Vigogo na Watoto wa Vigogo wana mitaji lakini mbona hawajiajiri?

Vigogo na Watoto wa Vigogo wana mitaji lakini mbona hawajiajiri?

Na huyo :Richa" ni mtoto wa "kigogo" pia?

Itakuwa hujawaona watoto wa Kinondoni, umezowea kuwaona wa kigogo wenzako tu.

Vipi wewe, wanakupiga hao watoto wa kigogo?
Yaani Faiza, sisi wengine tumezaliwa kaskazini huko hatuwezi kutofautisha R na L sometimes.
 
Kwanza nikiri watoto wa vigogo wengi wamesoma sana na wana bidii sana kwenye masomo.

Zamani niliaminishwa vijijini kwamba watoto wa matajiri hawapendi shule na kwamba huwa wanafeli.

Baada ya kusogea mbele ki elimu nikahama mkoa niliokuwa naishi huko vijijini nilikutana na ulimwengu wa tofautu kabisa.

Watoto wa vigogo yaani RC, DC, DAS, Ma generali wa jeshi, Wakurugenzi wa Tasis za serikali kama BOT, NSSF, PSSF, TPDC, TANESCo, bila kusahau watoto wa wenyeviti na makatibu wa ccm ngazi mbali mbali Taifa, mkoa na wilaya niligundua wako serious sana na masomo na ni vichwa sana.

Wanajituma kusoma na wana sapoti nzuri kutoka kwa wazazi wao ikiwemo pesa na matumizi mengine ya kujikimu.

Ilikuwa ni jambo la kawaida mtoto wa kigogo kukuta ana akiba ya pesa kuanzia Laki moja kwenda mbele huku tukiwa Boarding school na kila kitu nakula hapo hapo.

Hali ile nilijua inawapa sana motisha watoto wao kusoma na kutokata tamaa. Na wengi waliongoza kwa ufaulu darasani. Ikitokea mtoto wa kabwela amefaulu kuwazidi basi inakuwa kwa uchache sana.

Richa ya hayo yoote bado linapokuja swala la ajira watoto wa vigogo wenye utajiri na mitaji hatuoni wakijiajiri badala yake Wazazi wao wanapigana vikumbo kuhakikisha watoto wao wanapata nafasi za ajira serikalini.

Majaji, wabunge na mawaziri ndio hivyo hivyo.

Huku wakiwambia watoto wa kabwela kuwa kuajiriwa ni umaskini na kujiajiri ndio mpango mzima.

Je tunapigwa?
Mkuu hawa wana jiajiri na bado wako kwenye hizo nafasi nyeti..

Kwa ufupi wanapiga zote zote kujiajir na kuajiriwa
 
Kwa uzoefu wangu hawa jamaa wana miradi mingi kuliko makabwela.

Angalia wamiliki wa sheli, mabasi ya mikoani, hisa kwenye makampuni makubwa, viwanda vya kati, wachimbaji/wafanyabiashara wa madini, wamiliki wa maroli, shule na vyuo binafsi,mashamba makubwa na makampuni ya ujenzi bila kusahau real estate business.

Hizo business zote wamejaa wanasiasa, viongozi wakubwa wa umma na mabalozi wetu. Lakini pamoja na kumiliki vyote hivyo hawaachi ajira zao. Kwa nini?

Simply kwa sababu zina maslahi makubwa na zina mianya ya kuiba pesa za umma au kufuja kwa kutumia madaraka yao ( kuchota ). Wanaishi bila wasiwasi na biashara zao nyingi zinaenda vema kwa kukwepa kodi na magumashi nyingi.

Wanaposema watoto wa masikini wajiajiri bila kuwa na mitaji ina maana hizi biashara za uchuuzi, kuwa machinga, au duka la mangi. Kama ni kilimo basi ni kile cha bustani.

Hata hivyo hakuna haja ya kulalamika maana bado jamii ya wajinga ni wengi Tanzania ambao hawaoni umuhimu wa katiba mpya na tume huru ya uchaguzi. Maana katiba iliyopo inaendelea kuwapa wenye nchi fursa nzuri na watoto wa masikini wataendelea kuisoma namba.
 
Nafasi wanazopiganiwa na baba zao serikalini ni zile za mishahara minono na ya upigaji pesa. Hizo kazi mtu kuongiza milion 10 kwa mwezi ni kawaida (salary plus wizi).

Sio hizo za halmashauri. Ndo tofauti iliopo
 
Nafasi wanazopiganiwa na baba zao serikalini ni zile za mishahara minono na ya upigaji pesa. Hizo kazi mtu kuongiza milion 10 kwa mwezi ni kawaida (salary plus wizi).

Sio hizo za halmashauri. Ndo tofauti iliopo
Aisee kumbe wanajua
 
Hata hivyo hakuna haja ya kulalamika maana bado jamii ya wajinga ni wengi Tanzania ambao hawaoni umuhimu wa katiba mpya na tume huru ya uchaguzi. Maana katiba iliyopo inaendelea kuwapa wenye nchi fursa nzuri na watoto wa masikini wataendelea kuisoma namba.
Hili nalo neno Mkuu
 
Back
Top Bottom