Vijana wa Kiume badilikeni

Vijana wa Kiume badilikeni

Tatizo kubwa lipo kwenye jamii sio vijana.. yani kijana akimaliza chuo akaendesha bodaboda au kufanya Kazi ya saidia fundi watu wengi huanza kusema vibaya kumchukulia kama kitendo cha kwenda shule alipoteza muda.. na hakuna maarifa aliyo yapata ya ziada tofauti na walio baki mtaani hii kitu sio kizuri kwenye jamii yetu, na ndo kimefanya vijana wengi wajifungie majumbani.

Yani ili nchi iendelee inatakiwa tujifunze kuwasifia watu wanao kujituma kufanya Kazi kwa bidii hata kama ikiwa ni Kazi ya kuzibua choo.. na kingine pia tujifunze kwa nchi zilizo endelea.

Jamii yetu inaona kama mtu ukimaliza kusomea Uhandisi ukaenda kulima au kujiajiri katika fani tofauti unakuwa umepotea.. kwa mtazamo wangu kitu kikubwa kinacho kwamisha vijana ni majungu kutoka kwenye jamii.

Mfano niulize tu.. ni wazazi wangapi wataruhu mwanao aliesomeshwa kwa gharama mpaka chuo akawe bodaboda,saidia fundi, au hata kuwa mpishi mgahawani?? Wazazi kama mpo humu naomba mjibu kwa uwazi kabisa [emoji1488]
hata michongo yenyewe watakupa Kwanza mpaka wakudiscuss Kwanza Kama ni nimchongo watakupa kwa kuona kuwa unadhiki.
 
Naomba kukuliza pia.. kwenye kikundi chenu cha vikoba wengi hutoa pesa kutoka kwenye biashara na sio kwa kuhongwa na wanaume?..

Maana ninajua list ya wadada ambao wanamaduka lakini still mtaji wao mkubwa ni kutoka kwa wanaume na biashara husika zimekuwa kama bosheni tu, maana wanaume wengine wanaamini ukimuweka mwanamke kwenye frame unamfunga miguu asichepuke kirahisi.. kuna wadada wangapi mjini ambao wauza matunda na degree zao?!
Kuna hili kundi ambalo pia linaonekana ni super women! Kumbe bure tu wanakaa kwenye vifremu wanapiga mizinga wabustiwe kodi na mtaji deile! Danga akiamsha unashangaa tu mtu biashara imemshinda😂
 
Mtoa mada ,mtoa mada umeangalia kwa makini au umeandika andika tu?, umeshawai kumuona mwanamke akiuza ice cleam za bakhresa kwa vile vibaiskeli? Umekwenda pale buguruni ukute vijana wangapi wa kiume wanafanya kazi za kupakia ngano , ushawai kukuta gari za pespi ,koka, au za kusambaza maji wanapakia au kushusha wanawake. Ushawai unajua waendesha bajaji asilimia kubwa ni wanaume, unajua boda boda wengi wanaume ,unajua makondacta na madeleva wa daladala wengi wanaume, ukija na hoja fanya tasmini kwanza sio unakuja kubwabwajatu, kama ulikuwa hujui mwaka huu ndio tumepata rais nwanamama huko kote tulikuwa na marais wa wanume

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu tatizo lipo inawezekana uwasilishaji wake ukawa namapungufu lakini wadogo zetu wamekwama
 
Tatizo kubwa lipo kwenye jamii sio vijana.. yani kijana akimaliza chuo akaendesha bodaboda au kufanya Kazi ya saidia fundi watu wengi huanza kusema vibaya kumchukulia kama kitendo cha kwenda shule alipoteza muda.. na hakuna maarifa aliyo yapata ya ziada tofauti na walio baki mtaani hii kitu sio kizuri kwenye jamii yetu, na ndo kimefanya vijana wengi wajifungie majumbani.

Yani ili nchi iendelee inatakiwa tujifunze kuwasifia watu wanao kujituma kufanya Kazi kwa bidii hata kama ikiwa ni Kazi ya kuzibua choo.. na kingine pia tujifunze kwa nchi zilizo endelea.

Jamii yetu inaona kama mtu ukimaliza kusomea Uhandisi ukaenda kulima au kujiajiri katika fani tofauti unakuwa umepotea.. kwa mtazamo wangu kitu kikubwa kinacho kwamisha vijana ni majungu kutoka kwenye jamii.

Mfano niulize tu.. ni wazazi wangapi wataruhu mwanao aliesomeshwa kwa gharama mpaka chuo akawe bodaboda,saidia fundi, au hata kuwa mpishi mgahawani?? Wazazi kama mpo humu naomba mjibu kwa uwazi kabisa [emoji1488]

Hili unalolisema lina ukweli mkubwa tu. Tatizo sisi tuna tabia ya kudharau aina fulani fulani za kazi na kuziona kama ni kazi za watu fulani mf wasiosoma.

