Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Kuna mtoto wa mpangaji mwenzangu hapa kitaa

Ni katoto ka kike kana miaka minne hivi....

Kuna siku nilikakuta kameandaliwa kuogeshwa,kalivyoniona tu hivi kakafichwa ikulu yake kwa kutumia mikono.

Duh!!nikajiuliza kumbe hata haka katoto kanajua pale kati haparuhusiwi kuonwa.

Na kwa nini hakakuficha/kuziba sehemu nyingine.
 
Wanangu 7yrs na 5yrs walikuwa wanabishana na binti Msaidizi wa kazi nyumbani juu ya udocta wa Rais wetu, maana walisikia kwenye habari wakisema dkt Magufuli, wakashangaa wakasema huyu kakosea maana huyu si dkt ni Rais yeye hatibu wagonjwa, dada alivyozidi kung'ang'ania wakamuuliza ni dkt wa hospitali gani?
Pia walishangaa kumwona alipoenda muhimbili na mke wake mama Janet, wakauliza huyu kwani ana wake wawili? Nikawaambia hapana wakasema mbona huyu nae wamesema ni mke wa rais? Ilibidi niwaulize nyie mnamjua yupi? Wakasema si mama Samia Suluhu? Ikabidi niwaeleweshe yule si mke wake ni makamu wa Rais lakini walikubali tu yaishe, maana picha nyingi wanamwona yupo pembeni yake.

My boy 3yrs alinifwata jikoni na kuniambia sili chapati za dada nataka unazopika wewe, nikamjibu hizi za baba, akadai hata yeye atakuwa baba. Nikamwambia baba ndie ameleta haya mayai namtengenezea mwenyewe, akajibu na mimi nikiwa baba nitakuletea hayo mayai.
Nikashindwa mie.

Siku dada yake akasema leo mama mimi nalala na wewe chumbani kwako, dogo wakiume akasema weeee hamna chumbani kwa mama wanalala boys tu, baba boy na mimi boy.

Kwa kweli watoto ni baraka na Furaha ndani ya nyumba, unaweza toka huko umeudhiwa ukifika home unasahau yote.
 
Watoto katika hatua zao za ukuaji na kujifunza wanakua na mambo flani flani ya kufurahisha sana yaani mwanao anaweza kukuvunja mbavu balaa.
Mfano
1. Mwanangu (1.5years) anaweza kua anatazama TV akisikia unaongea na simu au umeweka music kwenye simu anakimbia kuja kuangalia simu hata kama TV ilikua na TV program ya katuni nzuri kiasi gani[emoji23] [emoji23] [emoji23]

2. Ukitaka alale we nenda kitandani weka music kwenye sim yako atakuja mwenyewe hata kama alikua anakwepa kulala[emoji23]

3. Anaheshimu simu yangu kama kituo cha polisi ila ya mama yake kashaipasua ukiiona utajua mama yake anafanya kazi idara ya miamba (geology)[emoji23]

4.Kupenda safari akiona mtu anatoka tu anaanza kuaga bye bye akijua nayeye anahusika na safari[emoji23] [emoji23]

5. Chakula kikiwa tayari, kabla sijaitwa kula yeye akiona mambo yako tayari anakuja kunipigapiga mgongoni(hajajua kuongea) akiashiria msosi tayari basi ukipotezea anaenda anarudi mpaka utakapoinuka[emoji23] [emoji23]

6. Mwanangu anatabia flani kama wivu, akiona naongea na mama yake mara nimemshika mkono tunaongea kama jambo la siri anakuja fasta analia anataka mama yake ambembe[emoji23]
Nadhani hajajua kwamba mama yake ni mke wangu[emoji23] [emoji23] [emoji23]

Hivi ni baadi ya vituko vya watoto mdau ongeza vya mwanao
Watoto wanaleta raha sanaaa
d5369b5f1d01053ec979d4cb549b2c33.jpg
Wazazi wapya.
 
Mi wa kwangu balaa natamani akue kidogo labda nitapata zuri la kueleza, leo ni wiki ya tatu sijalala nakesha, dogo analala mchana wakati mimi nipo job, usiku halali na akilala mikononi ukimuweka kitandani tuu yani kabla hata hujakiacha kitanda kishaamka na kelele nyingi, kingine asee usikae karibu na mamaake ugomvi wake c mdogo atalia hapo hadi utashangaa, kingine tangu wiki iliyopita hajacheka sijui ndo kutabasamu hakuna. Ana miezi 4. Hataki kulazwa kama watoto wengine anapokuwa macho, yeye anataka kukaa na anakaa...huyo ni mdogo, kakayake yeye anapenda ngumi, anajua bunduki zote kwa majina, hili nimejaribu kumuonya mamayake asiwe akimuwekea movie za mapigano zaidi ya cartoon lakini sijui huyu kijana anajifunzia wapi maana hakawii kukwambia anataka awe mwanajeshi sababu hapendi majambazi, huyo Ana miaka mi 4, anajua kikorea, kajifunza wapi mi sijui...ila ana shida moja anapenda tambi tuu, vyakula vingine kula mpaka mpigizane kelele sana na husingizia anataka kukojoa akienda harudi..ana huruma sana na mamayake, mjanja mjanja sana ukikasiririka atajua jinsi ya kukufanya ucheke tuu, shida usimuache na mdogo wake peke yao, unaweza kuta mtoto analishwa ugali.
hii kitu mwanangu wa mwaka na nusu naye anayo anasema pot kukojoa ukigeuka hayupoo, anapigana sana na dada yake ukimuudhi anakuvizia na kitu anarusha huyoo anakimbia...ana vituko viingi nikieleza hapa sitamaliza.
 
