Video: Afande IGP Sirro anamjibu nani hapa?!

Video: Afande IGP Sirro anamjibu nani hapa?!

Soma post yote taratibu mimi sijajikita sana kwenye siasa bali alichoongea Sirro mwenyewe.

Imechukua miezi mitatu IGP kupata habari askari polisi wametenda uhalifu, tena kupitia mitandao ya kijamii inavyoonekana.

Sakata lenyewe analoliongelea IGP marehemu alichukuliwa mbele ya mashahidi, sasa jiulize ni kitu gani kilichowafanya watu kuogopa kutoa habari mapema ndio maana raisi akasema watu wanakosa imani na jeshi la polisi.
Siro alikuwa anajitetea.Pili kama muundo wa Polisi una shida urekebishwe afu ikitokea matukio kama haya Ma RPC wawe wanaondolewa fasta kwa kuletwa Makao makuu au kupangiwa majukumu mengine.
 
Sirro kwisha habari yako, huko jikoni Bi Zuhra anapika barua yako.

Kwanza huyu Sirro ana kinga kisheria asishtakiwe? Kama hana mimi maoni yangu ilibidi afunguliwe faili mahakamani na kwa kuanzia tuanze na shambulio la Ndugu yetu Tundu Lissu.

Huu mchezo hauitaji hasira!
Hizi akili huwa mnatoa wapi? Kwenye tukio la Lissu unaitenganishaje Polisi na CCM?

Kwamba Siro aliamua tu mwenyewe (ikiwa ni yeye) kwenda kumshambulia Lissu? Hiyo hata Samia hawezi kuifufua.

Hahaha vita ya CCM kwa CCM haiwezi kuwanufaisha CDM hata siku moja, nyinyi mnachotakiwa kufanya ni kutafuta namna ya kuingia kwenye system.
 
Mkuu una maslahi na Siro.Kwa hiyo anachofa Siro ni sahihi?

Kwa Maoni yangu anachofanya sasa Siro ndio kuhamasisha mgomo baridi,anatakiwa kuondolewa right now kwa sababu kuzidi kuchelewa ndio kutaeneza zaidi hii Hali.

Wako maofisa Wana weledi na wanaaminiwa na askari wa chini.Rais mfute Kazi IGP Ili nae apangue baadhi ya ma RPC na wakuu wa upelelezi.

Mwisho awaongezee posho maaskari kupunguza vishawishi kwa sababu hata huko TRA watu wanalipwa vizuri zaidi Ili kupunguza ushawishi.
Sirro aweza kuwa mpuuzi kwa kiwango fulani,ila hazuii nia nzuri ya maslahi bora kwa askari kama ipo kwa huyo rais wake.

Sirro amezungumza kama mwenye taaluma ya polisi chombo anachokiongoza,kwamba kama shida anayo yeye,apigwe yeye kwa namna yote.ila kuinyea taasisi nzima sio jambo salama.

Embu nieleze hao maofisa bora si wako kazini saa hii wakiugulia maumivu ya vichambo kama polisi wengine wasio waadilifu???
 
Siro alikuwa anajitetea.Pili kama muundo wa Polisi una shida urekebishwe afu ikitokea matukio kama haya Ma RPC wawe wanaondolewa fasta kwa kuletwa Makao makuu au kupangiwa majukumu mengine.
Na ndio maana sijamlaumu IGP moja kwa moja kwa sababu alipopata habari alishugulikia akaondoa chain nzima ya wahusika.

Lakini tumefikaje hapo hadi ndugu walalamike mitandaoni ndio IGP ajue. Issue ya msingi inaonekana wananchi hawana imani na jeshi la polisi kwenye kuripoti matukio ya uhalifu wa polisi na ndicho alichoongea raisi pia.

Ndio maana kwenye post ya kwanza uliyo quote nikatoa suggestion either namba ya kuripoti uhalifu iwe independent na polisi; au kuwe na number maalum wizara ya mambo ya ndani ya kuripoti matukio ya uhalifu wa polisi ili waziri na IGP wawe briefed mapema to take actions.
 
Kuna tatizo ktk mfumo wa kikazi (operations) katika jeshi la Polisi.




Haiwezekani mtu anaingia Polisi Station/ Polisi Post huku kasindikizwa na mtu, halafu apotelee ndani ya kituo cha Polisi, ni upungufu kubwa ktk mfumo wa Polisi habari imfikie IGP kuwa mtu huyo aliyekamatwa na jeshi la Polisi akaingia kituoni kuwa akuuawa na askari wa jeshi la Polisi miezi miwili baadaye.

