Video: Vijana wakamatwa kwa uchawi

Video: Vijana wakamatwa kwa uchawi

Unaamini hao watu, wanafanikiwa kuliko wewe na Mungu muweza wa yote wanaomwamini wanaishi kwenye lindi la umaskini?
Kufanikiwa wote wa Mungu na WA shetani wanafanikiwa hata wasioamini Mungu au shetani wanafanikiwa pia
 
Ni umasikini na ujinga, nieleze mara ngapi chief?

Na ukiona hiki ki post tu kuwa ni "maelezo yote" nikitaka tujadili kwa undani kabisa mambo ya matatizo ya saikolojia na utamaduni Afrika, kwa kuzama mpaka kwa John Mbiti na Jean-Paul Sartre tutaweza?

Huoni kuwa na wewe unarudi kule kule nilikokulalamikia kwenye utamaduni wa kutaka majibu mafupi, rahisi, ya mkato, kwenye maswali yanayotaka mazungunzo ya kina, ya kimantiki na yenye kuangalia mambo kwa muktadha mpana?

Naogopa kuzama kwenye maongezi ya kina kwa maana naona tayari kama ushanipa tahadhari ya "comments ziwe fupifupi".

Na hata hizo "comment fupi fupi" nilizoanza nazo kwa kusema hili ni tatizo la ujinga na umasikini, hazieleweki, zinahitaji maelezo zaidi.

Kwa hivyo comment zikiwa fupi hazieleweki, kwa sababu ni fupi zinahitaji maelezo marefu.

Comment zikiwa ndefu, naambiwa nielezee bila maelezo marefu.

Tutaelewana kweli hapa?
Hapa nimekuelewa mkuu.. lakin nafikiri hiz ni sehemu ya mila na desturi katika jamii nyingi za kiafrika. Sasa ina maana kwamba culture yetu haina maana kama haya ni sehemu yake kwa mtazamo wako
 
Mkuu,

Nikianzisha dini yangu na kujenga majengo ya hiyo dini, nikasema mimi ndiye Mungu muumba vyote, nikapata wafuasi, hayo majengo na kuwapo kwa wafuasi wa hiyo dini yangu vitanifanya mimi niwe kweli Mungu muumba vyote?
Itategemea na kipi unawalisha wafuaasi wako kwa kufanya miujiza wakuamini
 
Hapa nimekuelewa mkuu.. lakin nafikiri hiz ni sehemu ya mila na desturi katika jamii nyingi za kiafrika. Sasa ina maana kwamba culture yetu haina maana kama haya ni sehemu yake kwa mtazamo wako
Kuna good culture na bad culture hii hata kwa Mila za kiafrika inapingwa thus wanauwawa au kufukuzwa vijijini
 
Tuuangalie mambo kwa muktadha wa hadithi.

Kuna mtu alikuwa akiitwa bwana Msafiri aliishi kale , kabla ya sayansi na teknolojia kushika hatamu.

Bwana Msafiri alikuwa anataka kutoka Magogoni kwenda Kigamboni, aende sehemu inaitwa Mjimwema kuanzisha makao mapya sehemu yenye nafasi zaidi.

Sasa, alivyofika Magogoni, akakutana na maji. Akasema hapa siwezi kuogelea, itabidi nipate msaada wa wenyeji kuvuka kwa mtumbwi. Hakuna jinsi.

Akakubaliana na wenyeji wamsaidie avuke kwa mtumbwi kutoka Magogoni mpaka Kigamboni.

Baada ya kuvuka, wale wenyeji wakamwambia, ili uweze kusafiri kwa salama huko mbele, ambako hatukujui vizuri na unaweza kukutana na mto , inakubidi uuchukue huu mtumbwi uubebe. Ukikutana na mto mwingine, uweze kuvuka kwa mtumbwi. Hivyo tutakuuzia huu mtumbwi. Popote unapoenda, usiuache kamwe.

Bwana Msafiri akakubali. Akaununua ule mtumbwi, akaubeba. Mtumbwi ulikuwa mzito sana, na Msafiri hakujua kama huko mbele kutakuwa na mto mwingine au hakutakuwa na mto. Ila, akaona ni bora aubebe mtumbwi tu, kwa kuwa hawezi kubahatisha kwenye suala muhimu kama hili.

Baadaye akafika Mjimwema. Akajua kuwa baada ya kuvuka kuja Kigamboni, hapo mbele kuja Mjimwema hakuna mto. Akamaliza shughuli zake. Akapapenda Mjimwema na kuhamia huko.

Basi Msafiri akawa kila akitoka nyumbani kwake, lazima atoke na mtumbwi kaubeba, akawa anasafiri hivyo, miaka nenda, miaka rudi. Hata akirudia njia ambayo alishaijua na haina mto, aliamua kuubeba tu mtumbwi, maana alisema "Huwezi kujua, mambo yanaweza kubadilika, ni bora kuwa salama kwa kubeba mtumbwi".

Watu wakimuona wakawa wanamwambia, wewe bwana Msafiri, kwa nini unaubeba mtumbwi huu kila unapoenda? Shida yako nini?

Msafiri akiwajibu, "Huwezi kujua siku utakayohitaji kuvuka maji, hivyo ni bora ubebe mtumbwi".

Wale jirani zake Msafiri wakawa wanamcheka, wengine waliomhurumia wakawa wakimwambia, siku hizi kuna magari, kuna pantoni, kuna madaraja yamejengwa, inawezekana zamani ulivyokuja Kigamboni ulihitaji kutembea na mtumbwi, lakini, siku hizi huhitaji. Unaweza hata kupanga safari yako kwa kuangalia ramani kwenye mtandao, ukajua barabara zote utakazopita.