Mfano kwa nchi zilizoendelea, ni kawaida kabisa kukuta kijana lets say hawa wanaosoma vyuoni, kipindi cha likizo anaweza kuomba kazi kwenye mgahawa, bar, supermarket nk na anakua anafanya kwa masaa fulani anaingiza kipato. Hii inamjenga hata siku akimaliza chuo hakosi cha kufanya na kila mtu anaheshimu kazi ya mwenzake.

Sasa njoo hapa kwetu. Kijana wa chuo au aliemaliza chuo hata bar ya baba yake hawezi kukaa kaunta auze, anaona kama ni kujidhalilisha! Graduate hawezi kuendesha hata daladala au bajaji ya nyumbani kwao anaona anajidhalilisha, matokeo yake ndio tunakua na vijana wanakaa tu kutwa nzima hamna wanachofanya.
 
Tatizo kubwa lipo kwenye jamii sio vijana.. yani kijana akimaliza chuo akaendesha bodaboda au kufanya Kazi ya saidia fundi watu wengi huanza kusema vibaya kumchukulia kama kitendo cha kwenda shule alipoteza muda.. na hakuna maarifa aliyo yapata ya ziada tofauti na walio baki mtaani hii kitu sio kizuri kwenye jamii yetu, na ndo kimefanya vijana wengi wajifungie majumbani.

Yani ili nchi iendelee inatakiwa tujifunze kuwasifia watu wanao kujituma kufanya Kazi kwa bidii hata kama ikiwa ni Kazi ya kuzibua choo.. na kingine pia tujifunze kwa nchi zilizo endelea.

Jamii yetu inaona kama mtu ukimaliza kusomea Uhandisi ukaenda kulima au kujiajiri katika fani tofauti unakuwa umepotea.. kwa mtazamo wangu kitu kikubwa kinacho kwamisha vijana ni majungu kutoka kwenye jamii.

Mfano niulize tu.. ni wazazi wangapi wataruhu mwanao aliesomeshwa kwa gharama mpaka chuo akawe bodaboda,saidia fundi, au hata kuwa mpishi mgahawani?? Wazazi kama mpo humu naomba mjibu kwa uwazi kabisa [emoji1488]
Kwani asiposifiwa shida iko wapi?

Ukiendesha bodaboda watu wakakusema kwani unakufa?

Ndio maana tunasema vijana wenyewe hawajitambui. Kama mtu unamaliza chuo alafu unaogopa kufanya kazi flani kwamba watu watanionaje huku unapigika kwa njaa maana ake hujitambui.
 
Mimi nilitoka advance nikiwa nina mhemko balaa kwamba siwezi kufundisha shule bila kulipwa Tsh 150,000 ( enzi hizo shule za kata zimeshamiri sana na hazina walimu ). Na shule nyingi zilikuwa zinalipa laki 1 mpaka 120.

Nilivyofika home nikamkuta mama anafanya kazi ya kulipwa 1,500 kwa siku yaani Tsh 45,000 kwa mwezi. Nilijiona mpumbavu sana, nakataaje Tsh 100,000 wakati mama analipwa elfu 45.

Nikaamua kwenda kufundisha, mshahara ni Tsh 100,000 ila take home ni 95,000 baada ya kukatwa elfu 5 ya chai.

Vile vile, baada ya kuhitimu chuo 2016 nilijua tu hapa nikijifanya msomi uchwara nitajuta. Nilienda oufanya kazi za ulinzi ( kampuni niliyoenda recruitment yake utafikiri unaomba kazi usalama wa taifa wakati mshahara ni 250,000 )

Yaani baada ya muda ( wakati wengine bado wanasubiri kazi za ndoto zao wakiwa wamekaa ) mimi nina mambo yangu mengine tu. Vile vile huko NSSF tayari nina kama 3M.

Dunia haijawahi kuwa na huruma na mtu yeyote.

Kaa Dar uzeeke, urudi kijijini kuongea kiingereza kwenye vijiwe vya gongo na kuwasilimulia uliomakiza nao lasaba habari za Dar. Time flies so fast.
Aisee, hongera sana
 
Wewe ndio umenena. Wazazi wanowaruhusu wapo. Shida ndio ipo kwenye jamii wanakuonea huruma sijui kama wao ndio wanafanya.
Kabisa mkuu.. jamii yetu inatakiwa kubadilika ili vijana waone ni kawaida kupambana nje ya box sababu wakichanganya na elimu yao speed ya kufanikiwa inaweza kuwa kubwa kuliko ambao hawakupata nafasi ya elimu ya juu..
 
Mimi nilitoka advance nikiwa nina mhemko balaa kwamba siwezi kufundisha shule bila kulipwa Tsh 150,000 ( enzi hizo shule za kata zimeshamiri sana na hazina walimu ). Na shule nyingi zilikuwa zinalipa laki 1 mpaka 120.

Nilivyofika home nikamkuta mama anafanya kazi ya kulipwa 1,500 kwa siku yaani Tsh 45,000 kwa mwezi. Nilijiona mpumbavu sana, nakataaje Tsh 100,000 wakati mama analipwa elfu 45.

