Vifo vya Samaki Mto Mara: Kamati ya Dharura yaundwa kuchunguza Samaki wanaodaiwa kufa kwa Sumu

Vifo vya Samaki Mto Mara: Kamati ya Dharura yaundwa kuchunguza Samaki wanaodaiwa kufa kwa Sumu

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Tuweke mzigo mezani

Ndugu zangu kuna hii taarifa, yupo yeyote ambaye anajua ukweli wake, maana mtu ambaye yupo ndani mgodini amenitumia ujumbe huu ambao nimeambatanisha na picha alizotuma:

BARRICK NORTH MARA YAFUNGULIA MAJI YA SUMU NA KUTEKETEZA SAMAKI MTO MARA

Jitihada zimefanyika ili kujua ukweli wa hii habari. Ametafutwa mmoja wa ‘supervisor’ katika Mgodi wa Barrick North Mara, Elly Shimbi na kuulizwa kuhusu ukweli wa taarifa hiyo alisema:

“Mimi siwezi kulizungumzia hilo suala, mtafute msimamizi mkuu wa mradi ndiye atakwambia, kama una taarifa hizo mimi siwezi kukwambia chochote.”

Elly Shimbi hakutoa ushirikiano wa mawasiliano ya mkuu wake wa kazi ambaye alitaka atafutwe yeye kuhusu suala hilo.

Licha ya kutotoa ushirikiano huo, Ofisi ya Barrick iliyopo Dar es Salaam ilithibitisha kuwa Shimbi ni mmoja wa ‘supervisor’ ambaye bado yupo kwenye majukumu yake Barrick North Mara.

Tayari bosi ambaye ndiye msimamizi wa mgodi huo ametumiwa taarifa hii kwa njia ya e-mail baada ya namba yake kutopatikana lakini haijajibiwa.

======

Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Eng. Samuel Gwamaka Mafwenga, ameiambia JamiiForums leo tarehe 10/03/2022 kwamba, kutokana na taharuki iliyotokea baada ya Picha za Samaki waliokufa kusambaa Mitandaoni wanaodaiwa ni kwenye Mto Mara, tayari timu ya Dharura imeundwa kuchunguza swala hilo.

Mafwenga amesema timu hiyo inahusisha Watu kutoka NEMC, Bonde la maji la Ziwa Victoria, Mkemia Mkuu wa Serikali na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mara.

"Hivi sasa tunapozungumza, tayari Kamati ipo Sehemu ya tukio Wakichunguza ili tujue chanzo ni nini na kimetoka wapi. Sisi tunaangalia afya na Uhai wa Binadamu na Wanyama." amesema Mafwenga.

Pia soma ;
1). Madai ya sumu Mto Mara kutoka migodini, wananchi wazuiwa kutumia maji, kula samaki, uvuvi, Serikali yatoa tamko

2). Eti, "Kinyesi cha mifugo chatajwa kuwa chanzo cha kufa samaki mto Mara"

3). Madai ya sumu Mto Mara kutoka migodini, wananchi wazuiwa kutumia maji, kula samaki, uvuvi, Serikali yatoa tamko

8a976eba-3638-45be-a15f-0624dc6efea0.jpg


57f5ad54-c8ef-4ca4-8bfd-01b11ce1fe26.jpg


5295ccb2-3208-4016-92a3-0e8fa4a09782.jpg


0301c4a6-95d6-41b8-b656-285a7d1c56c3.jpg

efb33292-ab5d-406a-b7bc-17ac916e04d7.jpg
 
Watanzania huwa hatutaki serikali inayosimia sheria, itabidi tuendelee na maisha tiliyo nayo. Angewapo yule jamaa, ni wazi kuwa Sinclair angepanda ndege binasfi kwenda Dodoma kuomba "Mea Culpa, mea Culpa, mea Maxima Culpa". Barrick wangetoa pesa za kusafisha sumu hiyo.
 
Tuweke mzigo mezani

Ndugu zangu kuna hii taarifa, kuna yeyote ambaye anajua ukweli wake, maana kuna mtu ambaye yupo ndani mgodini amenitumia ujumbe huu ambao nimeambatanisha na picha alizotuma:

BARRICK NORTH MARA YAFUNGULIA MAJI YA SUMU NA KUTEKETEZA SAMAKI MTO MARA

=====

Jitihada zimefanyika ili kujua ukweli wa hii habari. Ametafutwa mmoja wa ‘supervisor’ katika Mgodi wa Barrick North Mara, Elly Shimbi na kuulizwa kuhusu ukweli wa taarifa hiyo alisema:

“Mimi siwezi kulizungumzia hilo suala, mtafute msimamizi mkuu wa mradi ndiye atakwambia, kama una taarifa hizo mimi siwezi kukwambia chochote.”

Elly Shimbi hakutoa ushirikiano wa mawasiliano ya mkuu wake wa kazi ambaye alitaka atafutwe yeye kuhusu suala hilo.

Licha ya kutotoa ushirikiano huo, Ofisi ya Barrick iliyopo Dar es Salaam ilithibitisha kuwa Shimbi ni mmoja wa ‘supervisor’ ambaye bado yupo kwenye majukumu yake Barrick North Mara.

Tayari bosi ambaye ndiye msimamizi wa mgodi huo ametumiwa taarifa hii kwa njia ya e-mail baada ya namba yake kutopatikana lakini haijajibiwa.

View attachment 2145795

View attachment 2145796

View attachment 2145797

View attachment 2145812
View attachment 2145816
Where's NEMC? Huu mgodi miaka yote umekuwa unaripotiwa kumwaga sumu mara kadhaa Ila hatuoni kama kuna hatua zinachukuliwa.
 
Okay.....
Kwenye ule mgodi maji hutiririka kutoka kwenye kifusi madini kinachoitwa Puff, kisha maji yanaelekezwa kwenye one of the water treatment pond. Kisha yale maji yanatibiwa na baadae watu (kitengo) cha maabara huchukua sampuli na baada ya kujiridhisha kwamba maji hayana sumu, basi maji yale huelekezwa kwenye mto Tigite ambao mto huelekeza maji kule mto Mara hadi lake Victoria.

Anyway......
Kama hiyo itakua na ukweli (sijathibitisha) basi hapo maanayake kuna mmoja kati ya wafanyakazi hakuwajibika mujarab.
Na huyo dogo Shimbi mnapo msema hatoi ushirikiano "binafsi nadhani mnamuonea ama mnamlazimisha ajibu tuhuma ambazo hazimuhusu".

Shimbi yupo kwenye kitengo cha usalama na mafunzo, wakati hiyo issue ipo chini ya watu wa mazingira".

Kwaleo naomba niishie hapo
 
Huu ni uongo ukijumuisha na figisu figisu……..,
Mleta uzi ebu tuambie ni aina gani ya sumu walio ifungulia hao ‘mabeberu’ ???
 
Kiukweli inauma na kusikitisha sana, mimi nimeyashuhudia hayo kwenye baadhi ya migodi ya wachimbaji wadogo kanda ya ziwa na upo uzi humu niliandika, mamlaka za Serikali wekeni nguvu za kutosha katika migodi ili kulinda mazingira na afya za watu, Mimi baada ya kwenda na kujionea hali, kwa sasa samaki aliyevuliwa ziwa victoria na mito yake naogopa kumtumia kabisa.
 
Back
Top Bottom