Vijana mliopo A-level: Technique rahisi nilizotumia kupiga Division One ya 3 form six bila kukesha darasani

Vijana mliopo A-level: Technique rahisi nilizotumia kupiga Division One ya 3 form six bila kukesha darasani

kwenye miti hakuna wajenzi.. yaani na ma AAA yako yote umeishia kuajiriwa serikalini kwa mshahara wa hazina... ma scholarship yote yaliyojaa duniani umeyaacha unahangaika na forex na mwisho wa siku unatapeliwa na wadogo zako kina ontario...

wahuni wana div 3 za mwisho tena za HKL ila ajira za maana kwenye mabalozi.. au wanajiajiri wenyewe wanagombania tenda na kupiga hela..

nashangaaga sana best students kuwaona udsm... ukikomaa kweli kweli na ukawa na washauri sahihi unatembea mapema sana.. bongo nyoso
mkuu maisha ni machaguo,kufauli haimanishi uwe na hela nyingi mbeleni la hasha yawezekana maono yake ni kuwasaidia watanzania wenzake kupitia kuajiliwa serikalini analifanikisha hilo
 
anafikiri AAA za physics ukienda nazo dukani unapewa unga,,, au unanunua gari kwa cheti cha AAA huku ni maujanja ujanja tu.. mwisho wa siku dogo ontario kamtapeli hela zake pamoja na AAA zake.. huo ndio mtaaa sasa
Kumbe alitapeliwa!
 
Haki ya nani, nilipoona maelezo yako haya imebidi nirudie kumsoma tena Engineer ili nione mahali aliposema "kaajiriwa na serikali"; Walahi sijapaona, eti ni wapi!?

sisi wapemba tunajuana kwa vilemba.. ndio maana hajaja kupinga.. huyu tunajuana toka miaka mingi enzi za forex ni biashara ambayo benk haitaki ujue
 
Kuna jamaa tulikuwa naye PCM aisee balaa; tangu form five sikuwahi kuona anaandika notice; yeye alikuwa na makaratasi tu anaandika mambo yake mwingine huelewi kitu. Hasomi kazi yake ni kuzunguka kwa room za wenzake kupiga soga. Ukishidwa swali nenda kwake anaku solvia fastaa ka machine; jamaa aliondoka na point tatu.

Akili inatokana na genetic ya ukoo; hizi zetu za kuungaungaa aisee unahangaika sana.
ahhahahhaha jamaa angu m1 alikua anasemaga hesabu zinafataga ukoo..af mbaya zaid ukoo wao aziwataki
 
kaka heshima kwako.. umeongea point tupu... humu tunaponda sababu huyu engineer ana dharau sana.. alitutukana sana zama za forex.. sasa amepigwa na dogo ontario.. na sisi zamu yetu kumueleza ukweli... hajui ku reason ndio maana ana maisha magumu.. alishawai kupanga hadi kuzitapeli benk huyu huyu engineer vyeti tu... kuchwan hamna kitu ukiongelea elimu ya mtaa

Uzi huu umenizibitishia ambavyo hekima bila noti, uishia kuzalauliana.

Mleta mada, kwa namna yoyote ile ni kijana smart upstairs.

Kwa nchi za wenzetu vipaji Kama hivi ni lulu na ni asset kubwa na utazamawa kwa jicho la hekima hata kama hana hela.

Ubora wa mtu hauko kwenye uwezo wa kuwa na gari kali au kuishi kwenye mjengo wa maaana

Context za maisha yetu hutofautiana, likewise hata destiny za maisha yetu

Siku za hivi karibuni kuna watu wanaojiita wana elimu ya kitaa na wana make bingo ya maana, hali inayopelekea hata just discourage wasomi.

Kwa bahati nzuri kundi hili ukiri wao ni watu wa mishe, frankly speaking wengi ni watu wasio heshimu maadili, kila aina ya dili regardless itamtaka kuiba, kuua, na hata kufanya ushenzi wowote kisa atapata fedha, yeye ajali kitu. Kinachoangaliwa ni pesa


Vijana smart, wengi walijikuta kwenye mfumo rasmi huu wa kibongo, wamejikuta trapped na mfumo usiojari vipaji na uwezo wa watu katika utumishi na kujikuta ujira wao unapangwa kwa ngazi za mishahara na pengine pasipo kuzingatia ufanisi wao. Ndo maana haishangazi TO anaefanya kazi katika almashauri X kuzidiwa maisha na kilaza mmoja aliajiriwa kwa mchongo wa mjomba BOT Kama afsa manunuzi, lakini ana opportunity kibao za 10 percent kwenye denda za wizara.