Nikaamua kwenda kufundisha, mshahara ni Tsh 100,000 ila take home ni 95,000 baada ya kukatwa elfu 5 ya chai.

Vile vile, baada ya kuhitimu chuo 2016 nilijua tu hapa nikijifanya msomi uchwara nitajuta. Nilienda oufanya kazi za ulinzi ( kampuni niliyoenda recruitment yake utafikiri unaomba kazi usalama wa taifa wakati mshahara ni 250,000 )

Yaani baada ya muda ( wakati wengine bado wanasubiri kazi za ndoto zao wakiwa wamekaa ) mimi nina mambo yangu mengine tu. Vile vile huko NSSF tayari nina kama 3M.

Dunia haijawahi kuwa na huruma na mtu yeyote.

Kaa Dar uzeeke, urudi kijijini kuongea kiingereza kwenye vijiwe vya gongo na kuwasilimulia uliomakiza nao lasaba habari za Dar. Time flies so fast.
Hongera mkuu umeliona
 
Mimi binafsi ni afadhali mtu anayefanya chochote kuliko mkaaji, kikubwa mazngira ya kazi yawe salama tu

Mimi binafsi mdogo wangu anayenifata amesomea nursing amefanya kazi hospital binafsi kama miaka mitano akashindwa kutokana na uonevu na kubanwa

Kaenda kuazisha mgahawa wake mahali anauza na yuko happy tu

Mimi dadake siwezi sema kazi yake anazalilika eti kisa msomi, madam ni mtu mzima ameamua mwenyewe na anapata hela afanye tu
Safi sana..
 
Kwani asiposifiwa shida iko wapi?

Ukiendesha bodaboda watu wakakusema kwani unakufa?

Ndio maana tunasema vijana wenyewe hawajitambui. Kama mtu unamaliza chuo alafu unaogopa kufanya kazi flani kwamba watu watanionaje huku unapigika kwa njaa maana ake hujitambui.
Exactly ndo manake
 
Sana, then kama hatuzibi UFA tunakwenda kujenga ukuta siku si nyingi, coz tumeandaa kina mama kwa muda wa kutosha ila vijana wakiume wamesahaulika, sasa mama akishakuwa na nguvu economical, social, na hata kifikra ni ngumu mwanaume kukubali hiyo hali kutokana na nature

Nature inataka mwanaume awe na nguvu kiuchumi, kifikra na kimawazo alafu mwanamke awe kawaida ili maisha yaende
Dunia tunayoelekea ni kinyume chache, sasa tayari TAASISI ya familia inaharibika kuanzia kwenye Mizizi yake
Ipo haja ya kuanza semina kuwafungua akili vijana wa kiume coz kiukweli hata Kwenye mahusiano mengi siku hz kumekuwa na mashindano kat ya mwanaume na mwanamke kwakua ...tayar mwanamke ashaanza kupata coverage Kwenye uchumi ..na wanaume n kama wamelala hv
 
Mtoa mada ,mtoa mada umeangalia kwa makini au umeandika andika tu?, umeshawai kumuona mwanamke akiuza ice cleam za bakhresa kwa vile vibaiskeli? Umekwenda pale buguruni ukute vijana wangapi wa kiume wanafanya kazi za kupakia ngano , ushawai kukuta gari za pespi ,koka, au za kusambaza maji wanapakia au kushusha wanawake. Ushawai unajua waendesha bajaji asilimia kubwa ni wanaume, unajua boda boda wengi wanaume ,unajua makondacta na madeleva wa daladala wengi wanaume, ukija na hoja fanya tasmini kwanza sio unakuja kubwabwajatu, kama ulikuwa hujui mwaka huu ndio tumepata rais nwanamama huko kote tulikuwa na marais wa wanume

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata mimi nimemshangaa sana pengine ni huyo ndugu yake tu na alipaswa kumsaidia sio kumsema vile. Hajui watoto wa kiume wanavyopambana kwa machungu na hasira.
 
Kama kibarua kipi kwa mfano unachokijua wewe?
Kuna kazi za ulinzi hapa Dar ukienda siku hiyo hiyo unapata kazi hata kama ni LASABA.

Mshahara mpaka Tsh 160,000.

Tena uzuri wa hizi kazi ni kukaa na kutembea tembea tu kidogo.

Kuna watu Dar hii wanabebeshwa viroba vya unga usiku mzima kwenye maviwanda na hawapati hiyo. Asubuhi kunakucha wako hoiiiii
 
Ipo haja ya kuanza semina kuwafungua akili vijana wa kiume coz kiukweli hata Kwenye mahusiano mengi siku hz kumekuwa na mashindano kat ya mwanaume na mwanamke kwakua ...tayar mwanamke ashaanza kupata coverage Kwenye uchumi ..na wanaume n kama wamelala hv
Sana
 
Back
Top Bottom