) na ajira rasmi bado, mimi ajira naiona ni moja ya vyanzo vingi vya mapato. Kama ajira bado basi vipo vyanzo vingine vingi vya mapato (Fursa) mbalimbali. Ni kujipanga, kufanya research za fursa mbali mbali na kuanza fursa.
 
"Mtaji Mtaji Mtaji"

Nimemnukuu graduate mmoja hapa makumbusho.
Mtaji mkubwa kabisa ni 1. Akili 2. Nguvu zako 3. Mdomo. Kama unayo mitaji hii basi unaweza kujipanga na kutengeneza mtaji pesa. Kivipi? Unaweza kutumia mtaji wa akili, nguvu na mdomo ukajiwekea malengo ya miezi kadhaaa ukafanya udalali wa vitu vinavyouzwa kama nyumba, magari, kiwanja n.k Ukapata mtaji pesa, Katika huo mtaji pesa utaopata unajiwekea malengo, mwisho wa siku utapata mtaji pesa wa kutosha kuanza project yoyote. Kikubwa malengo+nidhamu ya pesa+uvumilivu
 
Mtaji mkubwa kabisa ni 1. Akili 2. Nguvu zako 3. Mdomo. Kama unayo mitaji hii basi unaweza kujipanga na kutengeneza mtaji pesa. Kivipi? Unaweza kutumia mtaji wa akili, nguvu na mdomo ukajiwekea malengo ya miezi kadhaaa ukafanya udalali wa vitu vinavyouzwa kama nyumba, magari, kiwanja n.k Ukapata mtaji pesa, Katika huo mtaji pesa utaopata unajiwekea malengo, mwisho wa siku utapata mtaji pesa wa kutosha kuanza project yoyote. Kikubwa malengo+nidhamu ya pesa+uvumilivu
Unahakika kuwa wewe si keyboard worrior??
 
Ni muda sasa nimekuwa natafuta kazi zilizo za professional yangu na zisizo zangu Ila kikubwa nina uwezo wa kufanya kazi yoyote ile halali na ambayo inahitaji skills za kawaida na hata zile complicated maana naamini hamna kinachoshindikana ukiamua. Sasa tatzo huja hapa.

Nmehudhuria interview 16 mpaka sasa na kufika mpaka 10 Bora lakini mwishoni hii kitu inaitwa connection na kujuana inanifanya naishia kuwa na uzoefu mwingi wa kujibu maswali ya interview bila kuwa na mafanikio ya kazi.

Niseme Jambo moja kama wewe umetoka familia au ukoo ambao wewe ndo inahitaji ufanikiwe ili utengeneze hyo connection kwa wengine, basi kazi unayo maana nchi imegubikwa na rushwa za ngono na kujuana hadi sisi tunaotokea familia za kawaida hatupati haki ya kusikilzwa pamoja na uwezo au vipawa tulivyo navyo.

Kuna muda natamani nifanye biashara lakini nakumbuka lengo la kutafuta ajira pia ni kutaka kupata mtaji utakaoniwezesha kujiajiri ili nije nipambane na hii kitu sabu inauma sema hatuna pakwenda hadi inafika hatua inatubidi tukimbie mazingira tulioishi ili tusiwakatishe tamaa wadogo zetu wanaoaminishwa kupitia Elimu maisha yao yatabadilika, kwahiyo wakiwa wanatuona kaka zao tupo mitaani hatuna tunachofanya na ikiwa miaka kadhaa nyuma waliambiwa tupo vyuoni tunasoma na ikajulikana hivo kuwa sisi ni wasomi na mbaya zaidi wapo walioweka nia ya kutaka kufika hapa nilipo mimi.

Sasa je, wakajua uhalisia wa haya ninayopitia nani atapata moyo wakuendelea na Elimu?

All in all Kuna mafundisho mengi sana napitia japo najua ipo siku ntahitimu lakini nkifikiria pesa iliyowekezwa kwa shida na wazazi wangu ili mimi nisome wakijua ntawasaidia kulea wadogo zangu kumbe nimerud kuwa mzigo tena kwao.