Huyu kilaza mtaani ataheshimika sana kuliko smart mind aliyeko almashauri akipigika kusubiri fedha ya OC ili alipwe overtime.

Issues kama hizi zinanilazimisha kuamini tunahitaji kutathimini value of our life. Lazima tuheshimiane kwa kile tunavyoweza ongeza value kwenye maisha ya watu.

Haijalishi kwa kuwa ni mwalimu na mfumo wa kiutumishi ujanipa kipaumbele, unizalau coz siendeshi gari ya maana.
 
hata chuo sijafika.. ila maisha nayoishi ni wachache sana wameyafikia.. mimi hata a level sijasoma.. niliishia o level tu then college ya kizushi kisha nikazama mtaani.. karibu sana tupambane kitaa.. huku hakuhitaji A za physics bali ni kujua kuusoma mtaa[/QUOT
Umeongea vitu ambavyo waajiriwa wengi hawatavifurahia japo inawezekana una ukweli ndani yake
 
Last week nilikua napitia matokeo ya madogo wa form six kwa Special Schools (Mzumbe, Tabora Boys, Kibaha na Ilboru) lengo ni kuhesabu One za Tatu yaani ni za kutafuta kwa tochi... Nimeambulia kuona moja tu ya dogo wa Mzumbe alokua T.O (dogo mwenyewe PCB, sijui PCM siku hizi wamerogwa na nani).

Huu ni ushauri kwa madogo ambao mpo Advance na mna munkari wa kupiga One Kali tatizo hamjui strategies zipi mtumie. Kuna tofauti kubwa kati ya kusoma sana na kufaulu. Kusoma sana sio kufaulu, bali kusoma kwa technique.

Mbinu nilizotumia kupiga One ya 3 bila kukesha darasani:

Target Audience:
Wanafunzi waliopo Advance (five na six) hasa PCM (shule za Private hawahusiki sababu wana walimu na miundombinu ya kutosha)

Malengo:
Weka malengo ya kupiga One Kali. Yaani kila somo lisome ukiwa na mind za kupata A. Ukijiwekea malengo ya kupiga A lazima utakua unasoma kwa focus.
Mie wakati naingia form five nikaweka malengo kuwa lazima nipige one ya 3 na niingie Top 3 kitaifa. Na ikawa hivo mwisho wa siku.

Timetable:
Sikua na fixed (defined) ratiba kama wenzangu walivokua wamebandika ndani ya matranka yao au ukutani pembeni ya kitanda. Mie nilikua nasoma kwa mood.
Nilikua na alternate kati ya Physics na Chemia. Napiga maswali ya Gravitation nikichoka nafunga kesho napitia Inorganic Chemistry.

Hesabu nilikua napitia kila siku nikitaka kulala (somo la kulalia). Mfano nikitoka class kupiga maswali ya Electronics narudi Dom nafungua pure II napiga maswali yangu 20 ya Complex Number then nalala.

Kuna wakati najikuta nasoma Physics hata week nzima (mfano napoamua kupitia Mechanics), yaani kifupi sikua na ratiba fixed, nasoma kutokana na nataka nikave topic zipi kwenye somo husika.

Achana na tabia ya kusoma kwa ratiba, soma kulingana na somo lipi topic ipi upo nyuma sana. Topic ipi hujapitia maswali mengi, topic ipi umeanza kusahau. Lazima upige One ya 3.

Kabla sijasahau: Mie usiku mwisho wangu kusoma ilikua saa nne. Mchana ndio muda wangu wa kupiga kitabu, giza likiingia tu basi nakua zoba. Usually ikifika saa tatu usiku kama sijaenda prepo basi siendi tena, napitia hesabu kitandani nalala.
But mchana hunikuti nafanya upuuzi (labda jioni kwenye jogging uwanjani).
Lazima upige One ya 3.