Nilipomaliza chuo nilifanya kazi kampuni moja ya binafsi, ilikuwa ya ukandarasi huyo bosi alikuwa na watoto 6, kati ya hao mmoja tu ndio alikuwa wa kiume na wa mwisho mwisho kuzaliwa, akawa anasema natamani ingekuwa na uwezo wa kumvuta mtoto akue haraka ili huyu jembe anisaidie majukumu wakati huo alikuwa class seven, sasa hivi yule kijana kamaliza chuo ana degree baada ya kumaliza form four pale ST.. Costantene Arusha akampeleka chuo Nairobi, ila jamaa amekuwa MZIGO, ZOBA yaani hana afanyalo pale zaidi ya kuendesha magari ya baba, siku moja nikaenda kusalimia maana nilishaondoka kitambo hapo, nikamuuliza vipi sasa amekua kuna msaada unaopta kama ulivotamani kumkuza fasta, aliniangalia kwa huruma sana yaani kama anajuta mtoto kukua, alijua acha tu nibebe msalaba wangu nikifa vikiisha basi sitakuwa na la kulaumiwa, nilimuhurumia.. Alipokuwa mdogo alikuwa anapenda sana kuja ofisini na hukaa na mzee wake kwa umakini kama kuna jambo ana hakikisha haliharibiki.
 
Asiyepata bahati ya kuishi na mtoto wake akiwa na umri wa miaka kuanzia 2 hadi 4 atakuwa amekosa uhondo wa kupindukia. Ndiyo kipindi kizuri cha kufurahia ubunifu wa mtoto aliyeanza kuongea kabla hajaanza utundu wa shuleni. Ni kipindi cha faraja ya ajabu kushuhudia ubunifu wa kiasili wa binadamu unaoonyeshwa na mtoto mkamilifu.


Mama aliwahi kuniambia kwamba mwanamke akienda kwao na mtoto mdogo 0-6years akirudi walikua wakimlipisha fain. Maana aliondoa furaha ya familia
 
Ana miezi 5 yeye hata akiwa analia jifanye unaongea na simu ananyamaza kusikiliza maongezi ukiacha tuu anashusha kilio....anapenda sana kusikiliza maongezi ya simu hata kama anasinzia ataamka
Duh dogo ana nyota ya Umbea.[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Nilipomaliza chuo nilifanya kazi kampuni moja ya binafsi, ilikuwa ya ukandarasi huyo bosi alikuwa na watoto 6, kati ya hao mmoja tu ndio alikuwa wa kiume na wa mwisho mwisho kuzaliwa, akawa anasema natamani ingekuwa na uwezo wa kumvuta mtoto akue haraka ili huyu jembe anisaidie majukumu wakati huo alikuwa class seven, sasa hivi yule kijana kamaliza chuo ana degree baada ya kumaliza form four pale ST.. Costantene Arusha akampeleka chuo Nairobi, ila jamaa amekuwa MZIGO, ZOBA yaani hana afanyalo pale zaidi ya kuendesha magari ya baba, siku moja nikaenda kusalimia maana nilishaondoka kitambo hapo, nikamuuliza vipi sasa amekua kuna msaada unaopta kama ulivotamani kumkuza fasta, aliniangalia kwa huruma sana yaani kama anajuta mtoto kukua, alijua acha tu nibebe msalaba wangu nikifa vikiisha basi sitakuwa na la kulaumiwa, nilimuhurumia.. Alipokuwa mdogo alikuwa anapenda sana kuja ofisini na hukaa na mzee wake kwa umakini kama kuna jambo ana hakikisha haliharibiki.


Tatizo shule alizompeleka
 
Kuna mtoto wa mpangaji mwenzangu hapa kitaa

Ni katoto ka kike kana miaka minne hivi....

Kuna siku nilikakuta kameandaliwa kuogeshwa,kalivyoniona tu hivi kakafichwa ikulu yake kwa kutumia mikono.

Duh!!nikajiuliza kumbe hata haka katoto kanajua pale kati haparuhusiwi kuonwa.

Na kwa nini hakakuficha/kuziba sehemu nyingine.
Ulikuwa unaitolea [emoji102] ndo maana
 
Ni jukumu letu kama wazazi kuwalea watoto katika njia ipasayo, akimpendeza Mungu maana mwisho wa siku tutaulizwa kwanini huyu mtoto yuko hivi?

Tusifurahie matendo wafanyao watoto, huku hayo matendo tukijua kabisa yatakuja kuwa na athari kwenye maisha yake ya baadae, mtoto mdogo kupiga wenzake, kudanganya unajitafutia matatizo ya huko mbeleni.
 
mimi wa kwangu ana 3yrs anamuita mdogo wake wa mwaka na nusu "mwanangu' Na
huyo wa mwaka na nusu karibu kila siku lazima aamke saa 11 au 12 kasoro siku akipitiliza lazima nichelewe kazini..
Na akiamka nyumba nzima tunaamshwa sababu lazima atoke,,alie kufunguliwa mlango akaite kinadada..Na
Siwezi kununua zawadi ya mmoja lazima ninunue mbili lasivo kunatokea vita ya majimaji hapo ndani..
Na ole waone hata mkono umeshikwa tu na baba yao ni atamwambia mwache na kuanza kulia,,,amewahi kuongea yupo kama kasuku,,,
ukuta wa home ni balaa lingine..
 
Back
Top Bottom