Msafiri alikuwa ni mtu mwenye kung'ang'ania alichokijua tangu utoto wake, hakutaka kubadilika, hakutaka kujifunza mambo mapya. Aling'ang'ania kutembea na mtumbwi wake popote alipokwenda. Alikataa hata kupanda gari akisema kuwa mtumbwi wake ni bora kuliko gari.

Matokeo yake, Msafiri alidhoofika sana kutokana na kutoweza kusafiri mbali, kutokana na kushindwa kufanya shughuli nyingi za kiuchumi. Kazi ya kubeba mtumbwi kila sehemu ilimfanya apate kibiongo. Zaidi, watoto walimcheka na kumjaza sonona. Kila alipoenda aliitwa kichaa. Yeye alijigamba kwamba yeye ni kati ya watu wa kwanza kukaa Mjimwema, na yeye ndiye mtunza utamaduni, na anaweza kutembea mbali huku kabeba mtumbwi wake bila ya msaada wa gari.

Baadaye Msafiri alikufa mapema kabla ya umri wa wastani wa kufariki, kwa sababu ya shurba za kubeba mtumbwi kila alipokwenda.

Wengi waliusema ujinga wake wa kutaka kubeba mtumbwi kila alipokwenda kuwa ni sababu kubwa iliyomtia umasikini na kifo cha mapema.

Waliobaki wakamtungia nyimbo na kumuandikia historia kukumbushana juu ya maisha ya Bwana Msafiri.
 
Wachawi wameshikwa na watu wanaamini 😂 😂

Kama wachawi kwanini wasipotee hapo kichawi?

Kwanini wote huwa wanashikwa chini hatujawahi kuwaona wakiwa huko juu angani?

Haya ni maigizo kama maigizo mengine yote. Hao vijana ni wahanga.

Hakuna uchawi ila kuna imani za kishirikina. Imani hizi zinatamalaki kwenye jamii za watu WAJINGA na MASKINI. Huwezi kuta habari kamaa hii Dar sehemu yenye watu wenye vipato vya kati na walioelimika let alone Ulaya. Inabidi uwe zwazwa first class kuamini uchawi upo na unafanya kazi.
 
Hapa nimekuelewa mkuu.. lakin nafikiri hiz ni sehemu ya mila na desturi katika jamii nyingi za kiafrika. Sasa ina maana kwamba culture yetu haina maana kama haya ni sehemu yake kwa mtazamo wako

Huko ndiko dunia nzima ilipotokea, si monopoly ya tamaduni za Africa. Ukisoma historia ya Ulaya kabla ya mwaka 1500 utaona imani za uchawi zilivyokuwa zimejikita huko. Kwa kiasi kikubwa kupitia imani za dini. Ni vigumu sana kutenganisha imani za dini nanimani za uchawi.

Lakini, wenzetu wamejiongeza. Wamesoma sayansi, wameondoa ujinga.

Sisi tunadanganyana kwamba tunasoma sayansi, lakini kiukweli hatujaikubali bado, tumeshikilia mambo ya tamaduni za kale za kabla ya sayansi.

Culture inabadilika mkuu.

Na culture inabadilika sana kwa kwenda na teknolojia.

Zamani kulikuwa na culture ya kutuma ujumbe kwa kutumia moshi na ngoma.

Watu wanachoma moto vifuu fulani vinatoa moshi wa aina fulani, kisha wanapiga ngoma ya mdundo fulani, watu mpaka kijiji cha sita wanajua kuwa kuna shughuli nyumbani kwa Chifu fulani, tena kwa mujibu wa ngoma na moshi watu watajua kuna mtoto kazaliwa, kuna sherehe ya ndoa, au kuna msiba.

Lakini teknolojia hafifu hii ilikuwa na changamoto nyingi, unaweza kuchoma kitu moshi uende juu, moshi ukapeperushwa na upepo usiende juu. Moshi hata ukienda juu utaonekana mpaka kijiji cha sita tu.

Sasa leo tumepata smartphone na internet, tunaweza kutuma message Whatsapp ikafika dunia nzima kwa dakika moja tu, bado tutegemee message za moshi na ngoma tu? Hususan kama message za moshi hazisomeki vizuri na za Whatsapp zinasomeka bila utata wowote popote?
 
Itategemea na kipi unawalisha wafuaasi wako kwa kufanya miujiza wakuamini
Kwa hiyo nikiwachezea mchezo wa karata tatu nikawaambia huu ni muujiza wangu Mungu muumba vyote, wakaniamini, hapo nitakuwa kweli Mungu muumba vyote?

Unaelewa kuwa kukiamini kitu kuwa ni kweli hakukifanyi kuwa kweli?

Vinginevyo wote tungejiaminisha sisi ni mabilionea wa US dollars, na kujiaminisha hivyo kungetufanya kweli tuwe mabilionea, unaelewa hilo?
 
Kuna msemo niliwahi kuusikia unasema "Siku hizi wachawi sio wazee".

Nadhani huo msemo unaendana na hili tukio la vijana hawa kushikiliwa na jeshi la Polisi kwa Uchawi.

ANGALIA VIDEO HAPA
View attachment 2887164

Nini maoni yako?

Written by Mjanja M1
Vijana wa Kiislam hao, jamani shule ni muhimu, hakuna shortcut maishani. Msiposoma shule haya ndiyo maisha halisi mtakayoishi.
 
Back
Top Bottom