T 1990 ELY
JF-Expert Member
- Sep 7, 2014
- 12,674
- 29,643
Cousin 🙁cuisine=aina/namna ya upishi wa chakula
Natumaini ulikusudia cousin.
WoteeeerrrrHahaa. Kumbe ni karibia watoto wote tabia hiyo ya kuchora chora wanayo. Daah
Wangu sijui angekuaje, ametangulia mbele ya haki, katakua mbinguni kanacheza huko...
Wazazi wapya.Watoto katika hatua zao za ukuaji na kujifunza wanakua na mambo flani flani ya kufurahisha sana yaani mwanao anaweza kukuvunja mbavu balaa.
Mfano
1. Mwanangu (1.5years) anaweza kua anatazama TV akisikia unaongea na simu au umeweka music kwenye simu anakimbia kuja kuangalia simu hata kama TV ilikua na TV program ya katuni nzuri kiasi gani[emoji23] [emoji23] [emoji23]
2. Ukitaka alale we nenda kitandani weka music kwenye sim yako atakuja mwenyewe hata kama alikua anakwepa kulala[emoji23]
3. Anaheshimu simu yangu kama kituo cha polisi ila ya mama yake kashaipasua ukiiona utajua mama yake anafanya kazi idara ya miamba (geology)[emoji23]
4.Kupenda safari akiona mtu anatoka tu anaanza kuaga bye bye akijua nayeye anahusika na safari[emoji23] [emoji23]
5. Chakula kikiwa tayari, kabla sijaitwa kula yeye akiona mambo yako tayari anakuja kunipigapiga mgongoni(hajajua kuongea) akiashiria msosi tayari basi ukipotezea anaenda anarudi mpaka utakapoinuka[emoji23] [emoji23]
6. Mwanangu anatabia flani kama wivu, akiona naongea na mama yake mara nimemshika mkono tunaongea kama jambo la siri anakuja fasta analia anataka mama yake ambembe[emoji23]
Nadhani hajajua kwamba mama yake ni mke wangu[emoji23] [emoji23] [emoji23]
Hivi ni baadi ya vituko vya watoto mdau ongeza vya mwanao
Watoto wanaleta raha sanaaa
mtoto wa sister angu akisikia nyimbo ya hainaga ushemeji hata kama kalala anaamka kisha atacheza
hii kitu mwanangu wa mwaka na nusu naye anayo anasema pot kukojoa ukigeuka hayupoo, anapigana sana na dada yake ukimuudhi anakuvizia na kitu anarusha huyoo anakimbia...ana vituko viingi nikieleza hapa sitamaliza.Mi wa kwangu balaa natamani akue kidogo labda nitapata zuri la kueleza, leo ni wiki ya tatu sijalala nakesha, dogo analala mchana wakati mimi nipo job, usiku halali na akilala mikononi ukimuweka kitandani tuu yani kabla hata hujakiacha kitanda kishaamka na kelele nyingi, kingine asee usikae karibu na mamaake ugomvi wake c mdogo atalia hapo hadi utashangaa, kingine tangu wiki iliyopita hajacheka sijui ndo kutabasamu hakuna. Ana miezi 4. Hataki kulazwa kama watoto wengine anapokuwa macho, yeye anataka kukaa na anakaa...huyo ni mdogo, kakayake yeye anapenda ngumi, anajua bunduki zote kwa majina, hili nimejaribu kumuonya mamayake asiwe akimuwekea movie za mapigano zaidi ya cartoon lakini sijui huyu kijana anajifunzia wapi maana hakawii kukwambia anataka awe mwanajeshi sababu hapendi majambazi, huyo Ana miaka mi 4, anajua kikorea, kajifunza wapi mi sijui...ila ana shida moja anapenda tambi tuu, vyakula vingine kula mpaka mpigizane kelele sana na husingizia anataka kukojoa akienda harudi..ana huruma sana na mamayake, mjanja mjanja sana ukikasiririka atajua jinsi ya kukufanya ucheke tuu, shida usimuache na mdogo wake peke yao, unaweza kuta mtoto analishwa ugali.
Asiyepata bahati ya kuishi na mtoto wake akiwa na umri wa miaka kuanzia 2 hadi 4 atakuwa amekosa uhondo wa kupindukia. Ndiyo kipindi kizuri cha kufurahia ubunifu wa mtoto aliyeanza kuongea kabla hajaanza utundu wa shuleni. Ni kipindi cha faraja ya ajabu kushuhudia ubunifu wa kiasili wa binadamu unaoonyeshwa na mtoto mkamilifu.
Duh dogo ana nyota ya Umbea.[emoji23] [emoji23] [emoji23]Ana miezi 5 yeye hata akiwa analia jifanye unaongea na simu ananyamaza kusikiliza maongezi ukiacha tuu anashusha kilio....anapenda sana kusikiliza maongezi ya simu hata kama anasinzia ataamka
Khaa ya kweli haya mkuu?ana miaka 10 ana akili sana now yupo form three jambe langu
Nilipomaliza chuo nilifanya kazi kampuni moja ya binafsi, ilikuwa ya ukandarasi huyo bosi alikuwa na watoto 6, kati ya hao mmoja tu ndio alikuwa wa kiume na wa mwisho mwisho kuzaliwa, akawa anasema natamani ingekuwa na uwezo wa kumvuta mtoto akue haraka ili huyu jembe anisaidie majukumu wakati huo alikuwa class seven, sasa hivi yule kijana kamaliza chuo ana degree baada ya kumaliza form four pale ST.. Costantene Arusha akampeleka chuo Nairobi, ila jamaa amekuwa MZIGO, ZOBA yaani hana afanyalo pale zaidi ya kuendesha magari ya baba, siku moja nikaenda kusalimia maana nilishaondoka kitambo hapo, nikamuuliza vipi sasa amekua kuna msaada unaopta kama ulivotamani kumkuza fasta, aliniangalia kwa huruma sana yaani kama anajuta mtoto kukua, alijua acha tu nibebe msalaba wangu nikifa vikiisha basi sitakuwa na la kulaumiwa, nilimuhurumia.. Alipokuwa mdogo alikuwa anapenda sana kuja ofisini na hukaa na mzee wake kwa umakini kama kuna jambo ana hakikisha haliharibiki.
Ulikuwa unaitolea [emoji102] ndo maanaKuna mtoto wa mpangaji mwenzangu hapa kitaa
Ni katoto ka kike kana miaka minne hivi....
Kuna siku nilikakuta kameandaliwa kuogeshwa,kalivyoniona tu hivi kakafichwa ikulu yake kwa kutumia mikono.
Duh!!nikajiuliza kumbe hata haka katoto kanajua pale kati haparuhusiwi kuonwa.
Na kwa nini hakakuficha/kuziba sehemu nyingine.
Ukamjibu nn?Wakwangu anamiaka 4 juzi kaniuliza baba nani kamzaa shetani