Samahani kwa nitakayemuudhi na kwa aliye na wakati kama wangu ajipe moyo asikate tamaa kwani haya yote yana mwisho.
Nikikumbuka waliofanikiwa kuendelea na shule walivyoniacha mtaani kwa mbwembwe na dharau najikuta sihisi chochote nikisikia msomi analia
 
Tatizo siku hizi vijana mnachagua sana kazi. Kama huna kazi ni ngumu sana kupata kazi namaanisha mchongo wa kazi halali hata kama ni kusaidia fundi ndio unaondoa gundu ndio mwanzo wa safari
 
Mungu anamuona anayepambana, nakumbuka nimefanya kazi zote za hovyo nikiwa mtaani

Mungu akaniletea ajira miguuni mwangu

Wala sikuwa na connection yoyote na mpaka leo sina mtu mkubwa nayefahamiana naye serikalini
M

Mungu asaidie dunia kwakweli.
 
Unajua shida yetu tulioweng ni wepesi kushauri kulingana na mazoea au kilichopo mdomoni Sana huku uhalisia tukiujua! Fatilia hata motivational speakers wanavitu vya msingi wanazungumza Ila wanasahau kitu inaitwa mtaa na maisha ya mtaa ni SoMo lisilohitaji tuition lazma utumie akili ya ziada na pia uhalisia wa like wanachosema haupo kivitendo Bali nadharia zaidi. Leo hii unanilaumu mm kwa kuwa na Imani kwenye ajira na kuntaka niangalie upande wa pili huku ukijisauhulisha kuwa hiyo Elimu ambayo imejaa nadharia zaidi na ambayo imekosa uhalisia wa kilichopo mtaani nmeipata sio 100% nmetaka mwenywe.... Miaka ile mzazi gani au jamii gani ilikuwa haiamini katika Elimu? Ngeacha kusoma kufata kilennachokiamini ili jamii na wazazi wanitenge? Unamkataliaje mzazi kusoma shule? Mm nmemaliza 4m 4 nkalia mpaka machozi nataka kwenda chuo Cha ufundi nipate ujuzi wa moja kwa moja ambao utanipa pesa bila hata kusubr ajira ya mtu nkiwa na lengo la kukusanya mtaji ili nije niwekeze kwenye ujuzi wangu! Lakin nlitaka had kutengwa na ukoo kwa kile kinachowazwa kuwa nmeanza kuvuta bangi ndio maana natoa mawazo hayo... Haya wewe unafanyaje hapo? Tusilaumu Wala kutoa ushauri kwa mtu anaeugua Bali tuangalie wale ambao bado hawajapata homa hiyo Ila mm nnachotaka hapa ni dawa tu na sio wapi nilipatia ugonjwa.
hakika hakika💯%
 
Mimi ni kijana wa miaka 17 nikiwa na Elimu ya chuo kikuu shahada ya uhandisi wa mitandao na mitambo! Naomba kutumika Kama msaidizi Kwa kutumwa kazi mbalimbali maana najua watu wengi wako bize na Mambo ya kiofisi hata kushindwa kupata muda wa kufanya au kusimamia vitu vingne. Nipo tayari kutumwa popote Kwa mskubaliano maalumu ya malipo.
Nina ujuzi wa udereva pia na leseni na uzoefu wa kuendesha magari Kwa zaidi ya miaka 5 hapa Dar es salaam!
Nitume popote pia nafanya typing Kwa haraka na ishu zoote za stationary hivyo Kwa mahitaji hayo tuwasiliane Kwa namba 0776662470
 
Naomba kujuzwa chimbo la vibarua hapa mjini ni wapi? Na kazi zipi za part time hapa bongo? Kuna mtu nlimsikia kuwa posta karibu na clock tower kuna sehemu watu wanakusanyika kusubiri vibarua na nje ya bandari ni kweli? Kama kweli taratibu zipoje? Na malipo yakoje?

Tujuzane wakubwa
Duh! Umenikumbusha mbali Sana Mkuu, maisha haya ya vibarua yalinitesa Sana, nakumbuka Kama ilivyokuwa kawaida yangu kuamka Alfajiri ya saa kumi na moja Alfajiri ili niwahi kupon ya kuingia kiwanda Cha kutengeneza nondo pale vertinary, Mzee Mohammed ndio ilikuwa kazi yake kugawa kupon, utakuta Ana kupon 20 halafu tunaotaka kazi tupo 50! Kwa kweli ni huzuni kuu, ataanza kuangalia anaowafahamu Kwanza.
Nilibahatika kupata kupon Mara Tatu tu lakini nilikua natimba pale kwa karibu Kila siku.
Ila Mungu ni mwema Kaka usikate tamaa, pambana! Tambua ww ni mshindi.
 
