Uchaguzi 2020 VIDEO: Wachambuzi wa siasa Kenya washangazwa na muundo wa uchaguzi wa Tanzania, wasema walitoka huko kitambo sana

Uchaguzi 2020 VIDEO: Wachambuzi wa siasa Kenya washangazwa na muundo wa uchaguzi wa Tanzania, wasema walitoka huko kitambo sana

Hapana kaka yangu Tanzania hakuna ukabila kabisa, ukabila upo Kenya

Pia nimesoma katiba ya kenya inamapungufu mengi kuliko ya Tanzania

Mimi sina chama ni Mzalendo
Ni kweli ukabila ni tatizo Kenya . Lakini pia ukabila ni tatizo hapa Tanzania . Labda kidogo mijini watu hawajali ukabila. Lakini nje ya miji mikubwa ukabila ni tatizo .

Tukirudi kwenye hoja yao, ni ya msingi . Ukiwapinga ni mpungufu wa akili. Katiba yetu ina mapungufu sana na uelekeo wake ni wa ki communist. Wa kumsifu na kumuabudu kiongozi hata pale anapotenda majukumu yake ya kikatiba. Na kama si kiongozi basi ukitukuze chama tawala hata kama sera zao haziwezi kuisaidia nchi . Mfano ni Korea kaskazini.

Huwezi kuwa na tume ya aina hii karne hii labda Tanzania tu.
 
Pale Kenya sasa hivi ni kama hamna mkubwa! Kila mtu ni kambare! Wamejaa ukabila, hayo ndio waliyoendelea hakuna kingine.

Fikiria uchaguzi bado miaka 2 lakini ofisi ya rais Kenyata ina mgogoro wa kugombea madaraka ya 2022
Mkuu jadili hoja. Simba na Yanga zinakutana uwanjani referi, kibendela na kamisaa na uwanja vyote ni vya Simba, Yanga atakuwa na chake? Hiyo ndo hoja.
 
Hivi wewe ni kwamba hauna akili au? Mpaka leo watu watatu wameshalala kaburini kutokana na uchaguzi au hujui?


Kenya maelfu kwa maelfu wanauliwa kila uchwao, hao watatu wa kwetu kama ni kweli Mungu awarehemu kila pumzi ina thamani, isitoshe hao Wakenya wako kila anayeshindwa Uchaguzi anaikataa Tume ambayo wanasema iko huru, Raila mpka leo hajakubali kama alishindwa kihalali anasema aliibiwa kura na ,, Tume huru'' haikumtangaza alienda kuapishwa ingawaje alishindwa Uchaguzi sasa wanatuambia nini?
 
Lakini bado wanakataa matokeo ya uchaguzi na anayeshindwa kusema ameibiwa kura, na kuanza kuuwa watu hovyo, TZ yetu hakuna aliyeuliwa sababu ya Uchaguzi.

Low IQ!
Mkapa amekiri kuu watu kutoka na uchaguzi,wewe mburula unasema hakuna.
 
Hapana kaka yangu Tanzania hakuna ukabila kabisa, ukabila upo Kenya

Pia nimesoma katiba ya kenya inamapungufu mengi kuliko ya Tanzania

Mimi sina chama ni Mzalendo
Hapa ndiyo kuna ukabila sasa. 2016 wakuu wa mikoa 26, lakini 13 walikuwa wa kabila moja !!. Fanya utafiti ndiyo ukane .
 
Mkapa katika kitabu chake alikiri kua serikali yake iliua watu wengi baada ya uchaguzi 2001
Sasa wewe ni nani unampinga watu hawajafa kwa uchaguzi?


OK kama ni kweli hiyo ni mpya kwangu sikujua, ...
 
Pale Kenya sasa hivi ni kama hamna mkubwa! Kila mtu ni kambare! Wamejaa ukabila, hayo ndio waliyoendelea hakuna kingine.

Fikiria uchaguzi bado miaka 2 lakini ofisi ya rais Kenyata ina mgogoro wa kugombea madaraka ya 2022
Usilinganishe demokrasia iliyoko Kenya na ujinga unaofanyika hapa Tanzania, tatizo mnajifanya wajuaji lkn machoni pa dunia mnaonekana wajinga flani tu.
 
Ni kweli ukabila ni tatizo Kenya . Lakini pia ukabila ni tatizo hapa Tanzania . Labda kidogo mijini watu hawajali ukabila. Lakini nje ya miji mikubwa ukabila ni tatizo .

Tukirudi kwenye hoja yao, ni ya msingi . Ukiwapinga ni mpungufu wa akili. Katiba yetu ina mapungufu sana na uelekeo wake ni wa ki communist. Wa kumsifu na kumuabudu kiongozi hata pale anapotenda majukumu yake ya kikatiba. Na kama si kiongozi basi ukitukuze chama tawala hata kama sera zao haziwezi kuisaidia nchi . Mfano ni Korea kaskazini.

Huwezi kuwa na tume ya aina hii karne hii labda Tanzania tu.
Hao nyang'au watawadanganya makamanda uchwara tu.
 
Hapana kaka yangu Tanzania hakuna ukabila kabisa, ukabila upo Kenya

Pia nimesoma katiba ya kenya inamapungufu mengi kuliko ya Tanzania

Mimi sina chama ni Mzalendo
Tanzania Asili yetu hatuna ukabila ila kuanzia 2015 mambo yamebadilika
Mshika funguo za hazina ya Tanzania nzima ni mtoto wa dadake Pombe
Mwenyekupewa kandarasi bila zabuni za serikali ni mume mwenza
60%ya wateuliwa ni kabila moja mkuu wa majeshi. Na majeshi mengine kabila lile lile
Anyway miaka mitano inayo Kuja kama tukiendelea hivi Tanzania itajikuta pabaya
Hakuna makabila ya kaskazini serikalini ila wawe kada wa chama
Wafanyabiashara wa maeneo fulani wamefilisiwa
Fanya utafiti utagundua hekma ya Nyerere kwa makabila makubwa
 
Sio kweli kaka yangu Tanzania hakuna ukabila huo ni uwongo unatungwa kuchafua viongozi

Mimi sina chama
Tanzania Asili yetu hatuna ukabila ila kuanzia 2015 mambo yamebadilika
Mshika funguo za hazina ya Tanzania nzima ni mtoto wa dadake Pombe
Mwenyekupewa kandarasi bila zabuni za serikali ni mume mwenza
60%ya wateuliwa ni kabila moja mkuu wa majeshi. Na majeshi mengine kabila lile lile
Anyway miaka mitano inayo Kuja kama tukiendelea hivi Tanzania itajikuta pabaya
Hakuna makabila ya kaskazini serikalini ila wawe kada wa chama
Wafanyabiashara wa maeneo fulani wamefilisiwa
Fanya utafiti utagundua hekma ya Nyerere kwa makabila makubwa
 
Back
Top Bottom