Twende kwenye masomo husika sasa:

Physics:
Vitabu nilivosoma mpaka napiga pepa: (Chandy, Nelkon na Roger Muncaster).
Katika somo unalotakiwa upitie vitabu vingi ni Physics. Lakini mie nilikua mjanja. Nilipitia vitabu ambavyo NECTA wanapenda kutoa maswali basi. Vingine nikaachana navyo.

Nilianza na Chandy, then nilipo kimaliza nikaja Nelkon (hiki hata sikusoma, bali nilifanya maswali yote ya mle sababu hakina maelezo mengi). Then form six mwishoni nikamalizia Roger (japo kina maswali magumu, nilijitahidi kufanya, yaliyonishinda nikaachana nayo)

Ukitaka kuelewa Physics basi soma Chandy (wahindi wanaeleza mpaka una enjoy), but ukitaka kufaulu Physics NECTA piga maswali karibu yote ya Nelkon na Roger Muncaster. NECTA wanapenda kutoa maswali kutoka kwenye Nelkon na Roger.

Practical za Physics zote nilifoji wakati wa pepa. Ukijifanya kupiga practical real hutomaliza muda hautoshi. Ukikaribia NECTA jifunze namna ya kufoji practical za Mechanics, Heat na Umeme.

Lazima upige One ya 3.

Chemistry:
Katika masomo yaliokua mteremko kwangu basi ni Chemistry. Kwanza kabisa ndio somo ambalo sikuwahi kabisa kusoma Vitabu. Niliishia kusoma Notes tu pamoja na kupitia Past Papers za NECTA.
Yaani nilikua nashangaa watu wanakomaa kusoma Ramsden usiku wa manane wakati Chemia ni mwendo wa notes tu unapiga banda. Practical zake ndio chai kabisa.

Kifupi ni kuwa ukitaka kupiga banda la Chemia with minimum efforts fanya hivi:
Soma notice za topic husika (mfano Electrochemistry), ukishaelewa chukua Review ya NECTA, pitia pepa moja baada ya nyingine kwa topic (achana na tabia ya kupitia pepa zima matopic yote utaloose concentration, nenda topic by topic).
Ukimaliza rudi tena kwenye notice, soma topic nyingine (mfano Organic) then njoo tena kwenye Review, fanya hivo hivo. Hadi umalize topic zote.

Practical za Chemia zote nilifanya real, sikufoji hata moja. Sababu praki za Chemia ni simple, sinafanyika ukifata procedure. Kifupi Chemia hutakiwi kukosa A au B+. Mie nilipiga A kali nikaongoza Chemia kitaifa form six yetu. Watu wamekomaa na mavitabu nikawakimbiza kama kawa.
Lazima upige One ya 3.
View attachment 818007



Advanced Mathematics:
Katika somo ambalo nilikua nasomea kitandani ni hesabu. Kwanza kabisa sikua na ratiba maalum ya kusoma hesabu. By the way hesabu hatusomi, bali huwa tuna solve.
Nilianzaga kukomaa na Tranter kubabake kikanishinda. Nikaachana nacho.
Nikakomaa na Pure I na II nikakomaa nazo na sikuwahi kusoma kitabu kingine chochote zaidi ya hivi viwili.
Style yangu ile ile, nasoma topic (mfano Integration) then nazama kwenye NECTA Review napiga maswali yote ya Integration mpaka yaishe. Nikimaliza natafuta another topic hivo hivo.
Lazima upige One ya 3.

Mwisho Kabisa:
Watu wanaamini kuwa ili ufaulu masomo ya sayansi kwa One kali lazima uende ukapige mapindi kwa tuition center za Dar (Mgote, Moody, Mtiga, Mbuga etc).
Hilo sio kweli, sio kweli, ni uongo.

Mie sikuwahi kusoma tuition yoyote Dar. Nilipiga mapindi ya vichochoroni tu.
Mengine tulifundishana na wenzangu shule. Na topic zingine niliamua kusoma mwenyewe baada ya kukosa mtu wa kunifundisha (mfano Modern Physics, Static Electricity, Complex Numbers, Statistics).