Ugumu wa maisha ulianza pale wasomi walipokuwa hawaajiliwi,wasomi wakawa wanalundikana na kuingilia biashara ambzo walipaswa kufunya wasio na elimu...sasa kama wasomi na wasiosoma wanafanya biashara moja je nani atakuwa mteja. Tuombe Mungu mama etu aangalie kwny swala la ajira namin Kila kitu kitakuwa sawa chochote utachouza kitakuwa na mteja.
 
Ni muda sasa nimekuwa natafuta kazi zilizo za professional yangu na zisizo zangu Ila kikubwa nina uwezo wa kufanya kazi yoyote ile halali na ambayo inahitaji skills za kawaida na hata zile complicated maana naamini hamna kinachoshindikana ukiamua. Sasa tatzo huja hapa.

Nmehudhuria interview 16 mpaka sasa na kufika mpaka 10 Bora lakini mwishoni hii kitu inaitwa connection na kujuana inanifanya naishia kuwa na uzoefu mwingi wa kujibu maswali ya interview bila kuwa na mafanikio ya kazi.

Niseme Jambo moja kama wewe umetoka familia au ukoo ambao wewe ndo inahitaji ufanikiwe ili utengeneze hyo connection kwa wengine, basi kazi unayo maana nchi imegubikwa na rushwa za ngono na kujuana hadi sisi tunaotokea familia za kawaida hatupati haki ya kusikilzwa pamoja na uwezo au vipawa tulivyo navyo.

Kuna muda natamani nifanye biashara lakini nakumbuka lengo la kutafuta ajira pia ni kutaka kupata mtaji utakaoniwezesha kujiajiri ili nije nipambane na hii kitu sabu inauma sema hatuna pakwenda hadi inafika hatua inatubidi tukimbie mazingira tulioishi ili tusiwakatishe tamaa wadogo zetu wanaoaminishwa kupitia Elimu maisha yao yatabadilika, kwahiyo wakiwa wanatuona kaka zao tupo mitaani hatuna tunachofanya na ikiwa miaka kadhaa nyuma waliambiwa tupo vyuoni tunasoma na ikajulikana hivo kuwa sisi ni wasomi na mbaya zaidi wapo walioweka nia ya kutaka kufika hapa nilipo mimi.

Sasa je, wakajua uhalisia wa haya ninayopitia nani atapata moyo wakuendelea na Elimu?

All in all Kuna mafundisho mengi sana napitia japo najua ipo siku ntahitimu lakini nkifikiria pesa iliyowekezwa kwa shida na wazazi wangu ili mimi nisome wakijua ntawasaidia kulea wadogo zangu kumbe nimerud kuwa mzigo tena kwao.

Samahani kwa nitakayemuudhi na kwa aliye na wakati kama wangu ajipe moyo asikate tamaa kwani haya yote yana mwisho.
Dahh.. Njia ni ngumu mno...Ila iko siku kaka hayo yote yatabaki kuwa story..! Usikate Tamaa.
 
Niliwahi kuwa konda aisee, ila kazi shikamoo,
Gari ruti mbagara to mawasiliano,
Ikifika mida ya saa 8 mpaka 2 usiku kichwa kimevurugwa, nam mambo kibao.
1. Watu wamechoka kinoma hawana furaha utadhani wametoka sehemu moja ( haswa kwenye tarehe za 9-19)
2. Perfume za aina tofauti + harufu za makwapa haswa ukiwa unadai nauli.
3. Foleni za kijinga na abiria ambao wanaongea kizungu au kutishiana,
4. Uchovu wa siku nzima na kuwahi kuamka,

Sasa hayo yote ukifika mbagara( unaenda mawasiliano) kwa sababu kichwa kimejamu unashangaa unaita mawasiliano, buguruni kwa azizi ali mbagara, mbagara [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] upo busy mwenyewe unaita!
Shikamoo maisha, shikamoo wapambanaji

Sent from my SM-J701F using JamiiForums mobile app
Ila tuseme ukweli makonda wanamake aise...je ulifanikiwa kuzikusanya?
 
Back
Top Bottom