Kesi tajwa aliyoitaja IGP ya Mtwara ni kielelezo tosha cha mfumo mbovu uliopo ndani ya jeshi lisilofuata PGO, haki ya mtuhumiwa kuongea na mlinda amani / wakili au ofisa wa Mahakama n.k
CASE STUDY 1: Mtwara: Mfanyabiashara madini: auawa

Polisi saba mkoani Mtwara, Kusini mwa Tanzania wanatuhumiwa kufanya mauaji na kuutupa porini mwili wa mfanyabiashara wa madini aliyekuwa na umri wa miaka 25.

Kijana Mussa Hamisi mkazi wa wilaya ya Nachingwea mkoa jirani wa Lindi, anadaiwa kukamatwa na askari wa polisi octoba 20, mwaka jana akiwa katika nyumba ya kulala wageni hapa Mkoani Mtwara akituhumiwa kuwa mwizi wa pikipiki na kufikishwa kituo cha poilisi kwa ajili ya mahojiano.

Baada ya kuhojiwa alibainika kuwa na fedha zipatazo shilingi million mbili na laki tano (2.5m), na kutaja kiasi kingine ambacho alikihifadhi nyumbani kwao wilayani Nachingwea Mkoani Lindi, ambako maofisa hao walifunga safari hadi wilayani humo katika nyumba ya wakazi wake kupekua na kubaini kiasi kingine cha dola za kimarekani 13,500 na kuondoka nazo wakiwa wamemuweka chini ya ulinzi.

Hawa Bakari ni mama mzazi wa kijana huyo, ambaye anasema mara ya mwisho kuonekana machoni mwa ndugu zake kijana wake ni januari 5, mwaka huu 2022, anaeleza namna askari walivyofika nyumbani kwao, kwa ajili ya kuchukua pesa alizokuwa nazo.

Soma pia: Bado hakuna mwafaka Mtwara

Matangazo

Kashfa mpya ya polisi Tanzania​

Siku chache kijana huyo aliachiwa na jeshi la polisi kwa dhamana na kurudi uraiani bila kurejeshewa fedha zake, ndipo January 5 mwaka huu akiwa na mjomba wake anayeitwa Salum Ng,ombo walikwenda kituoni hapo kwa ajili ya kufuatilia.

Soma pia : Polisi Tanzania yadai muuaji wa maafisa usalama alikuwa gaidi

Kufuatia tukio hilo, DW ilifika ofisi ya kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mtwara ACP Marck Njera ili kujuwa ukweli, ambapo amethibitisha kufanyika kwa mauaji hayo na kubainisha kuwa jeshi hilo limewakamata na kuwafikisha mahakamani Maafisa wa Polisi saba kwa tuhuma hizo za mauaji lakini amesita kutaja njia ya mauji iliyotumika na maofisa hao.

Amesema tukio hilo lilifanyika January 5, mwaka huu na mwili wa marehemu ulitupwa katika pori la kijiji cha Hiari wilaya ya Mtwara.
Kando na maofisa hao saba, afisa mwingine ambaye anadaiwa kuhusika na mauaji hayo ni mkaguzi msaidi wa polisi Greyson Mahembe anatajwa kujinyonga kwa tambala la kudekia akiwa mahabusu ya polisi mkoani hapa Source : Maafisa saba wa polisi Mtwara wafikishwa mahakamani | DW | 26.01.2022

Inatakiwa mtu akiingizwa ndani ya kituo chochote cha Polisi basi uhai wake uhakikishiwe pia hata mtuhumiwa akikamatwa nje ya kituo cha Polisi pia mfumo wa jeshi lazima unakili mara moja ktk mfumo wake kuwa kuna mtu amekamatwa. Hii itazuia jambo lolote lisilotarajiwa ktk utaratibu rasmi (wa PGO) kutotokea au mianya ya rushwa kuwepo, mahabusu / watuhumiwa kufichwa, kunyimwa haki ya dhamana n.k n.k

Sasa Ofisi ya makao makuu ya Polisi taifa pia Ofisi ya IGP inapaswa kuweka mfumo thabiti utaofuatilia na kunakili (ku register) ukamataji nje ya kituo cha Polisi au ktk kituo cha Polisi na kutekeleza kazi kwa kufuata PGO na kuhusisha wajumbe wa nyumba kumi kumi na wana familia kuhusu kuwa mtu ktk eneo lao au makazi amekamatwa na Jeshi la Polisi .

