Uchaguzi 2020 VIDEO: Wachambuzi wa siasa Kenya washangazwa na muundo wa uchaguzi wa Tanzania, wasema walitoka huko kitambo sana

Muundo wa NEC, na jinsi inavyopatikana, ni upuuzi wa hali ya juu. Hakuna mwenye akili timamu, hata shetani anayeweza kukiri kuwa muundo wa NEC ni sahihi. Ni ujinga wa hali ya juu.

Tukibahatika kumpata Rais mwenye akili nzuri, mwenye hekima, upeo na uelewa, ambaye hana roho ya shetani, hata bila kulalamikiwa, yeye mwenye atasema, sitaki muundo huu wa NEC maana unanifanya nionekane mjinga na shetani.

Ndiyo maana Mkapa baada ya kurudiwa na akili aliona aheri ajutie ujinga ule wa kuwa na NEC ya muundo ule. Mwisho akasema, angependa kuona tume iliyo huru. Na Mungu hakumpa nafasi hiyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siasa za Kenya ni za ubaguzi wa kikabila.

Kenya wapambane kwanza waondoe hili kabla ya wao kukosoa wengine.
Hizo siasa za ukabila ndiyo anazozipenda na kuzipalilia mgombea wa CCM. Hukumsikia anasema, nichagueni, mimi ni msukuma mwenzenu? Mgombea wako anazitamani sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
OK kama ni kweli hiyo ni mpya kwangu sikujua, ...
Sasa inatakiwa ujue Tanzania Ndio nchi pekee ambayo mgombea anachagua wasimamizi wa uchaguzi
Mimi sio mwana siasa wala Hua sipigi kura
Kwa akili ya kawaida simba na yanga wakicheza halafu kipa wa yanga awe Ndio muamuzi
Haileti maana
 
Nzuri kwenye maandishi.
Jaji mkuu CJ maraga alisema ana mamlaka ya kumtaka raisi kulivunja bunge, ila raisi kakataa na hakuna wa kumfanya chochote.
Hadi leo hii tunapozungumza Raisi na makamu wa raisi hawaelewani, jana polisi wameingia kanisani kupiga mabomu.
Bwana jela,

Umesoma katiba ya Kenya? Huwezi kuilinganisha na ya Tz. Ni nzuri mno!
 
Hiyo heshima imeanza lini? Jana tu huko kenya wameongia kanisani kupiga mabomu.
Hadi leo hii raisi na makamu wa raisi hawaelewani
 
Hapana kaka yangu Tanzania hakuna ukabila kabisa, ukabila upo Kenya

Pia nimesoma katiba ya kenya inamapungufu mengi kuliko ya Tanzania

Mimi sina chama ni Mzalendo
Inawezekana hujui hata ni vitu gani vinafanya katiba kuwa nzuri.

Nadhani ni miaka miwili iliyopita, ndipo ilipoelezwa na wataalam wa masuala ya katiba Africa kuwa katiba nzuri kabisa Afrika, ni Katiba ya Afrika Kusini, na inayofuatia ni Kenya, na kisha katiba ya Ghana.

Nyingine ni Botswana, Tunisia na Morocco.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio kweli kaka yangu Tanzania hakuna ukabila huo ni uwongo unatungwa kuchafua viongozi

Mimi sina chama
Hata mimi Sina Jama
Jaribu ku Google Dotto James utagundua ni mtoto wa dadake pombe
Na mengine fanya utafiti
Mpaka saaa bado hatujahidi ukabila kwa sababu kwa miaka 60 tulikua hatuna ukabila
Miaka mi5 hii bado haijakolea ila baadae utagundua
Sehemu za Kazi na biashara zitashikwa na wasukuma utaona tuombe uhai
Wachaga. Wahaya na wanyakyusa hakuna serikalini na biashara zao zinafilisiwa na TRA
 
Huko Kenya kila mtu ana ndevu anataka kuonekana Mbabe uchaguzi bado ila huo mtifuano mtu na Deputy wake hawaivi.

Sasa ndio mnataka hayo yake hapa Tanzania watu wanapoheshimiana NO WAY.

October 28 kura zote ni kwa JPM,

JPM ANATOSHA
CCM USHINDI NI JADI
 
Sasa inatakiwa ujue Tanzania Ndio nchi pekee ambayo mgombea anachagua wasimamizi wa uchaguzi
Mimi sio mwana siasa wala Hua sipigi kura
Kwa akili ya kawaida simba na yanga wakicheza halafu kipa wa yanga awe Ndio muamuzi
Haileti maana


Hata kama ni hivyo hakuna ushahidi kwamba hao wanaofanya vingine njia yao ni bora zaidi, mfano hao Kenya wenyewe mnaowasifia anayeshindwa hajawahi kukubali kushindwa hata siku moja, kwanza hata Tume yenyewe wanaikataa na kusema haiko huru wakati haiteuliwi na Raisi, sasa tofauti iko wapi?
 
Hapana kaka yangu huo ni uwongo unatungwa kuchafua viongozi

Ila kusema ukweli Rais Magufuli anapendwa sana jamani
 
Pale Kenya sasa hivi ni kama hamna mkubwa! Kila mtu ni kambare! Wamejaa ukabila, hayo ndio waliyoendelea hakuna kingine.

Fikiria uchaguzi bado miaka 2 lakini ofisi ya rais Kenyata ina mgogoro wa kugombea madaraka ya 2022
Wanashangaa nini hawa? Wapambane na corona yao
 
Hapana kaka yangu Tanzania hakuna ukabila kabisa, ukabila upo Kenya

Pia nimesoma katiba ya kenya inamapungufu mengi kuliko ya Tanzania

Mimi sina chama ni Mzalendo
Una uhakika Tanzania hakuna ukabila? Angalia jpma alivyojaza wasukuma serikalini CDF, mkurugenzi wa pccb, doto James na mawazili kibao
 
Sasa huoni kama ni wajinga kuchaguana kikabila? Ukabila una nafasi gani karne hii?
Ndio mambo ya kuiga toka Kenya hayo?
 
Nimesoma kaka ile katiba ya kenya imejaa ubaguzi wa kabila
Yetu imejaa ubaguzi wa kukipendelea chama kilichopo madarakani kiendelee kubaki madarakani. Ukiambiwa utaje kifungu kinachopendelea au kubagua makabila huwezi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…