Vijana wa Kiislamu hawaogopi ndoa kama Wakristo

[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]makobasi
 
Muislamu anaoa kwa elfu 20 mahari unadhani kuna ndoa hapo, ndio maana wanaachana hovyo hovyo.
Mshamba wa wapi we kuachana ni zama izi tumeshuhudia ndoa za gharama kubwa ziko wapi hata mastar wa bongo Tena watu wa injili

Uislamu unaendana na maendeleo ya dunia na pia unaheshimu maumbile ya binadamu hujui talaka sheria zake zimeweka kipind ambacho ni ngumu watu kuachana kwa ajili ya kizazi kijacho unajua laana ya kutoa talaka mpaka mbingu na ardhi zina kulaani Zina tetemeka hujui

Kaa usome utajua talaka kuitoa ni laana ila kwa kizazi Cha Sasa ni muhimu kuepuka madhara makubwa kama kuua mwenza
 
Unadhani yale Maneno mkaishi katika shida na raha mpaka kifo kitakapo watenganisha, Ni mepesi?
 
Muislamu anaoa kwa elfu 20 mahari unadhani kuna ndoa hapo, ndio maana wanaachana hovyo hovyo.
Mbona unatumia hoja za kitoto kabisa.

Usukumani huko mtu atalewa mahari ya makumi ya ng'ombe au mbuzi na bado ndoa inavunjika.

Think twice.
 
Muislam barua unatuna na elfu 30 ndani inajibiwa kuwa umekubaliwa na harusi ukiwa na elfu 60 umemaliza fasta tuu .njoo kwa wakristo sasa mara shuka la bibi mara kitenge cha shangazi mara koti la babu mara redio ya picha na kabati la mbeho au pikapu la nyasi sa ng'ombe ndio maana tunaogopa kuoa tunaishia kutandika mimba unalala mbele baadae unaandaa hela kidogo kama faini ya matunzo ya mtoto unachukua mwanao mama yake anaishia kwao kuuza ndizi visukari na beseni barabarani
 
Najuwa wajuwa ila umekuja kupima upepo.Ni kwamba wakristo wengi hawafungi ndoa kwakuwa wanamuda zaidi kujiandaa kisaikolojia,pia huchukulia tukio muhimu hujipa muda kujiandaa,wenzetu hawa marafiki zetu na nimesoma kwenye shule zao.Wakiwa na sh50au laki kwisha.
 
Ha ha makobasi ya nini tena [emoji3][emoji3]

Ila kiukweli waislam nawapenda hawana complications kwenye suala la kuoa

Sent from my Redmi Note 9S using JamiiForums mobile app
 
Muislamu anaoa kwa elfu 20 mahari unadhani kuna ndoa hapo, ndio maana wanaachana hovyo hovyo.
Hayo mawazo mgando! Kuna jamaa alilipa mahari milion tatu,ile ndoa ilidumu kwa miezi sita tu.hivyo kiasi cha mahari hakiweki gerentii ya ndoa kudumu, unaweza kulipa mahari elfu 20 ndoa ikadumu,na unaweza kulipa mahari milioni tatu ndoa ikadumu,na vice versa is true
 
Fikiria tena ulichofikiria! Kaa chini tuliza kichwa na ufikirie vizuri. Kuna sisi wengine bibi zetu miaka hiyo waliolewa kwa shilingi 50 tu! Na walidumu kwa zaidi ya miaka 80!
Huyo jamaa uwezo wake wa kufikiri ni mdogo,anadhani mahari kuwa kubwa ndo ndoa kudumu,kumbe msingi wa ndoa kudumu ni maridhiano ya wanandoa,tena mahari ikiwa kubwa sana inaweza kuleta hasadi tu kwa muoaji na familia ya muolewaji,ukawa uhasama tu badala ya undugu
 
Watu wanachanganya ndoa na harusi, hivi hawajui kuwa ukilipa mahari unaweza kuchukua watu kadhaa mukafungishwa ndoa kanisani au msikitini ikawa imeisha hiyo, bila hata kukodi ukumbi!
 
Muislamu anaoa kwa elfu 20 mahari unadhani kuna ndoa hapo, ndio maana wanaachana hovyo hovyo.
Hivi umeandika ili mradi uwandike au ulifikiria japo kido,
Kuna andiko lolote kwenye sheria ya ndoa ya kikristo kilichopanga kiasi cha pesa za mahari??
 
Kuoa mwanamke kiislam ni simple Sana.
Hakuna hata mbwembwe za ndoa.

Shida ipo huku kwetu wakristo.
Ili uoe lazima ujipange.
Unateseka kuja kuishi na mtu ambaye kila kitu atakuwa anamuachia house girl.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…