Vijana acheni kulala, wekeni malengo ya kupiga One kali ili inapofika stage ya kuomba vyuo unak ua na wide selection ya kwenda chuo na course unayotaka.
Lazima upige One ya 3.

View attachment 818008
CCIE lini kiongozi?? Maana bongo wapo 2 tu wenye nayo tena wahindi.
 
Hongeren kwa nafas zenu.
Cha msingi tutimize majukum yetu.


Kama haujasoma na umefanikiwa sawa-SAIDIA JAMII

kama umesoma na umefanikiwa -JITAHID UFAIDISHE NA WENGNE ELIMU YAKO.

NB:
ILA KWA MANENO HAYO@CCNP ENGINEER....UNAONEKANA HUJAFAIDIKA VYAKUTOSHA
 
Hongeren kwa nafas zenu.
Cha msingi tutimize majukum yetu.


Kama haujasoma na umefanikiwa sawa-SAIDIA JAMII

kama umesoma na umefanikiwa -JITAHID UFAIDISHE NA WENGNE ELIMU YAKO.

NB:
ILA KWA MANENO HAYO@CCNP ENGINEER....UNAONEKANA HUJAFAIDIKA VYAKUTOSHA
Hiyo NB tegemea povu
[emoji23]
 
kwenye miti hakuna wajenzi.. yaani na ma AAA yako yote umeishia kuajiriwa serikalini kwa mshahara wa hazina... ma scholarship yote yaliyojaa duniani umeyaacha unahangaika na forex na mwisho wa siku unatapeliwa na wadogo zako kina ontario...

wahuni wana div 3 za mwisho tena za HKL ila ajira za maana kwenye mabalozi.. au wanajiajiri wenyewe wanagombania tenda na kupiga hela..

nashangaaga sana best students kuwaona udsm... ukikomaa kweli kweli na ukawa na washauri sahihi unatembea mapema sana.. bongo nyoso
hata chuo sijafika.. ila maisha nayoishi ni wachache sana wameyafikia.. mimi hata a level sijasoma.. niliishia o level tu then college ya kizushi kisha nikazama mtaani.. karibu sana tupambane kitaa.. huku hakuhitaji A za physics bali ni kujua kuusoma mtaa
anafikiri AAA za physics ukienda nazo dukani unapewa unga,,, au unanunua gari kwa cheti cha AAA huku ni maujanja ujanja tu.. mwisho wa siku dogo ontario kamtapeli hela zake pamoja na AAA zake.. huo ndio mtaaa sasa
Aisee maisha ya bongo bana, unapiga 1 unakuja kusukuma spacio, watu wa 3 na wasio soma wana range na discovery 7[emoji2]
Kusoma sana ni Uwoga wa maisha
Inaonekana ww bado upo chuoni karibu sana kwenye maisha ya kitaa. mwaka niliomaliza mm kuna jamaa yangu alipiga one ya 4 PCB kwa sasa ni daktari yupo Nyasa huko. Mimi nilijipigia three ya 14 kwa sasa hua namualika kwenye semina jamaa anakujaga amechoka balaa na kila mara ananipigiaga simu kuniulizia kama kuna training nimchomekee angalau apunguze ukali wa maisha
Muulizeni huyo jamaa na mi AAA yake wasio soma wangapi wanamzidi asituaminishe maisha ni kusoma tu..
Nna jamaa yangu alikuwa TO ila yuko kitaa magomeni kapanga chumba kimoja akipiga mapindi. Kusoma na kupata maksi kubwa bila kuwa na akili za kitaa utaishia kunung'unika moyoni ... AAA zisizokusaidia ni kazi Bure
Waafrika wana roho ya kwanini sana. Hawapendi kuona mwenzao ana kitu kizuri.

Kila mtu asifiwe kutokana na jema alilonalo. Ninyi wenye hela mtasifiwa kwa hela zenu, na wenzenu wenye akili watasifiwa kwa akili zao. Ninyi mna hela, na wenzenu wana akili.

Japo mimi nilifeli form four, ila ninawathamini sana wenye akili, na ninafurahi sana ninapoona mtu kapata one kali.

Hizo gari zenu zimetokana na wenye akili, zimetengenezwa kutokana na elimu. Bila ya hawa wenye akili, vitu vingi mnavyomiliki msingekuwa navyo.

