Video | Serikali ya Djibouti yavunja mkataba na DP World kuhusu uendeshaji wa bandari ya Doraleh

Video | Serikali ya Djibouti yavunja mkataba na DP World kuhusu uendeshaji wa bandari ya Doraleh

Una IQ hafifu sana umesahau hata lengo la mjadala huu.
Unamkashifu mwenzako kwamba ana akili finyu ilhali umesahau ukweli kwamba kule Uingereza kampuni la DP World limesajiliwa kwa sheria za nchi ile na kuitwa DP World London Gateway. Huku kwetu hilo kampuni limesajiliwa lini kule BRELA na kupewa A CERTIFICATE OF COMLIANCE ?

Halafu ambalo hufahamu ni kwamba DP World kule Uingereza amepewa bandari moja tu ya London Gateway, bandari nyingine ambazo ziko kwenye mfumo wa PORT OF LONDON zinaendeshwa na mashirika mengine makubwa. Huku kwetu bandari zote kuanzia Mtwara hadi Tanga kapewa DP World. Hivi ninyi watu huwa mna akili gani hadi kukaza shingo kushabikia huu upumbavu ?​
 
Hiyo stori ni ya siku nyingi na Djibouti ameshashindwa kwenye mahakama ya kimataifa.
Na hapo ndhani ni kile kipengele Cha Kwa sababu yeyote Ile mkataba huu hautavunjwa na na pande zinazohusika na mkataba. Hiki kipo kwenye huu wa kwetu
 
Somaliland ni taifa huru liliingia kwenye Muungano kwa hiari yake tena bila maandishi na 18 may 1988 wakaamua hiari yao kujitoa kwenye muungano wewe Mtanganyika yako yamekushinda usiwaingilie Wasomali hao.
Kama Somaliland ni nchi huru kwanini Bunge la Somalia lilitupilia mbali mkataba na DP World ?
 
Huku kwetu hilo kampuni limesajiliwa lini kule BRELA na kupewa A CERTIFICATE OF COMLIANCE ?
Baada ya makubaliano haya ya awali mkataba utakaofuatia ni lazima DP World watajisajili Brela mbona hilo teyari limetolewa ufafanuzi.
 
Muhtsari
  • Serikali ya Djibouti yavunja Mkataba wa Bandari ya Doraleh na DP World
  • Sababu za kuvunja Mkataba ni kutokuwepo kwa maslahi kwa Taifa la Djibouti na rushwa iliyotolewa na mkuu wa bandari
  • Serikali ya Djibouti yaishtaki DP World kwa madai ya ukiukwaji wa Mkataba

Serikali ya Djibouti imeamua kuvunja mkataba wa uendeshaji wa bandari ya Doraleh iliyokuwa inasimamiwa na kampuni ya DP World kutoka Falme za Kiarabu. Hatua hii imefuatia uchunguzi uliofanywa na serikali hiyo uliobaini kuwa mkataba huo ulikuwa na masharti yasiyo na tija kwa taifa la Djibouti na ulikuwa umeingiwa kwa njia ya rushwa na aliyekuwa mkuu wa bandari.

Serikali ya Djibouti imesema kuwa imefungua kesi dhidi ya DP World kudai fidia na kurejesha mali zake zilizokuwa chini ya usimamizi wa kampuni hiyo. Serikali pia imesema kuwa itatafuta mshirika mpya wa kuendesha bandari hiyo muhimu kwa uchumi wa nchi hiyo na ukanda mzima.

Pia soma |
Huu upuuzi ndiyo kijambio mashungi anataka kutuingiza
 
Kama Somaliland ni nchi huru kwanini Bunge la Somalia lilitupilia mbali mkataba na DP World ?
Ugomvi kati ya Qatar na UAE ndio uliingia Mogadisho Qatar ikawa inatoa mishahara ya Raisi wa Somalia ili awachonganishe Wasomali lakini Qatar keshapewa bandari nyingine katulia kimya.

Wasomali ni tofauti sana na sisi.
 
Tutawanyonga, tutawafilisi na tutawapatiliza wana maovu ya baba zao hata kizazi cha nne cha watakaouza bandari zetu
Hiyo ndiyo dawa yao ...baada ya samia kugundua akubaliki na watanzania sasa anafanya chuki yake kutukomoa wabara
 
Kwanza Dp World iliwafanyia fever kuinunua P&O hiyo kampuni ilikuwa na ha hali mbaya.
Kwahio watu wenye hali mbaya ndio unawaleta hapa kama Case Study ?

Issue ni figisu za DP World; Umahili / Umakini wa UK au Uzuri wa hali / ubaya wa UK....; Nadhani tungeongelea Point moja baada ya nyingine...

Ubaya wa hali wa leo haimaanishi ndio ubaya wa kesho ila decisions mbaya / nzuri unazofanya leo matunda yake utayaona kesho (mazuri au otherwise) sasa malalamiko yao leo it might mean their deed was not that great....
 
Wewe ndio umeileta.
Nimeileta baada ya wewe kusema jamaa kama ni matapeli wangewatapeli UK; na mimi sikufanya ajizi nikakupa article moja what the average Joe's think about the above mentioned....
 
Back
Top Bottom