DOKEZO VIDEO: Wazazi angalieni Walimu Shule ya Sekondari Majaliwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Huyo mwalimu aliyekutumia badala ya kuchukua hatua kwanza na yeye ni mpumbavu tu.
Walimu hawajitambui.Kama huyu mwalimu aliye mrecord mwenzake, kama alikuwa Hana Kazi angeenda nyumbani kulisha kuku.
 
Akamatwe aliyerekodi video hii mara moja!! Kwanza ni mchochezi pili siioni shida Kwa mwanafunzi kuadhibiwa kisha akaendelea na shule kuliko kufukuzwa, haya ni majungu kudadqdeki!!
 
Sasa nimeamini adui namba 1 wa mwalimu, ni mwalimu mwenzake. Sijaona mantiki ya kurekodi hizo videos na kuziweka mtandaoni.

Ilikuwa ni rahisi tu kwa mwalimu kumshauri mwalimu mwenzake kuacha kutoa adhabu iliyopitiliza kwa mwanafunzi. Na kama hashauriki, bado kuna uongozi wa shule! Vikao vya staff, nk. Ifikie wakati baadhi ya walimu waache mambo ya kitoto.
 
Sasa wasiporekodi hilo tukio litafikaje kwa Waziri Mkuu? Kama ni kuchapwa kwa ukatili, itakuwa walishachapwa sana tu, hii sio mara ya kwanza. Na huenda alishawaonya, hawaonyeki na alishapeleka tarifa hadi kwa Afisa Elimu, hatua hazijachukuliwa. Wewe ulitaka afanyeje? Hata kama ni kumuonya au kumshauri aache tabia ya kuwachapa wanafunzi, utadhani atakuwa naye kama bodigadi wakati wote ili siku nyingine akitaka kuchapa amnyanganye fimbo? Acha hizo mkuu. Hapa JF ni mass media itamfikia kila mtu, hadi Rais Samia ataona.

Kurekodi ni vizuri kwa kuwa ukimwambia mtu kwa maneno anaweza asiamini. Kuona ni kuamini. Acha kulialia mkuu. Subiri serikali ione, ichukue hatua.
 
Walimu hawajitambui.Kama huyu mwalimu aliye mrecord mwenzake, kama alikuwa Hana Kazi angeenda nyumbani kulisha kuku.
Lazima uhuni urekodiwe.

Na ikibidi mfukuzwe kazi tuajiri watu wengine wenye maadili.

Tuna rizevu ya walimu zaidi ya AFTATU mtaani ambao hawana kazi.
 
Swadakta......
 
Sasa nimeamini adui namba 1 wa mwalimu, ni mwalimu mwenzake. Sijaona mantiki ya kurekodi hizo videos na kuziweka mtandaoni..[/I]

Kwahiyo ulitaka wasirekodi ili muendelee kuumiza watoto!?

Tate mwaka huu lazima ufukuzwe kazi!!!

Samia hataki uhuni mashuleni!
 
We fala Sana wewe, watoto wa huko kusini wanapenda shule? Mwalimu akilegeza Tu, wote wanapata maziro Acha kupost post ujinga, na utakamatwa tu
 
Kwahiyo ulitaka wasirekodi ili muendelee kuumiza watoto!?

Tate mwaka huu lazima ufukuzwe kazi!!!

Samia hataki uhuni mashuleni!
Watoto wa shule za kata ni wasumbufu sana. Walimu wanatakiwa kuishi na hao watoto kwa tahadhari kubwa. Na wakati huo huo mashinikizo ya kulazimisha wafaulu, hata kama hawataki shule, wana uwezo mdogo wa kuyamudu masomo! hutamalaki kila upande.

Mzazi kama una uwezo, na mtoto wako anajitambua; ni bora umpeleke tu shule za private. Binafsi sijutii kuwasomesha watoto wangu shule za private. Shule za kata zimejaa watoto wengi wasumbufu, watukutu, wasiojitambua, nk. huku wale wastaarabu na wanaojielewa wakibakia kuwa wachache.
 
Acha wasichapwe ili matako yakutwe fresh!

Hawa mawaziri na walioliongoza hili taifa kufikia tulipo,wote tulichapwa hivyo.

Walimu sio wehu kuchapa watoto bila sababu!

Tunakuza taifa la kishoga kwa kuulea upimbavu eti kisa haki za Binadamu!

Halafu tunazalisha Panya Road kila uchao.
 
Elimu sio kwa ajili ya kila mtu.

Wasiofundishika achana nao, na sio kuwapa vipigo vya kikatili.

Ukifanya hivyo tutakushughulikia na kazi utapoteza.

Bora lipi?
 
Tunakuza taifa la kishoga kwa kuulea upimbavu eti kisa haki za Binadamu!

Halafu tunazalisha Panya Road kila uchao.
Unajifanya una uchungu na maadili mwenyewe!

We umiza mtoto wa mtu ushughulikiwe na hata hicho kibarua utapoteza pia.

Ukijifanya mjuzi utashughulikiwa tu.

Fanya yanayokuhusu, mengine achana nayo. FUNDISHA, RUDI NYUMBANI.

Usijifanye polisi wa maadili utajiponza. Hakuna aliyewahi kufanikiwa katika hilo.
 

Kwaiyo mbadala wa kutoa usumbufu kwa watoto ndo kuwapiga kama wanaua nyoka? Waalimu wanatengeneza kizazi cha watu makatili….nimesoma shule ya kata tulikua tunapigwa mpaka wanafunzi wengine waliacha shule kwasababu ya kupigwa kama hivo [emoji174]

Na kuhusu swala la uwezo wa kuyamudu masomo sometimes ni juhudi za mwalimu husika wa somo na siku hizi walimu mwenyewe hawana huo ueledi wanaitisha tu hela za tuition usipolipia ndo imekula kwako.
 
Elimu sio kwa ajili ya kila mtu.

Wasiofundishika achana nao, na sio kuwapa vipigo vya kikatili.

Ukifanya hivyo tutakushughulikia na kazi utapoteza.

Bora lipi?
Huenda mabadiliko ya mitaala yakianza kutumika katika shule zetu, huenda yakazaa matunda.

Watoto wenye uwezo wa wastani na ule hafifu wakipelekwa kwenye vyuo vya VETA, badala ya sekondari; itasaidia kupunguza kizazi cha wanafunzi wanaosoma shule kwa kulazimishwa, na mwisho wa siku kuingia katika vita na baadhi ya walimu wenye msongo wa mawazo.
 
Yes, hii ni nzurii zaidii.
 
Acha warekodi tuone uozo wao, walimu ni mafala sana, nawachukia zaidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…