Wenye akili wanaitengeneza dunia.
PUMBAVU NYIE.
 
Kuna komenti nyingine unajikuta tu unawaza kwa sauti...hivi wewe unayesema kuwa AAA za darasani si mali kitu una watoto unasomesha?? Unatoa taswira gani kwa wanao? Ndio nyinyi hata homework au maendeleo ya mtoto shuleni unamwachia mke au housegirl. Dah maumivu. Hiyo ya kuwa waliofaulu wana maisha ya shida kuliko ya waliofeli au ambao hawajaenda shule sijui mnatumia denominator gani na wala sijui mmeverify vipi?

Mdogo wangu hongera sana kwa kutoa somo kali kwa wenetu, wadogo zetu wenye kujua maana ya elimu. Hayo ya kuchagua kuajiriwa na serikali au hapana ni maamuzi ya mtu na malengo yake na wala sio kutokujua ukitakacho. Wanaonanga hata wao wangefaulu pia wangeseek government employment.

Tujifunze kukubali na kusifia juhudi za wenzetu.
 
Mkuu kusema kweli sina mpango. Level nilofika naona inanitosha.
Mkuu hujanijibu why hukutaka kufundisha? Pale COET au ndio tuseme enzi hizo unahitimu ni vile ma prof wa pale hawakuona wewe unafaa au ndio ile kubebana maana nimeliona hili la kubebana sana kama unafahamiana na prof na performance yako iko vizuri kwako?
 
Waafrika wana roho ya kwanini sana. Hawapendi kuona mwenzao ana kitu kizuri.

Kila mtu asifiwe kutokana na jema alilonalo. Ninyi wenye hela mtasifiwa kwa hela zenu, na wenzenu wenye akili watasifiwa kwa akili zao. Ninyi mna hela, na wenzenu wana akili.

Japo mimi nilifeli form four, ila ninawathamini sana wenye akili, na ninafurahi sana ninapoona mtu kapata one kali.

Hizo gari zenu zimetokana na wenye akili, zimetengenezwa kutokana na elimu. Bila ya hawa wenye akili, vitu vingi mnavyomiliki msingekuwa navyo.

Wenye akili wanaitengeneza dunia.
PUMBAVU NYIE.
Mkuu umeelewa comment yangu ? Rudi uisome vizuri, mimi sijaelezea chochote kuhusu huyu jamaa, kuna mtu nilimjibu tu ualisia wa bongo nikiwa na maana nchi yetu elimu haithaminiki mtu unasoma unapiga 1 then ka mshahara kadogo so unaishia kusukuma spacio
Kwa vyovyote sijamsema mleta mada
Siku nyingine utumie ustaarabu na akili ,kama matusi hata mi nayajua
 
Waafrika wana roho ya kwanini sana. Hawapendi kuona mwenzao ana kitu kizuri.

Kila mtu asifiwe kutokana na jema alilonalo. Ninyi wenye hela mtasifiwa kwa hela zenu, na wenzenu wenye akili watasifiwa kwa akili zao. Ninyi mna hela, na wenzenu wana akili.

Japo mimi nilifeli form four, ila ninawathamini sana wenye akili, na ninafurahi sana ninapoona mtu kapata one kali.

Hizo gari zenu zimetokana na wenye akili, zimetengenezwa kutokana na elimu. Bila ya hawa wenye akili, vitu vingi mnavyomiliki msingekuwa navyo.

Wenye akili wanaitengeneza dunia.
PUMBAVU NYIE.
Kwahiyo mwenye pesa hana akili? kufaulu shule sio akili nyingi ila ni kumbukumbu tu ya uliyoyasoma ,.........mwenye pesa ndiye mwenye akili Siku zote
 
Dah nilichokiona katika huu Uzi kuna watu mna historia na upinzani wa chini kwa chini kumbe ambao sie wengine tulikuwa hatuujui kumbe mnafahamiana kutoka huko FOREX sasa sie tuliodandia mmetuingiza chaka na kutafuta upande wa kulaumu kuwa hauthamini upande mwingine.

Ushauri wangu tupambane tu na maisha mliosoma na ambao pia hatukusoma maana hiyo ndo dhamira ya kila binadamu.
 
Back
Top Bottom