Uchaguzi 2020 Video: Polisi wakisindikiza msafara wa Lissu unaoshangiliwa na kupungiwa mikono na maelfu ya wananchi

Uchaguzi 2020 Video: Polisi wakisindikiza msafara wa Lissu unaoshangiliwa na kupungiwa mikono na maelfu ya wananchi

Hasira gani tena!?, huo ni moto wa magazeti. Mwisho wake ni jumanne wiki ijayo. Najua utarudi hapa na thread kibao huku umefura na ID tofauti tofauti.
Mlisema Chadema imekufa, ikapita
Mlisema lissu akifika airport dar, atafikia mikononi mwa polisi ikapita

Leo mnasema atakatwa na tume, nalolitapita
 
Hakika kuna Nguvu ya Mungu(Power of Nature) iliyo nyuma ya Lissu.
Mashetani mnachekesha sana. Watu wenyewe ni kidogo sana, halafu kusindikizwa na polisi nayo imekuwa issue, mbona hiyo ni hali ya kawaida tu, kila mgombea urais anapata kinga tena akiomba mpaka TISS wanamlinda. Nyie idiot sana. Mnapenda kukuza vitu vidogo vidogo
 
Lisu ameanza kampeni mapema kinyume na sheria za uchaguzi.
Ajitahidi kuzingatia sheria

Unafahamu kuwa yeye ni mwanasheria na amesema katika sheria zetu hakuna kitu kinaitwa kuanza kampeni mapema kwakuwa kampeni zinaanza baada ya kuidhinishwa wagombea na NEC sasa ukisema ameanza kampeni mapema kisheria yeye hajawa mgombea kwahiyo huwezi kusema anafanya kampeni wakati siyo hajaidhinishwa kuwa mgombea. Na kampeni inafanywa na mgombea. Hiyo lugha ni sahihi kwenye vyama siyo kwenye NEC haipo.
 
Mkuu atakayeapishwa ni JPM, mwaka 2015 tulibet nikawapiga ela nyingi, waliamini Lowassa atakuwa Rais, mwaka huu bado natafuta ajipendekeze akiamini Lissu anaweza kuwa Raisi. Iwe mvua iwe jua, Lissu hawezi kuwa Rais wa nchi hii, na soon pesa ya kampeni inakata.

Lowassa na kujiandaa kote September katikati 2015 alianza kuomba michango, Lissu hata pesa za uzinduzi wa kampeni sijui kama zitakuwepo. Hakuna mtu atakayewekeza kwa mtu ambaye tayari kashafeli.
Tutachanga kama tulivyowachangia kina Mbowe. Swali lingine tafadhali
 
Mungu alipanga mwisho wa CCM kwa namna ambayo akili ya mwanadamu haiwezi kuelewa kirahisi. Aliamua aje mtu mgeni kwenye chama (Magufuli) ambaye atawanyang'anya chama wakongwe (Makamba, Kinana, Kikwete, Membe nk) na kuingiza watu wake wapya (Bashiru, Makonda, Polepole).
Hawa wapya kwa namna yake watakivuruga chama na misingi yake kwa maagizo yake Mafufuli. Wataleta chuki na maovu kama utekaji (Mo Dewji, Roma ) na uuaaji (Ben Sanane, Azory Gwanda nk).

Halafu watamshambulia mmoja wa viongozi wa upinzani (Lissu) kwa risasi za bunduki ya vita lakini mtu huyo hatokufa. Nchi nzima itashangaa namna mtu huyo alivyoshambuliwa, kunyimwa matibabu, kunyang'anywa mshahara kisha kufukuzwa ubunge.

Wanaposhangaa hayo na kumhurumia ndiyo watataka awe Rais wao wa 2020-25
Mungu ana sababu kwa kila jambo. Mwisho wa CCM ni mwaka huu. Alilopanga Mungu Binadamu hawezi kubadilisha. Hata kama NEC itaiba kura na kumtangaza Maguduli, nguvu ya umma itamtoa tu Ikulu. Wananchi wamechoka maonezi, dhuluma, ukandamizaji, ubaguzi na dharau
2010 hadi 2015 wenzio walitoa hadi sadaka za shukrani kwa kusema Mungu alimuweka kikwete ccm ili ifie mkononi mwake

Jibu la kilichotokea muulize EL
 
Back
Top Bottom