Video: Afande IGP Sirro anamjibu nani hapa?!

Nafikiri aijipi anapigwa vita vya chini chini nae kaona isiwe shida,Tatizo sio aijipi bali muundo wa jeshi la polisi......

Polisi kwa yale masilahi inabidi waangaliwe tena aisee.....ili wawe wanafanya kazi kwa weledi....

Fikra zangu tu
True muundo wa police ni kutii maagizo amri ya mwanasiasa.Katiba hii haitenganishi police na siasa
 

Siasa ndio maisha, unaitengaje siasa na maisha?

Kwa taarifa yako hilo jeshi la polisi limepoteza weledi baada ya kuwa ni nguzo muhimu ya kuingiza viongozi madarakani.

Hivyo viongozi wanapoingia madarakani kwa njia za kihalifu, unakuta hawana nguvu ya kuwawajibisha polisi hata taarifa ikitolewa kwani polisi ndio waliowaingiza madarakani.

Kuna mahusiano makubwa ya kihalifu baina ya serikali na jeshi la polisi, hii inapelekea wananchi kukosa sehemu ya kushitaki, kwani serikali na polisi wanakuwa ni washirika kwenye uhalifu, ambapo polisi anamsaidia kiongozi kuingia madarakani bila ridhaa ya umma, kisha kiongozi akiingia madarakani anafumbia macho uovu wa polisi.

Kwa maneno marahisi, ni kuwa serikali na polisi wana kitu waswahili wasemacho nilinde kwa jua nikulinde kwa mvua.

Ukitaka kujua ukweli wa hiki nisemacho, nenda magereza ukaone jinsi watu walivyojazwa gerezani kwa kubambikiwa kesi na polisi huku hakuna uchaguzi, na serikali haichukui hatua yoyote.
 
Sirro kwisha habari yako, huko jikoni Bi Zuhra anapika barua yako.

Kwanza huyu Sirro ana kinga kisheria asishtakiwe? Kama hana mimi maoni yangu ilibidi afunguliwe faili mahakamani na kwa kuanzia tuanze na shambulio la Ndugu yetu Tundu Lissu.

Huu mchezo hauitaji hasira!
 
Hapo Siro ameamua kukomaa, kama noma iwe noma, Siro ni kama anasema hatoki mtu hapa. Siro sio Ndugai, Samia safari hii ajipange haswaa.
Unavoongea kana kwamba akitaka kumtema kesho asubuhi atashindwa.

Sirro anaweza kujikuta mkulima huko Sirari kesho mapema tu ikimpendeza mama, wala hakuna mtu atakayekohoa
 
Muda utasema kama ni leo,kesho au mtondo goo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…