CASE STUDY 2:
Vijana wakamatwa na Polisi eneo la Kariakoo Dar es Salaam,; Familia zalia wametoweka mikononi mwa Polisi, hawajui tuhuma zao wala walipo


TAHARUKI: Familia zilizopotelewa na ndugu zao watano katika mazingira ya kutatanisha tangu Desemba 26, 2021 maeneo ya Kariakoo ‘Kamata’ wamepanga kuonana na Waziri wa Mambo ya Ndani awasaidie.

Kwa mujibu wa familia hizo, wamefikia hatua hiyo baada ya kushindwa kupata msaada kutoka kwa Jeshi la Polisi tangu waliporipoti jambo hilo Desemba 27, 2021. Soma zaidi:
Waliopotea ni Tawfiq Mohamed, Self Swala, Edwin Kunambi, Hemed Abass na Rajabu Mdoe.

Badhi ya ndugu wa waliopotea walisema leo wanatarajia kufanya kikao cha pamoja ambacho ni maandalizi ya kwenda kumuona Waziri wa Mambo ya Ndani.

Naye Sylvia Quentin ambaye ni Mama mzazi wa Tawfiq Mohamed, alisema siku ya mwisho mmoja wao alituma ujumbe mfupi wa simu (sms) kuwa wamekamatwa eneo la Kariakoo wakiwa kwenye gari aina ya Toyota IST nyeusi na wanapelekwa Kituo Kikuu cha Polisi.

Alisema baada ya kupata taarifa hizo ndugu hao walianza kuwafuatilia, ikiwamo kuzunguka kwenye vituo vingine vya polisi bila mafanikio, ndipo walianza kuzungukia kwenye hospitali mbalimbali katika vyumba vya kuhifadhia maiti, hata hivyo hawajawapata ndugu zao.

Kamanda wa polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amekiri kupata taarifa hizo na kuongeza kuwa polisi kwamba wanaendelea kuchunguza na kuwatafuta.

“Hao watu walishafika na stori hizo nilishazisikia, waliniambia walikuwa watano, si kwamba kila anayepotea anakuwa amechukuliwa na Polisi na si kila anayepotea anakuwa amekufa, mara ngapi watoto wanapotea na baadaye wanaonekana? Kwa hiyo mtu akipotea utulivu unahitajika,” alisema.
 
Sirro aweza kuwa mpuuzi kwa kiwango fulani,ila hazuii nia nzuri ya maslahi bora kwa askari kama ipo kwa huyo rais wake.

Sirro amezungumza kama mwenye taaluma ya polisi chombo anachokiongoza,kwamba kama shida anayo yeye,apigwe yeye kwa namna yote.ila kuinyea taasisi nzima sio jambo salama.

Embu nieleze hao maofisa bora si wako kazini saa hii wakiugulia maumivu ya vichambo kama polisi wengine wasio waadilifu???
Acha kutetea upuuzi mkuu,ukosoaji hauwi vile unavyotaka wewe kiasi kwamba unaota vichambo sijui mioasho nk.

Afu Polisi hawajaanza leo kuzingua na watu kama sio wote hawana Imani na Polisi,hao polisi wamesimamia mauaji awamu iliyopita lazima wabadilishwe.
 
Aigipii anazifuata nyao za yule spika aliye sahaulika kwa bidii! Bado press mbili tu, ya kuomba msamaha, (“nimekosa mimi!”) na kung’atuka!
 
Mkuu ni sawa na wewe ukaombe ushauri kuhusu matatizo ya mkeo kwenye ndoa yenu kwa kijana fulani kisha akujibu simple tu,fukuza mke huyo asikusumbue.
Utagundua hajui vingi kuhusu ndoa.
IGP sio beki tatu kwamba humtaki unampa nauli,unaweza fukuza 7 ndani ya wiki,ukija shtuka ni mgomo baridi,tayari polisi wote hawakutaki.
Utasimamiwa na baba yako wa ubatizo ushinde uchaguzi[emoji1][emoji1]
Chawa wa mama hawezi kukuelewa
[emoji23][emoji23]

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Jana chui jike nae alisema akiwalalamikia police wanamjibu tu kuwa mbona hana imani na vyombo vyake vya usalama,Takukuru nao wakisemwa wananuna.
Nchi ngumu sana hii.
Mama aendee Kwa step wanaweza kuzira kufanya naye Kazi ikawa shuuli kwel
 
Back
Top Bottom